SEHEMU YA 35...
“Unajidanganya! Nilipokuona mara ya kwanza, nilidhani nimekutana na jini. Nilipokusalimia, hakika mtoto una sauti nzuri sana, hivi ushawahi kuimba kwaya?” aliuliza David.
“Hapana!”
“Kwa sisi tuliowahi kuimba, sauti yako ni sauti ya kwanza, ile inayowafanya wenye mapepo walipuke, ni sauti ambayo ukiimba kwa muda mrefu, Mungu atasimama kwenye kiti chake cha enzi na kujivunia uumbaji wake, kujivunia kumpa msichana mmoja sauti nzuri ya kumsifu na kumuabudu,” alisema David.
Kila mstari aliomwambia Paulina, alilainika, akamuona david kuwa mwanaume mzuri, ambaye alistahili kuwa maishani mwake. Akasimama kutoka kitandani, akakisogelea kioo na kuanza kujiangalia. Sifa za mwanaume huyo zikaanza kujirudia kichwani mwake, kweli, kile alichokisema David ndicho alichokiona, akalitingisha kidogo kalio lake.
“Ahsante Mungu kwa kunipa hii silaha matata!” alisema Paulina kisha kutoa tabasamu.
Paulina alianza kubana, akabana na kubana lakini akashindwa kuvumilia. Katika siku ambayo hakuitarajia, akajikuta akilala kwenye kitanda cha David, akaipanua miguu yake na kuvunja amri ya sita na mwanaume huyo.
Hilo likawa kosa, damu zikakutana, akajiona kama amemalizwa kila kitu, hakuwa na ujanja tena, mwanaume huyo aliitumia nafasi hiyohiyo kukutana naye kimwili, hata kama alikuwa hataki, alikumbushwa namna alivyokuwa fundi kitandani, akakumbushwa jinsi alivyokuwa akiguna juu ya sita kwa sita na mwisho wa siku kumkubalia tena.
Wakabanjuka na kubanjuka, starehe zikaongezeka, baada ya miezi miwili, msichana Paulina akaanza kujisikia tofauti, hakutaka kuchelewa, akaenda kupima, majibu yakatoka na kuambiwa kwamba alikuwa na mimba.
Alijuta, alimtafuta David na kumwambia kuhusu ujauzito huo, kama ilivyokuwa kwa Sarafina, akamkatalia, akamwambia kwamba haikuwa yake, na kama alikuwa na mchezo wa kupata mimba sehemu nyingine kisha kumsingizia, basi wasijuane.
Paulina akaumia lakini hakuwa na jinsi, akakubaliana na mwanaume huyo, alichokifanya ni kutoa mimba na maisha yake kuendelea huku akijiahidi kwamba asingeweza kuuruhusu mwili wake uchezewe na mwanaume mwingine kama ilivyokuwa kwa David.
Je, nini kitaendelea?