Nyakijooga
JF-Expert Member
- Dec 9, 2018
- 427
- 666
Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu amesema kwamba hawaogopi kukabiliana na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi Mkuu 2025 kwamba Chama hicho kitashiriki.
Amesema kwamba katika uchaguzi huo wataweka wagombea kwenye Kata na majimbo yote nchini, kwamba hawezi kuiacha CCM bila kupingwa au bila ushindani madhubuti.
Amewatangazia wote wenye nia za kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi Mkuu waanze kutangaza nia zao.
Aidha amesema kwamba Mei 30, 2025 wanatarajia kuzindua operesheni maalum Mkoani Mwanza kwa ajili ya kukijenga Chama, ambapo amesema kwamba kwa siku 16 watanzunguka mikoa yote nchini.
“Kuanzia Tarehe 30 Mei 2025,Tutakuwa na uzinduzi wa C4C itakayofanyika jijini Mwanza hivyo wanachama wote wa chaumma nendeni mkajiandae na Ujio wa ugeni huu tutapiga ziara angani na ardhini ” Katibu Mkuu Chaumma Tanzania,Salum Mwalimu.
Amesema kwamba katika uchaguzi huo wataweka wagombea kwenye Kata na majimbo yote nchini, kwamba hawezi kuiacha CCM bila kupingwa au bila ushindani madhubuti.
Amewatangazia wote wenye nia za kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi Mkuu waanze kutangaza nia zao.
Aidha amesema kwamba Mei 30, 2025 wanatarajia kuzindua operesheni maalum Mkoani Mwanza kwa ajili ya kukijenga Chama, ambapo amesema kwamba kwa siku 16 watanzunguka mikoa yote nchini.
“Kuanzia Tarehe 30 Mei 2025,Tutakuwa na uzinduzi wa C4C itakayofanyika jijini Mwanza hivyo wanachama wote wa chaumma nendeni mkajiandae na Ujio wa ugeni huu tutapiga ziara angani na ardhini ” Katibu Mkuu Chaumma Tanzania,Salum Mwalimu.