Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Rais Samia Suluhu Hassan amesema kuwa mwanzoni mwa mwaka 2026 Serikali imejipanga kujenga umoja wa kitaifa ambapo mchakato wa kuunda Tume ya Maridhiano tayari umeanza na Serikali itashirikiana na wadau wote ili kukubaliana muundo wa Tume hiyo.
Katika hotuba yake ya kuaga mwaka 2025 na kuukaribisha mwaka 2026 Ikulu Zanzibar, Samia amesema "Mwaka 2025 pamoja na mafanikio tuliyoyapata tulipitia pia changamoto na mitihani iliyotugusa sote tutakumbuka kuwa mwezi octoba mwaka huu tulipitia nyakati ngumu zilizohitaji subira mshikamano na uzalendo kwa dhati kabisa ninavishukuru Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama nchini na Wananchi wote kwa ujumla kwa kuendelea kudumisha amani umoja na mshikamano wa taifa letu."
“Tumeweza kuuthibitishia ulimwengu kwamba Tanzania ni taifa imara, himilivu na lenye kujitahidi kushughulikia changamoto zake. Tunapouanza mwaka 2026 Serikali imejipanga kujenga umoja wa kitaifa nchini hatua za kuunda Tume ya Maridhiano zimeanza kuchukuliwa, Serikali itashirikiana na wadau wote katika kukubaliana kuhusu muundo wa tume aina ya wajumbe, majukumu yao na muda wa kazi wa tume hiyo"
Katika hotuba yake ya kuaga mwaka 2025 na kuukaribisha mwaka 2026 Ikulu Zanzibar, Samia amesema "Mwaka 2025 pamoja na mafanikio tuliyoyapata tulipitia pia changamoto na mitihani iliyotugusa sote tutakumbuka kuwa mwezi octoba mwaka huu tulipitia nyakati ngumu zilizohitaji subira mshikamano na uzalendo kwa dhati kabisa ninavishukuru Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama nchini na Wananchi wote kwa ujumla kwa kuendelea kudumisha amani umoja na mshikamano wa taifa letu."
“Tumeweza kuuthibitishia ulimwengu kwamba Tanzania ni taifa imara, himilivu na lenye kujitahidi kushughulikia changamoto zake. Tunapouanza mwaka 2026 Serikali imejipanga kujenga umoja wa kitaifa nchini hatua za kuunda Tume ya Maridhiano zimeanza kuchukuliwa, Serikali itashirikiana na wadau wote katika kukubaliana kuhusu muundo wa tume aina ya wajumbe, majukumu yao na muda wa kazi wa tume hiyo"