Nadhani huyu mama kwao ni Singida kama sikosei!
Salma Kikwete ni mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Twawala. Mkuu wa Mkoa ni mteuliwa wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Kada wa Chama Twawala. Hivyo ili uwe karibu na Rais lazima umkirimu mke wake na jamaa zake wa karibu. Hivyo usijeshangaa na mtoto wa Rais naye akisomewa risala na mkuu wa mkoa.
Labda tujiulize hivi hawa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wana kazi gani zinazowashughulisha kila siku? Mimi nadhani hizi post zote hazina shughuli yoyote ya maana zaidi ya kuwa vibaraka wa Rais na Chama Tawala.
Walikuwamo wafanyabiashara humo ndani ha ha ha ha kila enzi na tamaduni zek tehetehetehe ni sawa na mama Obama kwenda kufundisha shule , kualikwa katika mazoezi na kufanya kicheni pati za kimarekani kwani si tamaduni tu mnasahau kwamba taasisi yake inamwaga mafedha katika miradi mbalimbali ya wamama na watoto tehe tehe tehe watu bwana wanacha kuulizia chumvi wanaweka taa kwenye mvungu ha ha ha haMkuu hata mimi nashangaa mno, jana pia kafungua shule kabla ya kuhutubia, kweli sioni mantiki ya yeye kufanya yote haya, ziara kibao kama waziri fulani hivi.Hebu tukumbuke Mama Maria Nyerere, Mama Sitti Mwinyi na Mama Anna Mkapa, mbona wao hawakuwa kama yeye? Ndo haki za mwanamke labda.Tuyaacheni jamani tutafuter ugali wetu.
Hii imekaa safi na salama kama salma mwenyewe go big girl go!!!!! hata mke wa chifu uluguruni alikuwa na heshima kubwa na alilindwa kama anavyolindwa chifu anayesema wanawake zenu si wabadala wenu waanze kuzungumza hadharani ha ha ha ha ha ha ha ha nyi nyie jadilini maendeleo na namna ya kuwezesha nchi hii kujamp si kutembea kigoigoi machifu wakifika mahali watu huneemeka kwani hawajui mkono mtupu na hata nyie mlipitishia maombi yenu kwa mama zenu wacheni kudharau ukweli tehe tehe teheGO MAMA SALMA GO......! Usikatishwe tamaa na watu waangaliao karibu.....fanya uonalo vyema.....WAKUBWA TUACHANE KUCHONGA TUMPE HESHIMA YAKE...!
Huwa hawachinji watu baki....ni wao kwa wao
Kwa vile First Lady, anaishi nyumba moja moja na mkuu wa kaya, anafikiri kuwa First Lady ni sahihi kupokea taarifa na ataifikisha kwa mkuu wa kaya..... haa haaa. Hii inanikumbusha Lucy Kibaki , anavyowaingilia na hata kuwapiga vibao watendaji wasiojitambua kule Kenya. Huyu mkuu wa mkoa ni aina ya viongozi ambao mke wa kiongozi anaweza akawafanya lolote, kwani ni watupu! tupu! tupu!
Hebu sikiliza alichosema huyu First Lady, anawambia watu wa Tarime waache kuoa wake wengi!!! Ndiyo maana alihitaji ulinzi wa FFU, kwani alikuwa anasema mambo ambayo si kipaumbele kabisa cha watu wa Tarime.
Inamaanisha,
Kama Salma anapinga kuoa wake wengi je anaupinga uislam? Je mbona na yeye yupo katika ndoa ya wake wengi????