kiwiko
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 1,341
- 2,218
Ni mvurugano tu. Mbona makabila hayana hii salamu watu wote wanatumia salamu moja iwe mdogo au mkubwa. Inasemekana hii salamu imetokana na maisha ya utumwa. Kwa nini tumeishikilia kama salamu rasmi ya Kiswahili?
Hivi unajuaje kama mtu uliyekutana nae mara ya kwanza unastahili kumpa shikamoo kwa kumwangalia kwa macho? Ni mtu aliyekuzidi miaka mingapi anastahili hii salamu?
Solution itafutwe salamu moja ya Kiswahili itakayotumiwa na watu wa rika zote kama ilivo salamu za kidini, lugha za kigeni na lugha za makabila yetu. Tuondoe huu mvurugano kwenye jamii. Kama Serikali haina mbadala wa hii salamu itangaze mashindano wananchi wapendekeze mbadala.
C.c. Wizara ya Sanaa na Utamaduni
C.c. BAKITA
C.c. TATAKI
Hivi unajuaje kama mtu uliyekutana nae mara ya kwanza unastahili kumpa shikamoo kwa kumwangalia kwa macho? Ni mtu aliyekuzidi miaka mingapi anastahili hii salamu?
Solution itafutwe salamu moja ya Kiswahili itakayotumiwa na watu wa rika zote kama ilivo salamu za kidini, lugha za kigeni na lugha za makabila yetu. Tuondoe huu mvurugano kwenye jamii. Kama Serikali haina mbadala wa hii salamu itangaze mashindano wananchi wapendekeze mbadala.
C.c. Wizara ya Sanaa na Utamaduni
C.c. BAKITA
C.c. TATAKI