Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,915
- 30,259
SAKATA LA SHEIKH PONDA: MASIKINI "MASHEIKH RASMI" HAWAJUI KUWA HAWANA WAISLAM WANAOWAONGOZA, WAKO PEKE YAO
Awali ya yote mimi sitajiingiza katika propaganda za uchaguzi bali nitajaribu kueleza hali ya Waislam ilivyo.
Kwanza ni kuwa Waislam toka ilipovunjwa EAMWS na serikali mwaka wa 1968 na Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir kukamatwa na kufukuzwa nchini na serikali kuwaundia Waislam BAKWATA, Waislam wameishi na kinyongo miaka yote sasa inafika nusu karne.
Ndiyo unasikia lugha za "sheikh wa BAKWATA," Waislam wakijiweka mbali na BAKWATA.
Na ukweli ni kuwa BAKWATA haijaweza kukubalika na sababu ni ndogo kuwa si taasisi iliyoundwa na Waislam wenyewe.
Matokeo yake ni kuwa katika hii jamii kubwa ya Kiislam Waislam wana viongozi wao wanaowakubali, kuwaamini, kuwapenda na kuwasikiliza wanachowaambia.
Sheikh Ponda ni mmoja wa masheikh hawa.
Sheikh Ponda amewaeleza Waislam nani adui ya Waislam wa Tanzania na akasimama kupambana na adui huyu huku akiungwa mkono na Waislam wengi sana.
Katika juhudi hizi Sheikh Ponda kakutwa na shida nyingi.
Kalipa kwa ajili ya Allah kwa machozi na damu.
Kwa damu yake na machozi ya nduguze Waislam.
Nimeweka hapa FB makala fupi ya maisha ya Sheikh Ponda katika kuwatumikia Waislam sasa mtafute sheikh yeyote wa BAKWATA ambae amepata kusimama na Waislam katika dhiki na shida zao.
Hakuna.
Katika hali kama hii ni tabu sana kujaribu kumchafua sheikh kwa propaganda hizi za uchaguzi kwa kuwa Waislam wanamjua Ponda ni nani.
Ponda anawakilisha sauti ya Waislam wengi, wengi, wengi sana.
Wako waliotambua hili na wamejua nini wafanye waweze kupata kura za Waislam.
Hawa ni watu wenye kufikiri na kukubali ukweli kuwa Waislam wanaishi na kinyongo dhidi ya utawala kwa miaka mingi.
Hawa wametumia fursa hii kwa kuhaidi kutoka haki na fursa sawa kwa wote.
Ndiyo maana hujasikia Waislam wamefanya maandamano kumpinga Sheikh Ponda.
Wanaompinga Sheikh Ponda si masheikh bali ni "masheikh wa BAKWATA."
Chunguza.
Picha: Kulia ni Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir (1880 - 1979) na kushoto ni Sheikh Issa Ponda.
Awali ya yote mimi sitajiingiza katika propaganda za uchaguzi bali nitajaribu kueleza hali ya Waislam ilivyo.
Kwanza ni kuwa Waislam toka ilipovunjwa EAMWS na serikali mwaka wa 1968 na Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir kukamatwa na kufukuzwa nchini na serikali kuwaundia Waislam BAKWATA, Waislam wameishi na kinyongo miaka yote sasa inafika nusu karne.
Ndiyo unasikia lugha za "sheikh wa BAKWATA," Waislam wakijiweka mbali na BAKWATA.
Na ukweli ni kuwa BAKWATA haijaweza kukubalika na sababu ni ndogo kuwa si taasisi iliyoundwa na Waislam wenyewe.
Matokeo yake ni kuwa katika hii jamii kubwa ya Kiislam Waislam wana viongozi wao wanaowakubali, kuwaamini, kuwapenda na kuwasikiliza wanachowaambia.
Sheikh Ponda ni mmoja wa masheikh hawa.
Sheikh Ponda amewaeleza Waislam nani adui ya Waislam wa Tanzania na akasimama kupambana na adui huyu huku akiungwa mkono na Waislam wengi sana.
Katika juhudi hizi Sheikh Ponda kakutwa na shida nyingi.
Kalipa kwa ajili ya Allah kwa machozi na damu.
Kwa damu yake na machozi ya nduguze Waislam.
Nimeweka hapa FB makala fupi ya maisha ya Sheikh Ponda katika kuwatumikia Waislam sasa mtafute sheikh yeyote wa BAKWATA ambae amepata kusimama na Waislam katika dhiki na shida zao.
Hakuna.
Katika hali kama hii ni tabu sana kujaribu kumchafua sheikh kwa propaganda hizi za uchaguzi kwa kuwa Waislam wanamjua Ponda ni nani.
Ponda anawakilisha sauti ya Waislam wengi, wengi, wengi sana.
Wako waliotambua hili na wamejua nini wafanye waweze kupata kura za Waislam.
Hawa ni watu wenye kufikiri na kukubali ukweli kuwa Waislam wanaishi na kinyongo dhidi ya utawala kwa miaka mingi.
Hawa wametumia fursa hii kwa kuhaidi kutoka haki na fursa sawa kwa wote.
Ndiyo maana hujasikia Waislam wamefanya maandamano kumpinga Sheikh Ponda.
Wanaompinga Sheikh Ponda si masheikh bali ni "masheikh wa BAKWATA."
Chunguza.
Picha: Kulia ni Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir (1880 - 1979) na kushoto ni Sheikh Issa Ponda.