Sakata la viungo vya binadamu IMTU, Big picture

Sakata la viungo vya binadamu IMTU, Big picture

Jack Beur

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2010
Posts
222
Reaction score
246
Kama ilivyo kawaida ya Nchi yetu, ni Nchi inayoendeshwa kwa matukio, tukio lililopo kwenye peak kwa sasa ni hili la IMTU na masalia ya viungo vya binadamu, Cadaver remains, si lengo langu kushabikia kile kilichofanyika kwani ni kinyume kabisa na maadili ya kidaktari,Medical Ethics ,na haki za binadamu, Human rights. Hatua stahiki inabidi zichukuliwe dhidi ya wahusika.

Kumejitokeza mtiririko wa matamko mbalimbali,ikiwemo la MAT, Chama cha madaktari Tanzania, Human Rights Center etc, na tutegemee matamko mengine kufuatia. Siyo kitu kibaya ,wanatimiza wajibu wao kuonyesha wako 'alive",( justification for their existance).

Swali la kijiuliza ni iweje kunapotokea tatizo ndo tuone mtiririko wa matamko, kwanini tusiwe na utaratibu wa kuzuia mapema, iweje chuo na hospitali kubwa kama IMTU isiwe na INCINERATOR, ( ikumbukwe mwanafunzi mmoja wa IMTU analipa karibia milioni 6 za tuition fee, kwa wale wa kozi ya udaktari,kuna wanafunzi karibia 800 wa kozi hii, achilia mbali kozi zingine za maabara na Nursing, kweli hawa jamaa wanashindwa kununua incinerator hadi wategemee ile ya Muhimbili, ambayo tunaambiwa ni mbovu ndo maana wakaishia kwenda kutupa viungo hivi huko Bunju, kweli hawa jamaa wanapiga hela, (BIG PROFIT with low running cost ) mashine ya kuchomea taka, tunajua hospitali ni mahali panapozalishwa taka nyingi, Infectious and Biohazard wastes iweje hospitali iendeshwe bila kuwa na mfumo maalumu wa kuteketeza taka, mamlaka husika zinakuwa wapi, wizara ya afya, wizara ya mazingira, wizara ya elimu,Tume ya vyuo vikuu, Medical Association of Tanzania, MAT na wadau wengine, ikiwemo wa nje ya Nchi, make chuo chenyewe kinajitambulisha kama "International" Medical and Technology University,IMTU, je kinakidhi viwango vya kimataifa au ndo yale yale ya Saint flani flani international academy/ English medium school kama tunavyoona kwa hizi shule za english medium school.

Je hakuna utaratibu wa mara kwa mara kuangalia ubora, frequently quality check up kuanzia kwenye curriculum development and adherence, students recruitment/entry grades,staffing/human resources na miundo mbinu,Infrastructures. Kuna taarifa kulifanyika assessment kwenye hiki chuo,ilifanywa na baraza la madaktari wa binadamu na kinywa la Africa Mashariki, ( Medical Association of East Africa) mwaka 2010, mojawapo ya final recommendation ilikuwa ni chuo kisimamishe huduma hadi pale kitakapokidhi 'minimum requirement criteria, je utekelezaji wake uliishia wapi? au ndo mambo ya Nchi ya kitu kidogo.

Pia kuna hili tamko la kukifungia chuo, inawezekana ni tamko stahiki, lakini je tumefikiria hatima ya wanafunzi waliopo hapo chuoni, kuna karibia wanafunzi 1000, wataenda wapi, tukumbuke kuna walio mwaka wa tano, mwaka wa nne, mwaka wa 3, mwaka wa pili,na wa mwaka wa kwanza, waende wapi, na tukumbuke IMTU ndicho chuo chenye Tuition fee kubwa zaidi kuliko vyuo vyote hapa Nchini, wazazi na wanafunzi wataathirika kwa kiasi gani?, is it fair?

Tafakari.

Mwandishi ni medical professional.
 
Mkuu

'Makelele' baada ya matukio inasababishwa na mambo mengi, kubwa ni kubwa Quality Assurance and Control hapa kwetu ni tatizo sana sio tu kwenye suala la IMTU, bali karibia sekta zote. Pengine ni Business Model ya nchi ndio inachangia.
 
Mdau me naona lawama wabebe wizara ya afya na TCU hawalikwepi hili,wao ndo wanaopaswa kutembelea na kukagua,sidhan watu kama MAT wana uhalal wa kisheria kuikagua IMTU wao nafas yao ipo kwenye kulaan tu kama mimi,wewe, na asasi za kiraia,hapo tena sio kuangalia wanafunz wataathirika,ila chuo KIFUNGWE KABISA
 
Kweli mtoa hoja hapo pana shida ya mnyororo wote kwa kiasi tofauti!!!!!!

Hivi kamati ya bunge inayoshughulikia hii sekta ya afya, mazingira na sheria wamesema lolote???!!!
 
Mdau me naona lawama wabebe wizara ya afya na TCU hawalikwepi hili,wao ndo wanaopaswa kutembelea na kukagua,sidhan watu kama MAT wana uhalal wa kisheria kuikagua IMTU wao nafas yao ipo kwenye kulaan tu kama mimi,wewe, na asasi za kiraia,hapo tena sio kuangalia wanafunz wataathirika,ila chuo KIFUNGWE KABISA

Hivi ktk taasis kubwa na hatarishi kama hii serikali haijaweka shushu hata mmoja???, kama hakuna uthibiti si imtu inaweza ikawa inatuma wapiga nondo kugonga watu na kuwaletea mizoga????
 
Je hakuna utaratibu wa mara kwa mara kuangalia ubora, frequently quality check up kuanzia kwenye curriculum development and adherence, students recruitment/entry grades,staffing/human resources na miundo mbinu,Infrastructures. Kuna taarifa kulifanyika assessment kwenye hiki chuo,ilifanywa na baraza la madaktari wa binadamu na kinywa la Africa Mashariki, ( Medical Association of East Africa) mwaka 2010, mojawapo ya final recommendation ilikuwa ni chuo kisimamishe huduma hadi pale kitakapokidhi 'minimum requirement criteria, je utekelezaji wake uliishia wapi? au ndo mambo ya Nchi ya kitu kidogo.
Umeandika ukweli wote, hasa hapo nilipobold. Najiuliza hivi:Je kuna chombo/mamlaka yoyote ya serikali inayosimamia uzingatiaji wa maadili kwenye vyuo vya afya? Kitu kama:Tanzania Medical Practice Authority? Chombo kama hicho ndio kilitakiwa kishinikize IMTU ama kujenga Incinerator yake au kiache kuendesha mafunzo ya udaktari.

Lakini inavyoelekea ni kwamba watendaji wa Wizara ya Afya wanajifungia ofisini mwao wakidhani kwamba kila kitu kiko sawasawa kwenye tasnia ya afya. Sasa, haya ya IMTU yamefichua mengi na kuvuruga mawazo ya watanzania.Ukisoma kwenye mitandao, watu wameanza kuamini kwamba kumbe ndugu zao wanaopotea na kutoonekana tena wanaishia kwenye maabara za vyuo vya afya ili watumike kufundishia madaktari wa mwaka wa kwanza! Serikali kamwe isikae kimya na kuachia haya mawazo yaendelee kuwepo kwenye vichwa vya wananchi. Sitashangaa nitakaposikia maabara ya shule ya udaktari ya UDOM imevamiwa na wananchi wa Dodoma waliopotelewa na mpendwa wao.

Serikali haraka itoe kauli (tamko) haraka kuelezea mabaki ya viungo vya binadamuvilivyoonekana Bunju ni vya watu gani na waliotoka wapi. Ikumbukwe kwamba kwa Dares Salaam kumekuwepo matukio kadhaa ya watu kupotea na kutoonekana tena. Utamzuiaje mtu aliyepotewa na ndugu asiamini kwamba baadhi ya mabaki ya binadamu yaliyo gunduliwa si ya ndugu yake? Serikali haraka itoe tamko la kueleweka kuondoa mawazo haya na ieleze waziwaziitadhibitije hii hali ya utupaji ovyo wa mabaki ili isitokee tena popote hapa nchini.
 
Hili sakata inabidi kuwe na mnyororo wa watu wanaochukuliwa hatua kuanzia chuoni, taasisi zote zinazohusika kama tcu, hadi wizarani.
 
Kwani yale majengo na eneo la IMTU yalimilikiwa na nani kwanza na IMTU iliyapataje? na kwa style gani.na nani alifanikisha hiyo move? tuanzie hapo kwanza manake lazma kuna mkono wa mkubwa pale
 
Hivi ktk taasis kubwa na hatarishi kama hii serikali haijaweka shushu hata mmoja???, kama hakuna uthibiti si imtu inaweza ikawa inatuma wapiga nondo kugonga watu na kuwaletea mizoga????

unawaamin hao mashushushu??,me siwaamin kivile ila mrad wapo wache nao wapate ugal wao
 
Kwani yale majengo na eneo la IMTU yalimilikiwa na nani kwanza na IMTU iliyapataje? na kwa style gani.na nani alifanikisha hiyo move? tuanzie hapo kwanza manake lazma kuna mkono wa mkubwa pale

Inawezekeana kuna mmiliki lakini hana uhusiano na waendeshaji waliopo pale yeye anakula kodi yake tu, la msingi tujiulize nani mkaguzi wa taasisi kama hizi ndipo pa kuanzia
 
Kama ilivyo kawaida ya Nchi yetu, ni Nchi inayoendeshwa kwa matukio, tukio lililopo kwenye peak kwa sasa ni hili la IMTU na masalia ya viungo vya binadamu, Cadaver remains, si lengo langu kushabikia kile kilichofanyika kwani ni kinyume kabisa na maadili ya kidaktari,Medical Ethics ,na haki za binadamu, Human rights. Hatua stahiki inabidi zichukuliwe dhidi ya wahusika.

Kumejitokeza mtiririko wa matamko mbalimbali,ikiwemo la MAT, Chama cha madaktari Tanzania, Human Rights Center etc, na tutegemee matamko mengine kufuatia. Siyo kitu kibaya ,wanatimiza wajibu wao kuonyesha wako 'alive",( justification for their existance).

Swali la kijiuliza ni iweje kunapotokea tatizo ndo tuone mtiririko wa matamko, kwanini tusiwe na utaratibu wa kuzuia mapema, iweje chuo na hospitali kubwa kama IMTU isiwe na INCINERATOR, ( ikumbukwe mwanafunzi mmoja wa IMTU analipa karibia milioni 6 za tuition fee, kwa wale wa kozi ya udaktari,kuna wanafunzi karibia 800 wa kozi hii, achilia mbali kozi zingine za maabara na Nursing, kweli hawa jamaa wanashindwa kununua incinerator hadi wategemee ile ya Muhimbili, ambayo tunaambiwa ni mbovu ndo maana wakaishia kwenda kutupa viungo hivi huko Bunju, kweli hawa jamaa wanapiga hela, (BIG PROFIT with low running cost ) mashine ya kuchomea taka, tunajua hospitali ni mahali panapozalishwa taka nyingi, Infectious and Biohazard wastes iweje hospitali iendeshwe bila kuwa na mfumo maalumu wa kuteketeza taka, mamlaka husika zinakuwa wapi, wizara ya afya, wizara ya mazingira, wizara ya elimu,Tume ya vyuo vikuu, Medical Association of Tanzania, MAT na wadau wengine, ikiwemo wa nje ya Nchi, make chuo chenyewe kinajitambulisha kama "International" Medical and Technology University,IMTU, je kinakidhi viwango vya kimataifa au ndo yale yale ya Saint flani flani international academy/ English medium school kama tunavyoona kwa hizi shule za english medium school.

Je hakuna utaratibu wa mara kwa mara kuangalia ubora, frequently quality check up kuanzia kwenye curriculum development and adherence, students recruitment/entry grades,staffing/human resources na miundo mbinu,Infrastructures. Kuna taarifa kulifanyika assessment kwenye hiki chuo,ilifanywa na baraza la madaktari wa binadamu na kinywa la Africa Mashariki, ( Medical Association of East Africa) mwaka 2010, mojawapo ya final recommendation ilikuwa ni chuo kisimamishe huduma hadi pale kitakapokidhi 'minimum requirement criteria, je utekelezaji wake uliishia wapi? au ndo mambo ya Nchi ya kitu kidogo.

Pia kuna hili tamko la kukifungia chuo, inawezekana ni tamko stahiki, lakini je tumefikiria hatima ya wanafunzi waliopo hapo chuoni, kuna karibia wanafunzi 1000, wataenda wapi, tukumbuke kuna walio mwaka wa tano, mwaka wa nne, mwaka wa 3, mwaka wa pili,na wa mwaka wa kwanza, waende wapi, na tukumbuke IMTU ndicho chuo chenye Tuition fee kubwa zaidi kuliko vyuo vyote hapa Nchini, wazazi na wanafunzi wataathirika kwa kiasi gani?, is it fair?

Tafakari.

Mwandishi ni medical professional.

Wizara kesho utasikia tume imeundwa, kesho kutwa kamati teule ya bunge nk, nk, hayo ndo maisha yetu ya kill siku. Cinema ya UKAWA! ESCROW na nyingine nyingi hakuna majibu na kabla jibu la IMTU halijapatikana itakuja cinema ingine tupo na utaona mkuu.
 
Kumthamini na kuheshimu binadamu mwenzako sio katika uhai tu hata katika kifo.

Hebu jiulize daktari aliyepata mafunzo kwenye chuo ambacho wakufunzi wake wamekosa ethics kwa kiwango kikubwa kiasi hiki ataweza kweli kumthamini mgonjwa akienda kwake kupata huduma!!!!!!!!!!!

Ndio maana professionals wengi siku hizi hawana maadili, wanajifunza from the best waliobobea katika kuiuka kanuni na kuvunja sheria. Wanafunzi wanaona lecturer kafanya jambo fulani and he got away with it, hakuna hatua iliyochukuliwa dhidi yake na wao watafanya tu wakijua hakuna adhabu juu yao.

Ndio maana kila mahali unapoenda kutafuta huduma watendaji wako wako tu sio walimu, madaktari, polisi, waandishi wa habari na hata hao wanaotoa matamko kama wangekuwa wanafanya kazi zao ipasavyo sidhani kama kuna institution yeyote ya afya ingekosa incenerator
 
Nawapongeza IMTU kwa kudhihirishia umma kwamba shule ya pale ina practicals za kutosha sana kwa wanafunzi wake!
 
Jamani eee! pamoja na yoote hayo ulioongea mimi naomba tu unijulishe hizo maiti walizipata wapi? je ni watu wanaofia hapo hospital na kukosa ndugu wa kuwachukuwa? au ni mitego iliwekwa kupata hizo maiti? Au walizinunua? Unajua kuna ndugu zetu wanapoteaga na kutafutwa bila mafanikio ... isije ikawa wamo humo!
 
Inawezekeana kuna mmiliki lakini hana uhusiano na waendeshaji waliopo pale yeye anakula kodi yake tu, la msingi tujiulize nani mkaguzi wa taasisi kama hizi ndipo pa kuanzia

mkuu tutafute facts. Hii nchi ina mengi mno.
 
Back
Top Bottom