Greenwhich
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 1,337
- 968
Spika wa zamani Samwel Sitta anatarajiwa kutoa ya moyoni siku ya Jumatatu kuhusu kinachoendelea ndani ya CCM.
Taarifa kutoka watu wa karibu na kiongozi huyo aliyejipambanua kama mpiganaji wa vita dhidi ya ufisadi zinaeleza atazungumzia hali halisi iliyopo ndani ya CCM na huenda akatangaza vita zaidi dhidi ya ufisadi ndani ya chama hicho.
Waziri huyo wa Afrika Mashariki anasifika kama mtu asiyemumunya maneno na huenda akawasha moto mkubwa ndani ya chama hicho atakapozungumza.
Kwa sasa ndani ya CCM kuna mvurugano mkubwa kutokana na vita ya madaraka ambapo kwa wiki moja makada watano katika makundi mawili yanayoparurana wametuhumiana na kushambuliana mbele ya vyombo vya habari huku kila kundi likitumia kila silaha kushambulia lingine.Makada hao ni John Malecela,Paul Makonda,Richard Kyabo,John Guninita na Hamis Mgeja.
Taarifa kutoka watu wa karibu na kiongozi huyo aliyejipambanua kama mpiganaji wa vita dhidi ya ufisadi zinaeleza atazungumzia hali halisi iliyopo ndani ya CCM na huenda akatangaza vita zaidi dhidi ya ufisadi ndani ya chama hicho.
Waziri huyo wa Afrika Mashariki anasifika kama mtu asiyemumunya maneno na huenda akawasha moto mkubwa ndani ya chama hicho atakapozungumza.
Kwa sasa ndani ya CCM kuna mvurugano mkubwa kutokana na vita ya madaraka ambapo kwa wiki moja makada watano katika makundi mawili yanayoparurana wametuhumiana na kushambuliana mbele ya vyombo vya habari huku kila kundi likitumia kila silaha kushambulia lingine.Makada hao ni John Malecela,Paul Makonda,Richard Kyabo,John Guninita na Hamis Mgeja.