Mauaji katika Fungate (je ni kweli Shrien Dewan alipanga mauaji ya mke wake?)

mtafuta-maisha

JF-Expert Member
Nov 5, 2016
1,982
2,915
Mauaji katika Fungate (je ni kweli Shrien Dewan alipanga mauaji ya mke wake?)

anne and  shren.jpg anne and  shren.jpg


Tarehe 13, mwezi wa 11 mwaka 2010, wanandoa wawili wakiwa safari ya kula fungate Afrika ya Kusini baada ya ndoa yao ya kifahari iliyofungwa huko Mumbai India. Wakiwa kwenye tax, wakipita kwenye kitongoji kidogo kijulikanacho kama Gugulethu, kilichopo karibu na Cape Town, mara tax yao inavamiwa na na watu wawili wenye silaha, wanaiteka na kumwamuru dereva ateremke na kasha mmoja wao anaendesha tax kuelekea kitongoji kijulkanacho kama Harare. Huko mwanaume anaamuriwa ateremke na kumwacha mkewe ambapo watekaji wanaondoka naye.

Kesho yake mwili wa mwanadada unakutwa kwenye hiyo tax, ikiwa imeterekezwa, ambapo mwili wake ulikuuwa kwenye viti vya nyuma ukiwa na jeraha la risasi shingoni.

Msako mkali unaanzishwa kwa lengo la kuwapata wahusika wa mauaji hayo, waweze kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Upepelezi unapoendelea, polisi wa Afrika ya Kusini wanadai ya kwamba mpango wote wa kuuawa kwa mwanamama, umesukwa kwa umakini na mumewe hivyo mume anageuka kuwa ndiye mpangaji ya mauaji ya mkewe.

Historia fupi wanandoa


Shrien Dewan aliyekuwa na miaka 30 kipindi hicho, ni mfanyabiashara tajiri raia wa Uingereza mwenye chimbuko la India. Amezaliwa tarehe 29, mwezi wa 12, mwaka 1979 (age 38) huko Bristol Uingereza.

Shrien Dewan anamiliki kampuni mbalimbali huko Uingereza ikiwemo kampuni kubwa ya PSP Holdings Ltd.

Anni Ninna Dewani (Hindocha) alizaliwa tarehe; 12 Mwezi wa 3 mwaka 1982, huko Uswiss.

Familia yao yenye chimbuko la kihindi ilihamia Uswiss kutoka Uganda kipindi ambapo aliyekuwa raisi wa Uganda Idd Amin, alipowataka raia wa Kihindi kuondoka nchini humo.

Mwaka 2009, akiwa huko London uingereza alikuana na Shrien Dewan, na wakajikuta wako penzini, na aliporudi kwao Uswiss waliendelea na penzi lao wakiwa mbali mbali na walidumu katika hali hiyo kwa miezi 18, kabla ya Anni Dewan kuamua kuhamia Uingereza mwezi wa tatu mwaka 2010, kumfuata mchumba wake. Mwezi wa tano wakavalishana pete ya uchumba na tarehe 29 mwezi wa 10 mwaka 2010, walifunga ndoa huko Mumbai India.

Lakini kwa ushahidi uliopo unaonyesha katika kipindi walichovalishana pete ya uchumba, Anni alianza kuona kuwa yeye na Shrien hawaendani kwakuwa Shrien alikuwa ni mtu mwenye wivu sana na anayetaka kumtawala kwa kila namna.

Walikuwa hawaishi kugombana kulikuwa kuna mabishano na ugomvi wa mara kwa mara katika kipindi hico cha uchumba wao.

Hata baada ya ndoa inadaiwa Anni alitaka kuomba taraka siku ya tatu tu, akidai kwamba hampendi Shrien, anamchukia na anaona hawaendani maana Shrien ni mtu anayetaka mambo yake yaenda sawa kwa asilimia mia (perfectionist), wakati yeye Anni amezoea kuishi maisha ya kawaida tu.

Kuna ushahidi wa ujumbve mfupi wa simu ambao Anni alimtumia binamu yake akimuelezea kuhusu kumchukia Shrien na kuwa anajuta ni kwanini alikubari kuolewa naye.

Baada ya ndoa waliamua kuelekea kwenye fungate Afrika ya Kusini, huku wakiwa na mpango wa kuandaa tafrija kwa ajili ya ndugu na marafiki wao walioko huko Uingereza ambao hawakuweza kuhudhuria ndoa yao huko India, pindi tu watakapo rejea kutoka katika fungate lao.
Fungate

Tarehe 9, mwezi wa 11 mwaka 2010, baada ya ndoa yao huko Mumbai India. Wanadoa hao Shrien Dewan na Anni Dewan walisafiri kuelekea Afrika ya Kusini kula fungate. Walifika na kukaa siku nne katika hotel ya kifahari ya nyota tano ijulikanayo kama Chitwa Chitwa Game lodge iliyoko katika hifadhi ijulikanayo kama Kruger.


Tarehe 10, mwezi wa 11, mwaka 2010, baada ya kufika Afrika ya Kusini, Anni alimtumia tena ujumbe mfupi binadamu yake akimwambia kwamba anajaribu kuendana na Shrien kwa maana Shrien anajitahidi kumfurahisha na ni kijana mzuri tu.

Na kesho yake yani tarehe 11, alimtumia ujumbe mwingine binamu yake akidai kwamba, Shrien anazidi kuwa bora kuliko awali na akaongezaa kuwa ni ngumu kueleza hiyo hali ila atampigia simu atakaporejea Uingereza, akamalizia kwa kusema anachukua kusikia neon taraka kwa muda huo,

Hii inaonyesha kuwa fungate na ndoa yao ilikuwa inaenda vizuri na ule msuguano ulionekana awali ulikuwa unaanza kupotea na kugeuka ndoa yenye amani na furaha kwa wanandoa wapya.

Tarehe 12, mwezi wa 11, waliondoka kwa usafiri wa ndege kuelekea Capetown kwa ajili ya kuendelea kula raha na kufaidi fungate lao.

Hapo ndipo matukio mpaka kifo cha Anni dewan yanaanza.

Saa 30 kabla ya kuawa Anni dewan

Baada ya kuwasiri katika kiwanja cha ndege cha Cape Town, walitoka nje ya uwanja na kutafuta tax. Kati ya tax zilizokuwa uwanjani hapo kulikuwa na tax ya kijana ajulikanaye kama Zola Robert Tongo.

Akiwa na umri wa miaka 30 kwa kipindi hico, alikuwa amewahi kukamatwa na kosa moja tu lilimfikisha polisi na kosa hilo lilikuwa kuendesha gari pasipokuwa na leseni ya udereva.

Kwa maelezo ya Tongo anadai Dewan aliwafuata, akawauliza kama anaweza kupata tax, huyu Tongo ndiye shahidi namba moja katika kesi ya mauji ya Anne Dewan. Tongo na wenzake waliongea na Dewan na ikaonekana kwamba Tongo alikuwa na bei ya chini hivyo Dewan alichukua tax ya Tongo.


Ilimchukua Tongo dakika 25, kuwatoa uwanja wa ndege mpaka kwenye hoteli ya Cape Grace. Walipofika wakati Anne alipoingia ndani ya hotel, Tongo anadai Dewan alirudi na kumwambia anahitaji kusaidiwa kuua mtu flani. Tongo anadai alimwambia kwamba yeye hajihusishi na shughuli hizo ila naweza kumpigia mtu anayemfahamu ambaye anaweza kumsaidia kupata mtu wa kufanya mauaji hayo.


Kamera za hoteli zinaonyesha Dewan akirudi ndani ya hoteli na kuangana na mkewe, kasha baada ya muda anatoka tena kwa mara nyingine kuongea na Tongo yani mara mbili ndani ya muda wa dakika tisa tu.

Lakini kwa maelezo ya dewan anadai ya kwamba yeye na Tongo walikuwa wanazungumzia mipango ya Tongo kuwazungusha sehemu mbalimbali za cape town kwa tax yake hapo baadae.

Tongo yeye anadai kwamba, dewan alimwambia kwamba yuko tayari kulipa Rand 15,000 kwa ajili ya shughui hiyo na atalipa kwa kutumia Dolla, na anadai dewan alimwambia mtu anayehitajika kuawa ni mwanamke na atafika kwa ndge jioni ya siku hiyo.

Maswali la kujiuliza hapa ni kwamba, ikiwa kweli Anni ndiye mtu ambaye Shrien alihitaji auawe, kwanini hakumwambia Tongo kuwa ni yeye ukizingatia ya kwamba alitaka mauaji hayo yafanyike usiku wa siku inayofuata.

Na swali lingine, ni kwamba inawezekanaje mtu mgeni, ndiyo kwa mara ya kwanza amefika Afrika ya Kusini, hajui mazingira hana wenyeji anawezaji kumwambia jambo zito kama hili mtu aliyekutana naye kwa mara ya kwanza ndani ya dakika 40?

Baada ya kuondoka hapo hotelini Tongo alielekea Protea Colosseum hoteli ambayo ni mwendo wa dakika 20, kutoka kwenye hoteli walikofikia wanandoa hao.

Akiwa njiani anaelekea kwenye hoteli hiyo, Tongo alipiga simu hapo kwa mhudumu wa mapokezi ajulikanaye kama Monde Mbolombo, na kwa maelezo ya polisi na ushahidi wa video na sauti baina ya mazungumzo kati ya Tongo na Monde ni kwamba Monde ndiye alikuwa mtu wa kati ya kiunganishi kati ya Tongo na muaji aliyempiga Anni Dewan risasi.


Lakini jambo la kustaajisbisha katika kesi hii, ni kwamba Monde alipewa kinga kabisa ya kutoshitakiwa ikiwa kama atashirikiana na polisi kwa kutoa ushahidi wa mipango yote na uhusika wake katika mpango wa mauaji ya Anni.

Hili ni jambo la kustaajibisha kwakuwa bila ushirika wake kama mtu kati akiwaunganisha muaji na Tongo, basi huenda Anni asingeuawa, lakini bado polisi ilimpatia kinga mtu huyu ya kutoshitakiwa.

Wakati Tongo akiwa njiani kuelekea Colosseum kukutana na Monde, kamera za ulinzi za hoteli ya Cape Grace zinamuonyesha, Dewan akitoka chumbani kwake na kuelekea nje ya hotel.

Pia kamera za ulinzi za Colosseum zinaonyesha Tongo alipowasili, Monde anaweka mikono kichwani kama akishangilia hivi kasha wanatoka nje.

Tongo anadai alimwambia Monde kuwa kuna mtu anahitaji auawe mwadada, na yuko tayari kiulipa kiasi cha Rand 15,000. Monde alimjibu ya kwamba anafahamiana na kijana mmoja hapo mjini ambaye anaweza tekereza mauaji hayo.

Kamera zinawaonyesha Monde na Tongo wanarudi ndani ya hoteli sehemu ya mapokezi na Monde anachukua simu na kuanza kutafuta namba kisha anampigia kijana mwenye umri wa miaka 25 ajulikanaye kama Mziwama Dodo Qwabe ambaye hana ajira.


Monde na Qwabe wanazungumza na Monde anamwambia kwamba kuna kazi ya kuua mtu, kwa malipo ya Rand 5,000. Qwabe anakubari kufanya hiyo kazi kwa hayo malipo.

Jambo la kushangaza zaidi katika hii kesi, polisi pia waliingia makubariano na Qwabe kama waliyoingia nayo kwa Monde wakimtaka atoe ushahidi dhidi uhusika wa Shrien Dewan katika mauaji hao kwa makubariano ya kupunguza kifungo chake kutoka miaka 15 mpaka miaka saba.

Monde anampatia Tongo namba ya Qwabe, na anamwambia kwamba atahiotaji malipo ya Rand 5,000 kwa kumuunganisha Tongo na muaji ambaye ni Qwabe.

Lakini katika utetezi wake Monde anakataa kuwa hakuhitaji pesa kutoka kwa Tongo, akidai kuwa kupokea pesa inayotokana na kumwaga damu ya mtu ni vibaya, hivyo yeye hakuwa tayari kupokea pesa ya damu bali tu alishiriki kumsaidia rafiki yake Tongo kwa kumpatia mtu wa kufanya kazi hiyo.

Baada ya Tongo kuondoka hapo hotelini, kamera za hoteli zinamuonyesha Monde akiwa mwenye furaha akicheka na kushangilia peke yake. Maswali ya kujiuliza ni je Monde alikuwa akifurahia mpango wa mauaji au alikuwa anafurahia jambo linguine tofauti ukizingatia kwamba Monde hakuwahi kuwa na matatizo yote au historia ya uhalifu, iweje jambo la mauaji limfurahishe mtu ambaye hana historia ya kufanya uhalifu?

Jambo la kushangaza, hawa wote wahusika wakuu waliingia makubariano na polisi wa Cape Town kutoshitakiwa au kupewa adhabu ndogo pale watakapo kubari kutoa ushahidi dhidi ya ushirika wa shrien Dewan katika mpango wa kumuua mkewe.

Je hii ilikuwa sawa, ukizingatia hawa walikuwa waalifu na walikuwa tayari kusema lolote na kufanya jambo lolote kuepuka mkono wa sheria baada ya kufanya mauaji hayo?

Na je kauli zao na ushahidi waliotoa ni wa kuaminika kiasi gani mpaka polisi wautumie kama ushahidi tosha wa kujenga kesi dhidi ya Shrien Dewan?

Muda huo huo ambapo Tongo aliondoka kutoka kwa rafiki yake Monde, kamera za hoteli ya Cape grace zinamuonyesha Shrien Dewan akiwa anarejea kutoka alipokuwa amekwenda, ambapo alikuwa ameenda kwenye duka la kubadirisha fedha na kubadiri pounds 800, akapewa Rands kasha alienda duka la maua na kumnunulia mkewe maua ya Rose mekundu anayoonekana akiwa ameyabeba wakati anaingia hotelini.

Dakika tano baada ya Shrien kuingia chumbani, Anni alipiga simu kwenda kwa wazazi wake na kuzungumza na baba yake..


Kwa maelezo ya baba yake anadai sauti ya Anni haikuwa sawa, alionekana ni mtu ambaye hakuwa sawa na allihisi kuna jambo haliko sawa. Lakini Anni alipoulizwa na baba yake kama yuko sawa alimwambia yuko sawa. Na hiyo ndiyo ilikuwa mara ya mwisho Anni kuzungumza na baba yake.

Ijumaa saa 12 na dakika 41

Tongo alikuwa karudi nyumbani kwake katoka kuonana na Qwabe,

Kwa maelezo ya Qwabe anadai kwamba Tongo walipoonanan alimwambia kuna mtu anataka asaidiwe kutekeleza mauaji, wakati wakizungumza mara Qwabe alipokea simu kutoka kwa rafiki yake aitwaye Kolile Mngeni, ambapo Qwabe aliamua kumshirikisha katika mpango huo kama msaidizi wake.


Kwa maqelezo ya Qwabe anadai kwamba yeye na Mngeni walizungumza kwa kina juu ya mauaji hayo, na Mngeni akamwambia yuko tayari kushiriki ikiwa dau litaongezeka mpaka kufikia Rand 15,000.

Huyu Mngeni tofauti na wenzake, ndiye pekee aliyekataa kuingia makubariano na polisi ya kupunguziwa adhabu kwa kutoa ushahidi unaoonyesha ushirika wa Shrien katika mpango wa mauaji ya Anni Dewan. Na ni Mngeni pekee ambaye maelezo yake hayamhusishi Shrien katika mpango wa kutekeleza mauaji hayo.

Ni Mngeni aliyekutwa na hatia ya kumuua Anni, na alipatikana na hatia hiyo kutokana na ushahidi aliotoa Qwabe juu yake akahukumiwa kifungo cha maisha. Na ajabu alifaariki akiwa gerezani.

Ijumaa saa 2 na dakika 13

Wakati hayo yakiendelea, kamera za hoeli ya Cape Grace zinawaonyesha wanandoa Bwana na Bibi dewan wakiwa wanatoka chumbani kwao, wakielekea kwenye bar ya hoteli hiyo, kisha baadae wanaenda kupata chakula kwenye mgahawa ulioko mwendo wa dakika chache kutoka hapo hotelini.

Kwa maelezo ya mhudumu aliyewahudumia siku hiyo, anawakumbuka na anadai kwamba amehudumu meza kadhaa za watu wanaokuwa kwenye fungate, ila siku hiyo ilikuwa tofauti kwa akina Dewan.

Anadai kwa kawaida watu wakiwa fungate uwa wanaonyesha mapenzi sana, wanashikana, wanabusiana wanatazamana wanassemezana na kuonyesha kila aina ya mahaba lakini anadai wao hawakuwa hivyo walikuwa kimya sana.

Pia anadai kuna wakati alienda kuhakikisha kama kuna kitu kingine wanachohitaji, lakini Shrien hakuwa mezani alikuwa aktoka nje ya mgahawa ni bi dewan tu aliyekuwa mezani peke yake na alimwambia mhudumu kuwa Shrien katoka nje kuzungumza na simu inayohusiana na mambo ya kibiashara.

Mhudumu anadai kuwa watu wengi pale mghahawani walikuwa wakitazama ile meza aliyokuwa kaka Anni wakimuonea huruma huku wakishangaa na kuongea juu ya mwanaume aliyemuacha Bibi yake mezani peke yake wakiwa kwenye fungate.

Ijumaa saa 3 na dakika 21

Kamera zilizo nje ya huo mgahawa zinamuonyesha Shrien akiwa anatembea kurudi hotelini, na kamera za hoteli sinamuonyesha akiingia chumbani kwake akatoka akuwa kashika simu yake mkononi, jambo linaloonyesha kuwa ni kweli alikuwa kafuata simu yake.

Na kutokana na kumbukumbu kutoka kwenye mtandao wa simu, Shrien alikuwa kuna ujumbe mfupi wa maneno kutoka kwa Tongo ambapo Shrien alimpigi Tongo na kuzungumza naye kwa dakiaka 5 na sekunde 26,

Ukitazama kwa umakini utagundua hakuna ushahidi wowote ambao unamhusisha Dewan katika mpango wa mauaji moja kwa moja, ila kitu ambacho kinatia shaka ni mpangilio wa simu nbaina yake na Tongo pamoja jinsi walivyokuwa akitoka na kuzungumza naye wakati akiwa hotelini.

Kwa maelezo ya Tongo anadai kwenye simu walizungumza na akamtaarifu kuwa ameongea na rafiki yake ambaye amemuunga na kijana anayeweza fanya kazi hiyo ya mauaji na kasema atahitaji malipo ya Rand 15,000/

Ijumaa saa 5 na dakika 23

Kameera za hoteli zinawaonyesha Bwana na bibi Dewan wakiwa wanarejea kwenye chumba chao huku Shrien akiwa anaonekana mwenye furaha akitabasamu. Akiwa katangulia mbele na Anni akiwa nyuma, Shrien anageuka huku akicheka anaonyesha ishara ya kama namlenga kwa pistol Anni kwa kutumia vidole vya mikono yake yote miwili.


Anni haonyeshi furaha wala kushtushwa na kitendo hicho cha Shrien kumuonyesha ishara ya kama anamlenga kwa pistol. Wanaingia kwenye chumba chao.

Nini lilikuwa lengo la Shrien kumuua Anni, na je nini ambacho angefaidika nacho kutokana na kifo cha Anni kwa maana Anni hakuwa na Life Insurance hivyo Shrien asingeweza kupata pesa kutokana na kifo chake.

Polisi wa Afrika ya Kusini wao wana mawazo tofauti, wanadai Shrien alipanga mauaji hayo kutokana na tama zake za kingono,

Kutokana na maelezo aliyotoa Malaya wa kiume ajulikanaye kama Leopold Leisser, anadai kwamba Shrien alikuwa ni shoga na alikuwa akimlipa kwa ajili ya kufanya naye mapenzi. Leisser alidai kwamba Shrien alikuwa kafanya naye mapenzi mara tatu na mara ya mwisho ilikuwa na mwezi mmoja kabla ya ndoa yake.


Aliendelea kusema kuwa Shrien alidai Anni ni msichana mrembo, mzuri na anampenda ila asingependa kumuoa kutokana na sababu ya kuwa yeye Shrien ni shoga na anafurahia kitendo cha kuingiliwa zaidi kuliko kumwingilia mwanamke.

Laisser anadai ya kwamba Shrien alimwambia angependa kusitisha ndoa isifungwe ila anaogopa endapo atafanya hivyo, familia itamtenga hivyo inabidi ndoa ifungwe lakini atafute njia ya kuondoa tatizo hilo.

Kutokana na maelezo ya Laisser, polisi wanaamini ya kwamba Shrien alimaanisha njia ya kuondoa tatizo ilikuwa ni kumuondoa Anni katika maisha yake ili apate kuendelea kuishi maisha yake ya siri kama shoga.

Jumamosi ya tarehe 13, mwezi wa 11 mwaka 2010 ndani ya Jiji la cape Town

Hii ndiyo siku Anni alipouawa.

Kamera za hoteli zinawaonyesha Bwana na Bi Dewan wakiwa wanatoka chumbani kwao wakielekea kwenye mghahawa wa hoeli kupata kifungua kinywa.


Tongo anadai alizungumza na Shrien ambapo Shrien alimpigia simu saa 5 na dakika 30 asubuhi, na kumwambia amfuate na kumchukua hapo hotelini. Laini kutokana na kumbukumbu zilizochukuliwa kutoka kwenye mtandao wa simu zinaonyesha kuwa Tongo anadanganya hakukuwa na simu ya aina yoyote ambayo Shrien alimpigia Tongo muda huo.

Je kwanini tongo aseme uongo juu ya kupigiwa simu? Ikiwa ameza kudanganya juu ya hilo, je Tongo ni kwanini Tongo aaminike kwa mambo mengine aliyosema juu ya Shrien?

Jumamosi saa 5 na dakika 56

Nusu saa baada ya hiyo simu ya kusadika ambayo Tongo anadai alipigiwa na Shrien, Tongo anafaika kaiwa na Tax yake kuja kumchukua Shrien. Kamera za hoteli zinaonyesha gari ya Tongo ikiingia kwenye sehemu ya kuegesha magari ya hoteli na pia zinamuoneysha Shrien akitoka hotelini na kuingia kwenye tax ya Tongo kasha wanaondoka.

Kutokana na maelezo ya Tongo anadai kwamba, Shrien alimuomba mapeleke sehemu atakapoweza kubadirisha fedha, na Tongo aliamua kumpeleka sehemu ambako hiyo biashara inaendeshwa bila uhalali (Black Market).

Tongo aliampeleka kwenye duka linalojihusisha na kuuza vito vya thamani lijulikanalo kama The Golden touch Jewellers, lakini pia linafanya shughuli ya kubadiri pesa za kigeni bila vibari.

Wamiliki wa hilo duka wanadai Shrien alibadiri 15,000$ akapewa Rand 10,200. Kwa maelezo haya ukipiga hesabu kuwa alikuwa amekwishabadiri pound 900 ambazo zilikuwa sawa na rand 11,000 , ukajumuisha na Rand 10,200 za sasa jumla utapata Rand 21,000 ambazo ni zaidi ya kiasi kinachodaiwa na Tongo kuwa kilihitajika kutekeleza mauaji hayo.

Katika upepelezi wa mauaji ya kulipiwa, mzunguko wa pesa ya malipo uwa ni muhimu, lakini kwa polisi wa Afrika ya Kusini wameshindwa kuonyesha malipo hayo yalikofanyika na niwa wapi hiyo pesa ilipo kwa hao waliolipwa. Yani hakuna sehemu yoyote kwenye mafaili ya polisi pesa Rand 15,000 ya malipo inakoonyeshwa ililipwa na wahusika waligawanaje hiyo pesa na matumizi ya kila mmoja na kiasi kilichobaki ili kitumike kama ushahidi. Kwa kifupi ni kwamba hiyo pesa ilipotea tu hata hakuna sehemu wala ushahidi wa kuoneysha Shrien alimpatia Tongo au muaji pesa hiyo.

Kutokana na kumbukumbu za minara ya simu polisi waliweza kufuatilia ni wapi Shrien alielekea baada ya kubadiri pesa, na inaonyesha kuwa alirudi moja kwa moja Cape Grace hotel ambapo ni afari kama ya dakika 10 kutoka hapo alipobadirishia pesa.

Kwa maelezo ya Tongo anadai wakiwa katika safari ya kurudi hotelini, Shrien alianza kumueleza Tongo ni jinsi gani anataka mauaji hayo yatekelezwe. Anadai Shrien alimwambia kuwa anataka ionekane kama gari limevamiwa na majambazi halafu Tongo na Shrien watupwe nje ya gari kasha watekaji waondoke na gari pamoja na anayetakiwa kuuawa.

Haya maelezo ya Tongo yana ukakasi, kwakuwa inaonyesha kwamba Shrien na Tongo hawakuwa na muda wa kutosha kujadiri utekelezaji wa mauaji hayo kwa kina. Kama tulivyoona awali Anni alikuwa anadai moja ya kitu asichopenda kwa Shrien ni mtu anayependa mambo yake yaend kwa usawa kabisa (perfectionist), je mtu kama huyo anawezaje kupanga mauaji ndani ya dakika kumi apange mpango mzima utakavyotekelezwa bila kuhofia kutokea makosa?

Ni jambo la kushangaza kweli kuwa watu wawili wapange mpango mzima wa mauaji ndani ya dakika kumi bila kufanya makosa kutokana na kutokuwa na muda wa kutosha wa kuhakiki mpango mzima.

Tongo anaendelea kudai kwamba pia Shrien alimuahidi kuwa atamlipa kiasi cha Rand 5,000 badda ya kazi hiyo kutekelezwa. Na pia anadai aliikubari kuwa atamlipa kijana atakayefanya hiyo kazi Rand 15,000 taslimu.

Jambo la kushangaza ni kwamba, muajiri wake Tongo yani mmiliki wa hiyo tax anadai anashangaa kwanini Tongo alikubari kushiriki kwenye mpango huo wakati hiyo pesa aliyoahidiwa ilikuwa ni ndogo kulinganisha na mshahara wake wa kila mwezi ambao ulikuwa Rand 15,000-20,0000 mara tatu au nne zaidi ya ela ambayo Tongo anadai Shrien aliahidi kumpatia.

Tongo anadai kwamba walikubariana na Shrien kuwa aje kuwachukua saa 1 na dakika 30 jioni.

Jumamosi saa 8 na dakika 26

Baada ya Tongo kuondoka Cape Grace hoteli, alimpitia Monde, ambaye kama tulivyokwisha ona ndiye alikuwa kiunganishi kati ya Tongo na muaji Qwabe, Tongo alimpa msaada wa kumpeleka Monde kazini kwenye hoteli ya Colesseum.

Monde anadai wakiwa kwenye gari alimuuliza tena Tongo kwanini unahitaji mtu wa kutekel;eza mauaji, na Tongo alimjibu kuwa na mtu ndiye anahitaji mtu flani auawe.

Anasema mara simu ya tongo iliita na Tongo akasema kuwa huyu anayenipigia ndiye anayehitaji mauaji hayo yafanyike. Andai Tongo alipokea simu na Monde anadai alikuwa tu akisikia Tongo akijibu “Ndiyo niko njiana, niko njianai, ndiyo niko njiani, niko njiani.”. Anadai baada ya hapo aliweka simu chini na kusema “eeish, huyu jamaa haniamini”

Jambo la kushangaza kutokana na kumbukumbu za simu, inaonyesha hakuna rekodi yoyote kwenye mtandao wa simu inayoonyesha kuwa Shrien alipiga simu hiyo kwenda kwa Tongo. Hivyo kwa mantiki hiyo ni kwamba Monde alikuwa naongopa kuhusu simu hiyo.

Shrien Dewan kutokana na fedha aliyobadiri alikuwa na Rand 10,200 pamoja na pond 900. Je hii pesa yote alihitaji kwa ajilii ya shughuli gani kama siyo kuwalipa wauaji wa watakaotekeleza mauaji ya Anni?

Kwa amaelezo ya watu waliozungumza Dewan kabla, wanadai alikuwa anampango wa kumfanyia “Surprise” Anni kwa kuandaa safari ya kuzunguka mji kwa kutumia Helkopta siku inayofuata yani Jumapili. Hili polisi hawakulifuatilia kuhakiki kama ni kweli Shrien alitaka kufanya hivyo.
Jumamosi saa 8 na dakika 48

Kamera za hoteli ya Colesseum zinamuonyesha gari la Tongo likiingia kwenye eneo la kuegesha magari katika hoteli hiyo na Monde anateremka. Na pia kamera zinawaonyesha wafanyakazi wenzake Monde pale mapokeziwakiwa wanaongelea juu ya safari ya helkopta na malipo ya Rand 10,00 kwa ajili ya kuandaa safari hiyo ya mteja aliyempata Monde. Pia wahudumu wanazidi kuzungumza wakidai kuwa kuna mtu anataka kumfanyia Surprise mkewe huku wakidai ni ghali sana.

Colesseum Hotel anakofanya kazi Monde wana huduma hiyo ya kukodi helkopta kwa ajili ya safari au mizunguko, kwenye kumbukumbu za video za ulinzi wahudumu wamerekodiwa wakiwa wanazungumza na kusema kuwa atafanyiwa punguzo mpaka Rand 7,200 badala ya bei ya kawaida ya Rand 10,000 kwa safari ya saa moja..

Je hii ilikuwa bahati mbaya Monde kuzungumza juu ya Rand 15,000 za safari ya helkopta na kuom,ba apewe punguzo mpaka Rand 7,250 badala ya Rand 10,000.

Kamera bado zinamuonyesha Monde anaingia mapokezi akiwa kaambatana na Tongo, na anaoneka Monde akiwa anaendeleza mjadara wa safari ya helkopta wahudumu hao waliokuwa wakiizungumzia na wanamsifia kwamba Monde uwa anajua kukutana matajiri kweli na atapata faida kwenye safari hiyo maana kiasi kinachobaki atakichukua yeye.

Anaskika Monde akisema kuwa ndiyo nakutana na matajiri, ila huyu amekwishatapeliwa. Je hii kauli ya Monde inamzungumzia Shrien kama ndiye huyo tajiri? Na vipi juu yauli yake ya kuwa amekwishatapeliwa, je anazungumzia gharama za juu walizompa kuhusu kukodi helkopta kwamba ni Rand 15,000 kumbe ni Rand 10,000 tena hapo akiwa hajapewa punguzo?


Saa 8 na dakika 57

Baada ya dakika tano toka Tongo na Monde wafike pale hotelini, Tongo aliondoka kuelekea katikati ya mji kukutana na watekaji Qwabe na Mngeni wakiwa pamoja kwa mara ya kwanza.

Qwabe anadai walipokutana na Tongo aliwambia kuwa mhusika anataka mkewe auawe, na anataka ionekane kama ni utekaji wa gari kwa ajili ya unyanganyi katikati ya kitongoji cha mji wa Cape Town.

Jambo la kushangaza tena hakuna kumbukumbu yeyote kwenye mtandao wa simu inayoonyesha Tongo kumpigia dewan kumpa taarifa kuhusu kukutana na wauaji au hata kumtaarifu kuwa mpango ulikuwa tayari uko kwenye utekerezaji ksms eslivyopanga baada ya kukutana na Qwabe na Mngeni.

Je inaingia akilini kwa mtu ambaye alitazamwa na Anni, familia yake na familia ya Anni kwamba alikuwa ni mtu anayependa kutawala na anayetaka mambo yake yaende kwa uhakika bila makosa (perfectionist), angethubutu kufanya mpango wa mauaji pasipo kutaka kupata majibu ya mpango toka kwa Tongo?

Usiku wa mauaji ya Anni Dewan

Jumamosi saa 12 na dakika 17

kamera za hoteli zinawaonyesha wanadoa wakitoka kwenye chumba chao na kuelekea kwenye bar ya hoteli hiyo. Wanapigwa picha kadhaa kutoka kwa mpiga picha wa hapo hotelini kasha wanaonekana wakipigana mabusua mara kwa mara wakiwa wamekaa kwenye meza moja wapo hapo kwenye bar.

Saa 12 na dakika 35

Kamera za hoteli ya Colesseum zinamuonyesha Monde ambaye anadai yeye tu alikuwa mhusika wa kumuunga Tongo na Qwabe, ila mazungumzo yaliyonaswa na kamera yanaonyesha kuwa alikuwa anahusika zaidi ya kuwa mtu wa kati.

Kumbukumbu za simu zinaonyesha kwamba alikuwa akizungumza na Tongo, na mazungumzo yaliyonaswa na kamera za ulinzi yanaonyesha kwamnba yeye ndiye aliyekuwa mpangaji watukio zima litakavyofanyika, huku akimpa Tongo maelekezo mpaka ya jinsi gani malipo yatakavyogawanywa baina yao.

Kwa mazungumzo hayo inaonyesha Monde ndiye alikuwa kiongozi na mpangaji wa kila kitu lakini jambo la kustaajabisha ni kwamba mpaka leo yuko huru, alipewa kinga ya kutoshitakiwa na polisi kwa ajili ya kutoa ushaidi.

Katikia hoteli ya Cape Grace, ilifika saa 1 na nusu, Tongo akiwa hajafika kuwachukua akina Dewan kama ambavyo ilitakiwa, Shrien anaamua kumpigia Tongo inapofika saa 1 na dakika 45 kumuuliza yuko wapi kwanini kachelewa kuwafuata.

Lakini tongo na wanasheria wake wao wanatoa maelezo tofauti juu ya hili, wanadai Shrien alimpigia Tongo akiwa kakasirika akimuuliza yuko wapi, na akidai lazima mauaji hayo yafanyike siku hiyo na kama hayatofanyika Shrien atamuua Tongo kwa kutotekeleza makubariano yao.

Lakini kamera za ulinzi hapo hotelini zinaonyesha kitu tofauti, zinamuonyesha Shrien wakati anazungumza na Tongo hakuwa anazungumza kwa hasira na alikuwa kaka na mkewwe pembeni huku akizungumza na Tongo. Tongo anadai Shrien alizungumza kuhusu mauaji ya mkewe na kumtishia kumuua tongo kama hayatatekelezwa, Je inawezekana vipi Shrien azungumze mambo hayo akiwa kaka pembeni ya mke wake?

Inapofika saa 2 na dakika 57, Tongo ndipo anawasili pale hotelini. Kama Shrien alikuwa ni kweli ana mpango kuwa mke wake auawe, basi hakuwa kionyesha dalili yoyote ya hilo jambo kutokana na video zilizonaswa na kamera za hapo hotelini.

Alionekana ni mtu mwenye furaha na ambaye alikuwa akipiga picha kila mara yeye na mkewe kabla ya kupanda tax ya Tongo na kuondoka hapo hotelini.

Tongo mwenyewe anaunga mkono kwamba hali ya furaha na kucheka waliokuwa nayo iliendela hata wakiwa kwenye gari, walikuwa wakiongea wakibusiana na kucheka sana.

Anadai ya kwamba Shrien alimpa maelekezo ya kuendesha tax kuzunguka mji kwakuwa walitaka kuona madhari ya mji unavyofanana usiku.

Kwa maelezo ya Tongo ni kwamba utekaji wa tax ilibidi ufanyike katika kitongoji cha Gugulethu, muda mfupi baada ya Tongo kuwachukua akina Dewan kutoka hotelini. Tongo anadai kwamba alipofika hapo watekaji hawakuwepo hilo eneo na Qwabe anadai kwamba walikuwa wameamua kauchana na utekelezaji wa tukio hilo.

Lakini jambo la kushangaza ni kwamba kutoka na kumbukumbu za simu inaonyesha kwamba simu na jumbe fupi za maneno kati ya Tongo, Monde na Qwabe muda wote wakati Tongo anawazungusha akina Dewan mawasiliano baina yao yalienmdelea.

Muda mchache baadae waliwasili katika mghahawa wa Strand Beach Resort, Tongo anadai Shrien alikuwa kakasirika sana.

Tongo anadai aliongoza nao kuelekea kwenye mgahawa na walipofika sehemu ya kuingilia ndani, Anni alitangulia kuingia Shrien hakuingia alimgeukia Tongo na kumwambia kwanini mpango haujatekerezwa? Anadai kwamba Shrien alimtshia kumuua kama akishindwa timiza mpango wao.

Lakini jambo la kustajabisha ni kiwamba, kamera za mgahawa huo zilizoko ndani zinazoonyesha eneo la kuingia ndani ya mghahawa huo, zinawaonyesha wote wakiingia kwa pamoja na ni Shrien aliyekuwa katangulia na wala siyo Anni . pia mhudumu aliyewapokea anakubarina na hilo kwamba waliingia wote na Shrien ndiye alikuwa katangulia.

Ajabu, inaonyesha kwamba Tongo anazidi kudanganya na inashangaza ni kwanini polisi walikubari kuamini ushaidi wa mtu kama Tongo ambaye maelezo yake yamejaa uongo zaidi ya mara moja.

Kutokana na muda video ya CCTV inaoonyesha, sekunde 8 tu baada ya Dewan na mkewe kupotea kwenye CCTV kwa kuelekea ndani kabisa ya mghahawa, kumbukumbu za simu zinaonyesha Tongo aloimpigia Monde.

Qwabe pia anadai Tongo alimpigia akimwambia ya kwamba anataka mpango wao uendelee na kazi ifanyike usiku huo huo. Pia Tongo alipigiwa simu na Shrien akimuuliza kama ameshawapanga watekaji kwa ajili ya kazi.

Ni kweli kumbukumbu za simu zinaonyesha Shrien alimpgia Tongo saa 3 na dakika 56 na walizungumza kwa sekunde 93.

Lakini maelezo ya Shrien anadai ya kwamba alimpigia kumwambia aje kuwafuata baada ya nusu saa na aliwakuta wakiwa nje ya mghahawa wakimsubiri.

Saa 4 na dakiak 40.

Tongo anadai wakiwa kwenye gari alimtumia ujumbe mfupi Shrien akimwambia kuwa asisahau kuhusu pesa ya malipo na anadai Shrien alimjibu kuwa pesa iko kwenye bahasha nyeupe kwenye pochi nyuma ya siti ya abiria ya mbele.

Japo ni kweli inaonyesha katika kumbukumbu za polisi kuwa ni kweli Tongo alimtumia ujumbe mfupi Shrien, lakini haionyeshi ni ujumbe gani aliandika na wala haionyeshi kama Shrien alijibu huo ujumbe.

Kwa hiyo utaona ushirika wa Shrien unatokana na ushahidi unaotolewa na hawa wauaji lakini hauna kitu chochote cha kuonyesha kuunga mkono ushahidi wanaotoa. Hakuna sehemu inayoonyesha ni nini kilikuwa kwenye ujumbe wa maneno wala hakuna namna ambayo mazungumzo ya simu baina yao yalikuwa yamerekodiwa ila tu maelezo ya Tongo ndiyo polisi walikuwa wanayaamini, maana kwa teknolojia ya mtandao wa simu kipindi cha mwaka 2010, Afrika Kusini ilikuwa haiwezekani kuona ujumbe uliotumwa wala nini kiliongelewa kwenye simu. Ila tu ilikuwa inaonyesha simu ilipigwa muda flani kwenda namba flani na ujumbe ulitumwa muda flani kwenda namba flani.

Tongo aliendesha tax kueleke akatikati ya kitongoji cha Gugulethu, akiwapeleka kwenye mikono ya watekaji Qwabe na Mngeni.


Tongo anadai alipofika eneo ambalo walikuwa wamepanga kuwakuta watekaji alipunguza mwendo na mara ghafla watekaji walijitokeza wakiwa na bunduka na kuamuru asimame. Anadai waliamuru afungue milango akafungua .

Anadai Qwabe alishika usukani na ndiye akaanza kuendesha gari, huku Mngeni yeye alikaa nyuma akiwa kaelekeza bunduki kwa akina Dewan. Qwabe anadai alijifanya anaogopa lakini ukweli aliujua yeye akiwa kaka mbele siti ya abiria.

Shrien anadai mkewe alianza kulia yeye akawa kamkumbatia, ila anadai mkewe hakutaka kuwaachia pochi yake na pete yake ya uchumba na ndoa iliyokuwa na thamani ya Euro 25,000. Anadai yeye alikuwa akiwambia watekaji wachukue chochote wanachotaka waondoke wawaache tu.

Pia andai ya kwamba yeye aliwakabadhi pesa yote aliyokuwa nayo ambayo ilikuwa ni kiasi cha Rand 400, nah ii inathibitishwa na ushahidi wa Mngeni ambaye yeye ndiye alikataa kuingia makubariano na polisi ya kutoa ushaidi juu ya ushiriki wa Shrien.

Ukitazama video iliyorekodiwa wakati akifanya mahojiano na polisi kabla ya Shrien kuwa mtuhumiwa wa kushiriki mauaji ya mke wake, Mngeni anasikika akisema kuwa Shrien alitoa pesa yote aliyokuwa nayo kaisi cha Rand 400, akasema tafahdali msimuue wala msiniue chukua chochote mnachotaka. Anadai kuwa yeye alimjibu kuwa hapana hamtouawa.

Walipofika sehemu, walisimamisha tax na kumtoa Tongo nje ya tax na aliwaelekeza pesa ilipo kasha wakamwacha hapo na kuendelea kuzunguka nagari wakiwa wamewashikiria mateka Shrien na mke wake.

Waliendesha gari mpka kwenye kitongoji cha Kariche na Shrien anadai waliwaambia kuwa hawatowadhuru wao wanachohitaji ni gari yeye wakamwambia ateremke hapo na kumwambia mkewe atateremshwa mbeleni wakidai kuwa hawataki wateremke pamoja wanataka kila mmoja wamuache eeneo tofauti na mwenzake.

Lakini Shrien anadai kuwa alikataa akawambia kuwa Yule ni mkewe naomba wawaache waondoke wakiwa pamoja.

Qwabe anaamfokea Shrien na kumwamuru kuwa atoke kwenye gari akisema toka, toka , toka.

Haya maelezo bado yanaungwa mkono na maelezo ya Mngeni ambaye alikataa kuingia makubariano na polisi. Anadai kuwa Qwabe alidai kuwa hakuna atakayeumizwa ni kwamba tu anamshusha Shrien eneo moja na mkewe naenda kumshusha mbeleni wao wanaondoka na gari. Pia anaunga mkono kuwa Shrien aligoma kuteremka akidai kwamba hawezi kumuacha mkewe.

Kumbuka Shrien na Mngeni hawakuwahi zungumza wala kuonana kabla na maelezo ya Mngeni yalitolewa kabla hata Shrien hajawa mmoja kati ya watuhumiwa katika upangaji wa mauaji hayo, lakini maelezo yao bado yanaendana.

Je inawezekana vipi Shrien akatae kuteremka atake ateremke na mkewe kama kweli alikuwa kapanga mauaji ya mkewe?

Shrien anateremka na kuachwa katikati ya kitongoji ambacho na maarufu kwa uahalifu wa kutumia bunduki, kwa amelezo yake anadai baada tu ya yeye kuteremka gari liliondolewa kwa kasi ya ajabu.

Kwa bahati nzuri anakutana na na mkazi wa eneo hilo ambaye ni mhasibu ajulikanaye kama Simbonile Natakazi ambaye anamuona Shrien akipiga kelele kama kicha analia na kukimbia ovyo.

Simbonile anadai alimpigia binamu yake simu ambaye ni askari polisi, anadai pia Shrien alikuwa hakai na alikuwa anapandwa hasira kwakuwa iliwachukua muda mrefu mpaka polisi kufika pale.

Simbonile anaendelea kusema siku zambele baada ya kusikia kuwa Shrien anatuhumiwa kwa kushiriki mauaji ya kupanga dhiodi ya mkewe, alishangaa kwa kuwa haamini kama kweli Shrien alishiriki katika mauaji ya mkewe kwa jinsi alivyokuwa kachanganyikiwa sana siku ile.

Saa 7 usiku

Baada ya kumtafuta Anni Dewan na utafutaji kutozaa matunda, polisi waliamua kumrudisha hotelini Cape Grace. Kamera za hoteli zinamnasa Shrien akiwa anapita peke yake kwenye korido ya hoteli akilia akiwa kama mwendawazimui, anaingia chumbani kwake na kutoka kila mara akiwa analia kama kapagawa na kuwafuata akiwafokea polisi waliokuwa kwenye chumba cha internet cha hoteli hiyo akiwauliza kwanini hawafanyi juhudi za kumtafuta mkewe bado wamekaa tu hapo.

Jambo la kushangaza Tongo naye alikuwa pale pale hotelini, na anadai alimsikia Shrien akiwa anawambia polisi kanini hawamtafuti mkewe na anadai ndipo kwa mara ya kwanza aligundua kumbe Shrien na Anni walikuwa wanandoa na kumbe Shrien alikuwa anataka mkewe ndiye auawe.

Inashangaza kuwa Tongo anadai kuwa hakujua kama Shrien na Anni walikuwa wanandoa japokuwa ni yeye aliyewatoa uwanja wa ndege, nay eye alikuwa akiwaendesha kwa tax yake muda wote. Ajabu kweli..

Mngeni anadai baada ya kumteremsha Shrien waliendela kuzunguka huku Anni akilia sana nyuma ya gari, anadai kuwa Qwabe alitaka kumnyanganya Anni pochi ambapo Anni ailing’ang’ania ndipo Qwabe aliegesha gari pembeni akateremka na kwenda mpaka kwenye dirisha la mlango wa nyuma akampiga risasi ya shingoni bahati mbaya wakati bato wakigombea ile pochi. Hivyo kwa maelezo ya Mngeni ni kwamba hawakuwa na lengo la kufanya mauaji ilikuwa tu wana lengo la kufanya wizi.

Anadai alimuuliza Qwabe kwanini umempiga risasi, Qwabe hakujibu.

Ila Qwabe anadai kwamba aliyempiga risasi Anni ni Mngeni na alimpiga akiwa amekaa siti ya mbele uoande wa abiria kama walivyokuwa wamekubarina mpango wa kumuua Anni ulikuwa umekamilika. Ila anadai wakati anampiga risasi yeye Qwabe ambaye ndiye alikuwa akiendesha gari hakutarajia maana hakumwambia wala kumpa ishara kuwa anamaliza kazi waliyotumwa.

Waliterekeza gari wakiwa wameuacha mwili wa Anni ukiwa umelala kwenye siti ya nyuma ya gari, wakaondoka na pochi ya Anni, simu zao, saa na bangiri za thamani pamoja na vito vingine vya thamani.

Polisi wanathamanisha kwamba vito walivyochukua vina thamani ya 8,600 pounds huku pete yake ya uchumba polisi waliikuta kaililia na pete yake ya ndoa yenye thamani ya Euro 25,000 akiwa kaificha kwenye mfuko wa kuifadhia vitu nyuma ya siti ya abiria ya mbele.

Swali la kujiuliza kama kweli hili lilikuwa tukio la mauaji lenye lengo lionekane kama wizi, kwanini hawakuchukua hizo pete maana zilikuwa na thamani mara sita zaidi ya vitu vingine walivyochukua.

Na kama kweli lengo ilikuwa ni tukio la mauaji, kwa maelezo ya Mngeni hawakuangalia kuhakikisha kama kweli Anni kafariki ila tu wao walichukua walichoweza wakaterekeza gari na kukimbia.

Polisi wa Afrika ya Kusini wanadai Ushahidi (Forensic evidence) unaonyesha kuwa kweli Anni alikuwa kaka siti ya nyuma akiwa ameegemea sit, na alipigwa risasi kutoka mbele upane wa abiria, huku aliyempiga akiwa kampiga kimakusudi mdomo wa bunduki ukiwa karibu ya shigo la Anne kati ya sentimita 5-10, hivyo wanadai kifo chake hakikuwa cha bahati mbaya.

Mtaalam wa Forensic Science, DR. Richard Shephered, alipitia ushaidi wote, nay eye anapingana na hoja ya polisi. Yeye anadai haiwezekani Anne apigwe risasi toka siti ya mbela ya abiria, pia anadai haiwezekani Anne awe kapigwa risasi makusudi kwakuwa mauaji ya makusudi mtu ulenga kichwani, au sehemu ya moyo kwakuwa ndizo sehemu amabzo mtu akipigwa muaji anakuwa na uhakika kuwa aliyempiga hawezi kupona na siyo shigoni.

Pia anadai kama kweli angekuwa amekaa kuegemea siti ya ngum, alipopigwa risasi kungekuwa na damu imeruka na kutapakaa sehemu alipokuwa kaegemea shingo lake kitu ambapo hakipo.

Yeye anadai Anni atakuwa alikuwa kaegemea mbele aidha kaegemea mapaja yake, akiunga mkono maelezo ya Mngeni kuwa Anni alikua akilia huku kakumbatia pochi yake amejikunja. Pia anadai au kama hakuwa kajikuja kwa kulalia mapaja yake basi alikuwa kaka kwenye kingo za siti yani hajaegemea nyuma bali kasogea sana mbele.

Inaendelea kwenye comment #10 na #17 na #35
 

Attachments

  • shren.jpg
    shren.jpg
    54.5 KB · Views: 152
  • anne.jpg
    anne.jpg
    19.4 KB · Views: 170
  • chitwa chitwa.jpg
    chitwa chitwa.jpg
    328.8 KB · Views: 138
  • tongo.jpg
    tongo.jpg
    36.3 KB · Views: 169
  • grace.jpg
    grace.jpg
    247.9 KB · Views: 146
  • protea.jpg
    protea.jpg
    10 KB · Views: 141
  • mbondo.jpg
    mbondo.jpg
    25.8 KB · Views: 157
  • qwabe.jpg
    qwabe.jpg
    30.6 KB · Views: 164
  • father.jpg
    father.jpg
    45 KB · Views: 148
  • mngeni.jpg
    mngeni.jpg
    5.6 KB · Views: 133
  • table.jpg
    table.jpg
    30.6 KB · Views: 143
  • gun sign.jpg
    gun sign.jpg
    80.2 KB · Views: 152
  • leopold-560650.jpg
    leopold-560650.jpg
    32.7 KB · Views: 145
  • bar breakfast.jpg
    bar breakfast.jpg
    37.9 KB · Views: 147
  • jewwelers.jpg
    jewwelers.jpg
    41.2 KB · Views: 140
  • mbondo cct v.jpg
    mbondo cct v.jpg
    31.9 KB · Views: 141
  • last day shren and anne.jpg
    last day shren and anne.jpg
    93.3 KB · Views: 155
  • guglethu.jpg
    guglethu.jpg
    246.8 KB · Views: 123
hii kesi ni ngumu.. ngoja umalizie sehemu ya pili labda nitapata mwanga nani namuhisi ni muhusika..
 
hapo conclusion ni 2 tuu
1=kweli shrien alhusika ila Kwa kua ni perfectionist wanashindwa kumpata na hatia
ushahidi pekee ambao ungeweza kumpata ni maongezi ya cm katiyake na dreva tax
either aliyachezea au aljua tuu kwa kipindi hicho SA haikua na uwezo wa kungamua maongezi yao (alkua ni tajiri na ametoka nchi ilooendelea so chochote knaezekana )

2= mfanyakazi wa hotel aliamua kugawa mchongo/kuwashawishi au nae alpewa mchongo na dereva wa kuwaibia ao Wanandoa ila bahat mbaya yakatokea mauwaji(kwa Maelezo hayo apo juu mi binafs nakubal risasi iltoka baat mbaya) dizain hawakujua waibe nini ni kama waliambiwa tuu hao ni matajiri pigeni kazi....

kwa hii namba2 yule dereva alkua anajua kiasi cha pesa alchochenchi c's ye ndo alkua anampeleka duka la fedha!! nauakika hawakujua abar za pete pia

myb walamua kubaki na dem maana alkua kashika mkoba so wakajua ela ipo


[HASHTAG]#hii[/HASHTAG] ya polisi na kukubaliana waalifu ipo sana kwa wenzetu na kosa walofanya polisi wa sa ni kua na assumption zao zilzopelekea kumhic 1kwa1 bwana shrien

sjui nmepatia? anyway malzia story kwanza!!
 
Malizia kwanza sehemu inayofuata.
kwani hadi hapo tunaona jamaa alichezesha game kwa akili sana
 
Mauaji katika Fungate (je ni kweli Shrien Dewan alipanga mauaji ya mke wake?)

View attachment 690951 View attachment 690951


Tarehe 13, mwezi wa 11 mwaka 2010, wanandoa wawili wakiwa safari ya kula fungate Afrika ya Kusini baada ya ndoa yao ya kifahari iliyofungwa huko Mumbai India. Wakiwa kwenye tax, wakipita kwenye kitongoji kidogo kijulikanacho kama Gugulethu, kilichopo karibu na Cape Town, mara tax yao inavamiwa na na watu wawili wenye silaha, wanaiteka na kumwamuru dereva ateremke na kasha mmoja wao anaendesha tax kuelekea kitongoji kijulkanacho kama Harare. Huko mwanaume anaamuriwa ateremke na kumwacha mkewe ambapo watekaji wanaondoka naye.

Kesho yake mwili wa mwanadada unakutwa kwenye hiyo tax, ikiwa imeterekezwa, ambapo mwili wake ulikuuwa kwenye viti vya nyuma ukiwa na jeraha la risasi shingoni.

Msako mkali unaanzishwa kwa lengo la kuwapata wahusika wa mauaji hayo, waweze kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Upepelezi unapoendelea, polisi wa Afrika ya Kusini wanadai ya kwamba mpango wote wa kuuawa kwa mwanamama, umesukwa kwa umakini na mumewe hivyo mume anageuka kuwa ndiye mpangaji ya mauaji ya mkewe.

Historia fupi wanandoa


Shrien Dewan aliyekuwa na miaka 30 kipindi hicho, ni mfanyabiashara tajiri raia wa Uingereza mwenye chimbuko la India. Amezaliwa tarehe 29, mwezi wa 12, mwaka 1979 (age 38) huko Bristol Uingereza.

Shrien Dewan anamiliki kampuni mbalimbali huko Uingereza ikiwemo kampuni kubwa ya PSP Holdings Ltd.

Anni Ninna Dewani (Hindocha) alizaliwa tarehe; 12 Mwezi wa 3 mwaka 1982, huko Uswiss.

Familia yao yenye chimbuko la kihindi ilihamia Uswiss kutoka Uganda kipindi ambapo aliyekuwa raisi wa Uganda Idd Amin, alipowataka raia wa Kihindi kuondoka nchini humo.

Mwaka 2009, akiwa huko London uingereza alikuana na Shrien Dewan, na wakajikuta wako penzini, na aliporudi kwao Uswiss waliendelea na penzi lao wakiwa mbali mbali na walidumu katika hali hiyo kwa miezi 18, kabla ya Anni Dewan kuamua kuhamia Uingereza mwezi wa tatu mwaka 2010, kumfuata mchumba wake. Mwezi wa tano wakavalishana pete ya uchumba na tarehe 29 mwezi wa 10 mwaka 2010, walifunga ndoa huko Mumbai India.

Lakini kwa ushahidi uliopo unaonyesha katika kipindi walichovalishana pete ya uchumba, Anni alianza kuona kuwa yeye na Shrien hawaendani kwakuwa Shrien alikuwa ni mtu mwenye wivu sana na anayetaka kumtawala kwa kila namna.

Walikuwa hawaishi kugombana kulikuwa kuna mabishano na ugomvi wa mara kwa mara katika kipindi hico cha uchumba wao.

Hata baada ya ndoa inadaiwa Anni alitaka kuomba taraka siku ya tatu tu, akidai kwamba hampendi Shrien, anamchukia na anaona hawaendani maana Shrien ni mtu anayetaka mambo yake yaenda sawa kwa asilimia mia (perfectionist), wakati yeye Anni amezoea kuishi maisha ya kawaida tu.

Kuna ushahidi wa ujumbve mfupi wa simu ambao Anni alimtumia binamu yake akimuelezea kuhusu kumchukia Shrien na kuwa anajuta ni kwanini alikubari kuolewa naye.

Baada ya ndoa waliamua kuelekea kwenye fungate Afrika ya Kusini, huku wakiwa na mpango wa kuandaa tafrija kwa ajili ya ndugu na marafiki wao walioko huko Uingereza ambao hawakuweza kuhudhuria ndoa yao huko India, pindi tu watakapo rejea kutoka katika fungate lao.
Fungate

Tarehe 9, mwezi wa 11 mwaka 2010, baada ya ndoa yao huko Mumbai India. Wanadoa hao Shrien Dewan na Anni Dewan walisafiri kuelekea Afrika ya Kusini kula fungate. Walifika na kukaa siku nne katika hotel ya kifahari ya nyota tano ijulikanayo kama Chitwa Chitwa Game lodge iliyoko katika hifadhi ijulikanayo kama Kruger.


Tarehe 10, mwezi wa 11, mwaka 2010, baada ya kufika Afrika ya Kusini, Anni alimtumia tena ujumbe mfupi binadamu yake akimwambia kwamba anajaribu kuendana na Shrien kwa maana Shrien anajitahidi kumfurahisha na ni kijana mzuri tu.

Na kesho yake yani tarehe 11, alimtumia ujumbe mwingine binamu yake akidai kwamba, Shrien anazidi kuwa bora kuliko awali na akaongezaa kuwa ni ngumu kueleza hiyo hali ila atampigia simu atakaporejea Uingereza, akamalizia kwa kusema anachukua kusikia neon taraka kwa muda huo,

Hii inaonyesha kuwa fungate na ndoa yao ilikuwa inaenda vizuri na ule msuguano ulionekana awali ulikuwa unaanza kupotea na kugeuka ndoa yenye amani na furaha kwa wanandoa wapya.

Tarehe 12, mwezi wa 11, waliondoka kwa usafiri wa ndege kuelekea Capetown kwa ajili ya kuendelea kula raha na kufaidi fungate lao.

Hapo ndipo matukio mpaka kifo cha Anni dewan yanaanza.

Saa 30 kabla ya kuawa Anni dewan

Baada ya kuwasiri katika kiwanja cha ndege cha Cape Town, walitoka nje ya uwanja na kutafuta tax. Kati ya tax zilizokuwa uwanjani hapo kulikuwa na tax ya kijana ajulikanaye kama Zola Robert Tongo.

Akiwa na umri wa miaka 30 kwa kipindi hico, alikuwa amewahi kukamatwa na kosa moja tu lilimfikisha polisi na kosa hilo lilikuwa kuendesha gari pasipokuwa na leseni ya udereva.

Kwa maelezo ya Tongo anadai Dewan aliwafuata, akawauliza kama anaweza kupata tax, huyu Tongo ndiye shahidi namba moja katika kesi ya mauji ya Anne Dewan. Tongo na wenzake waliongea na Dewan na ikaonekana kwamba Tongo alikuwa na bei ya chini hivyo Dewan alichukua tax ya Tongo.


Ilimchukua Tongo dakika 25, kuwatoa uwanja wa ndege mpaka kwenye hoteli ya Cape Grace. Walipofika wakati Anne alipoingia ndani ya hotel, Tongo anadai Dewan alirudi na kumwambia anahitaji kusaidiwa kuua mtu flani. Tongo anadai alimwambia kwamba yeye hajihusishi na shughuli hizo ila naweza kumpigia mtu anayemfahamu ambaye anaweza kumsaidia kupata mtu wa kufanya mauaji hayo.


Kamera za hoteli zinaonyesha Dewan akirudi ndani ya hoteli na kuangana na mkewe, kasha baada ya muda anatoka tena kwa mara nyingine kuongea na Tongo yani mara mbili ndani ya muda wa dakika tisa tu.

Lakini kwa maelezo ya dewan anadai ya kwamba yeye na Tongo walikuwa wanazungumzia mipango ya Tongo kuwazungusha sehemu mbalimbali za cape town kwa tax yake hapo baadae.

Tongo yeye anadai kwamba, dewan alimwambia kwamba yuko tayari kulipa Rand 15,000 kwa ajili ya shughui hiyo na atalipa kwa kutumia Dolla, na anadai dewan alimwambia mtu anayehitajika kuawa ni mwanamke na atafika kwa ndge jioni ya siku hiyo.

Maswali la kujiuliza hapa ni kwamba, ikiwa kweli Anni ndiye mtu ambaye Shrien alihitaji auawe, kwanini hakumwambia Tongo kuwa ni yeye ukizingatia ya kwamba alitaka mauaji hayo yafanyike usiku wa siku inayofuata.

Na swali lingine, ni kwamba inawezekanaje mtu mgeni, ndiyo kwa mara ya kwanza amefika Afrika ya Kusini, hajui mazingira hana wenyeji anawezaji kumwambia jambo zito kama hili mtu aliyekutana naye kwa mara ya kwanza ndani ya dakika 40?

Baada ya kuondoka hapo hotelini Tongo alielekea Protea Colosseum hoteli ambayo ni mwendo wa dakika 20, kutoka kwenye hoteli walikofikia wanandoa hao.

Akiwa njiani anaelekea kwenye hoteli hiyo, Tongo alipiga simu hapo kwa mhudumu wa mapokezi ajulikanaye kama Monde Mbolombo, na kwa maelezo ya polisi na ushahidi wa video na sauti baina ya mazungumzo kati ya Tongo na Monde ni kwamba Monde ndiye alikuwa mtu wa kati ya kiunganishi kati ya Tongo na muaji aliyempiga Anni Dewan risasi.


Lakini jambo la kustaajisbisha katika kesi hii, ni kwamba Monde alipewa kinga kabisa ya kutoshitakiwa ikiwa kama atashirikiana na polisi kwa kutoa ushahidi wa mipango yote na uhusika wake katika mpango wa mauaji ya Anni.

Hili ni jambo la kustaajibisha kwakuwa bila ushirika wake kama mtu kati akiwaunganisha muaji na Tongo, basi huenda Anni asingeuawa, lakini bado polisi ilimpatia kinga mtu huyu ya kutoshitakiwa.

Wakati Tongo akiwa njiani kuelekea Colosseum kukutana na Monde, kamera za ulinzi za hoteli ya Cape Grace zinamuonyesha, Dewan akitoka chumbani kwake na kuelekea nje ya hotel.

Pia kamera za ulinzi za Colosseum zinaonyesha Tongo alipowasili, Monde anaweka mikono kichwani kama akishangilia hivi kasha wanatoka nje.

Tongo anadai alimwambia Monde kuwa kuna mtu anahitaji auawe mwadada, na yuko tayari kiulipa kiasi cha Rand 15,000. Monde alimjibu ya kwamba anafahamiana na kijana mmoja hapo mjini ambaye anaweza tekereza mauaji hayo.

Kamera zinawaonyesha Monde na Tongo wanarudi ndani ya hoteli sehemu ya mapokezi na Monde anachukua simu na kuanza kutafuta namba kisha anampigia kijana mwenye umri wa miaka 25 ajulikanaye kama Mziwama Dodo Qwabe ambaye hana ajira.


Monde na Qwabe wanazungumza na Monde anamwambia kwamba kuna kazi ya kuua mtu, kwa malipo ya Rand 5,000. Qwabe anakubari kufanya hiyo kazi kwa hayo malipo.

Jambo la kushangaza zaidi katika hii kesi, polisi pia waliingia makubariano na Qwabe kama waliyoingia nayo kwa Monde wakimtaka atoe ushahidi dhidi uhusika wa Shrien Dewan katika mauaji hao kwa makubariano ya kupunguza kifungo chake kutoka miaka 15 mpaka miaka saba.

Monde anampatia Tongo namba ya Qwabe, na anamwambia kwamba atahiotaji malipo ya Rand 5,000 kwa kumuunganisha Tongo na muaji ambaye ni Qwabe.

Lakini katika utetezi wake Monde anakataa kuwa hakuhitaji pesa kutoka kwa Tongo, akidai kuwa kupokea pesa inayotokana na kumwaga damu ya mtu ni vibaya, hivyo yeye hakuwa tayari kupokea pesa ya damu bali tu alishiriki kumsaidia rafiki yake Tongo kwa kumpatia mtu wa kufanya kazi hiyo.

Baada ya Tongo kuondoka hapo hotelini, kamera za hoteli zinamuonyesha Monde akiwa mwenye furaha akicheka na kushangilia peke yake. Maswali ya kujiuliza ni je Monde alikuwa akifurahia mpango wa mauaji au alikuwa anafurahia jambo linguine tofauti ukizingatia kwamba Monde hakuwahi kuwa na matatizo yote au historia ya uhalifu, iweje jambo la mauaji limfurahishe mtu ambaye hana historia ya kufanya uhalifu?

Jambo la kushangaza, hawa wote wahusika wakuu waliingia makubariano na polisi wa Cape Town kutoshitakiwa au kupewa adhabu ndogo pale watakapo kubari kutoa ushahidi dhidi ya ushirika wa shrien Dewan katika mpango wa kumuua mkewe.

Je hii ilikuwa sawa, ukizingatia hawa walikuwa waalifu na walikuwa tayari kusema lolote na kufanya jambo lolote kuepuka mkono wa sheria baada ya kufanya mauaji hayo?

Na je kauli zao na ushahidi waliotoa ni wa kuaminika kiasi gani mpaka polisi wautumie kama ushahidi tosha wa kujenga kesi dhidi ya Shrien Dewan?

Muda huo huo ambapo Tongo aliondoka kutoka kwa rafiki yake Monde, kamera za hoteli ya Cape grace zinamuonyesha Shrien Dewan akiwa anarejea kutoka alipokuwa amekwenda, ambapo alikuwa ameenda kwenye duka la kubadirisha fedha na kubadiri pounds 800, akapewa Rands kasha alienda duka la maua na kumnunulia mkewe maua ya Rose mekundu anayoonekana akiwa ameyabeba wakati anaingia hotelini.

Dakika tano baada ya Shrien kuingia chumbani, Anni alipiga simu kwenda kwa wazazi wake na kuzungumza na baba yake..


Kwa maelezo ya baba yake anadai sauti ya Anni haikuwa sawa, alionekana ni mtu ambaye hakuwa sawa na allihisi kuna jambo haliko sawa. Lakini Anni alipoulizwa na baba yake kama yuko sawa alimwambia yuko sawa. Na hiyo ndiyo ilikuwa mara ya mwisho Anni kuzungumza na baba yake.

Ijumaa saa 12 na dakika 41

Tongo alikuwa karudi nyumbani kwake katoka kuonana na Qwabe,

Kwa maelezo ya Qwabe anadai kwamba Tongo walipoonanan alimwambia kuna mtu anataka asaidiwe kutekeleza mauaji, wakati wakizungumza mara Qwabe alipokea simu kutoka kwa rafiki yake aitwaye Kolile Mngeni, ambapo Qwabe aliamua kumshirikisha katika mpango huo kama msaidizi wake.


Kwa maqelezo ya Qwabe anadai kwamba yeye na Mngeni walizungumza kwa kina juu ya mauaji hayo, na Mngeni akamwambia yuko tayari kushiriki ikiwa dau litaongezeka mpaka kufikia Rand 15,000.

Huyu Mngeni tofauti na wenzake, ndiye pekee aliyekataa kuingia makubariano na polisi ya kupunguziwa adhabu kwa kutoa ushahidi unaoonyesha ushirika wa Shrien katika mpango wa mauaji ya Anni Dewan. Na ni Mngeni pekee ambaye maelezo yake hayamhusishi Shrien katika mpango wa kutekeleza mauaji hayo.

Ni Mngeni aliyekutwa na hatia ya kumuua Anni, na alipatikana na hatia hiyo kutokana na ushahidi aliotoa Qwabe juu yake akahukumiwa kifungo cha maisha. Na ajabu alifaariki akiwa gerezani.

Ijumaa saa 2 na dakika 13

Wakati hayo yakiendelea, kamera za hoeli ya Cape Grace zinawaonyesha wanandoa Bwana na Bibi dewan wakiwa wanatoka chumbani kwao, wakielekea kwenye bar ya hoteli hiyo, kisha baadae wanaenda kupata chakula kwenye mgahawa ulioko mwendo wa dakika chache kutoka hapo hotelini.

Kwa maelezo ya mhudumu aliyewahudumia siku hiyo, anawakumbuka na anadai kwamba amehudumu meza kadhaa za watu wanaokuwa kwenye fungate, ila siku hiyo ilikuwa tofauti kwa akina Dewan.

Anadai kwa kawaida watu wakiwa fungate uwa wanaonyesha mapenzi sana, wanashikana, wanabusiana wanatazamana wanassemezana na kuonyesha kila aina ya mahaba lakini anadai wao hawakuwa hivyo walikuwa kimya sana.

Pia anadai kuna wakati alienda kuhakikisha kama kuna kitu kingine wanachohitaji, lakini Shrien hakuwa mezani alikuwa aktoka nje ya mgahawa ni bi dewan tu aliyekuwa mezani peke yake na alimwambia mhudumu kuwa Shrien katoka nje kuzungumza na simu inayohusiana na mambo ya kibiashara.

Mhudumu anadai kuwa watu wengi pale mghahawani walikuwa wakitazama ile meza aliyokuwa kaka Anni wakimuonea huruma huku wakishangaa na kuongea juu ya mwanaume aliyemuacha Bibi yake mezani peke yake wakiwa kwenye fungate.

Ijumaa saa 3 na dakika 21

Kamera zilizo nje ya huo mgahawa zinamuonyesha Shrien akiwa anatembea kurudi hotelini, na kamera za hoteli sinamuonyesha akiingia chumbani kwake akatoka akuwa kashika simu yake mkononi, jambo linaloonyesha kuwa ni kweli alikuwa kafuata simu yake.

Na kutokana na kumbukumbu kutoka kwenye mtandao wa simu, Shrien alikuwa kuna ujumbe mfupi wa maneno kutoka kwa Tongo ambapo Shrien alimpigi Tongo na kuzungumza naye kwa dakiaka 5 na sekunde 26,

Ukitazama kwa umakini utagundua hakuna ushahidi wowote ambao unamhusisha Dewan katika mpango wa mauaji moja kwa moja, ila kitu ambacho kinatia shaka ni mpangilio wa simu nbaina yake na Tongo pamoja jinsi walivyokuwa akitoka na kuzungumza naye wakati akiwa hotelini.

Kwa maelezo ya Tongo anadai kwenye simu walizungumza na akamtaarifu kuwa ameongea na rafiki yake ambaye amemuunga na kijana anayeweza fanya kazi hiyo ya mauaji na kasema atahitaji malipo ya Rand 15,000/

Ijumaa saa 5 na dakika 23

Kameera za hoteli zinawaonyesha Bwana na bibi Dewan wakiwa wanarejea kwenye chumba chao huku Shrien akiwa anaonekana mwenye furaha akitabasamu. Akiwa katangulia mbele na Anni akiwa nyuma, Shrien anageuka huku akicheka anaonyesha ishara ya kama namlenga kwa pistol Anni kwa kutumia vidole vya mikono yake yote miwili.


Anni haonyeshi furaha wala kushtushwa na kitendo hicho cha Shrien kumuonyesha ishara ya kama anamlenga kwa pistol. Wanaingia kwenye chumba chao.

Nini lilikuwa lengo la Shrien kumuua Anni, na je nini ambacho angefaidika nacho kutokana na kifo cha Anni kwa maana Anni hakuwa na Life Insurance hivyo Shrien asingeweza kupata pesa kutokana na kifo chake.

Polisi wa Afrika ya Kusini wao wana mawazo tofauti, wanadai Shrien alipanga mauaji hayo kutokana na tama zake za kingono,

Kutokana na maelezo aliyotoa Malaya wa kiume ajulikanaye kama Leopold Leisser, anadai kwamba Shrien alikuwa ni shoga na alikuwa akimlipa kwa ajili ya kufanya naye mapenzi. Leisser alidai kwamba Shrien alikuwa kafanya naye mapenzi mara tatu na mara ya mwisho ilikuwa na mwezi mmoja kabla ya ndoa yake.


Aliendelea kusema kuwa Shrien alidai Anni ni msichana mrembo, mzuri na anampenda ila asingependa kumuoa kutokana na sababu ya kuwa yeye Shrien ni shoga na anafurahia kitendo cha kuingiliwa zaidi kuliko kumwingilia mwanamke.

Laisser anadai ya kwamba Shrien alimwambia angependa kusitisha ndoa isifungwe ila anaogopa endapo atafanya hivyo, familia itamtenga hivyo inabidi ndoa ifungwe lakini atafute njia ya kuondoa tatizo hilo.

Kutokana na maelezo ya Laisser, polisi wanaamini ya kwamba Shrien alimaanisha njia ya kuondoa tatizo ilikuwa ni kumuondoa Anni katika maisha yake ili apate kuendelea kuishi maisha yake ya siri kama shoga.

Jumamosi ya tarehe 13, mwezi wa 11 mwaka 2010 ndani ya Jiji la cape Town

Hii ndiyo siku Anni alipouawa.

Kamera za hoteli zinawaonyesha Bwana na Bi Dewan wakiwa wanatoka chumbani kwao wakielekea kwenye mghahawa wa hoeli kupata kifungua kinywa.


Tongo anadai alizungumza na Shrien ambapo Shrien alimpigia simu saa 5 na dakika 30 asubuhi, na kumwambia amfuate na kumchukua hapo hotelini. Laini kutokana na kumbukumbu zilizochukuliwa kutoka kwenye mtandao wa simu zinaonyesha kuwa Tongo anadanganya hakukuwa na simu ya aina yoyote ambayo Shrien alimpigia Tongo muda huo.

Je kwanini tongo aseme uongo juu ya kupigiwa simu? Ikiwa ameza kudanganya juu ya hilo, je Tongo ni kwanini Tongo aaminike kwa mambo mengine aliyosema juu ya Shrien?

Jumamosi saa 5 na dakika 56

Nusu saa baada ya hiyo simu ya kusadika ambayo Tongo anadai alipigiwa na Shrien, Tongo anafaika kaiwa na Tax yake kuja kumchukua Shrien. Kamera za hoteli zinaonyesha gari ya Tongo ikiingia kwenye sehemu ya kuegesha magari ya hoteli na pia zinamuoneysha Shrien akitoka hotelini na kuingia kwenye tax ya Tongo kasha wanaondoka.

Kutokana na maelezo ya Tongo anadai kwamba, Shrien alimuomba mapeleke sehemu atakapoweza kubadirisha fedha, na Tongo aliamua kumpeleka sehemu ambako hiyo biashara inaendeshwa bila uhalali (Black Market).

Tongo aliampeleka kwenye duka linalojihusisha na kuuza vito vya thamani lijulikanalo kama The Golden touch Jewellers, lakini pia linafanya shughuli ya kubadiri pesa za kigeni bila vibari.

Wamiliki wa hilo duka wanadai Shrien alibadiri 15,000$ akapewa Rand 10,200. Kwa maelezo haya ukipiga hesabu kuwa alikuwa amekwishabadiri pound 900 ambazo zilikuwa sawa na rand 11,000 , ukajumuisha na Rand 10,200 za sasa jumla utapata Rand 21,000 ambazo ni zaidi ya kiasi kinachodaiwa na Tongo kuwa kilihitajika kutekeleza mauaji hayo.

Katika upepelezi wa mauaji ya kulipiwa, mzunguko wa pesa ya malipo uwa ni muhimu, lakini kwa polisi wa Afrika ya Kusini wameshindwa kuonyesha malipo hayo yalikofanyika na niwa wapi hiyo pesa ilipo kwa hao waliolipwa. Yani hakuna sehemu yoyote kwenye mafaili ya polisi pesa Rand 15,000 ya malipo inakoonyeshwa ililipwa na wahusika waligawanaje hiyo pesa na matumizi ya kila mmoja na kiasi kilichobaki ili kitumike kama ushahidi. Kwa kifupi ni kwamba hiyo pesa ilipotea tu hata hakuna sehemu wala ushahidi wa kuoneysha Shrien alimpatia Tongo au muaji pesa hiyo.

Kutokana na kumbukumbu za minara ya simu polisi waliweza kufuatilia ni wapi Shrien alielekea baada ya kubadiri pesa, na inaonyesha kuwa alirudi moja kwa moja Cape Grace hotel ambapo ni afari kama ya dakika 10 kutoka hapo alipobadirishia pesa.

Kwa maelezo ya Tongo anadai wakiwa katika safari ya kurudi hotelini, Shrien alianza kumueleza Tongo ni jinsi gani anataka mauaji hayo yatekelezwe. Anadai Shrien alimwambia kuwa anataka ionekane kama gari limevamiwa na majambazi halafu Tongo na Shrien watupwe nje ya gari kasha watekaji waondoke na gari pamoja na anayetakiwa kuuawa.

Haya maelezo ya Tongo yana ukakasi, kwakuwa inaonyesha kwamba Shrien na Tongo hawakuwa na muda wa kutosha kujadiri utekelezaji wa mauaji hayo kwa kina. Kama tulivyoona awali Anni alikuwa anadai moja ya kitu asichopenda kwa Shrien ni mtu anayependa mambo yake yaend kwa usawa kabisa (perfectionist), je mtu kama huyo anawezaje kupanga mauaji ndani ya dakika kumi apange mpango mzima utakavyotekelezwa bila kuhofia kutokea makosa?

Ni jambo la kushangaza kweli kuwa watu wawili wapange mpango mzima wa mauaji ndani ya dakika kumi bila kufanya makosa kutokana na kutokuwa na muda wa kutosha wa kuhakiki mpango mzima.

Tongo anaendelea kudai kwamba pia Shrien alimuahidi kuwa atamlipa kiasi cha Rand 5,000 badda ya kazi hiyo kutekelezwa. Na pia anadai aliikubari kuwa atamlipa kijana atakayefanya hiyo kazi Rand 15,000 taslimu.

Jambo la kushangaza ni kwamba, muajiri wake Tongo yani mmiliki wa hiyo tax anadai anashangaa kwanini Tongo alikubari kushiriki kwenye mpango huo wakati hiyo pesa aliyoahidiwa ilikuwa ni ndogo kulinganisha na mshahara wake wa kila mwezi ambao ulikuwa Rand 15,000-20,0000 mara tatu au nne zaidi ya ela ambayo Tongo anadai Shrien aliahidi kumpatia.

Tongo anadai kwamba walikubariana na Shrien kuwa aje kuwachukua saa 1 na dakika 30 jioni.

Jumamosi saa 8 na dakika 26

Baada ya Tongo kuondoka Cape Grace hoteli, alimpitia Monde, ambaye kama tulivyokwisha ona ndiye alikuwa kiunganishi kati ya Tongo na muaji Qwabe, Tongo alimpa msaada wa kumpeleka Monde kazini kwenye hoteli ya Colesseum.

Monde anadai wakiwa kwenye gari alimuuliza tena Tongo kwanini unahitaji mtu wa kutekel;eza mauaji, na Tongo alimjibu kuwa na mtu ndiye anahitaji mtu flani auawe.

Anasema mara simu ya tongo iliita na Tongo akasema kuwa huyu anayenipigia ndiye anayehitaji mauaji hayo yafanyike. Andai Tongo alipokea simu na Monde anadai alikuwa tu akisikia Tongo akijibu “Ndiyo niko njiana, niko njianai, ndiyo niko njiani, niko njiani.”. Anadai baada ya hapo aliweka simu chini na kusema “eeish, huyu jamaa haniamini”

Jambo la kushangaza kutokana na kumbukumbu za simu, inaonyesha hakuna rekodi yoyote kwenye mtandao wa simu inayoonyesha kuwa Shrien alipiga simu hiyo kwenda kwa Tongo. Hivyo kwa mantiki hiyo ni kwamba Monde alikuwa naongopa kuhusu simu hiyo.

Shrien Dewan kutokana na fedha aliyobadiri alikuwa na Rand 10,200 pamoja na pond 900. Je hii pesa yote alihitaji kwa ajilii ya shughuli gani kama siyo kuwalipa wauaji wa watakaotekeleza mauaji ya Anni?

Kwa amaelezo ya watu waliozungumza Dewan kabla, wanadai alikuwa anampango wa kumfanyia “Surprise” Anni kwa kuandaa safari ya kuzunguka mji kwa kutumia Helkopta siku inayofuata yani Jumapili. Hili polisi hawakulifuatilia kuhakiki kama ni kweli Shrien alitaka kufanya hivyo.
Jumamosi saa 8 na dakika 48

Kamera za hoteli ya Colesseum zinamuonyesha gari la Tongo likiingia kwenye eneo la kuegesha magari katika hoteli hiyo na Monde anateremka. Na pia kamera zinawaonyesha wafanyakazi wenzake Monde pale mapokeziwakiwa wanaongelea juu ya safari ya helkopta na malipo ya Rand 10,00 kwa ajili ya kuandaa safari hiyo ya mteja aliyempata Monde. Pia wahudumu wanazidi kuzungumza wakidai kuwa kuna mtu anataka kumfanyia Surprise mkewe huku wakidai ni ghali sana.

Colesseum Hotel anakofanya kazi Monde wana huduma hiyo ya kukodi helkopta kwa ajili ya safari au mizunguko, kwenye kumbukumbu za video za ulinzi wahudumu wamerekodiwa wakiwa wanazungumza na kusema kuwa atafanyiwa punguzo mpaka Rand 7,200 badala ya bei ya kawaida ya Rand 10,000 kwa safari ya saa moja..

Je hii ilikuwa bahati mbaya Monde kuzungumza juu ya Rand 15,000 za safari ya helkopta na kuom,ba apewe punguzo mpaka Rand 7,250 badala ya Rand 10,000.

Kamera bado zinamuonyesha Monde anaingia mapokezi akiwa kaambatana na Tongo, na anaoneka Monde akiwa anaendeleza mjadara wa safari ya helkopta wahudumu hao waliokuwa wakiizungumzia na wanamsifia kwamba Monde uwa anajua kukutana matajiri kweli na atapata faida kwenye safari hiyo maana kiasi kinachobaki atakichukua yeye.

Anaskika Monde akisema kuwa ndiyo nakutana na matajiri, ila huyu amekwishatapeliwa. Je hii kauli ya Monde inamzungumzia Shrien kama ndiye huyo tajiri? Na vipi juu yauli yake ya kuwa amekwishatapeliwa, je anazungumzia gharama za juu walizompa kuhusu kukodi helkopta kwamba ni Rand 15,000 kumbe ni Rand 10,000 tena hapo akiwa hajapewa punguzo?


Saa 8 na dakika 57

Baada ya dakika tano toka Tongo na Monde wafike pale hotelini, Tongo aliondoka kuelekea katikati ya mji kukutana na watekaji Qwabe na Mngeni wakiwa pamoja kwa mara ya kwanza.

Qwabe anadai walipokutana na Tongo aliwambia kuwa mhusika anataka mkewe auawe, na anataka ionekane kama ni utekaji wa gari kwa ajili ya unyanganyi katikati ya kitongoji cha mji wa Cape Town.

Jambo la kushangaza tena hakuna kumbukumbu yeyote kwenye mtandao wa simu inayoonyesha Tongo kumpigia dewan kumpa taarifa kuhusu kukutana na wauaji au hata kumtaarifu kuwa mpango ulikuwa tayari uko kwenye utekerezaji ksms eslivyopanga baada ya kukutana na Qwabe na Mngeni.

Je inaingia akilini kwa mtu ambaye alitazamwa na Anni, familia yake na familia ya Anni kwamba alikuwa ni mtu anayependa kutawala na anayetaka mambo yake yaende kwa uhakika bila makosa (perfectionist), angethubutu kufanya mpango wa mauaji pasipo kutaka kupata majibu ya mpango toka kwa Tongo?

Usiku wa mauaji ya Anni Dewan

Jumamosi saa 12 na dakika 17

kamera za hoteli zinawaonyesha wanadoa wakitoka kwenye chumba chao na kuelekea kwenye bar ya hoteli hiyo. Wanapigwa picha kadhaa kutoka kwa mpiga picha wa hapo hotelini kasha wanaonekana wakipigana mabusua mara kwa mara wakiwa wamekaa kwenye meza moja wapo hapo kwenye bar.

Saa 12 na dakika 35

Kamera za hoteli ya Colesseum zinamuonyesha Monde ambaye anadai yeye tu alikuwa mhusika wa kumuunga Tongo na Qwabe, ila mazungumzo yaliyonaswa na kamera yanaonyesha kuwa alikuwa anahusika zaidi ya kuwa mtu wa kati.

Kumbukumbu za simu zinaonyesha kwamba alikuwa akizungumza na Tongo, na mazungumzo yaliyonaswa na kamera za ulinzi yanaonyesha kwamnba yeye ndiye aliyekuwa mpangaji watukio zima litakavyofanyika, huku akimpa Tongo maelekezo mpaka ya jinsi gani malipo yatakavyogawanywa baina yao.

Kwa mazungumzo hayo inaonyesha Monde ndiye alikuwa kiongozi na mpangaji wa kila kitu lakini jambo la kustaajabisha ni kwamba mpaka leo yuko huru, alipewa kinga ya kutoshitakiwa na polisi kwa ajili ya kutoa ushaidi.

Katikia hoteli ya Cape Grace, ilifika saa 1 na nusu, Tongo akiwa hajafika kuwachukua akina Dewan kama ambavyo ilitakiwa, Shrien anaamua kumpigia Tongo inapofika saa 1 na dakika 45 kumuuliza yuko wapi kwanini kachelewa kuwafuata.

Lakini tongo na wanasheria wake wao wanatoa maelezo tofauti juu ya hili, wanadai Shrien alimpigia Tongo akiwa kakasirika akimuuliza yuko wapi, na akidai lazima mauaji hayo yafanyike siku hiyo na kama hayatofanyika Shrien atamuua Tongo kwa kutotekeleza makubariano yao.

Lakini kamera za ulinzi hapo hotelini zinaonyesha kitu tofauti, zinamuonyesha Shrien wakati anazungumza na Tongo hakuwa anazungumza kwa hasira na alikuwa kaka na mkewwe pembeni huku akizungumza na Tongo. Tongo anadai Shrien alizungumza kuhusu mauaji ya mkewe na kumtishia kumuua tongo kama hayatatekelezwa, Je inawezekana vipi Shrien azungumze mambo hayo akiwa kaka pembeni ya mke wake?

Inapofika saa 2 na dakika 57, Tongo ndipo anawasili pale hotelini. Kama Shrien alikuwa ni kweli ana mpango kuwa mke wake auawe, basi hakuwa kionyesha dalili yoyote ya hilo jambo kutokana na video zilizonaswa na kamera za hapo hotelini.

Alionekana ni mtu mwenye furaha na ambaye alikuwa akipiga picha kila mara yeye na mkewe kabla ya kupanda tax ya Tongo na kuondoka hapo hotelini.

Tongo mwenyewe anaunga mkono kwamba hali ya furaha na kucheka waliokuwa nayo iliendela hata wakiwa kwenye gari, walikuwa wakiongea wakibusiana na kucheka sana.

Anadai ya kwamba Shrien alimpa maelekezo ya kuendesha tax kuzunguka mji kwakuwa walitaka kuona madhari ya mji unavyofanana usiku.

Kwa maelezo ya Tongo ni kwamba utekaji wa tax ilibidi ufanyike katika kitongoji cha Gugulethu, muda mfupi baada ya Tongo kuwachukua akina Dewan kutoka hotelini. Tongo anadai kwamba alipofika hapo watekaji hawakuwepo hilo eneo na Qwabe anadai kwamba walikuwa wameamua kauchana na utekelezaji wa tukio hilo.

Lakini jambo la kushangaza ni kwamba kutoka na kumbukumbu za simu inaonyesha kwamba simu na jumbe fupi za maneno kati ya Tongo, Monde na Qwabe muda wote wakati Tongo anawazungusha akina Dewan mawasiliano baina yao yalienmdelea.

Muda mchache baadae waliwasili katika mghahawa wa Strand Beach Resort, Tongo anadai Shrien alikuwa kakasirika sana.

Tongo anadai aliongoza nao kuelekea kwenye mgahawa na walipofika sehemu ya kuingilia ndani, Anni alitangulia kuingia Shrien hakuingia alimgeukia Tongo na kumwambia kwanini mpango haujatekerezwa? Anadai kwamba Shrien alimtshia kumuua kama akishindwa timiza mpango wao.

Lakini jambo la kustajabisha ni kiwamba, kamera za mgahawa huo zilizoko ndani zinazoonyesha eneo la kuingia ndani ya mghahawa huo, zinawaonyesha wote wakiingia kwa pamoja na ni Shrien aliyekuwa katangulia na wala siyo Anni . pia mhudumu aliyewapokea anakubarina na hilo kwamba waliingia wote na Shrien ndiye alikuwa katangulia.

Ajabu, inaonyesha kwamba Tongo anazidi kudanganya na inashangaza ni kwanini polisi walikubari kuamini ushaidi wa mtu kama Tongo ambaye maelezo yake yamejaa uongo zaidi ya mara moja.

Kutokana na muda video ya CCTV inaoonyesha, sekunde 8 tu baada ya Dewan na mkewe kupotea kwenye CCTV kwa kuelekea ndani kabisa ya mghahawa, kumbukumbu za simu zinaonyesha Tongo aloimpigia Monde.

Qwabe pia anadai Tongo alimpigia akimwambia ya kwamba anataka mpango wao uendelee na kazi ifanyike usiku huo huo. Pia Tongo alipigiwa simu na Shrien akimuuliza kama ameshawapanga watekaji kwa ajili ya kazi.

Ni kweli kumbukumbu za simu zinaonyesha Shrien alimpgia Tongo saa 3 na dakika 56 na walizungumza kwa sekunde 93.

Lakini maelezo ya Shrien anadai ya kwamba alimpigia kumwambia aje kuwafuata baada ya nusu saa na aliwakuta wakiwa nje ya mghahawa wakimsubiri.

Saa 4 na dakiak 40.

Tongo anadai wakiwa kwenye gari alimtumia ujumbe mfupi Shrien akimwambia kuwa asisahau kuhusu pesa ya malipo na anadai Shrien alimjibu kuwa pesa iko kwenye bahasha nyeupe kwenye pochi nyuma ya siti ya abiria ya mbele.

Japo ni kweli inaonyesha katika kumbukumbu za polisi kuwa ni kweli Tongo alimtumia ujumbe mfupi Shrien, lakini haionyeshi ni ujumbe gani aliandika na wala haionyeshi kama Shrien alijibu huo ujumbe.

Kwa hiyo utaona ushirika wa Shrien unatokana na ushahidi unaotolewa na hawa wauaji lakini hauna kitu chochote cha kuonyesha kuunga mkono ushahidi wanaotoa. Hakuna sehemu inayoonyesha ni nini kilikuwa kwenye ujumbe wa maneno wala hakuna namna ambayo mazungumzo ya simu baina yao yalikuwa yamerekodiwa ila tu maelezo ya Tongo ndiyo polisi walikuwa wanayaamini, maana kwa teknolojia ya mtandao wa simu kipindi cha mwaka 2010, Afrika Kusini ilikuwa haiwezekani kuona ujumbe uliotumwa wala nini kiliongelewa kwenye simu. Ila tu ilikuwa inaonyesha simu ilipigwa muda flani kwenda namba flani na ujumbe ulitumwa muda flani kwenda namba flani.

Tongo aliendesha tax kueleke akatikati ya kitongoji cha Gugulethu, akiwapeleka kwenye mikono ya watekaji Qwabe na Mngeni.


Tongo anadai alipofika eneo ambalo walikuwa wamepanga kuwakuta watekaji alipunguza mwendo na mara ghafla watekaji walijitokeza wakiwa na bunduka na kuamuru asimame. Anadai waliamuru afungue milango akafungua .

Anadai Qwabe alishika usukani na ndiye akaanza kuendesha gari, huku Mngeni yeye alikaa nyuma akiwa kaelekeza bunduki kwa akina Dewan. Qwabe anadai alijifanya anaogopa lakini ukweli aliujua yeye akiwa kaka mbele siti ya abiria.

Shrien anadai mkewe alianza kulia yeye akawa kamkumbatia, ila anadai mkewe hakutaka kuwaachia pochi yake na pete yake ya uchumba na ndoa iliyokuwa na thamani ya Euro 25,000. Anadai yeye alikuwa akiwambia watekaji wachukue chochote wanachotaka waondoke wawaache tu.

Pia andai ya kwamba yeye aliwakabadhi pesa yote aliyokuwa nayo ambayo ilikuwa ni kiasi cha Rand 400, nah ii inathibitishwa na ushahidi wa Mngeni ambaye yeye ndiye alikataa kuingia makubariano na polisi ya kutoa ushaidi juu ya ushiriki wa Shrien.

Ukitazama video iliyorekodiwa wakati akifanya mahojiano na polisi kabla ya Shrien kuwa mtuhumiwa wa kushiriki mauaji ya mke wake, Mngeni anasikika akisema kuwa Shrien alitoa pesa yote aliyokuwa nayo kaisi cha Rand 400, akasema tafahdali msimuue wala msiniue chukua chochote mnachotaka. Anadai kuwa yeye alimjibu kuwa hapana hamtouawa.

Walipofika sehemu, walisimamisha tax na kumtoa Tongo nje ya tax na aliwaelekeza pesa ilipo kasha wakamwacha hapo na kuendelea kuzunguka nagari wakiwa wamewashikiria mateka Shrien na mke wake.

Waliendesha gari mpka kwenye kitongoji cha Kariche na Shrien anadai waliwaambia kuwa hawatowadhuru wao wanachohitaji ni gari yeye wakamwambia ateremke hapo na kumwambia mkewe atateremshwa mbeleni wakidai kuwa hawataki wateremke pamoja wanataka kila mmoja wamuache eeneo tofauti na mwenzake.

Lakini Shrien anadai kuwa alikataa akawambia kuwa Yule ni mkewe naomba wawaache waondoke wakiwa pamoja.

Qwabe anaamfokea Shrien na kumwamuru kuwa atoke kwenye gari akisema toka, toka , toka.

Haya maelezo bado yanaungwa mkono na maelezo ya Mngeni ambaye alikataa kuingia makubariano na polisi. Anadai kuwa Qwabe alidai kuwa hakuna atakayeumizwa ni kwamba tu anamshusha Shrien eneo moja na mkewe naenda kumshusha mbeleni wao wanaondoka na gari. Pia anaunga mkono kuwa Shrien aligoma kuteremka akidai kwamba hawezi kumuacha mkewe.

Kumbuka Shrien na Mngeni hawakuwahi zungumza wala kuonana kabla na maelezo ya Mngeni yalitolewa kabla hata Shrien hajawa mmoja kati ya watuhumiwa katika upangaji wa mauaji hayo, lakini maelezo yao bado yanaendana.

Je inawezekana vipi Shrien akatae kuteremka atake ateremke na mkewe kama kweli alikuwa kapanga mauaji ya mkewe?

Shrien anateremka na kuachwa katikati ya kitongoji ambacho na maarufu kwa uahalifu wa kutumia bunduki, kwa amelezo yake anadai baada tu ya yeye kuteremka gari liliondolewa kwa kasi ya ajabu.

Kwa bahati nzuri anakutana na na mkazi wa eneo hilo ambaye ni mhasibu ajulikanaye kama Simbonile Natakazi ambaye anamuona Shrien akipiga kelele kama kicha analia na kukimbia ovyo.

Simbonile anadai alimpigia binamu yake simu ambaye ni askari polisi, anadai pia Shrien alikuwa hakai na alikuwa anapandwa hasira kwakuwa iliwachukua muda mrefu mpaka polisi kufika pale.

Simbonile anaendelea kusema siku zambele baada ya kusikia kuwa Shrien anatuhumiwa kwa kushiriki mauaji ya kupanga dhiodi ya mkewe, alishangaa kwa kuwa haamini kama kweli Shrien alishiriki katika mauaji ya mkewe kwa jinsi alivyokuwa kachanganyikiwa sana siku ile.

Saa 7 usiku

Baada ya kumtafuta Anni Dewan na utafutaji kutozaa matunda, polisi waliamua kumrudisha hotelini Cape Grace. Kamera za hoteli zinamnasa Shrien akiwa anapita peke yake kwenye korido ya hoteli akilia akiwa kama mwendawazimui, anaingia chumbani kwake na kutoka kila mara akiwa analia kama kapagawa na kuwafuata akiwafokea polisi waliokuwa kwenye chumba cha internet cha hoteli hiyo akiwauliza kwanini hawafanyi juhudi za kumtafuta mkewe bado wamekaa tu hapo.

Jambo la kushangaza Tongo naye alikuwa pale pale hotelini, na anadai alimsikia Shrien akiwa anawambia polisi kanini hawamtafuti mkewe na anadai ndipo kwa mara ya kwanza aligundua kumbe Shrien na Anni walikuwa wanandoa na kumbe Shrien alikuwa anataka mkewe ndiye auawe.

Inashangaza kuwa Tongo anadai kuwa hakujua kama Shrien na Anni walikuwa wanandoa japokuwa ni yeye aliyewatoa uwanja wa ndege, nay eye alikuwa akiwaendesha kwa tax yake muda wote. Ajabu kweli..

Mngeni anadai baada ya kumteremsha Shrien waliendela kuzunguka huku Anni akilia sana nyuma ya gari, anadai kuwa Qwabe alitaka kumnyanganya Anni pochi ambapo Anni ailing’ang’ania ndipo Qwabe aliegesha gari pembeni akateremka na kwenda mpaka kwenye dirisha la mlango wa nyuma akampiga risasi ya shingoni bahati mbaya wakati bato wakigombea ile pochi. Hivyo kwa maelezo ya Mngeni ni kwamba hawakuwa na lengo la kufanya mauaji ilikuwa tu wana lengo la kufanya wizi.

Anadai alimuuliza Qwabe kwanini umempiga risasi, Qwabe hakujibu.

Ila Qwabe anadai kwamba aliyempiga risasi Anni ni Mngeni na alimpiga akiwa amekaa siti ya mbele uoande wa abiria kama walivyokuwa wamekubarina mpango wa kumuua Anni ulikuwa umekamilika. Ila anadai wakati anampiga risasi yeye Qwabe ambaye ndiye alikuwa akiendesha gari hakutarajia maana hakumwambia wala kumpa ishara kuwa anamaliza kazi waliyotumwa.

Waliterekeza gari wakiwa wameuacha mwili wa Anni ukiwa umelala kwenye siti ya nyuma ya gari, wakaondoka na pochi ya Anni, simu zao, saa na bangiri za thamani pamoja na vito vingine vya thamani.

Polisi wanathamanisha kwamba vito walivyochukua vina thamani ya 8,600 pounds huku pete yake ya uchumba polisi waliikuta kaililia na pete yake ya ndoa yenye thamani ya Euro 25,000 akiwa kaificha kwenye mfuko wa kuifadhia vitu nyuma ya siti ya abiria ya mbele.

Swali la kujiuliza kama kweli hili lilikuwa tukio la mauaji lenye lengo lionekane kama wizi, kwanini hawakuchukua hizo pete maana zilikuwa na thamani mara sita zaidi ya vitu vingine walivyochukua.

Na kama kweli lengo ilikuwa ni tukio la mauaji, kwa maelezo ya Mngeni hawakuangalia kuhakikisha kama kweli Anni kafariki ila tu wao walichukua walichoweza wakaterekeza gari na kukimbia.

Polisi wa Afrika ya Kusini wanadai Ushahidi (Forensic evidence) unaonyesha kuwa kweli Anni alikuwa kaka siti ya nyuma akiwa ameegemea sit, na alipigwa risasi kutoka mbele upane wa abiria, huku aliyempiga akiwa kampiga kimakusudi mdomo wa bunduki ukiwa karibu ya shigo la Anne kati ya sentimita 5-10, hivyo wanadai kifo chake hakikuwa cha bahati mbaya.

Mtaalam wa Forensic Science, DR. Richard Shephered, alipitia ushaidi wote, nay eye anapingana na hoja ya polisi. Yeye anadai haiwezekani Anne apigwe risasi toka siti ya mbela ya abiria, pia anadai haiwezekani Anne awe kapigwa risasi makusudi kwakuwa mauaji ya makusudi mtu ulenga kichwani, au sehemu ya moyo kwakuwa ndizo sehemu amabzo mtu akipigwa muaji anakuwa na uhakika kuwa aliyempiga hawezi kupona na siyo shigoni.

Pia anadai kama kweli angekuwa amekaa kuegemea siti ya ngum, alipopigwa risasi kungekuwa na damu imeruka na kutapakaa sehemu alipokuwa kaegemea shingo lake kitu ambapo hakipo.

Yeye anadai Anni atakuwa alikuwa kaegemea mbele aidha kaegemea mapaja yake, akiunga mkono maelezo ya Mngeni kuwa Anni alikua akilia huku kakumbatia pochi yake amejikunja. Pia anadai au kama hakuwa kajikuja kwa kulalia mapaja yake basi alikuwa kaka kwenye kingo za siti yani hajaegemea nyuma bali kasogea sana mbele.

Nitarudi kumalizia sehemu mbili za mwisho.
Hii documentary itapatikana kwenye pdf na video kwa lugha ya kiswahili kwa wale watakaohitaji...
Nitahitaji
 
Malizia kwanza sehemu inayofuata.
kwani hadi hapo tunaona jamaa alichezesha game kwa akili sana
ngoja amalizie sehemu inayofuata,lakini ukae ukijua kuwa hizo ni njama walizozipanga wauaji baada ya ishu kubumburuka, maelezo yanajitosheleza kuwa mwenye mke hajashiriki kwenye hayo mauaji,
 
Mtaalamu mwingine wa masuala ya kiuchunguzi (Forensic expert) Bwana Mark Mastaglio, anadai kwamba ukitazama kwa umakini umbo la tundu la risasi na mazingira risasi ilikopenya inaonyesha kwamba Anni alipigwa risasi bunduki ikiwa karibu na katika mvutano baina yake na aliyempiga risasi. Anaongeza kuwa kwa upande wake anahisi polisi wamefanya kosa kubwa sana katika uchunguzi wao kwa kutotazama mazingira haya kwa umakini.

Pia anaongeza kwamba silaha iliyotumika katika kumuua Anni hakuna ripoti ya kiunchunguzi inayoonyesha kuwa polisi waliifanyia uchunguzi wa kitaalamu kubaini kama ingeweza kuachia risasi kwa bahati mbaya wakati wa mvutano baina ya muaji na Anni.

Pia anaenda mbali zaidi kwa kudai hata uchunguzi wa kitabu wa mwili wa marehemu (Post-motem), unapingana na ripoti ya polisi inayodai kwamba Anni alipigwa risasi makusudi hivyo mauaji yake yalikuwa ya kupangwa.

Mark yeye kama Richard anadai kwamba kwa ripoti ya post-moterm kuonyesha kwamba risasi imepenyeza shingoni ni dhahiri kwamba ilikuwa bahati mbaya, kwa maana kama mtu alikuwa ana dhamira ya kuua asingempiga risasi ya shingo, bali inategemewa awe amepigwa risasi ya kichwani au upande wa kifua kushoto kwenye moyo.

Anadai kuwa haijawahi kutokea mtu mwenye dhamira ya kuua, ampige risasi aliyemkusidia kumuua kwenye shingo.

Tarehe 12, mwezi wa 11 mwaka 2012, Mngeni alikutwa na hatia ya kumuua Anni, na alipewa kifungo cha maisha pasipo kuweza kupewa msamaha wowote. Kumbuka Mngeni ndiye alikataa kuingia makubariano na polisi na ndiye yeye pekee ambaye hakutaja ushiriki wa Shrien. Pia Mngeni kumbuka yeye alidai aliyempiga risasi Anni ni Qwabe na siyo yeye, na kwa madai yake alimpiga risasi kupitia dirishani wakati wakigombea pochi, wakati yeye Mngeni akiwa kaka kwenye siti ya mbele ya abiria kwenye gari.

Lakini polisi waliamini zaidi maelezo ya Qwabe na kukataa maelezo ya Mngeni, wakakubariana kuwa risasi aliyopigwa Anni ilitoka kwa mtu aliyekaa siti ya mbele ya abiria ambaye ni Mngeni.

Kitu kingine ambacho polisi wa Afrika Kusini hawakukitilia maanani kwa makusudi au bahati mbaya, ni kukusanya mabaki ya vumbi la risasi (gunshot residue). Wakati risasi inapoachiwa, uwa unatokea mlipuko ambao uwa unaachia vumbi kutokana na kuungua mchanganyiko unaotengeneza unga uliomo kwenye risasi.

Hilo vumbi umrukia mpingaji risasi kwenye mkono ulioshika bunduki, pia kwenye nguo alizovaa hasa maeneo ya shingoni, usono na kifuani. Pia uwa linaweza kuruka maeneo ya karibu na mpingaji alipokaa au kusimama.

Mtaalamu wa silaha kutoka Uingereza Bi Angela Shaw, anasema ushahidi wa vumbi la mripuko wa risasi ungesaidia kujua ni nani hasa alipiga risasi, na alikuwa kaka upande gani wa gari. Lakiini kwa bahati mbaya polisi wa Afrika ya Kusini hakuna ushahidi unaonyesha kuwa walijaribu kuchunguza nguo za Qwabe na Mngeni kwa kuzifanyia vipimo ili wapate kujua ni nani nguo zake zilikuwa na hilo vumbi.

Pia alipojaribu kwenda kufanya vipimo kwenye gari mauaji yalipotokea, kwa bahati mbaya alishindwa kupata sample za kutosha kwa ajili ya kupata matokea. Hii ina maana kwamba gari lilikuwa limeshasafishwa kwa makusudi au kutokana na kutokuwa makini na kutunza gari kwa ajili ya uchunguzi zaidi watu walilishika shika kila mahali na kuondoa vumbi hilo.

Mngeni na Qwabe wao wanadai baada ya hapo, walikimbiria kwenye vichaka vya karibu huku wakiwa wamebeba pochi na pesa waliopata, ila maelezo yao yanatofautiana kwenye kiasi cha pesa kilichopatikana.

Qwabe yeye anadai kwamba Mngeni ndiye alichukua bahasha yenye pesa iloiyokuwa nyuma ya siti ya abiria ya mbele, kama walivyoelekezwa ila anadai alikuta kuna Rand 10,000 badala ya 15,000 kama malipo waliyokuwa wamekubariana na anadai hiyo ela waliigawana nusu kwa nusu baina yake yeey Qwabe na Mngeni.

Lakini Mngeni yeye anadai kuwa ela waliyopata ni ile Rand 4,000 aliyowapa Shrien na waliigawana nusu kwa nusu baina yake yeye na Qwabe. Na kumbuka ni Mngeni tu ambaye hajamhusisha Shrien kwenye mpango wa mauaji ya Anni na ni yeye ambaye hyakuingia makubariano na polisi ya kutoa ushaidi ili adhabu yake ipungue.

Na ushaidi wa kuunga mkono maelezo ya Mngeni ni kwamba alipokamatwa inaonyesha alikuwa kafanya manunuzi na matumizi ya Rand 1,700 huku mfukoni akiwa amebakiwa na Rand 300 tu. Ikiwa maelezo yake yangekuwa ni uongo na maelezo ya Qwabe yangekuwa kweli, hakuna ushahidi unaonyesha kuwa kulikuwa na kiasi cha Rand 10,000 kati yao.

Jumapili tarehe 14, mwezi 11 mwaka 2010

Ikiwa ni asubuhi ya saa 3 na dakiaka 19, kamera za kwenye ukumbi wa hotel ya Cape Grace zinamuonyesha Shrien akipokea simu kutoka kwa polisi ikimtaarifu kwamba Anni amepatikana akiwa kauawa.

Baadhi ya polisi, daktari na watu wengine hasa jamii yenye asili ya Kihindi wanaoishi Afrika Kusini wanaonekana kuja kumliwaza maa Shrien anaonekana analia kaipiga kelele kachanganyikiwa na hana nguvu. Habari hiyo inaonekana kumchanganya sana. Shrien anaomba akaonyeshwe mwili wa mke wake.

Saa 1 na dakika 37 jioni

Kamera za kwenye korido katika hoteli ya Cape grace, zinamnasa Shrien akiwa anazungumza na mtu kwenye simu huku akionekana yuko kawaida kabisa bila majonzi na akicheka kama mtu ambaye alikuwa sawa na usingeweza kufikiria ndiye ambaye alikuwa analia kwa kufiwa na mkewe mapema siku hiyo. Ni ajabu masaa kadhaa toka apokee taarifa ya mke wake awe amekuwa sawa na anaonekana akitabasamu wakati akizungumza kwa simu na rafiki yake.

Jumatatu saa 4 na dakika 27.

Kamera za hoteli zinamnasa akiwa nalia peke yake wakati akitoka chumbani kwake kuelekea mochwari kwa ajili ya kutambua mwili wa mke wake.

Jumanne saa7 na dakika 40

Kabala ya Shrien kuondoka Afrika ya Kusini, anakutana kwa mara ya mwisho na Tongo na wote kipindi hicho yani Tongo na Shrien walikuwa bado mashahidi na siyo watuhhumiwa. Kamera za hoteli zinamuonyesha Tongo akiwa kavaa kaptura na shati jeupe akiingiakwenye hoteli hiyo huku kichwani akiwa kava kofia nyeupe pia.

Tongo anadai kilichomleta pale hotelini ilikuwa ni kufuata malipo yake ya Rand 5,000 alizomuahidi kama malipo yake ya kuandaa watu wa kutekereza mauaji ya Anni.

Kamera zinamuonyesha Shrien akiwa amebebelea mfuko wa plastiki mweupe, anakutana na Tongo mapokezi, kasha wanaongozana na kuingia chumba cha Internet cha hoteli hiyo ambako hakuna kamera wala mtu yoyote kwa wakati huo.

Nadni ya dakika moja tu anaonekana Shrien akitoka kwenye chumba hicho akiwa hana ule mfuko mweupe aliokuwa amebeba wakati anaingia, pia baada ya sekunde nane anaonekana Tongo akitoka akiwa ndiye kabeba huo mfuko mweupe na anaelekea kwenye vyoo vya wanaume.

Tongo anadai alipoenda chooni kuangalia kwenye huo mfuko mweupe, alikuta kuna mfuko wa ngozi ambao ndani yake kulikuwa na kiasi cha Rand 1,000 badala ya Rand 5,000 kama walivyokubariana awali.

Tongo anaonekana kwenye kamera za hoteli akitoka kwenye chooni akiwa amebeba mfuko mweupe wazi wazi na kuelekea nje ya hoteli kasha kuondoka maeneo hayo. Ila yeye anadai baada ya kugundua Shrien kamtapeli alianza kumtafuta lakini hakumpata jambo ambalo si kweli ktuokana na ushahidi wa video zilizorekodiwa na kamera za hoteli.

Pia Tongo anadai baada ya hapo hakuwahi tena kuwasiliana na Shrien kabisa, jambo ambalo pia ni uongo kwakuwa kumbukumbu za simu zinaonyesha Shrien alimpigia Tongo simu mnamo saa 9 na dakika 32, pia tukio hili lilinaswa na kamera za hoteli wakati Shrien akizungumza na Tongo kwa sekunde 42.

Hivyo utaona kuwa maelezo mengi ya Tongo yamejaa uongo mwingi, kuna mengi anayodanganya kiasi kwamba ni vigumu kujua kipi anachoongea ni kweli.

Swali ni je Shrien ela aliyompatia Tongo ni kweli yalikuwa malipo ya kupanga mauaji ya Anni, au hizo Rand 1,000 alizompatia ilikuwa ni malipo ya Tongo kwa huduma yake ya tax?

Tongo alikamatwa wiki mmoja baada ya mauaji ya Anni, na siku iliyofuata aliingia makubariano na polisi kutoa ushidi dhidi ya Shrien ili apunguziwe adhabu apewe miaka 7 tu badala ya kifungo cha miaka 25 na ataachiwa mwaka 2020.

Baba yake Anni aliulizwa kama nakubariana na hayo makubarino ya polisi na Tongo, ili Tongo aongee ukweli wa ni kitu gani kilitokea, na baba yake Anni alikubari kwa kusema kuwa anakubariana na makubariano hayo ili mradi tu ukweli ujulikane.

Uharaka huu wa polisi kuingia naye makubariano siku ya pili tu toka akamatwe uliwashangaza watu wengi hasa wanasheria wabobezi, inakuaje polisiwakubari kuingia makubariano na wauaji mapema tu bila kujaribu kutumia njia nyingine kupata ushahidi na maelezo kutoka kwao.

Kipindi Tongo anakamatwa Shrien alikuwa amekwisha ondoka Afrika ya Kusini na kurudi kwao Uingereza. Wakati Shrien anaondoka alikuwa bado hajaanza kuchukuliwa kama mtuhumiwa.

Wiki mbili baada ya Tongo kukamatwa, mamlaka ya polisi ya Afrika Kusini inamtangaza Shrien kuwa ndiye mtuhumiwa namba moja katika njama za kupanga mauaji ya aliyekuwa mke wake Anni. Wanaomba mamlaka ya polisi Uingereza imrudisha Shrien Afrika Kusini ili apate kuja kujibu mashitaka yanayo mkabiri jambo ambalo yeye Shrien, familia yake na wanasheria wake wanalipinga.

Tongo na wenzake wanapewa hukumu pasipo polisi kusikiliza upande wa pili yaani upande wa Shrien, kwakuwa mamlaka za Uingereza ziliwahitaji polisi wa Afrika Kusini wasafiri kwenda kumhoji Shrien huko huko Uingereza, ila mamlaka ya Afrika Kusini iligoma kufanya hivyo.

Baadhi ya watu wanaamini kwamba polisi waAfrika Kusini walikuwa wanafanya mambo kutokana na msukumo wa kisiasa ili kupata majibu ya haraka wapate kuokoa sekta ya utalii ya nchi ambayo mauaji hayo yaliitia doa.

Kesi ya mauaji ya Anni iliteka hisia za watu wengi na vyombo vikubwa vya habari vya kimataifa kama BBC, CNN, FOX NEWS na kadhalika viliangazia sana., jambo ambalo lilikuwa hatari kwakuwa ilionyesha kuwa Afrika Ya Kusini siyo mahali salama kwa raia wa Kigeni hasa watalii.

Kuokoa jahazi, polisi walipewa msukumo wa kufanya haraka kutatua hiyo kesi ili kuondoa picha mbaya iliyoanza kujengeka ambayo ilikuwa inatishia sekta ya utalii wan nchi hiyo. Wachambuzi wengine wanazidi kudai ya kwamba ndiyo maana polisi hawakuwa tayari kufanya uchunguzi wa mambo mengi ila tu walitaka kuoneysha mhusika mkuu ni Shrien ambaye ndiye alikuwa mtalii mwaenyewe ndiye aliyepanga kumuua mke wake.

Inaendela comment #17
 
hapo conclusion ni 2 tuu
1=kweli shrien alhusika ila Kwa kua ni perfectionist wanashindwa kumpata na hatia
ushahidi pekee ambao ungeweza kumpata ni maongezi ya cm katiyake na dreva tax
either aliyachezea au aljua tuu kwa kipindi hicho SA haikua na uwezo wa kungamua maongezi yao (alkua ni tajiri na ametoka nchi ilooendelea so chochote knaezekana )

2= mfanyakazi wa hotel aliamua kugawa mchongo/kuwashawishi au nae alpewa mchongo na dereva wa kuwaibia ao Wanandoa ila bahat mbaya yakatokea mauwaji(kwa Maelezo hayo apo juu mi binafs nakubal risasi iltoka baat mbaya) dizain hawakujua waibe nini ni kama waliambiwa tuu hao ni matajiri pigeni kazi....

kwa hii namba2 yule dereva alkua anajua kiasi cha pesa alchochenchi c's ye ndo alkua anampeleka duka la fedha!! nauakika hawakujua abar za pete pia

myb walamua kubaki na dem maana alkua kashika mkoba so wakajua ela ipo


[HASHTAG]#hii[/HASHTAG] ya polisi na kukubaliana waalifu ipo sana kwa wenzetu na kosa walofanya polisi wa sa ni kua na assumption zao zilzopelekea kumhic 1kwa1 bwana shrien

sjui nmepatia? anyway malzia story kwanza!!
Sababu ya kumuua ni nini?
 
Sababu ya kumuua ni nini?
kwa shren myb sabab alkua shoga au sabab nyingine anayoijua yeye!!

kwa wasauzi ni tamaa ya pesa tuu! na mtindo huo sauz ni comon sana SA pekee kwa mwaka sio chini ya polisi 700 wanauawa
unaeza ukaona apo SA sio salama kwa mgeni!!!
 
huyo dereva tax ndye aliyepanga mauaji baada ya kuona hyo mhindi ana hela ...movement za kwenda kwny maduka ya kubadilishia fedha ndyo iliomponza hyo mhindi
 
Mvutano na mapambano ya kumrudisha Shrien Afrika Kusini

Baada ya polisi wa Africa Kusini kudai ya kwamba Shrien ndiye mhusika mkuu katika njama za kupanga na kutekeleza mauaji ya aliyekuwa mkewe Anni Dewan, polisi wa Afrika Kusini walitoa ombi kwa mamlaka ya Uingereza wakiomba Bwana Dewan arudishe Afrika Kusini ili aje kujibu mashitaka yanayomkabiri jambo ambalo wanasehria na familia ya Shrien ililipinga siyo tu kwa maneno bali hata kwa kupitia kuweka pingamizi kwenye mahakama za Uingereza.

Tarehe 7 mwezi wa 12 mwaka 2010, kikosi maalum cha polisi wa uingereza kinachohusika na kukamata na kuwarudisha watuhumiwa waliotanda uhalifu nchi nyingine, kilimkamata na kumweka chini ya ulinzi kutoka na ombi lilitolewa na mamlaka ya polisi ya Afrika Kusini. Lakini akiwa chini ya ulinzi hali ya afya ya Shrien ilionekana siyo nzuri hivyo alipelekwa hospitali, ambapo baadae iligundulika na matatizo ya kiakili kahahamishiwa hospitali ya Fromside inayohusika na kutibu magonjwa ya msongo wa mawazo na akili.

Kwa mujibu wa wanasehria wa Shrien, familia yake pamoja na yeye mwenyewe, walikuwa wakidai kwamba Shrien hayuko sawa kiafya ana matatizo ya msongo wa mawaza na matatizo ya kiakili toka alipompoteza Anni. Walidai kwamba Shrien yuko tayari kurudi Afrika Kusini kujibu mashitaka yanayo mkabiri pale tu atakapokuwa sawa kiafya, na hakuna shaka kuwa atafanya hivyo kwakuwa hata yeye mwenyewe angependa ukweli wa mambo ujulikane. Na kwa kuthibitisha hilo Shrien alikuwa akitibiwa kwenye kituo cha kutibu magonjwa ya akili huko katika mji wa Bristol.

Mvutano wa mamlaka za Afrika Kusini zikiungwa mkono na familia ya Anni pamoja na watu walioguswa na kifo cha Anni, uliendelea wakiitaka mamlaka ya Uingereza imrudishe Shrien Afrika Kusini, na katika kipindi cha kiangazi cha mwaka 2011, ombi la kumrudisha Shrien Afrika Kusini lilikubaliwa na alieyekuwa mwanasheria mkuu wa Uingereza Bwana Howard Riddle na aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani wa Uingereza kipindi hicho, Bi Theresa May, aliweka sahihi kuruhusu ombi hilo kutekerezwa.

Lakini wanasheria wa Shrien hawakukubari walikata rufaa mahakama kuu kupinga uamuzi wa Shrien kurudishwa Afrika Kusini kwa muda huo, na mwezi awa 3 mwaka 2012, mahakama kuu iliweka zuio la muda kwa Shrien kurudisha Afrika Kusini kwa madai kwamba itakuwa ni uvunjibu wa haki na ukandamizaji kumrudisha Shrien Afrika kusini huku hali yake kiakili hayuko sawa.

Mahakama ilitaka Shrien arudishwe Afrika Kusini pale hali yake itakapotengemaa akawa na uwezo wa kusimama mahakamani kujibu mashitaka yake. Ilidaiwa ya kwamba kuhusu swala la Shrien kurudishwa Afrika Kusini hilo halina ubishwi ni lazima arudi kwakuwa anatibiwa ni lazima atapona japo uponaji wake ni wa taratibu.

Ndugu na jamaa wa Anni Dewan hawakufurahisha na uamuzi wa mahakama kuu ila walisema kwamba wana imani huo ulikuwa mwanzo tu ila haki itapatikana. Dada yake Anni dewan ajulikanaye kama Ami Denborg alisikika akisema kwamba wao kwa muda huo wanachojali ni kuhusu Anni, na ni kutaka kujua nini hasa kilitokea. Aliongeza kuwa watapambana mpka mwisho na mapambano ndiyo kwanza yameanza. Akadai kuwa wanasubiri Shrien apone haraka awe katika hali nzuri ya kujibu mashitaka yake japo wanaona kama wanachelewa kuujua ukweli. “Inatuwia vigumu na tunapitia hali ngumu sisi kama familia tunahanaika kila siku” alimalizia.

Baba yake Anni Bwana Vonod Hindocha yeye alidai kwamba wao kama wazazi wanapitia hali ngumu pale wanaposikia mara hivi mara vile, kila kesi inapotajwa inabidi kuhudhuria , kila wakitazama runinga wakiona habari kuhusu kifo cha mtoto wao huku picha na zikiwa kila mahali. Inawaumiza sana.

Mwezi wa 7 mwaka 2013, waendesha mashitaka wa Afrika Kusini walihudhuria mahakama ya juu Uingereza wakiwa wanatetea uamuzi wao wa kutaka Shrien arudishwe Afrika Kusini. Katika utetezi wao walidai kwamba Shrien ambaye kipindi hicho alikuwa tayari ana umri wa miaka 33, miaka mitatu baada ya kifo cha Anni, alikuwa amekwisha kua na afya njema hivyo wangependa arudishwe Afrika Kusini kujibu mashitaka yake, pia waliongeza kwamba hata kama itaonekana hayuko sawa basi watampeleka akae kwenye kitengo cha magonjwa ya akili kilichopo Cape Town.

Mwendesha mashitaka wa Afrika Kusini Bwana Keith aliongeza kuwa anakubari kuwa awali Shrien alikuwa mgonjwa na alikuwa hawezi kuunganisha matukio yaliyotokea mpaka mkewe kuuawa. Ila alidai kwa muda huo Shrien ameonyesha maendeleo mazuri na hivyo angeoenda wamrudishe Aafrika Kusini maana kuendelea kuweka zuio kunamfanya azidi kutopona maana kutopona kwake ni faida kwake mwenyewe kwakuwa hataki kurudi Afrika Kusini kujibu mashitaka.

Mtaalamu wa magonjwa ya akili aliyeongea na Bwana Shrien, alidai kwamba SHrien alimwambia binafsi anataka arudi Afrika Kusini kwenda kupambana na mashitaka yaliyo juu yake. Aliongeza kuwa Shrien anataka kuwadhihirishia kuwa hakuusika katika kutenda jambo hilo.

Tarehe 31, mwezi wa 1 mwaka 2014, mahakama kuu ya Uingereza ilitupilia mbali pingamizi la wanasheria wa Shrien Dewan na kuondoa zuio la muda ililokuwa imeweka kuhusu Shrien kurudishwa Afrika Kusini. Majaji watatu waliokuwa wakisikiliza shauri hilo wakiongozwa na Jaji Thomas, waluitoa hukumu inayosema kwamba hakutokuwa na uvunjibu wa haki wala ukandamizaji ikiwa Bwana Shrien atasafirishwa kurudishwa Afrika Kusini endapo tu serikali ya Afrika Kusini itasema ni kwa muda gani Bwana Shrien atakaa nchini humo.


Kurudishwa Afrika Kusini

Hatimaye baada ya mvutano wa miaka minne toka kifo cha Anni, hatimaye tarehe 7, mwezi wa 4 mwaka 2014, Shrien alisafirishwa kurudishwa Afrika Kusini kujibu mashitaka yanayomkabiri juu ya kupanga mauaji ya kumuua mkewe tarehe mwaka 2010. Alichukuliwa kutoka hoispitali ya magonjwa ya akili ijulikanayo kama Fromside iliyoko mjini Bristol, akasindikizwa na kikosi maalumu cha polisi kinachohusika na kuwasindikiza wahalifu mpaka uwanja wa ndege wa Bristol, ambapo walimkabithi kwa wawakilishi wa serikali ya Afrika Kusini ambao waliondoka naye kuelkea Afrika Kusini.

Uendeshaji wa kesi dhidi ya Shrien akiwa Afrika Kusini

Alipofikishwa Afrika Kusini moja kwa moja alipelekwa katika mahakama ya Western Cape Town, kufunguliwa mashitka rasmi.

Alikuwa anasindikizwa na na daktari, nesi na askari polisi kwakuwa alikuwa ni mtuhumiwa huku ni mgonjwa. Waandishi wa habari waliruhusiwa kuingia chumba cha mahakama na waliruhusiwa kupiga picha na kuchukua video ila walitakiwa kuzima kila kitu pale jaji atakapoingia kwenye chumba cha mahakama.

Kusikilizwa kwa kesi ya Shrien kulianza rasmi tarehe 6, mwezi wa 10 mwaka 2014 na hapa chini chini ya jaji Jeanette Traverso.


UTETEZI WA SHRIEN DEAN KWA TAFSIRI ISIYO RASMI



MAHAKAMA KUU YA AFRIKA KUSINI

KITENGO CHA MAGHARIBI CHA CAPE TOWN

Case No: CC15/2014

Katikia shauri baina ya;

SERIKALI

Na

SHRIEN PRAKASH DEWAN Mtuhumiwa

MAELEZO YA AWALI KAMA ILIVYONBAINISHWA KWENYE KIFUNGU 115 YA SHERIA YA MAKOSA YA JINAI YA MWAKA 1997.

Mimi ndiye mtuhumiwa katika shauri hili, ninatambua mashitaka yaliyopo juu yangu na ninatoa maelezo yangu kama ifuatavyo:

1. Ad Count 1

1.1.Sihusiki na shitaka hili la kupanga njama kama ilivyo kwa mujibu wa kidogo cha 18/2/(a) cha sheeria ya Riotoud ya mwaka 1956

1.2.Ninapinga kuwa nilishirikiana na Zola Tongo, Mziwamadodo Qwabe na Xollo Mendi au mtu mwingine yoyote kutekereza uharifu unaozungumziwa hapa.

1.3.Ninaomba pia maelezo yaliyoko kwenye haya ya 6 mpaka 105 hapo chini yahusike.

2. Ad Count 2

2.1. Sihusiki na tuhuma za kuteka.

2.2. Ninaomba pia maelezo yaliyoko kwenye haya ya 6 mpaka 105 hapo chini yahusike.

3. Ad Count 3

3.1. Sihusiki na tuhuma hizi za unyanganyi.

3.2.Ninaomba pia maelezo yaliyoko kwenye haya ya 6 mpaka 105 hapo chini yahusike.

4. Ad Count 4

4.1.Sihusiki na tuhuma hizi za mauaji ya kukusudia.

4.2.Ninaomba pia maelezo yaliyoko kwenye haya ya 6 mpaka 105 hapo chini yahusike.

5. Ad Count 5

5.1. Sihusiki na tuhuma hizi za kutaka kupindisha haki.

5.2. Ninaomba pia maelezo yaliyoko kwenye haya ya 6 mpaka 105 hapo chini yahusike.



MAELEZA YA VIFUNGU HAPO JUU

Utangulizi

6. Maelezo haya hapa chini yatatoa mwaka na kuonyesha ni kwanini ninakataa kuhusika na hayo makosa yaliyo dhidi yangu.


Kuhusu jinsia yangu

7. Nimekuwa na mahusiano kati ya jinsia zote za kike na kiume. Ninajichukulia mimi kuwa nina jinsia mbili (bi-sexual). Mahusiano yangu kingono na jinsia ya kiume ilikuwa mara nyingi ni kimwili au kupitia mazungumzo ya ujumbe mfupi kwa barua pepe baina yangu na watu nilikutana nao mtandaoni, au kwenye kumbi za starehe; wakiwemo Malaya kama Leopold Leisser. Mahusiano ya kingono na jinsia ya kike mara nyingi yalikuwa ni katika kutafta mwenza na yalihusisha mambo mengine and yalikuwa ya kihisia zaidi.

Mahusiano yangu na marehemu (‘Anni’)

8. Nilikutana na Anni tarehe 30 mwezi wa 4 mwaka 2009 baada ya rafiki yangu kunipa mawasiliano yake. Siku ya mtoko wetu wa kwanza nilivutiwa naye kimapenzi moja kwa moja, nilivutiwa na uchangamfu wake na ilionekana tuliendana kwakuwa nay eye alionekana kuvutika kwangu.

9. Anni alikuwa akifanya kazi Sweden kipindi hicho, ila mara kwa mara alikuwa akija UK ambapo tulikuwa tukitumia muda huo kuwa pamoja. Na mimi pia nilikuwa nikipaa nafasi nasafiri kumfuata Sweden, kweli tulipendana sana. Sote tulikuwa na matarajio makubwa juu ya maisha yetu ya baadae. Na sote tulikuwa hatutaki kujishusha jambo lililofanya tuwe mara kwa mara tulibishana.

10. Mnamo mwezi 12 mwaka 2009, nilitaarifiwa na mtaalamu wa mambo ya uzazi kuwa kutokana na tatizo la hormone zangu kuwa katika kiwango cha chini, kuna uwezekano wa kupata tatizo la kutopata watoto. Alinishauri kama ninataka kuongeza uwezekano wa kupata watoto inatakiwa niwe nadungwa hormone za testelerone kama njia ya matibabu. Ila pia alinionya kuhusu matatizo yanayoambatana na matibabu hayo ikiwemo uwezakano wa damu kuganda, kulala lala kila mara, kubadirika badirika kitabia (mood swings), kuongezeka matiti, kunyonyoka nywele, kuongeza mwili na uzito. Niliamua kwamba nitafanya hayo matibabu hata kama kulikuwa kuna matatizo yake lakini kwangu kuwa na familia lilikuwa jambo la muhimu sana.

11. Nilizungumza tatizo langu na Anni kwakuwa nilijua naye alihitaji kuwa na watoto. Pia baadae nilizungumza hili tatizo na wazazi wangu ambao nao walionyesha kunitia moyo na nguvu kwa kuniunga mkono. Pia walijaribu kunipa baadhi ya njia mbadara ya kutatua tatizo hili.

12. Mimi na Anni tulienda sehemu tofauti katika likizo za mwezi wa 12, mwaka 2009 mpaka mwezi wa kwanza mwaka 2010 na katika kipindi hiki mahusiano yetu ni kama yalikuwa yamepoa. Tarehe 14 mwezi wa kwanza 2010 Anni alisitisha mahusinao yetu kwa kunitumia barua pepe. Mwezi wa 3 mwaka 2010 Anni alihamia London akitokea Stockholm. Tukawa tunaonana mara kwa mara.

13. Katika kipindi hicho niliambiwa kuwa kiwango cha hormone zangu kilikuwa kimeongezeka hicyo hali yangu ya kuzalisha watoto iko katika nafasi nzuri. Nilifurahi sana na kujihisi ni mwenye bahati.

14. Mwishoni mwa mwezi wa 4 mwaka 2010, tulianza kujadiri maisha yetu ya baadaye pamoja na mahusiano yetu yalirudi na kuwa mazuri. Anni alitaka nimkutanishe na wazazi wangu hivyo tulifanya mpango akakutana na mama yangu tarehe 29 mwezi wa 4 mwaka 2010. Baba yangu alikuwa kasafiri, hivyo tulifanya mpango wazazi wake Anni waje Bristol tarehe 8 mwezi wa 5 mwaka 2010 ili wakutane na wazazi wangu.

15. Katika kupanga maisha yetu ya ndoa mimi na Anni tulikuwa tukijadiri jinsi tutakavyoishi. Tulikubariana kuwa tutafanya makazi yetu maalumu kuwa Bristol, ambako ofisi yangu ilikuwa, lakini pia tuwe na nyumba ya mapumziko London kwa ajili ya siku za mwisho wa wiki. Hivyo tulianza mchakato wa kuzirekebisha nyumba zote mbili ili ziwe katika muonekano mzuri kwa wanandoa na pale tutakapo pata watoto.

16. Wakati wazazi wa Anni wakiwa Bristol, walipata kutembelea nyumba zote mbili na baba yake Anni alitupatia ushauri ambao ulitusaidia katika kufanya marekebisho.

17. Chumba change cha sasa ninachotumia Bristol, hakikuwa kizuri wakati huo. Kwa mfano hakikuwa chumba kinachojitegemea kwakuwa hakikuwa na nafasi kwa ajili ya kabati za nguo,au sehemu ya kuhifadhia viatu, mapochi wala vipodozi. Mimi na Anni tulichora michoro mbalimbali ya jinsi gani tulitaka vyumba vyetu kwa nyumba ziote mbili viweje. Anni alikuwa napenda sana kuwafurahisha wageni wake kwa mapishi na chakula kizuri hivyo tuliamua kutengeneza majiko ya kisasa yenye nafasi kubwa. Tulitumia muda wote kuchagua taa, rangi, sakafu na kila kitu kwa ajili ya nyumba zetu.

18. Mwishoni mwa mwezi wa 5 2010, mimi na Anni hatukubariana kuhusu jambo flani. Alinipigia simu akiwa kakasirika sana na akiwa anafoka. Kutoka na mazungumzo tuuliyoongea kwenye simu hiyo tarehe 24 mwezi wa 5 mwaka 2010 nilimwandikia barua pepe ifuatayo:

Mpendwa Anni

Nadhani ni bora zaidi nikikuandikia kuliko kuyasema haya ili upate kuyasoma na kuyarudia mara kwa mara…..nimefadhaika sana sana baada ya yale mazungumzo. Ninajua sisi ni watu wawili tofauti ila niliamini katika mahusiano mtu anaweza tatua hii changamoto ya utofauti uliopo. Tulipokutana moja kwa moja nilikupenda, na siyo kwasababu labda wewe ni mrembo, hapana ila ni kwasababu ulinifanya nicheke. Tulikuwa na wakati mzuri kwenye chakula chetu cha join kwenye mgahawa wa Asia de cuba.

Nilitamani sana kuwa na msichana ambaye ninaweza kuwa rafiki yake pia. Yule ambaye atanielewa japo ninajua siyo jambo rahisi. Najua mimi ni mtu niliye makini sana wa mambo kiasi kwamba watu wengine uwa wananiona ni mkotofi. Niko makini sana katika kutimiza mambo flani maishani, na siyo kuhusu kutengeneza pesa hapana pia kuwa na maisha bora. Familia, biashara na kuwa mtu nayesaidia jamii na kuleta m,abadiriko. Tulipokutana na kukaanzisha mahusinao niligundua wewe ndiye huyo msichana ninaye mhitaji.

Siyo lazima iwe sawa kwetu sote, japo siamini kama ni mimi ninayeenda kuandika hiki, na kusema kweli ninatokwa na machozi hapa ninapoandika, ila kama unaamini kuwa namimi hakutokufanya uwe mtu mwenye furaha, basi mahusiano haya siyo sawa kwako. Natumai sicho ulichomaanisha ila sitaki kujihisi kwamba nimekulazimisha katika mahusiano haya na hivyo sitaki wewe ukose furaha ninahitaji kuwa na wewe maisha yangu yote ila siyo kama mahusiano haya hayakupi furaha siko tayari kukuona ukiishi bila furaha. Ninatumai tutatua hii changamoto.

Nitazungumza na wewe baadae

Nakupenda siku zote

Shrien

19. Tulitatua matatizo yetu na sikuwa na shaka kuwa moyo wangu ulimpenda Anni na kuwa nilihitaji kutengeneza maisha tukiwa pamoja mimi nay eye. Alinihakikishia kuwa japo kuna kutoelewana kwa hapa na pale ila alikuwa akihitaji kuolewa na mim na alitaka kuwa na familia na mimi. Tulidangaza uchumba tarehe 27 mwezi wa 5 mwaka 2010.

20. Mwezi wa 6 mwaka 2010 nilimuomba msaidizi wangu binafsi Bwana Sion Haris, anisadie kuandaa safari ya surprise kwa ajili ya Anni wakati nitakapomvisha pete ya uchumba ambayo niliitengeneza kwa ajili yake na kwa urembo niliyochora mimi. Nilikodi ndege binafsi kwa ajili yangu na Anni kwenda Paris, Ufaransa siku ya tarehe 10, mwezi wa 6 mwaka 2010 ambapo niliomba aniruhusu nimuoe na kumvisha pete ya uchumba.

21. Mimi na Anni tulijadiri kuhusu mipango ya harusi na tulikuja na mipango kadhaa ya nammna harusi yetu itakavyofanyika. Sote tulitaka kuwa na majina ya maeneo ambayo tulitaka kutembelea hivyo mwezi wa 7 mwaka 2010 tulisafiri pamoja kwenda Dubai na tulipotoka Dubai tulielekea India. Baada ya kuzungumza na familia zetu tulikubariana kuwa ndoa itafungwa India. Tulipanga matukio mbalimbali kwa ajili ya wageni waalikwa kufanyika kuanzia tarehe 28 mpaka 30 mwezi 10, mwaka 2010. Ndoa ya kidini itakayofungwa Kiihindu ilipangwa kufanyika tarehe 29 mwezi wa 10 mwaka 2010.

22. Baada ya makubariano hayo mimi nilirudi Uk kuendelea na biashara zangu na kuendeleza na marekebisho ya nyumba wakati Anni alibaki India akiendelea na maandalizi ya harusi. Tuliendelea kuwasiliana kupitia simu, ujumbe mfupi na barua pepe. Mwezi wa 8 alikuja Uk bila taarifa kunifanyia surprise halafu alielekea Sweden kwa ajili ya kuhudhuria siku ya kuzaliwa ya mjomba wake.

23. Tarehe 31, mwezi wa 8 mwaka 2010, mimi na rafiki zangu tulisafiri kwenda La Vegas kwa ajili ya tafrija yangu ya kuaga useja. Tulikaa huko kwa wiki moja na kati ya mambo niliyofanya niliingia makubariano na kufanya mazungumzo ya kufanya safari ya helkopta kwa ajili yangu na Anni. Anni alikuwa India kwa wakati huo na alinitaarifu kuwa anahisi kuelemewa na kuchoka kwakuwa anahitajika kufanya kila kitu kinachihusu mipango ya harusi mwenyewe. Alidai inakuwa vigumu kwake kumfurahisha kila mtu na alikuwa analalamika kuwa mpaka muda huo hajafanyiwa kitchen party.

24. Hivyo nilielekea India tarehe 13, mwezi wa 9 mwaka 2010 nikiwa na bibi yangu ili amsaidie Anni. Yeye ndiye alisema kuwa anamhitaji bibi yangu ndiye aje kumsaidia kwa maana walikuwa nimarafiki.

25. Mimi na Anni tulikuwa tuna jambo moja tunaloshabihian, tulikuwa tunatak kujua kila kitu kinafanyikaje na kinafanyika kwa matarajio yetu wakati wa maandalizi ya harusi. Mara nyingi kulitokea kutokubariana mara kwa mara wakati tunafanya maandalizi ya harusi. Kwa mfano rangi ya mapambo, dhima ya tukio Fulani, aina ya mavazi nakadhalika. Hii ilileta kuvutana na mabishano. Mambo yalizidi kuwa mabaya tarehe 21 mwezi wa 9, pale ambapo Anni aliamua kuondoka katika hoteli tuliyokuwa tunakaa. Alinitumia ujumbe mfupi wa maneno kuwa hawezi tena kuendela na mipango ya harusi anataka harusi ifutwe. Nilijaribu kumpigia na kumtumia ujumbe mfupi wa maneno lakini hakupokea wala kunijibu hivyo nikaamua kumpigia baba yangu na kumueleza. Baadaye baba yake Anni alinipigia pia bibi yangu alinipigia pia. Nilizungumza na baba yake Anni nikamwomba ajaribu kumpigia Anni na kumtuliza, na alikubari kufanya hivyo. Nilikuwa nimechanganyikiwa sana na nilikuwa nikilia wakati nazungumza kwenye simu.

26. Kesho yake Anni alinipigia na alikuja pale hotelini ili tuzungumze. Tulienda pamoja kupata chakula cha mchana na Anni aliniambia kutopendeza kwake na baadhi ya vitu. Alidai mimi ni mtu ninayependa kumtawala mtu na nilikuwa nikijihusisha sana katika kila jambo. Alidai kwamba sikumuacha apange mipango ya harusi kama alivyotakabali nilikuwa kila mara nafuatilia kila jambo kuona anafanyaje jambo ambalo linamfanya ajisikie kukosa uhuru. Alikuwa akijihisi vibaya kuwa alikuwa India peke yake bila kuwepo hata mtu mmoja kutoka katika familia yake au hata rafiki wa kumsaidia kuandaa harusi yake. Tulizungumza kwa muda na sote tulikubariana kwamba inabidi kila mtu asikilize maoni ya mwenzake. Tulikubariana ya kwamba mara kwa mara tunatibuana ila ni kwakuwa tuko penzini na kila mtu anataka kilicho bora kwa ajili ya maisha yetu ya mbele.

27. Mimi nilirudi UK kuendelea na biashara zangu na marekebisho ya nyumba. Nikiwa UK nilijadiri wapi twende kwa ajili ya fungate na Preyern na Sian. Nilitaka kufanya kitu ambacho Anni hakuwahi kufanya kama surprise kwake. Nilikuwa nahitaji safari hasa mbuga za wanyama kwa maana kabla tuliwahi kuzungumza na Anni ikaonekana kwamba napenda sana safari na wanyama. Niliandika nini ninahitaji kwenye karatasi na nikamuomba Sian afanye tathimini ni wapi tunaweza kenda mimi na Anni kwa ajili ya fungate.

Harusi

28. Tarehe 15 mwezi wa 10 mwaka 2010, nilirudi Mumbai ili niweze kutoa msaada katika kufanya maandalizi ya mwisho ya harusi. Sherehe za awali kabla ya harusi zilianza Halhamisi ya tarehe 28, mwezi wa 10 mwaka 2010. Harusi ilifanyika Ijumaa joini yatarehe 29 mwezi wa 10 mwaka 2010. Hii ilifuatiwa na chakula cha mchana siku ya Jumamosi mchana na tafrija usiku.

29. Sian alikuwa akifanyia kazi mapendekezo yangu kwa ajili ya fungate na siku ya Jumatatu ya tarehe 1, mwezi 11 mwaka 2010 alinitumia mapendekezo yake yakiwa katika mfumo wa Microsoft Excel akionyesha sehemu mbalimbali alizochagua ili nichague sehemu moja ninayotaka. Nilijadiri na Preyern ambaye alikuwa bado yuko hotelini na sisi.

30. Mimi na Anni tuliondoka India na kuelekea Bristo tarehe 2, mwezi wa 11 mwaka 2010 tukiwa na wanafamilia. Lengo lilikuwa kuhadhimisha sikukuu ya Diwali, ambayo ni sikukuu kubwa kwa waumini wa Kihindu tukiwa na familia zetu, halfu ndipo twende kwenye funate. Halafu pia wajenzi walihitaji maelekezo kutoka kwa kwangu na Anni kuhusiano na baadhi ya mambo has sehemu za chumba chetu.

31. Siku ya Ijumma ya tarehe 5, mwezi wa 11 mwaka 2010 Anni alienda kuonana na daktari wetu wa hapo Bristol. Tulikuwa tuna haraka ya kupata watoto hivyo daktari alimshauri jinsi ya kufanya kuongeza nafasi ya kupata mimba.

32. Nilikuwa nimeshaamua kumpeleka Anni Afrika Kusini kwa ajili ya fungate, na hakuna kati yetu aliyewahi kufika Afrika Kusini kabla na ilitokea kwa nkifupi cha South Africa ya SA ilikuwa sawa na kifupi cha majina yetu ya Shrien Anni ‘SA”. Siku hiyo Ijumaa ya tarehe 5 mwezi wa 11, niliwaomba Sian na Preyern wanikatie tiketi za ndege pamoja na kufanya maandalizi kwenye hoteli ya Chitwa Chitwa, iliyoko katika hifadhi ya wanyama ya Kruger. Jambo hili nililifanya siri sikutaka Anni ajue kwakuwa nilitaka kumsuprise. Siku hiyo nilitoa pound 7,000 kwenye hifadhi yangu binafsi ya bank yangu ya Barclays.

33. Tulitumalizia siku za mwisho wa wiki tukiwa London.

Afrika ya Kusini –Jumanne mpaka Halhamisi.

34. Jumatatu join ya tarehe 8 mwezi wa 11 mwaka 2010, tuliondoka Bristol kwa ndege kuelekea Johannesburg. Tiketi zetu zilikua za daraja la kwanza, na zilikuwa ni tiketi za kwenda na kurudi zikiwa zinaweza badilishwa tarehe muda wowote tutkapohitaji. Tulipofika uwanja wandege tu nilibadili Pound 200 kwenye duka la America Express hapo hapo uwanjani na japokuwa tangazo lilionyesha Pound 1= na R10.83 ;akini baada ya Makati nilipokea Pound 1=10.37.

35. Tulikaa Chitwa Chitwa kuanzia Jumanne mpka Ijumaa ya tarehe 12 mwezi wa 11 mwaka 2010.

36. Nilipokuwa barua pepe kwenye simu yangu ya Blackberry juu ya kuopatikana kwa nafasi ya chumba katika hotel ya Cape Grace huko Cape town, siku ya Halhamisi tarehe 11, mwezi wa 11 mwaka 2010 mnamo saa 10 kamili.

Cape town- Ijumaa

37. Siku ya Ijumaa asubuhi tuliondoka kutoka Chitwa Chita kuelekea Cape Town na tulifika kati ya saa 10 kamili na saaa 10 na nusu.

38. Tulipofika nilienda kutafta tax wakati Anni alibaki akiwa na mizigo yetu. Hakukuwa na maafisa uhamiaji au wa forosha kwakuwa safari ya ndege ilikuwa ya ndani na watu wa kwanza kuzungumza nao ndani ya Cape Town lilikuwa kundi la madereva tax. Mmoja wao aliuliza kama ninahitaji huduma ya usafiri wa tas. Nilimwambia kwambaninahitaji usafiri wa tax kueleke ahoteli ya Cape Grace. Akadai kwamba yeye hupeleka sana wasafiri wenye hadhi kwenye hiyo hoteli. Alidai kuwa akichukua tax kwa mtu mwingine atatozwa R350 ila yeye atamtoza R250 na alijitambulisha kwake kwa jina la Robert Tongo, ambaye kwa sasa namfahamu kwa majina yake yote kwamba ni Zola Robert Tongo (ambapo kuanzia sasa nitakuwa ninamtaja kwa jina la Tongo). Nilimtaarifu kwamba mke wangu alikuwa bado yuko ndani na mizigo yetu. Mimi nayeye tuliongozana na nilimtabulisha kwa ANni na tukamtajia majina yetu. Tongo alikuwa akizungumza lugha ya Kingereza kwa ufasaha na alionekana kuwa mkarimu. Aliuliza tulikotoka na nini kilituleta Cape Town. Nilimwambia tunatoka UK na Anni alidakia kasema yeye natoka Sweden. Alistaajabu na kusema kuwa alidhani sisi tulikuwa Wahindi na tulikuwa kwenye fungate. Niligundua kuwa gari lake bado safi na nzima.

39. Wakati tukiwa safarini kuelekea hotelini maongezi yaliendelea baina yetu na tulimtaarifu kuwa tuko kwenye matembezi na tutakuwa Cape town kwa siku kadhaa.

40. Anni laimwambia kuwa hii safari ya kuja Afrika Kusini ilikuwa ni surprise kwa ajili yake, na akaendelea kumwambia kuwa niliwahi kumsuprise siku za nyuma kwa kumpeleka paris kwa ndege binafsi ya kukodi kwa ajili ya kumvisha pete ya uchumba. Alitaja majina ya baadhi ya watu wanaotokea Uingereza lakini kati yao hakuna tuliyemfahamu. Alituambia baadhi ya vitu vya kufanya tukiwa capetown na sehemu za kutembelea na alijitolea kuwa kiongozi wa msafara wetu wa matembezi. Alitaja baadhi ya vitu kama safari ya mvinyo wakati wa mchana, kusunguka mji wakati wa usku, kupanda mlima wa Table. Pia alighusia kuhusu kwenda kutazama nyangumi. Alikuwa akijaribu kutushawishi kwa kutaja vitu anavyoweza kutuonyesha. Na aktika hiyo safari alituonyesha baadhi ya vitu na kumbuka alituonyesha hospitali ambapo alidai operasheni ya kwanza ya moyo ilifanyika duniani. Alituambia kuwa ni mseja na anafurahia kuishi maisha ya kiseja. Pia tulimwambia kuhsu safari yangu ya kufanyiwa tafrija ya kuaga useja huko Las Vegas na safari ya Helkopta niliyoandaa na marafiki na kwa wakati huu nilikuwa nikiwaza niandae moja kwa ajili ya Anni kama surprise.

41. Pia katika mazungumzo kuna muda Anni alimwambia kuwa familia zetu mbili zilihudhuria harusi yetu huko India iliyofanyika kwa wiki nzima, hivyo tumechoka tunahitaji kupumzika na kupumua.

42. Tulipofika hotelini Anni alitangulia mapokezi na mizigo huku mimi nikibaki nyuma ili nimpe malipo yake. Nikiwa nje sikuweza kumona Anni akiwa mapokezi kwakuwa madirisha yalikuwa ya vioo vinavyoonyesha ndani. Tango alinihakikishia kuwa nauli ilikuwa R250 kama alivyoniambia pale uwanja wa ndge na nilimlipa pesa yake. Wakati namlipa pesa yake alisisitiza kuwa yuko tayari kutusaidia kuzunguka na kutuonyesha vivutio kama tutakuwa tumeridhika na huduma yake.

43. Hapo ndipo nilipomuuliza ni wapi ninapoweza kuandaa safari binafsi ya helkopta kama surprise kwa Anni. Alinijibu kuwa hilo haliwezi kuwa tatizo ana mtu anayeweza timiza hilo. Akadai atanipatia bei nzuri kwakua anafahamiana na rubani anayerusha ndege kwa ajili ya matembezi kwenye kampuni flani na anadhani atafurahi sana kuwatembeza. Tango alinipa business card yake na niliandika namba yake na kuihifadhi kwenye Blackberry yangu. Nilimwambia kuwa nitampigia simu baadae kwakuwa muda huo inabidi nielekeed mapokezi nataka nibadilishiwe chumba nipewe chenye hadhi zaidi, akajibu kuwa bado ana muda wakutosha ngoja aegeshe gari akanionyesha nafasi ya maegesho iliyowazi na kuniambia nitamkuta hapo nikimalizana na shughuli huko mapokezi.

44. Nilimkuta Anni akiwa mapokezi niliongea na mhudumu kama anaweza kutbadilishia chumba tupate chumba chenye hadhi ya fungate, na alijibu kuwa chumba cha hivyo kimekwisha chukuliwa mpaka Jumatatu ila ataona afanye nini kutusaidia. Tulijadiri kuhusu wapi tukale chakula cha usiku na tukachagua Sevuga na kusema tutaenda kula saa 3 na nusu usiku. Nilimwambia Anni kuwa naenda nje kuzungumza na dereva tax kuhusu kututembeza. Anni alinijibu kuwa yeye ataelekea chumbani kwakiuwa anataka kuanza kujiandaa. Nilitoka nje nikaenda kuzungumza na Tongo alikuwa kaka kwenye siti ya dereva na alinipungia mkono akinielekeza niingie nikae kwenye siti ya abiria. Alianza kwa kuniuliza tutakaa kwa muda gani Cape Town, nilimjibu tutakaa kwa siku chache bila kutaja ni sku ngapi. Alianza kurudia kuniambia juu ya kututembeza ila mimi nilimwambia ninachohitaji ni safari ya kuzunguka mji kwa helkiopta. Aliniambia kuwa helkopta uwa haziruki mbali sana kutoka kwenye hoteli, ila kasema kwamba mtu anaweza kufaidi mandhari ya mji ikiwa ataenda kenye milima ya Table kwa kutumia usafiri wa gari zinazosafiri kupita kwenye nya. Alitaja baadhi ya majina ya vivutio ambayo siwezi yakumbuka.

45. Mimi nilisisitiza kuwa ninachohitaji ni safari ya helkopta sawa na niliyopanda nikiwa Las vegas na pia nilirudia kumuhathia safari yangu na Anni kwa kutumia ndege binafsi kuelekea paris. Kulikuwa na viti sita kwa ajili ya abiria lakini vyote vilikuwa wazi na hivyo ilituwezesha mimi na Anni kupata burudani wakati tukiwa angani kwa maana nyuma tulikuwa peke yetu. Alisema inawezekana kuandaa kitu kama hicho na anadhani itakuwa kati ya R20,000-25,000, na mimi nilimjibu akiweza kuandaa safari hiyo kwa R15,000 niko tayari. Nilitaja hiki kiasi nikiwa nimehisi makisio yake yalikuwa makubwa na mimi nilitaja kutokana na kiasi nilicholipa nikwa La Vegas. Alinijibu kuwa atazungumza na rubani aone atakachosoema, mimi nilimwambia Jumapili ingekuwa siku nzuri kwa ajili ya safari hiyo.


Inaendelea #35
 
kwa shren myb sabab alkua shoga au sabab nyingine anayoijua yeye!!

kwa wasauzi ni tamaa ya pesa tuu! na mtindo huo sauz ni comon sana SA pekee kwa mwaka sio chini ya polisi 700 wanauawa
unaeza ukaona apo SA sio salama kwa mgeni!!!
Mpaka sasa unahisi Shrien ni masterplan?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom