Sarafu mpya yatolewa leo na BOT

Sarafu mpya yatolewa leo na BOT

na huyo kwenye picha ni nani?sasa muungano ukivunjika tutatengeneza nyingine au itabaki kama ilivyo?
 
Lakini kwa kweli kwenye mzunguko wa kifedha tunahitaji noti zenye thamani zaidi ya Sh 10,000, suala la kusema litazidisha mfumuko wa bei BOT ijipange vizuri kulidhibiti, angalau ziwepo za Sh 25,000.. manake ni usumbufu mkubwa sana kwa wale wafanyao biashara kubwakubwa za fedha taslim..kubebana nazo ni hatari hatari hatari, hawana amani kabisa..

Hata zikiwepo za 50,000 mkuu, kwa sasa kubeba nkononi milioni 100 ni shida kubwa
 
Tunazidi kwenda shimoni, yaani 500 ni sarafu, wachumi rudini kwenye drawing board.

Kinachofuata ni noti ya 50,000/= take my word
 
Wameshindwa kuifanya 500 ya noti kuwa durable sasa wanatuwekea macoins tutayabebaje?
 
Hivi ktk dola ya kimarekani kuna sarafu? Na dola kubwa kabisa ni dola ngapi wakuu!
 
Naona wameweka picha ya rais wa nchini Zanzibar ili kuwaridhisha jamaa.
 
Lakini kwa kweli kwenye mzunguko wa kifedha tunahitaji noti zenye thamani zaidi ya Sh 10,000, suala la kusema litazidisha mfumuko wa bei BOT ijipange vizuri kulidhibiti, angalau ziwepo za Sh 25,000.. manake ni usumbufu mkubwa sana kwa wale wafanyao biashara kubwakubwa za fedha taslim..kubebana nazo ni hatari hatari hatari, hawana amani kabisa..

Acha mambo yako wewe huku mitaani wafanyabiashara ndogondogo na zakati noti ya 10000 kupata chenji kazi sembuse noti ya 25000/:
 
Source!

Hivi hapo inamaana uchumi unashuka eeh!
Anyways,ngoja tuone bei mpya ya vyakula itakavyopaa!!!
Hii tathimini ya wapi kumbe sarafu mpya ikitoka ndiyo uchumi kushuka hiki nacho sijui ni kichwa gani cha huyu jamaa.
 
Acha mambo yako wewe huku mitaani wafanyabiashara ndogondogo na zakati noti ya 10000 kupata chenji kazi sembuse noti ya 25000/:

siyo kwamba wanadiscontinue hizo za 10k, 5k, 2k na 1k, zinatumika sambamba na hizo kubwa.
 
Back
Top Bottom