Kilala Makusaro
JF-Expert Member
- Oct 31, 2013
- 688
- 383
Watanzania wengi hawaelewi nini maana ya kutengeneza sarufu kwa pesa iliokuwa note. Hili ni anguko la thamani ya fedha. Kwa maana nyingine miatano itaungana na sarafu nyingine kwenda kununua pipi na mafungu ya nyanya. Haitakuwepo tena kwenye mauzo na manunuzi. mfno kama bati linauzwa 16500 linakwenda kuuzwa 17000 kuondokana na usumbufu wa sarafu. Sasa wajinga wa ccm hapa wanashangilia na kumpongeza Mwigulu eti uchumi unakua, Uchumi unaokuwa unajireflect kwe maintain the status qou ya pesa yenu. Uchumi wowote unaobadili note kuwa sarafu ni uchumi ambao sekta yake fedha inayumba. Hii inamaana vitu vimepanda bei kiasi 500 miatano imekuwa ya kununua bidhaa za chini sana. Pia gharama ya kuitengeneza mia tano ya note ni kubwa kuliko thamani yake. Wananchi watanzania ni watu wa mia tano yaani hali zao kiuchumi ni mbaya kiasi mia tano ni pesa inashikwa na watu wengi sana hivyo kuchakaa zaidi.