Elections 2010 Salma aeleza sababu kumkampeni Kikwete

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174
Na Heckton Chuwa, Moshi

MKE wa Rais Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete amesema anawajibika kumkampenia mumewe kwa kuwa yeye ni msaidizi mkubwa wa rais katika masuala ya kimaendeleo.

Mama Salma aliyasema hayo juzi, wakati akizungumza na wanawake wa Moshi Mjini, mkoani Kilimanjaro, ambapo pamoja na mambo mengine alimnadi Rais Kikwete, mgombea ubunge wa Moshi Mjini kwa tiketi ya CCM, Bw. Justin Salakana na wagombea wote wa udiwani wa manispaa ya Moshi kwa tiketi chama hicho.

"Mimi kama mwenzi wa Rais ni msaidizi wake mkubwa katika masuala ya maendeleo ya kijamii kupitia taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) na huu ni utaratibu wa kimataifa ambapo wenzi wa viongozi hufanya kazi za kijamii," alisema.


Mama Salma ambaye ameshutumiwa na wapinzani kwa kutumia raslimali za serikali kumkapmeni mumewe, aliendelea kusema kuwa taasisi ya WAMA imechangia masuala mengi ya kimaendeleo, yakiwemo kuwasomesha watoto yatima na wasio na uwezo wa kuchangia eimu kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini bila ubaguzi wa aina yoyote.


"Hata hapa Kilimanjaro mna watoto ambao taasisi hii imewachangia katika elimu na tayari wapo ambao watahitimu kidato cha nne mwaka huu na zaidi ya haya tumeanzisha shule kule Rufiji iitwayo WAMA na KAYAMA na ambayo ina watoto kutoka kila sehemu hapa nchini," alisema.


Aidha alisema taasisi hiyo ya WAMA pia imekuwa ikitoa mchango mkubwa katika kuwaendeleza wajasiriamali mbalimbali hususan akina mama jambo
ambalo limewasaidia kuinua hali zao za maisha.

Kuhusu kampeni zinazoendelea, Mama Salma aliwataka wanaCCM kuepuka kampeni za matusi na kashfa na badala yake wanadi sera za chama hicho tawala.


Akizungumza katika mkutano huo, Naibu Waziri wa Elimu na Ufundi Stadi, Bi. Mwantumu Mahiza, alisema ataweka kambi katika jimbo la Moshi Mjini ili kuhakikisha linampata mbunge kwa tiketi ya CCM.


"Wenzangu wa Moshi Mjini mmemkwaza Rais Kikwete kwa kumchagua mtu ambaye si rahisi kufanya naye kazi kutoka jimbo hili la Moshi Mjini, jamani mwaka huu badilikeni," alisema.
 
"Mimi kama mwenzi wa Rais ni msaidizi wake mkubwa katika masuala ya maendeleo ya kijamii kupitia taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) na huu ni utaratibu wa kimataifa ambapo wenzi wa viongozi hufanya kazi za kijamii," alisema.

Mama Salma ambaye ameshutumiwa na wapinzani kwa kutumia raslimali za serikali kumkapmeni mumewe, aliendelea kusema kuwa taasisi ya WAMA imechangia masuala mengi ya kimaendeleo, yakiwemo kuwasomesha watoto yatima na wasio na uwezo wa kuchangia eimu kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini bila ubaguzi wa aina yoyote.

"Hata hapa Kilimanjaro mna watoto ambao taasisi hii imewachangia katika elimu na tayari wapo ambao watahitimu kidato cha nne mwaka huu na zaidi ya haya tumeanzisha shule kule Rufiji iitwayo WAMA na KAYAMA na ambayo ina watoto kutoka kila sehemu hapa nchini," alisema.

...

Kesi nyingine kwa Chadema (maana wapinzani wengine ni CCM namba 2) maana sheria ya NGO (Reffer BAWATA case) hairuhusu NGO kama WAMA kushiriki siasa, hapa amenasa tena.
 
mwamtumu mahiza yamemshinda kule mkinga-tanga ...ataweza kuweka kambi moshi??...au kama ana bwana anamuwekea kambi....moshi aseme...tu...,maana naona baada ya kutoswa na wananchi anawania ubunge kwa tikti ya wama.......kapu la mama!!!
 
Kesi nyingine kwa Chadema (maana wapinzani wengine ni CCM namba 2) maana sheria ya NGO (Reffer BAWATA case) hairuhusu NGO kama WAMA kushiriki siasa, hapa amenasa tena.

u hit on the bull, yeye anajua wama sio chama cha kisiasa, hatakiwi kufanya hivyo, kama anapenda kufanya hizo kampeni yeye afuatane na huyo mwenza kwenye mikutano yake, sasa mwenza akitaka kumpa nafasi ya kuongea haina neno, lakini sio mwenza anaratiba yake na yeye ana ratiba yake as if na yeye kisheria atakuja kuwa mtoa maamuzi, au mwenza akiugua basi yeye ndio atashika njii.

na zaidi ya hapo hiyo misaada anayojisifia ni hela za nani? ni za kwake baada ya kujinyima matoke ya siku mbili tatu au zinatoka muhimbili, nssf, ppf nk nk, ambazo ni zite, huko kupitia wama ni kujaribu ku-mkeep busy mama otherwise hayo mashirika wangeweza kuzipeleka huko kunako husika bila kumshirikisha.
 
“Wenzangu wa Moshi Mjini mmemkwaza Rais Kikwete kwa kumchagua mtu ambaye si rahisi kufanya naye kazi kutoka jimbo hili la Moshi Mjini, jamani mwaka huu badilikeni,” alisema.
mwisho...

Watu wa Moshi hawana kifafa cha kuanguka-anguka hovyo.

Wana akili, wana pesa, wana maendeleo.

Wanataka kiongozi akisema hivi na afanye. Siyo kupiga kampeni za Nyasi kwa Nyasi na Shuka kwa Shuka.

Upupu kama huo kawamwagie watu wa Rufiji, Kisiju, Lindi, Tanga (na Mtwara kidogo)
 
Back
Top Bottom