Sakata la viungo vya binadamu IMTU, Big picture

Sakata la viungo vya binadamu IMTU, Big picture

Hivi hizi kadava huwa zinapatikanaje exactly..??! wanawaibia ndugu marehemu wao au wanafanyaje fanyaje..??! na hata kama wanaagizwa kutoka nje ya nchi.., huko wanakotoka pia wanapatina patikana vipi..??! kuna duka linauza au..??!
 
Hivi hizi kadava huwa zinapatikanaje exactly..??! wanawaibia ndugu marehemu wao au wanafanyaje fanyaje..??! na hata kama wanaagizwa kutoka nje ya nchi.., huko wanakotoka pia wanapatina patikana vipi..??! kuna duka linauza au..??!

Ndio nini hizo?
 
ngoja yakukute ndo utajua kama utakubali au la...nafanya nao kazi wengi and they are good
 
hata muhimbili kuna baadhi wabovu hawako makini na kazi zao kama yule aliefanya operation ya kichwa badala ya mguu
 
We umeulizwa "kadava" maana yake nn?jibu upewe jibu otherwise usituletee misamiati ya kuchosha akili
 
ni wale marehemu wanaotumiwa na imtu kufundishia
 
Hivi ktk taasis kubwa na hatarishi kama hii serikali haijaweka shushu hata mmoja???, kama hakuna uthibiti si imtu inaweza ikawa inatuma wapiga nondo kugonga watu na kuwaletea mizoga????
Mdau hapa haina haja ya shushushu,nimewaskia wanafunzi wa IMTU wanalalamika hapa magic fm,kumbe wao walishailalamikia sana wizara juu ya ujenz wa tanuru la kuteketezea maiti hizo,ila wizara imenyamaza,,,,na hapa hakuna haja ya kamati wala tume,
 
Kwa ushauri wangu hapa si chuo kufungwa ni kuwawajibisha wahusika wakuu, naamini pale chuoni kuna mgawanyo wa kazi na madaraka na ndio maana tunaambiwa tusubirie ripoti ya polisi, watakaowekwa wazi ndio wahusika cha kwanza bila kuangalia vyeo hata kama ni prof wafukuzwe kazi wanyang'anywe nakufutuwa vyeti kabisa, pili washitakiwe kwa mujibu wa sheria za nchi na za haki za binadamu ili iwe fundisho, ka kitengo husika wizara ya afya wasiachwe kabisa sababu naamini kipo pia. Na haya yasimamiwe na waziri vinginevyo ni siasa za kishenzi
 
Cadaver ni miili ya marehemu au marehemu wanaotumika kufundishia somo la maumbile ya mwanadamu(Anatomy) kwa wanafunzi wa vyuo vya tiba kama MUHAS, KCMC na hawa International Medical and Technological University(IMTU) waliosababisha taharuki kwa kutupa hadharani viungo mbalimbali vya Cadaver, Cadaver hupatikana kwenye matukio ya ajali ambapo wale marehemu wasiotambuliwa na ndugu zao huhifadhiwa kwa muda wa kama mwaka mmoja then kama hamna ndugu yeyote aliyejitokeza kudai huo mwili hutumika kama Cadaver, wengine hupatikana kwa kujitolea wenyewe mfano mtu anaandika 'Will'(wosia) kwamba akifa mwili wake utumike kama Cadaver ya kufundishia wanafunzi wa chuo cha tiba, mambo haya hufanyika kwa siri sana na kuna mbadilishano wa Cadaver kati ya nchi moja na nyingine kuepusha mazingira ya uwezekano wa mwanafunzi kukuta mwili wa ndugu yake kutumika kama cadaver, miili hii hudungwa sindano ili kuzuia kuharibika ili itumike kwa muda mrefu na baadaye huharibiwa kwa kuchomwa moto kwenye matanuru maalumu(incinerators) au kuzikwa kwa usiri sana
 
hata muhimbili kuna baadhi wabovu hawako makini na kazi zao kama yule aliefanya operation ya kichwa badala ya mguu

Mtoa mada ngoja upate Ukimwi halafu tutaona utakayemchagua shauri yako
 
IQ zetu bana..ngoja upate ngoma au OI(oportunistic infection) kama kaposis sarcoma uoene kama utachagua daktari..!!

Makubwa sana hayo mkuu, huyu cholera tu au dislocation. ...kama sio deep sitted abscess ya takko
 
Mtoa mada umekurupuka! Kajipange! Kwa hiyo wrong deposition ya viungo vya binadamu ndo kipimo cha utaalamu wa daktari? Pole sana!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Watanzania wengi wajinga sana.
Kwani Doctor ambae bado ni mwanafunzi alihusika vipi na kutupa hiyo miili na vipande vya watu?
Tunapenda sana kwenda na matukio ndio maana siki ya tukio watu waliongea mengi kila mtu na lake

Mwanafunzi anajifunza kila kitu ikiwa ni pamoja na wapi atapata hiyo miili ya watu, ataihifadhi vipi, ataiketeza/au ataificha vipi. ANAHUSIKA na ni shahidi na. 1
 
Back
Top Bottom