Salma Kikwete: Ni nani?

haki ya nani ipo siku mtasikia au kuona laivu anakagua gwaride. na hao wakuu wa mikoa in maana hawajui itifaki? risala anasomewa ili atoe taarifa gani kwa nani? nijuacho mimi hatima ya risala ni kufikisha ujumbe kunakotakiwa na penye uwezekano majibu au ahadi zitolewe. sasa mwalimu wangu salma, ana majibu gani juu ya mambo mazito ya nchi? kaaaazi kweli kweli, hata mimi sijui anpokwenda mikoani ankwenda kwa nafasi ipi. may be ankuwa amemwakilisha mkuu wa nchi. vinginevyo nadhani si sahihi kufanyiwa afanyiwavyo. kama ingekuwa kukagua maendeleo ya ka epa kake ka wama binafsi sioni tatizo.
 
hivi chuo cha diplomasia kurasini haruhusiwe kwenda kupiga msasa kidogo? au serikali haiwezi mpatia mwl binafsi akawa anaenda ikulu kumpiga msasa? au kama hilo haliwezekani, basi chuo nje ya nji, au mwl toka majuu? au marafiki ambao wamepitia mambo ya protocol hawawezi saidia? au vijarida kuhusu nini kinacho tegemea toka kwa Nke wa raisi? au UN hawa institution kwa ajili ya kuwa train staff wao ambapo Mama wa Kwanza anaweza kwenda kupata Ilimu kidogo, ya haya mambo ya Protokali na nini kinachotegemewa toka kwake?
Ama sivyo Werema aanmze taratibu za kubadili katiba yetu ili iweze kwenda na nia ya Mama wa kwanza kushiriki/kumsaidia Raisi katika Shughuli za kiutendaji, na hata ikiwezekana watoto na ndugu wengine wa familia na marafiki/swahiba.
 
Ndio kazi ya First Ladies wa Tanzania kuzurura zurura tu na kusumbua wanchi kupanga foleni kumpokea.
 
Salma Kikwete ni first lady, ana haki ya kikatiba ya kupewa ulinzi kwa nafasi yake. Hata waliotangulia walikuwa wakipewa ulinzi. Ila hilo la kupewa taarifa za maendeleo ya mkoa/wilaya si sahihi, kwani yeye hana MAMLAKA ya kutoa maamuzi. Taarifa za maendeleo hazitolewi kama hadithi, lakini kwa kumsomea huyo mama ni sawa na kusoma hadithi. Anachokifanya sasa hivi ni kampeni ya kumsaidia mumewe.

Hakuna nongwa kwa yeye kupewa ulinzi, yeye ni a part of our president na tunatakiwa kumlinda. Lakini kwanini apokee risala kuhusu maendeleo toka kwa wakuu wa wilaya, at what capacity. Kama ni mambo yanayohusiana na chama haina neno, lakini yanayohusiana na serikali ni tatizo, hata kama ni hadithi still ni tatizo why should that happen? Inawezekana watu hawajui itifaki au wanafanya kwa kujipendekeza au ni wajinga hawajui wanachofanya.
 
Waungwana mjue Tz kwa sasa haina katiba, inaendeshwa kwa nguvu za Mungu tu, ndo maana Hata Mh. Karume tar. 12 Jan, 2010 alipokea kiapo cha utii na kupigiwa mizinga 21kutoka JWTZ wakati Bwana mkubwa Mh. Kikwete akiwa mtu wa kawaida, na akimwaga tabasamu la ki-hand some.
Hivi hamjui kuwa tuliliwa zamani hayo ni makombo?
 
haki ya nani ipo siku mtasikia au kuona laivu anakagua gwaride. na hao wakuu wa mikoa in maana hawajui itifaki? risala anasomewa ili atoe taarifa gani kwa nani? nijuacho mimi hatima ya risala ni kufikisha ujumbe kunakotakiwa na penye uwezekano majibu au ahadi zitolewe. sasa mwalimu wangu salma, ana majibu gani juu ya mambo mazito ya nchi? kaaaazi kweli kweli, hata mimi sijui anpokwenda mikoani ankwenda kwa nafasi ipi. may be ankuwa amemwakilisha mkuu wa nchi. vinginevyo nadhani si sahihi kufanyiwa afanyiwavyo. kama ingekuwa kukagua maendeleo ya ka epa kake ka wama binafsi sioni tatizo.

watu mna mawazo jamani
 
Wanajamii Forums wenzangu habari za siku tele.

Nimekuwa kimya sana kwenye Mtandao kwa sababu nilikuwa Kijijini kwetu Likzo.

Suala la Mama Salma Kikwete kuwa KIMBELEMBELE ni kulinda Maslahi yake. Maana naambiwa na wadau kwamba HAYUPO peke yake kwa Bw. Kikwete. Sasa anachofanya ni kuwaonyesha hao Wanawake wengine kwamba yeye ndiyo "MKE WA RAIS" na siyo wao wengine.

Nasikia Kule Zanzibar kuna Mke mwenzake mmoja Msomi sana mwenye Phd na ni Mzuri sana kuliko mwanamke uliyewahi kumuona wewe.

Lakini hili la yeye kujiingiza katika masuala haya ndo nasema Urais siyo kikwete Urais ni Taasisi, kiasi kwamba hata asipokuwepo Kikwete Urais utakuwepo tu.

Kuna haja ya:

1. Kwenye Mahakama ya Katiba kuona tafsiri ya Mipaka ya MKe wa Rais anatakiwa kufanya nini?

Maana tukiachia hivi atakuja kwenda Mikoani na kupewa taarifa za "SIRI" za Usalama wa Taifa wakati yeye siyo tu siyo Mtumishi wa Umma lakini siyo pia Kiongozi wa Umma lakini pia hajaapishwa kulinda na kutunza Siri za Nchi.

Mimi nashangaa sana.

Hivi kweli Taasisi ya Rais inafanya kazi ya kumshauri Rais kweli?

HUUU NI UJINGA ambao hapa ndipo unapoona Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wetu walivyo "WAPUMBAVU" kwa sababu wanamsomea taarifa kama nani? na nani kampa Mamlaka?

Huku ni kuwajibika kwa kusubili fadhila ya aliyewateua kwamba wanaogopa kumuudhi.

HUU NI UJINGA
 
vipi wewe bana!!! Michele Obama huwa hapati hivyo ulivyouliza?

First lady yoyote duniani ana haki zake na nafasi yake katika nchi ikiwamo hizo hadhi na nafasi... hiyo hadhi ina-extend hadi watoto wa marais

Kuna haja ya kujua protocols za viongozi ili jamii ielewe zaidi

Hakuna ubishi bana umesoma na kuelewa hoja ni nini au basi unaandika tu ? Haki na Hadhi kama mke wa Rais (FL) wote tunafahamu na nimesema hivyo awali swali ni nini nafasi yake katka utumishi wa Umma, mamlaka na madaraka yake au ni sawia na mamlaka na madaraka ya mumewe ? Nisaidie maana unajua protocol za viongozi
 
FLs wahahaki kikatiba kwa sababu tu waume zao ndio viongozi wakuu wa nchi..Maamuzi mengine ya nchi yanaweza yakafanywa na mke wa kiongozi indirectly. Hii unaweza kuona hata katika enzi za simulizi za BIBLIA jinsi ma Malkia walivyo kuwa wakiwaendesha waume zao kufanya maamuzi yaliyo nje ya utashi wao. Kusomewa risala ya maendeleo ya nchi mmmmhh!!!!...Labda alitumwa na mzee!!!
 
Mimi nasikitika anavyomwacha mumewe akizunguka huku na kule peke yake
mwisho ataingia mtegoni jameni:D
asijelaumu akiletewa mke mwenza:confused:
 
Hapa ndugu inabidi upewe elimu ya uraia yaani 'civics' Kwani hufahamu wewe kuwa ulipompigia kura Kikwete kuwa Rais ndipo ulipompigia kura Mama Salma Kikwete kuwa 'First Lady'. Au unafikiri ni suala la utashi wa mtu binafsi kuamua majukumu na haki za mke wa Rais?

Kama wataalam wa 'political science' humu jamvini na wataalam wa sheria wana wakati watakusaidia kielimu. Lakini inategemea na makusudi uliyo nayo katika kuuliza swali, kama lengo ni kujifunza ninaamini utafundishwa tu.

Hakika lengo ni kujifunza na somo la uraia limenipiga chega kama hivyo ndivyo sahihi ya kupewa taarifa za maendeleo na wakuu wa mikoa na wilaya mbona haikuanza kwa mama Maria Nyerere na waliofuatia ? Sina tatizo hata kidogo na majukumu na haki za mke wa Raisi nisaidie kujua mamlaka na madaraka aliyo nayo na tafautisha kati ya Majukumu/Haki na Mamlaka na Madaraka na yameainishwa wapi.
 
Hajui majukumu yake, she is obsessed may be. Labda anataka kuonyesha kuwa yeye ni zaidi kuliko ndugu yake Hawa Ghasia, hivyo inabidi naye atembee watu wamjue kuwa yupo na ana powers (sasa sijui kazitoa wapi) maana hata mfagiaji Ikulu hawezi kumkanya!!
 
FLs wahahaki kikatiba kwa sababu tu waume zao ndio viongozi wakuu wa nchi..Maamuzi mengine ya nchi yanaweza yakafanywa na mke wa kiongozi indirectly. Hii unaweza kuona hata katika enzi za simulizi za BIBLIA jinsi ma Malkia walivyo kuwa wakiwaendesha waume zao kufanya maamuzi yaliyo nje ya utashi wao. Kusomewa risala ya maendeleo ya nchi mmmmhh!!!!...Labda alitumwa na mzee!!!

KICHWA MAJI, Kwa hiyo unataka tuendeshe nchi kwa kutumia hadithi za kwenye biblia, kama huna hoja si ukae kimya,
 
Wakuu Heshima Mbele,
Kiukweli Mke wa Rais anazohaki zake, Mfano haki ya kuwa na usafiri, haki ya kuwa na ulinzi , Kama ambavyo watoto wa Rais wana haki ya kupewa ulinzi pale inapobidi. Kule Marekani shule wanazosoma watoto wa Marais ni eneo maalum la ulinzi, na wale watoto wamepewa secret code za Ulinzi na C.I.A. ,Mfano Obama ni Renegade, Michele ni "Renaissance",Malia Obama's ni "Radiance," na Sasha Obama's ni "Rosebud." ili tu kuimarisha mawasiliano ya kiulinzi kwa emeregence.
Tatizo lililopo ni kwenye mipaka ya kazi, Mke wa Rais anaweza kushiriki kwenye shughuli za kijamii, lakini hii haiko kikatiba kwamba mke wa rais atafanya nini KATIKA KIPINDI CHA URAIS WA MUMEWE, mfano wakati Mkapa anaingia Ikulu Anna alikuwa afisa pale UNICEF, Aliacha shughuli zake na kuanzisha NGO yake ya EOTF.Huyu mama yetu sasa na yeye ana WAMA. Sijui huyo atakayekuja atakuja na kitu gani? Lakini iwepo mipaka Kisheria inayompa mke wa Rais kazi za Kufanya. kama ni Taasisi ijulikane na kila mke wa Rais anayeondoka madarakani aiache ili yule anayeingia aitumie ,Lakini pia ifahamike source ya Funds.

Umeongea viziri mkuu, ila nakufahamisha tu kuwa source za kodi ni mirahaba ya madini yetu,
 
Nafikiri swali hili lingejibiwa na waziri mama Ghasia ili tuweze kujua maana hilo jambo linazidi mipaka.
 
Mie nataka kujua pia hapa jana nimeona Mkuu wa Mkoa wa Mara akisoma Risala mbele ya mama Salma nikajiuliza maswali mengi kichwani bila majibu
Kwani anakazi gani katika nchi mpaka asomewe hiyo Risala ?
Huyu ni co-president. That is why.
 
...Tz jamhuri ya MABWEGE!!!! wachache sana wana akili timamu, waandishi wote wa habari ni mabwege!!

Niko nawe kwa asilimia 100, yule jamaa wa kenya alimwambiaje Mwalimu JK, namnukuu, UNATAWALA MAREHEMU,eti wao wanachojua ni amani na utulivu wakati hata haki zao za msingi hawajui ...mbav..
 
Inasikitisha inauzunisha inafadhaisha sana. Hawa wake wamarais hawana kitu wanafanya ila kutumia vibaya kodi zetu kama alivyo andika mmoja watu hawa watu wanatufanya Tz kichwa chamajiribio. NAIMAN TUNAITAJI KATIBA MPYA NA ITAKAYO WEKA MAMBO YOTE WAZI NASIO HUU UTUMBO VIONGOZ WANAFANYA. Ths is nation and not house of any presdent.
 
Back
Top Bottom