Papaa Muu
JF-Expert Member
- Nov 6, 2018
- 243
- 292
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto) inapenda kuwajulisha wadau wa maendeleo ya jinsia na wanawake pamoja na Watanzania kwa ujumla kuwa Tanzania itaungana na Nchi Nyingine Wanachama wa Umoja wa Mataifa kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa tarehe 8, Machi ya kila mwaka.
Kaulimbiu ya Kitaifa ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2019 inasema: “Badili Fikra Kufikia Usawa wa Kijinsia kwa Maendeleo Endelevu”.
Kwa mwaka huu, Maadhimisho yataendelea kufanyika katika ngazi ya Mkoa ili kutoa wigo mpana kwa wanawake, wadau mbalimbali na kila Mtanzania kutathmini hatua tulizofikia kama Taifa katika masuala ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake na wasichana. Aidha, Maadhimisho haya ni fursa ya kujadiliana namna ya kukabiliana na changamoto katika kufikia Maendeleo jumuishi.
Kaulimbiu ya Kitaifa ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2019 inasema: “Badili Fikra Kufikia Usawa wa Kijinsia kwa Maendeleo Endelevu”.
Kwa mwaka huu, Maadhimisho yataendelea kufanyika katika ngazi ya Mkoa ili kutoa wigo mpana kwa wanawake, wadau mbalimbali na kila Mtanzania kutathmini hatua tulizofikia kama Taifa katika masuala ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake na wasichana. Aidha, Maadhimisho haya ni fursa ya kujadiliana namna ya kukabiliana na changamoto katika kufikia Maendeleo jumuishi.