Samia: Anakuja anakataa, Anaingia anatoka

Samia: Anakuja anakataa, Anaingia anatoka

Beberu

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2017
Posts
4,706
Reaction score
10,229
Nikitazama utendaji kazi na mipango ya SSH naona napata mawenge 😂😂😂 ni kama anakuja kisha anakataa, kama anafunga kisha anapaisha, kama anatoa pasi ila ghafla unamuona kwenye kibendera akishangilia ameshafunga goli,

SSH ni Pro capitalist ambae inabaki kidogo aangukie kwenye Ubeberu, anaweka kila kitu kwa msingi wa Ubepari, anapambana kuboost performance ya serikali, ana outsource vitu, anajitahidi katika angle hii
✓ Anavutia wawekezaji
✓ Anajitahidi kuboresha maisha ya wafanyakazi (japo sio sana)
Anajitahidi kwenye miundombinu, shule na hospital anazipa mpunga mrefu na anajenga shule nyingi kweli
✓ Barabara tunaona mikataba imesainiwa ya km 2000+
✓ Katika yote ananifurahisha sio mtu wa media sana

Na mengine mengi, mpaka hapo naona SSH kama anakuja hiv
Ila ghafla bin Vuu unaona SSH
✓ Anashindwa kuwa mkali kwa wafanyakazi wake
✓ Ana entertain mno mamichezo, anajihusisha mno na Simba na Yanga
✓ Ana ukimya sana kwenye critical issues, hadi leo hajaongelea swala la Bandari, daima utamuona kimya tu, hafanyi Chochote ( kwenye macho yangu)

Ko mpaka hapo najikuta namkataa tena SSH, naishia kusema kama anakuja kama anakataa 😂
Ninyi wenzangu mnaonaje 🤔

Mimi wenu bepari niliekomaa, (BEBERU)
 
Anapoamua kuwa mkimya kwenye critical issues, kama suala la bandari, hapo maana yake ameamua kufumbia macho udhalimu tuliofanyiwa wabara, na anaufumbia macho sio kwa bahati mbaya, ni kwa makusudi kwasababu anajua maumivu yetu wabara kwenye issue ya bandari, ni furaha kwa wajomba zake wa Dubai.

Kutokana na hilo, kwangu sioni sababu ya kusema kama anakuja halafu anakataa, huyu kwangu ni haji, hasogei, wala hanikaribii kabisa, kitendo chake cha kuonekana kulifumbia macho suala la bandari kunaonesha wazi hana nia njema kwetu anaotuongoza, yupo pale kwa manufaa ya ndugu zake pekee.
 
Anapoamua kuwa mkimya kwenye critical issues, kama suala la bandari, hapo maana yake ameamua kufumbia macho udhalimu tuliofanyiwa wabara, na anaufumbia macho sio kwa bahati mbaya, ni kwa makusudi kwasababu anajua maumivu yetu wabara kwenye issue ya bandari, ni furaha kwa wajomba zake wa Dubai.

Kutokana na hilo, kwangu sioni sababu ya kusema kama anakuja halafu anakataa, huyu kwangu ni haji, hasogei, wala hanikaribii kabisa, kitendo chake cha kuonekana kulifumbia macho suala la bandari kunaonesha wazi hana nia njema kwetu anaotuongoza, yupo pale kwa manufaa ya ndugu zake pekee.
Suala la bandari mimi simuhukumu kwanza mpaka nisikie anasemaje yeye,
 
Suala la bandari mimi simuhukumu kwanza mpaka nisikie anasemaje yeye,
Kama mpaka leo ameshindwa kusema chochote kuendelea kumsubiri bubu aongee ni kujipotezea muda, bora ukafanye mambo mengine, wajomba wameshapewa bandari yetu.
 
Back
Top Bottom