McLaren
JF-Expert Member
- Feb 19, 2025
- 889
- 2,863
chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kimemteua Salum Mwalimu kugombea urais wa Tanzania katika uchaguzi mkuu Oktoba 2025.
Salum alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar kabla ya kuhamia CHAUMMA.
Wakuu,
Leo ndo tutajua nani atachaguliwa na CHAUMMA kuwa mgombea wake wa Urais.
Kumekuwa na tetesi kuwa baada ya kutuma wanae, leo Mwamba ndo ataibuka rasmi kwenye chama hicho na huenda akachaguliwa kuwa mgombea Urais
Kaeni karibu na uzi huu kujua nini kitajiri
===================================
Kinachoendelea Chaumma Mlimani City Dar
Ni wajumbe wa mkutano mkuu maalumu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma) wakisalimiana na kujadiliana katika makundi kwenye Ukumbi wa Malimani City, jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi Agosti 7, 2025.
Pamoja na mambo mengine, mkutano huo utapokea na kupitisha Ilani ya Uchaguzi Mkuu 2025/2030 na kuchagua au kumthibitisha mgombea urais wa Tanzania na Zanzibar.
View: https://www.youtube.com/watch?v=DBvaWPPGArE
Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mhe. Hashimu Rungwe amewasili katika ukumbi wa Mlimani City katika Mkutano Mkuu wa CHAUMMA Kuteua Mgombea Urais wa chama hicho.
Mwakilishi wa Chama cha Demokrasia na maendeleo ambaye pia mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Mwanga bwana Lawrence Mchome katika Mkutano Mkuu wa CHAUMMA Kuteua Mgombea Urais wa CHAUMMA
Mrema kuhusu ilani ya chama
"Mrema amesema kuwa CHAUMMA kwenye ilani yake imezingatia kikamilifu mahitaji ya watu wenye ulemavu kwahiyo ilani yetu itakapotoka tunaomba muipitie"
Maduu Wiliam kilio kikubwa cha Asasi za kiraia ni ulinzi wa haki za binadamu
Ndugu Maduu Wiliam kwa niaba ya kituo cha sheria na haki za biandamu akitoa salamu katika mkutano wa CHAUMMA Amesema kilio kikubwa cha Asasi za kiraia ni ulinzi wa haki za binadamu kwa nguvu zote na ulinzi wa utawala wa sheria.
Lawrence Mchome kuhusu naibu Mwenyekiti wa CHADEMA
akiwa nje ya Ukumbi mwakilishi wa CHADEMA kwenye mkutano wa CHAUMMA Lawrence Mchome amesema kuwa amejaribu sana kumshauri Heche lakini kiongozi huyo hashauriki.
Chama cha Ukombozi wa umma CHAUMMA kimemchagua Salum Mwalimu kuwa mgombea urais
Chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMMA kimemtangaza Salum Mwalim Juma kuwa Mgombea wao wa Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu.
Hayo yamejili leo hii katika mkutano mkuu wa chama hicho unaoendelea mda huu katika ukumbi wa Mlimani City.
Salum alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar kabla ya kuhamia CHAUMMA.
Wakuu,
Leo ndo tutajua nani atachaguliwa na CHAUMMA kuwa mgombea wake wa Urais.
Kumekuwa na tetesi kuwa baada ya kutuma wanae, leo Mwamba ndo ataibuka rasmi kwenye chama hicho na huenda akachaguliwa kuwa mgombea Urais
Kaeni karibu na uzi huu kujua nini kitajiri
===================================
Kinachoendelea Chaumma Mlimani City Dar
Ni wajumbe wa mkutano mkuu maalumu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma) wakisalimiana na kujadiliana katika makundi kwenye Ukumbi wa Malimani City, jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi Agosti 7, 2025.
Pamoja na mambo mengine, mkutano huo utapokea na kupitisha Ilani ya Uchaguzi Mkuu 2025/2030 na kuchagua au kumthibitisha mgombea urais wa Tanzania na Zanzibar.
View: https://www.youtube.com/watch?v=DBvaWPPGArE
Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mhe. Hashimu Rungwe amewasili katika ukumbi wa Mlimani City katika Mkutano Mkuu wa CHAUMMA Kuteua Mgombea Urais wa chama hicho.
Mwakilishi wa Chama cha Demokrasia na maendeleo ambaye pia mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Mwanga bwana Lawrence Mchome katika Mkutano Mkuu wa CHAUMMA Kuteua Mgombea Urais wa CHAUMMA
Mrema kuhusu ilani ya chama
"Mrema amesema kuwa CHAUMMA kwenye ilani yake imezingatia kikamilifu mahitaji ya watu wenye ulemavu kwahiyo ilani yetu itakapotoka tunaomba muipitie"
Maduu Wiliam kilio kikubwa cha Asasi za kiraia ni ulinzi wa haki za binadamu
Ndugu Maduu Wiliam kwa niaba ya kituo cha sheria na haki za biandamu akitoa salamu katika mkutano wa CHAUMMA Amesema kilio kikubwa cha Asasi za kiraia ni ulinzi wa haki za binadamu kwa nguvu zote na ulinzi wa utawala wa sheria.
Lawrence Mchome kuhusu naibu Mwenyekiti wa CHADEMA
akiwa nje ya Ukumbi mwakilishi wa CHADEMA kwenye mkutano wa CHAUMMA Lawrence Mchome amesema kuwa amejaribu sana kumshauri Heche lakini kiongozi huyo hashauriki.
Chama cha Ukombozi wa umma CHAUMMA kimemchagua Salum Mwalimu kuwa mgombea urais
Chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMMA kimemtangaza Salum Mwalim Juma kuwa Mgombea wao wa Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu.
Hayo yamejili leo hii katika mkutano mkuu wa chama hicho unaoendelea mda huu katika ukumbi wa Mlimani City.