Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,512
- 272,210
Eee bhana eee ! Mbona ccm imekufa haraka namna hii jamani ? Unajua bhana , mimi nilijua ni kweli itakufa , lakini nilijua itakufa 2015 na sikutegemea ife 2014 !
buku7 ktk issue kama hizi ukiwakuta ktk thread moja, wanakosoana hata wenyewe kwa wenyewe.ile team spirit waliyokuwa nayo siku zile haipo tena.Wapi Madada Pacha Simiyu Yetu na Simiyu Voice,Ritz,Msalani,Ifweero,Dada Hamida,Mwekundu,Chamviga et al.
Waache wafu wazike wafu wao.
Spika wa zamani Samwel Sitta anatarajiwa kutoa ya moyoni siku ya Jumatatu kuhusu kinachoendelea ndani ya CCM.
Taarifa kutoka watu wa karibu na kiongozi huyo aliyejipambanua kama mpiganaji wa vita dhidi ya ufisadi zinaeleza atazungumzia hali halisi iliyopo ndani ya CCM na huenda akatangaza vita zaidi dhidi ya ufisadi ndani ya chama hicho.
Waziri huyo wa Afrika Mashariki anasifika kama mtu asiyemumunya maneno na huenda akawasha moto mkubwa ndani ya chama hicho atakapozungumza.
Kwa sasa ndani ya CCM kuna mvurugano mkubwa kutokana na vita ya madaraka ambapo kwa wiki moja makada watano katika makundi mawili yanayoparurana wametuhumiana na kushambuliana mbele ya vyombo vya habari huku kila kundi likitumia kila silaha kushambulia lingine.Makada hao ni John Malecela,Paul Makonda,Richard Kyabo,John Guninita na Hamis Mgeja.
Chorus chochea hata kama ni magunzi chochea! Kazi moja tu.Mkuu Ben usimalize kuni zote wakati huu,huko mbeleni kuna Masika kubwa inakuja,chochea kidogo kidogo tuu,teh teh teh.
Sitta ndo ana haki kujivunia CCM, wananchi tunatambua mchango wake. Lakini Lowassa angezidi kula hela za Watz huku akiwapumbanza kwa kuwaaminisha kuwa mchapa kazi.
hao wengine bado wanaanda matamko tuvute subira hakuna atakae baki mradi wailshaajiita wapambanaji ngoja tuwasubiri ila kuwakusha ni muhimu, wasije wakajisahauNingemshangaa sana kama angekaa kimya kwa kudhalilishwa hivi.Ningemuona muoga.
Bado Joseph Msukuma wa Geita na Jesca wa Iringa
Hivi Mary Chatanda bado tu ?
Halafu wanawake wa CCM ni waoga.Vijana na wazee wameonyesha kusimama kidete kwenye hili swala.Nawashangaa akina Shelukindo wapo kimya.Hivi Anna Kilango ni coward kiasi hiki?
anasikilizia upepo!Mkuu Ritz mzee wa kuchochea kuni wiki hii sijamuona kabisa au kaishiwa kuni tumsaidieee! Tunamsubili M/kiti uvccm naye alipuke na yule dogo kwa kulipuka lazima ccm iwe chaliii labda asiruhusiwe kutoa tamko!!! JK yy kesho lazima atoe tamko yaani ni mwendo wa matamko mpaka ccm ziwe 2 mwaka huu
wanamtamanisha shigongo!!hakawii kuanzisha gazeti la siasa!Haya mazingaombwe ni mpaka 2015!
Magazeti yatauza sana safari hii
Hivi Zitto alichanga ngapi au yeye alichanga Chauma.?
Ningemshangaa sana kama angekaa kimya kwa kudhalilishwa hivi.Ningemuona muoga.
Bado Joseph Msukuma wa Geita na Jesca wa Iringa
Hivi Mary Chatanda bado tu ?
Halafu wanawake wa CCM ni waoga.Vijana na wazee wameonyesha kusimama kidete kwenye hili swala.Nawashangaa akina Shelukindo wapo kimya.Hivi Anna Kilango ni coward kiasi hiki?
krs one-raising to the top,cdm is raising