Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Hekima zaidi inahitajika kuliko jazba na utashi wa kimkundi, mimi naamini dr. nchimbi ameshawishiwa vibaya na si kweli kwamba hakujua kwamba huu ni wakati wa uchaguzi na maneno huwa mengi kuliko ukweli wa mambo, nawashauri jumuiya ya vijana kuliangalia hili kwa makini zaidi.

Sisi kama vijana tuna wajibu wa kuimarisha zaidi jumuiya na nchama chetu kwa kujenga misingi ya umoja na mshikamano kuliko kujenga makundi kwa maana ya kumalizana kisiasa, sote ndio tunaotegemewa kuitetea ccm huko tuendako ili iendelee kuongoza nchi, matendo yetu ya leo yatatuweka pabaya huko tuendako na watu watashindwa kutuamini mana tayari watakuwa wanayo historia na vigezo vingi vya kutupima.

Kwenye hili sote kama jumuiya ya vijana tumeshindwa kuona athari za matendo yetu hadi kuifanya ccm kuingilia kati, pia ushauri kwa viongozi wetu wa ccm watuangaliwe kwa karibu na kwa maana ya kutuunganisha badala ya kuongeza nyufa miongoni mwetu, sayansi ya kawaida jumuiya ya vijana na vijana wenyewe ndio viongozi wa kesho, inawa tuliowengi huwa hatulikubali hili ila huo ndio ukweli na hatuna budi kuuelewa, haina maana nyengine yoyote zaidi ya kwamba kuwa kwenye jumuiya ndio tanuru la kuoka viongozi walio bora, uvcc ondosheni tofauti zenu na mjitahidi kuangalia wale mnaowaongoza. tunategemea hili mtaliweka sawa kwa kuondoa tofauti zenu na kusameheana ili jumuiya iendelee kuwa kitu kimoja badala ya ilivyo sasa.

CCM chukua nafasi na uwe mtetezi wa haki badala ya uchochezi miongoni mwa vijana , wote ni vijna wenu wale walio na madaraa na mamlaka na wale wasio na madaraka wala mamlaka, ila kwa ujumla wote ni mazalio ya ccm na hivyo hatuna budi kuwahudumia kama wamoja na ili kutokuwagawa miongoni mwao na hivyo kuimarisha chama chetu.
 
Nchimbi, Makamba wamng'ang'ania Nape

na Rahel Chizoza Dodoma na Salehe Mohammed
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Dk. Emmanuel Nchimbi na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, wameendelea kumng'ang'ania mwanasiasa, Nape Nnauye, aliyeibua mjadala wa mradi wa ujenzi wa makao makuu ya umoja huo, yaliyopo Dar es Salaam.

Viongozi hao kwa nyakati tofauti, jana walilazimika kutoa taarifa za ufafanuzi juu ya nini kilichotokea Dodoma wakati wa vikao, kuanzia cha Baraza Kuu la Umoja wa Vijana, Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC).

Katika taarifa yake aliyoisambaza kwa vyombo vya habari jana, Mwenyekiti wa UVCCM, Dk. Nchimbi, alisema Nape amevuliwa uanachama si kwa sababu ya kukosoa mradi wa jengo hilo, bali kwa kuudanganya umma na kukipaka matope chama kwa kusema uongo.

Nchimbi ambaye ni mara yake ya kwanza kutoa ufafanuzi mwenyewe tangu mjadala huo ulipoibuliwa na Nape, alisema taarifa zinazotolewa hivi sasa kuwa Nape alivuliwa uanachama kwa sababu ya kukosoa ujenzi wa jengo hilo, si sahihi.

Alisisitiza kuwa Nape alipokutana na waandishi wa habari Julai 20 mwaka huu katika Hoteli ya Peacock, alisema uongo kuwa vikao vya UVCCM havikupitisha mchakato wa mradi wa ujenzi.

Alisema kimsingi mchakato wa ujenzi wa jengo hilo ulipitia katika ngazi zinazostahili, ikiwemo Baraza Kuu ambalo Nape alihudhuria, hivyo madai kuwa ujenzi huo haukufuata taratibu hayakuwa sahihi.

Alisema kutokana na kusema uongo huo, kamati ya utekelezaji ilimwita Nape na kumpa nafasi ya kujitetea, lakini alisukumia mzigo huo kwa vyombo vya habari kuwa vilitaka kufanya biashara kwa kutia chumvi suala hilo.

"Kutokana na utetezi huo, wajumbe wa kamati ya utekelezaji walitafuata ushahidi, kwa kuwa Nape alirekodiwa na kituo kimoja cha televisheni, hivyo kuonekana wazi akitoa shutuma hizo, hivyo wajumbe walimwona Nape amewadanganya na kutoa mapendekezo yao," alisema Nchimbi.

Alisema kamati hiyo iliwasilisha mapendekezo mawili kwa Baraza Kuu, mosi, kumsimamisha kushiriki vikao vya UVCCM kwa muda na pili CCM imchukulie hatua za kinidhamu kwa mujibu wa taratibu zake.

Alibainisha kuwa baada ya Baraza Kuu kupitia kwa kina mapendekezo ya Kamati ya Utekelezaji, liliridhika kuwa Nape alifanya makosa kwa kuvunja vifungu vya 17 (c) na 18 (b) vya kanuni ya UVCCM.

Alisema kutokana na kuridhika huko Baraza Kuu liliamua kumsimamisha Nape uanachama kwa mujibu wa kifungu cha 89(c) pamoja na kupendekeza avuliwe nyadhifa zake za uongozi ambazo uteuzi wake wa mwisho unafanywa na chama.

Alisema kuwa kama Nape hajaridhika na uamuzi huo, ana haki ya kuomba kusikilizwa tena na Baraza Kuu la UVCCM kwa mujibu wa ibara ya 89 (e).

Aidha, kuhusu mradi huo, alisema kuwa umoja huo una mamlaka kamili juu ya miradi yake, kupitia katika vikao mbalimbali ambavyo vilifanyika, pia rasimu ya mkataba imepitiwa na timu za wanasheria na wachumi.

Aliongeza kuwa timu hizo zilipitia mkataba huo kwa zaidi ya miezi 18 na hakuna wazo zuri ambalo lilitolewa na wataalamu hao na wengineo halikujumuishwa.

Alisema mchakato wa mradi huo ulipokamilia, walipeleka rasimu ya mkataba kwa Kamati Kuu ya CCM (CC) ili kupata baraka, ambapo iliwashauri mambo kadhaa kabla ya kusainiwa kwa mkataba.

Alitaja mambo hayo kuwa ni pamoja na gharama za mradi, ziwe wazi tangu mwanzo, mfumo wa hisa uiruhusu UVCCM kuongeza hisa zake, kuwepo kipengele kinachoonyesha jinsi ya kuvunja mkataba kama zitajitokeza sababu za kufanya hivyo.

Ushauri mwingine ni pamoja na kuainisha mambo ambayo mwenye hisa hawezi kuyaamua bila ya ridhaa ya mwenye hisa ndogo, na mwisho kuwe na chombo cha kusimamia ubia huo.

Wakati Dk. Nchimbi akitoa kauli hiyo, Makamba alisema CC imetoa wiki saba kwa timu ya watu watatu walioteuliwa kuboresha mkataba wa jengo hilo, wawe wamekamilisha kazi hiyo na kutoa taarifa ili mkataba huo usainiwe.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, Makamba alisema, ujenzi ambao umekuwa ukiendelea katika jengo hilo hautambuliki kamwe ndani ya CCM.

"Napenda kuwaambia kwamba ujenzi unaoendelea pale UVCCM, mkataba wake hautambuliki ndani ya CCM, na kama mkataba huo hautasainiwa na gharama zilizotumika mpaka sasa itakuwa ni hasara kwa mkandarasi na wala si UVCCM," alisema Makamba.

Makamba alisema kilichosababisha kuanza ujenzi huo kabla ya kukamilika kwa mkataba ni masharti ya fedha zilizotolewa, ambapo mkandarasi alitakiwa kuonyesha kazi iliyoanza kufanyika baada ya kupatiwa fedha hizo.

"Natumia fursa hii kusisitiza kwamba mkataba wa mradi wa jengo lile uliokuwa ukizungumzwa kwa muda mrefu, bado haujasainiwa na ujenzi unaendelea, wana CCM msiwe na wasiwasi juu ya hili," alisema Makamba.

Makamba alisema baada ya kuandaliwa kwa kina mkataba huo ulipelekwa kwenye Baraza la Wadhamini kwa ajili ya kupitiwa na kusainiwa.

Alisema baada ya kuwasilishwa kwenye baraza hilo, Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa UVCCM, Edward Lowassa, alikataa kuusaini baada ya kuona kuna kasoro ndani ya mkataba huo, ambazo zilipaswa kushughulikiwa kwanza kabla ya kusainiwa.

"Baada ya kupewa mkataba ule, Lowassa aligundua kuwapo upungufu, hivyo aliamua kuupeleka mkataba kwenye CC ili upitiwe na kufanyiwa marekebisho kabla ya kusainiwa," alisema Makamba.

Alisema CC ilipoupata mkataba huo, iliupitia na kubaini baadhi ya vipengele vingi ambavyo vingeongezwa na kurekebishwa kwa nia ya kupata masilahi zaidi kwa UVCCM," alisema Makamba.

"Tuelewane hapa, hatukuunda tume, tulichagua wenzetu watatu ili wasaidie kuboresha mkataba huo kutokana na taaluma zao na si kuchunguza kama inavyozungumzwa na baadhi ya watu, maana hakuna cha kuchunguza pale… narudia, tuelewane katika hili," alisema Makamba.

Alisema uteuzi huo, ulizingatia kigezo cha taaluma zao, wakiwemo wanasheria wawili ambao ni Andew Chenge na Pindi Chana, na mchumi mmoja, ambaye ni Dk. Abdalah Kigoda.

"Sasa tuhuma alizonazo mtu hazihusiani kabisa na kufuatilia mkataba huu, maana hakuna kinachochunguzwa, sisi tulichozingatia ni taaluma za watu, nashangaa kusikia watu wanahoji kuwa Chenge anatuhumiwa, kwanini ameteuliwa, tunachohitaji ni uanasheria wake ili atusaidie, siyo tuhuma," alisema Makamba.

Makamba alisema baadhi ya mambo yaliyopendekezwa na CC kuongezwa na mengine kurekebishwa katika mkataba huo ni pamoja na kuhakikisha UVCCM haipotezi umiliki wa eneo la kiwanja na gharama zote za mradi zijulikane, kuanzia hatua za awali hadi kukamilika kwa ujenzi huo.

Mengine ni kuweka wazi vifungu katika mkataba huo vinavyoiwezesha UVCCM kuongeza idadi ya hisa kutoka asilimia 25 walizonazo sasa, na kuwepo kipengele kinachoonyesha namna ya kushughulikia tatizo iwapo mmoja ataamua kuvunja mkataba kati ya mmiliki na mpangaji.

Kuhusu suala la Nape aliyenyang'anywa uanachama wa UVCCM, Makamba alisema chama bado kinaendelea kumtambua kuwa ni mwanachama na nyadhifa zote alizonazo katika chama zinaendelea kutambulika.

"Nawaambia kwamba Nape ni mjumbe halali wa NEC, hata kama aliingia katika NEC kwa tiketi ya vijana, maana katiba ya CCM haionyeshi mwanachama akipoteza sifa katika jumuiya yake amepoteza ujumbe wa NEC," alisema Makamba.

Alisema suala la Nape kukata rufaa lipo wazi na ameonyesha nia ya kufanya hivyo na kwamba chama kitakuwa tayari kusikiliza rufaa yake na yeye ndiye anajua akakate wapi rufaa.

"CCM ndiyo baba, yeye alete rufaa yake tutamsikiliza, kwa kawaida inapokuwepo migogoro katika familia, baba ndiyo huwa na wajibu wa kushughulikia migogoro hiyo, hilo halina tatizo," alisema Makamba.
 
Haya ni matokeo ya uongozi dhaifu wa JMK. Hawa mafisadi Nchimbi na Makamba wanabwabwaja bila kuheshimu maamuzi ya kikao kilichopita cha CCM. Nchi inayumba na CCM inayumba kutokana na uongozi dhaifu wa JMK.
 
Fisadi Kijana,

Nina uhakika kwamba Nape akikaa akatulia na kujipanga vizuri, hoja ya kwamba alisema uongo haipo. Ni ukweli kwamba mkataba ulisainiwa kabla ya kupata baraka za CC. Na ni utaratibu kwamba kila kitu kinachohusu maamuzi makubwa kwenye Jumuiya lazima kifikishwe CC kujadiliwa na CC itoe baraka.

Wanasheria wanasema kwamba Development Agreement nao ni mkataba lakini kwa jina tofauti na ilisainiwa Januari 2008. Kile ambacho Lowassa na wenzake wanasema ndiyo 'mkataba', umepelekwa kwa Makamba Julai 2008. Details za huo 'mkataba' zimetoka kwenye Development Agreement iliyosainiwa Januari 2008.

Kasoro zilizoainishwa na CC ndiyo ambazo ziliainishwa na Kubenea kupitia gazeti lake la MwanaHALISI. Na hizo kasoro ziko kuanzia kwenye Development Agreement na ndiyo maana hata huo 'mkataba' umeendelea kuwa na kasoro hizo hizo pamoja na wataalam wa UVCCM kutumia miezi 18 kuuandaa, huku waki-incorporate criticism za Kubenea ambazo hazikuwa addressed kwenye 'mkataba' wenyewe.

Nchimbi anasema wataalam wa UVCCM wametumia miezi 18 kuandaa mkataba huo, haya ni matusi kwa wale walioandaa huo mkataba na ni kosa kuwaita watalaam. Huwezi ukaandaa mkataba kwa kipindi kirefu namna hiyo halafu uje utolewe kasoro kibao ambazo ziko wazi kiasi kwamba hata layman wa sheria anaweza kuziona wazi.

Tatizo la akina Nchimbi walianza kuandaa huo 'mkataba' baada ya kuumbuliwa na walishindwa kubadilisha vipengele ambavyo walitakiwa kuvibadilisha kwa kuwa wanabanwa na Development Agreement ambayo ilishasainiwa tayari na hivyo kisheria ilikuwa inawabana.

Kitendo cha CC kuteua watu 3 ili kuuboresha na kuondoa kasoro zilizo wazi ni dalili kwamba CC iligundua makosa ya kisheria ambayo UVCCM wakiachiwa wafanye wenyewe hawawezi kuondoa hizo kasoro kwa kuwa wanabanwa na Development Agreement. Hiyo timu ya watu 3 itaufanyia kazi huo mkataba na kuurudisha tena UVCCM ili ufuate zile taratibu zinazotakiwa na hatimaye ufike CC tena na kupewa baraka. Mpaka hapo kuna dalili zote kwamba mafisadi wamepigwa bao, maana kamisheni lazima ipungue kwa kuwa maslahi ya wahindi yatapungua tofauti na jinsi ilivyokuwa mwanzo.

Makamba bado anakomaa kwamba mkataba haujasainiwa pamoja na kwamba ujenzi wa mradi umeishaanza. Anadai kwamba Ujenzi ulianza kwa kuwa wawekezaji walikopa hela na condition ya mkopo ilikuwa ni kwamba lazima waanze ujenzi. Swali ambalo waandishi wa habari walipaswa kumuuliza lilikuwa dogo sana, "ni Benki gani ambayo iliwakopesha hao wawekezaji bila ya kuwa na hati ya kiwanja au kuwa na mkataba uliosaniwa kuonyesha kwamba ule mradi wamepewa kuuendeleza?"

Nimegundua kwamba viongozi wako wa UVCCM hawajui vyema Katiba ya CCM na hawawezi hata ku-interpret vyema Kanuni za UVCCM na ndiyo maana wamejikuta wakijikanyaga kila wanapotoa maelezo. Nape akitulia, akasoma vyema katiba ya CCM na kanuni za UVCCM, na akapata ushauri mzuri wa kisheria ana nafasi ya kushinda rufaa yake na akishinda ni mtaji kwa ajili ya future yake kisiasa.
 
Kama kawaida ya kiburi chao, kundi la akina Nchimbi, Makamba, Lowassa n.k., walifikiri kuwa chama ni chao na hakuna atakayewapinga as long as JK ndie mwenye kigoda.

These fisadis should not underestimate a growing number of CCMers, who are now willing to voice out their ops openly or even sacrifice their positions in support of fairness/democracy within the party or probably just to be against the unpopular Lowassas & co.

Mkuu hapa ni sawa sawa, ninasema hivi kwa wanasiasa kama Lowassa na Nchimbi, ambao wana ambitions kubwa sana na uongzi wa taifa letu mbele ya safari, kwa kweli hii ishu ya Nape ni tatizo kubwa sana kwenye CV zao, sijui kama wanaelewa hilo,

Halafu kama nilivyotabiri huko nuyma kuwa itafikia siku hawa viongozi watakwiba mpaka kutakuwa hakuna cha kuiba tena ndipo wataanza kutafutana wenyewe kwa wenyewe, sasa ninaamini kuwa tunaelekea kufikia huko, na sauti zinazidi kujitokeza tena nzito sana, mapak wezi wenyewe nao wameanza kupiga makelele, I mean ndio ni very slow process lakini tunawakaribia na hawatatuibia milele.

Again Bravo Nape na wananchi wote walioelewa kilichotokea hapa na huu uchaguzi wa UV-CCM, kuwa in a bigger picture mafisadi wamepigwa kipigo kizito sana ingawa inaweza kuchukua muda kidogo kwa wao kukisikia vizuri.
 
Nape aendelea kukingiwa kifua, adai Nchimbi ana ajenda binafsi

Na Kizitto Noya

SIKU moja baada ya Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Dk Emmanuel Nchimbi, kutoa taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa Nape Nnauye amevuliwa uanachama kwa kosa la kusema uongo na si kuukosoa mkataba wa jengo la umoja huo, Nape amedai kuwa hali hiyo inaonyesha kuwa kiongozi huyo ana ajenda binafsi.

Nape aliiambia Mwananchi Jumapili kuwa, mjadala kuhusu adhabu yake umekwisha, hivyo hoja zinazoendelea kutolewa na UVCCM kuhusu suala hilo hazina msingi vinginevyo ni agenda binafsi za baadhi ya watendaji wa umoja huo.

''Uamuzi wa CC (Kamati Kuu) na NEC kutaka mkataba huo ukaboreshwe kwa kuwa una kasoro, unatosha kumaliza mjadala huo na kuthibitisha nani mkweli na nani mwongo, haya maelezo mengine ni ajenda binafsi za watu,'' alisema.


Alisema ajenda iliyoelezwa na Dk Nchimbi juzi kwamba, Baraza Kuu limemvua uanachama Nape kwa kosa la kusema uongo, haina mantiki kwani tayari vikao hivyo vya juu vya chama vimeshatoa taswira ya ukweli kuhusu suala hilo.


''Kimsingi vikao vya CC na NEC vimeshamaliza mjadala huo na hayo yanayoendelezwa sasa hayana maana, kwa kuwa tayari mwongo na mkweli wamejulikana,'' alisisitiza.


Alisema tangazo la Dk Nchimbi kwenye baadhi ya magazeti jana kwamba CC na NEC vimepitisha mkataba huo isipokuwa vimetaka nyongeza za vitu vichache, inapotosha kwani hiyo anayoita nyongeza ndizo kasoro alizokuwa (Nape) akizipigia kelele tangu awali.

Alibainisha kuwa kelele zake kuhusu mkataba huo hazikulenga kuwaharibia watu fulani ndani ya UVCCM bali kutetea haki kwa maslahi ya jumuiya yenyewe, hivyo si sahihi kwa baadhi ya watendaji kumwona kama ana chuki nao.

Juzi, Nchimbi alitoa taarifa kwa vyombo vya habari akieleza kuwa Nape amevuliwa uanachama wa UVCCM si kwa sababu ya kuukosoa mradi wa UVCCM bali kuudanganya umma na kukipaka matope chama kwa kusema uongo.


Alisema Nape alionekana kwenye televisheni akitoa tuhuma hizo kuwa, hakukuwa na vikao halali vilivyopitisha mkataba huo, wajumbe wa Baraza Kuu waliridhika kuwa aliwadanganya kwa kukana maneno hayo.

''Baraza Kuu liliridhika kuwa vikao vyote vya UV-CCM vinavyohusika na mchakato huo vilihusika kikamilifu, ikiwamo Baraza Kuu la tarehe 4/8/2007 na kikao kilichopitisha muhtasari wa Baraza Kuu cha tarehe 9/2/2008 ambacho Nape alishiriki,'' ameeleza Nchimbi katika taarifa yake.

Hata hivyo, Nchimbi anaonyesha katika maelezo yake kuwa uamuzi wa Baraza Kuu ulikuwa mkubwa kuliko mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM, ambayo ilitaka Nape asimamishwe kushiriki vikao vya umoja huo na CCM imchukulie hatua za kinidhamu kwa mujibu wa taratibu zake.


Badala yake Baraza hilo lilimvua uanachama na kupendekeza kwa CCM avuliwe nyadhifa zake zote.

Katika taarifa hiyo Nchimbi alisema mapendekezo ya kumvua Nape nyadhifa zake zote ndani ya CCM ameshayawasilisha kwa Katibu Mkuu wa chama hicho tawala na kuwa "Uamuzi wa chama katika suala hilo utakuwa wa mwisho.

Katika hatua nyingine, wakati Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), ukitoa taarifa rasmi inayoeleza sababu za kumvua Nape Nnauye uanachama, kada na mwanzilishi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Peter Kisumo amesema, anachoona katika adhabu hiyo ni utoto na hasira za vijana.

Kisumo aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa haoni sababu za Nape ambaye ni Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM na Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kuvuliwa uanachama kwa kusema uongo wakati hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha hilo.


''Mimi ninachoona katika adhabu hiyo ni utoto na hasira za vijana na naamini busara haikutumika,'' alisema.



Alisema UVCCM inatakiwa kupinga hoja za Nape kwa ushahidi utakaoonyesha kuwa, mkataba wa uendelezaji wa jengo la UVCCM hauna harufu ya rushwa badala ya kumwadhibu Nape kwa tuhuma za kusema uongo.


''Hata kama Nape amesema uongo, adhabu ya kumvua uanachama bado ni kubwa na naamini adhabu hiyo imetolewa kwa ushawishi wa watu wenye hasira na jazba kuliko busara,'' alisema Kisumo na kuongeza:

''Nasema busara haikutumika kwani ingekuwapo wangetafuta adhabu nyingine inayolingana na kosa, tena baada ya kuthibitisha kosa lake kwa ushahidi badala ya kufukuzana."

Kwa mujibu wa Kisumo, adhabu ya kumvua mtu uanachama ni kubwa na haina tofauti na kumfukuza mtu uraia wa nchi yake na siku zote CCM imekuwa ikikwepa kutumia adhabu hiyo kwa kuwa inakidhalilisha chama.


Lengo la kulinda heshima yake na mwanachama anayeadhibiwa.''Kama Nape kasema ukweli au uongo, nasema adhabu hiyo sio mwafaka. UVCCM wanatakiwa kuleta ushahidi kutetea hoja zao badala ya kutumia adhabu hiyo ambayo inakidhalilisha chama na wanachama,'' alisema na kuongeza:


''Kama Nape alisema ukweli lakini ukweli huo kasemea nje ya vikao sioni sababu za kumwadhibu.''

Kisumo alisema haoni sababu ya mwanasiasa huyo chipukizi kuvuliwa uanachama wa UVCCM kama tuhuma kwamba, mkataba wa jengo la UVCCM hauna maslahi ni za kweli.

Alisema CCM inatakiwa kuweka mikakati kudhibiti jumuiya zake kuwafukuza wanachama ili kulinda heshima yake na wanachama ambao uzoefu umeonyesha kuwa wengi waliopata adhabu hiyo wanakihama.

Katika hutua nyingine Mzee Kisumo alisema Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba amekosea kulishawishi Baraza Kuu la UVCCM kumfukuza Nape uanachama kwa tuhuma za kusema uongo.


Alieleza kuwa Makamba aliteleza kwenda kuzungumza na vijana kwa lengo la kuwashawishi kufikia uamuzi huo kwa kuwa hii sio kazi yake.


''Kazi ya Katibu Mkuu ni kushauri na sio kushawishi na hatua ya Makamba kuzungumza na vijana ilikuwa ushawishi na sio ushauri hivyo ni makosa,'' alisema.

Alisema CCM imejengwa katika misingi ya kila jumuiya yake kujiongoza hivyo kitendo cha viongozi hao kuingilia mambo ya vijana ni kinyume na misingi hiyo na kinakiuka kanuni.

Kauli ya Mzee Kisumo imekuja huku tuhuma alizotoa Nape dhidi ya mkataba huo zikionekana kuwa na nguvu baada ya Kamati Kuu kuunda timu ya watu watatu kupitia upya mkataba huo uli kuondoa kasoro na kuufanya uwe na maslahi ya UVCCM

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuchukua fomu za kugombea uenyekiti wa UVCCM Julai 15, Nape, ambaye ni mtoto wa mwanasiasa aliyekuwa na heshima ndani ya CCM, Moses Nnauye, alidai kuwa mkataba huo unanuka rushwa na kumshambulia Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la vijana, Edward Lowassa, mwenyekiti wa wake Dk Emmanuel Nchimbi na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Vijana, Amos Makalla kuwa walihusika.

Katika hatua nyingine, wakati UVCCM na CCM kupitia vikao vyao vya juu wanazidi kusisitiza kuwa mkataba wa jengo unaolalamikiwa haujasainiwa, mwekezaji katika eneo hilo anaendelea na ujenzi.


Mwananchi Jumapili jana lilishuhudia mafundi wa mwekezaji huyo wakifanya kazi kama ‘mchwa' licha ya kwamba mkataba wa uwekezaji huo unadaiwa haujatiwa saini.
 
inaonekana global publisher wamejiunga na harakati za makusudi zinatumika ili kummaliza nape kisiasa. ama kweli mfa maji atashika hata jani akiamini ataelea. hbeu soma hapa chini.
Kigogo wa CCM apata skendo akiwa kaburini
risasi mchanganyiko

Kigogo wa CCM apata skendo akiwa kaburini

Watoto anaodaiwa kuzaa Brigedia Jenerali huyo mstaafu, nje ya ndoa ni mwanasiasa chipukizi ambaye hivi sasa amekuwa gumzo kubwa, Nape Nnauye na Zuhura Nnauye.

Habari za kiuchuguzi zinasema kuwa, huku akijua kuwa alikuwa ndani ya ndoa na mama Mwanaisha Nnauye, waliyekuwa wakipendana kupita maelezo, Mzee Nnauye ‘alijiweka’ kwa kinadada wengine na kujikuta akipata watoto wawili ‘kidume Nape’ na dada yake aitwaye Zuhura Nnauye.

“Hii ni skendo kwa kigogo huyo wa CCM ambayo ameipata akiwa kaburini,” alisema mmoja wa wananchi walioongea na mwandishi wetu mara baada ya sakata la Nape ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM kuibuka na kutawala kurasa za mbele za vyombo vya habari.

Ingawa kuwa au kutokuwa na wanawake na watoto zaidi ya wanaofahamika sio kipimo cha uongozi nchini, watu waliohojiwa na gazeti hili wamedai kuwa, kitendo cha marehemu Nnauye kuzaa na mwanamke mwingine bila kumfahamisha mkewe ni kudhihirisha kuwa naye alikuwa ‘hajambo’ kwa dogodogo.

Kwa skendo hii iliyoibuka miaka saba baada ya kifo chake, Mzee Nnauye ambaye wakati anakufa alikuwa mshauri wa Rais anayeshughulikia siasa, anakuwa mwanasiasa mkongwe wa kwanza nchini kukumbwa na skendo la aina hiyo wakati akiwa tayari amekufa.

Hata hivyo, kubumbuluka kwa maisha yake ya siri ya kuzaa na mwanamke mwingine nje ya ndoa bila kumshirikisha mkewe, kunatokana na Nape kushupalia suala la mkataba wa mradi wa jengo la Umoja wa Vijana wa CCM kuwa haukupitishwa na vikao halali, hivyo kuvuta hisia za watu na kujikuta wakitaka kumfahamu vizuri kijana huyo.

Suala la Nape kuwa mtoto au si mtoto wa Nnauye limezua mtafaruku mkubwa baada ya mjane wa marehemu kumkana kuwa si mwana wa mzee Nnauye wakati kaka wa marehemu ambaye ni msimamizi wa mirathi na msemaji wa familia hiyo, Gallus Abeid amethibitisha kuwa, kijana huyo ni familia ya kiongozi huyo aliyefariki dunia.

Pamoja na Nape na dada yake Zuhura, watoto wengine wa marehemu Nnauye ni Mariam, Joseph, Mwate, Samora na Mussa.

Nape amekuwa gumzo hivi karibuni kutokana na kuibua suala la utata wa mkataba wa Jengo la Umoja wa Vijana wa CCM hivi karibuni ambapo alidai kuwa ulipitishwa kienyeji, bila kuridhiwa na vikao halali vya jumuiya hiyo ya Chama cha Mapinduzi.

Kufuatia kauli hiyo ya Nape, Baraza Kuu la Umoja huo liliamua kumvua uanachama ikiwa ni pamoja na kumvua nyadhifa zote alizokuwa nazo kupitia umoja huo kwa madai kuwa alisema uongo nje ya vikao.

Hata hivyo, Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM, Jumatano wiki hii ilitengua uamuzi huo wa Baraza la Umoja wa Vijana wa kumvua Nape uanachama wa umoja huo.

Mzee Moses Nnauye alifariki katika Hospitali ya Jeshi Lugalo, jijini Dar es Salaam saa 3.00 asubuhi, Desemba 6, 2001 kufuatia maradhi ya moyo na kuzikwa Desemba 7 katika makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Hadi kifo chake, mzee Nnauye alikuwa na umri wa miaka 64, baada ya kuzaliwa mwaka 1937 katika Kijiji cha Chiuta, Tarafa ya Nyangamala, Wilaya ya Lindi Vijijini, mkoani Lindi.

Mbali ya kuwa Brigedia Jenerali Mstaafu ndani ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, marehemu aliwahi pia kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya Chama cha Mapinduzi na serikali ikiwemo ya Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

source: Global Publishers - Tanzania Newspapers
 
HUU ni upuuzi mkubwa. Mbona hawaandiki kuwa viongozi kibao nao wana watoto wa nje? Hii ni siasa chafu na ukitaka kujua source wa hiyo habari soma Mtanzania la Jumatano iliyopita utajua ni ajenda mpya ya MAFISADI.... Wamechanganyikiwa na sasa wanataka tubadili vita na kuwaandama katika maeneo yao ya mitaani. Huko TUSIENDE WANAJULIKANA TUENDELEE NA HUKU HUKU KWENYE EPA, JENGO LA UVCCM, RICHMOND, MEREMETA, KIWIRA, ALEX STERWARTS, CITY WATER, TICTS, IMPORT SUPPORT, KAGERA SUGAR na Kadhalika
 
tutawaambia kwa sauti kubwa kwamba ni wapuuuzi nasi hatutaachilia yale muhimu kwa taifa letu ambayo kama mkuu halisi ulivyosema wnajitahidi tusahau.
washindwe kabisa
 
HUU ni upuuzi mkubwa. Mbona hawaandiki kuwa viongozi kibao nao wana watoto wa nje? Hii ni siasa chafu na ukitaka kujua source wa hiyo habari soma Mtanzania la Jumatano iliyopita utajua ni ajenda mpya ya MAFISADI.... Wamechanganyikiwa na sasa wanataka tubadili vita na kuwaandama katika maeneo yao ya mitaani. Huko TUSIENDE WANAJULIKANA TUENDELEE NA HUKU HUKU KWENYE EPA, JENGO LA UVCCM, RICHMOND, MEREMETA, KIWIRA, ALEX STERWARTS, CITY WATER, TICTS, IMPORT SUPPORT, KAGERA SUGAR na Kadhalika

Hao Waungwana wa Global Publisher wameishiwa....Haileti maana kwetu kujua Nape kazaliwa na nani?Tunachojali na kuheshimu ni Nape amefanya nini kwa jamii inayomzunguka....Haina maana yoyote kuelezwa hapa Nape kazaliwa na nani,awe Abdallah Natepe (RIP) au Abdullhaman Juma.Ni imani yangu kuwa Nape kafika hapo alipo kwa Juhudi zake binafsi za Utumishi wa Umma,na wala sio kwa sababu Baba yake alikuwa Muasisi wa CCM...Mbona hatuwaoni watoto wa Kamanda wa Vijana wa CCM (Ngombale Mwiru) wakiwa katika nafasi hizo?Nape usihudhunishwe na Maandishi ya hao Wachovu (Global Publisher).Simamia kile unachoamini..Hakuna Mtanzania bora kuliko mwingine,ni wazi HAKI itachukua nafasi yake...Aluta Continua!!!
 
HUU ni upuuzi mkubwa. Mbona hawaandiki kuwa viongozi kibao nao wana watoto wa nje? Hii ni siasa chafu na ukitaka kujua source wa hiyo habari soma Mtanzania la Jumatano iliyopita utajua ni ajenda mpya ya MAFISADI.... Wamechanganyikiwa na sasa wanataka tubadili vita na kuwaandama katika maeneo yao ya mitaani. Huko TUSIENDE WANAJULIKANA TUENDELEE NA HUKU HUKU KWENYE EPA, JENGO LA UVCCM, RICHMOND, MEREMETA, KIWIRA, ALEX STERWARTS, CITY WATER, TICTS, IMPORT SUPPORT, KAGERA SUGAR na Kadhalika

Naam Halisi, huu ni upuuzi mkubwa sana. Mafisadi kwa mara nyingine tena wanajaribu kumchafua Nape ambaye juhudi zake za kupambana na ufisadi ndani ya CCM zimempatia umaarufu mkubwa miongoni mwa Watanzania wa ndani na nje ya nchi. Wataweza kumchafua Nape miongoni mwa mafisadi wenzao kama Nchimbi na Makamba lakini kwa Watanzania tulio makini na tunaelewa kinachoendelea ndani ya chama cha mafisadi, kamwe hatuwezi kuukubali uwongo wao. Nape wala usipoteze muda wako kwa kujibizana na hawa mafisadi mahayawani. Hizi ni dalili za mafisadi wa CCM kuwa na wasi wasi mkubwa na Nape. Mungu atakulinda dhidi ya wote wale wanaokuchukia na wanataka upotee kabisa ndani ya CCM.
 
hawa jamaa kweli ni wapumbafu sana,wamekosa cha kuandika,mbona hawaandiki kuwa lowassa ana mtoto wa kike wa nje amezaa na mama wa kimasai na mkewe hajui,huyu mtoto anaka na bibi yake mtoni kijichi...wakiendelea kwa siasa hizi basi watachafuka wao mafisadi
 
Maadili ni muhimu uzinifu na kutoheshimu ndoa ni sehemu ya ufisadi. Kiongozi anaeisaliti ndoa yake na familia yake ( watu ambao yupo karibu nao sana kila siku ) hatoshindwa kuwasaliti watanzania kwa uwingi wao.

Nawapongeza Global publishers kwa uthubutu wao huu mkubwa. Vita ya ufisadi lazima ianzie huko majumbani mwao (charity begins at home) Hizi hoja za asie na dhambi aanze kurusha jiwe ( Bwana Yesu hakumaanisha kuhalalisha uzinzi) tunazitafsiri sivyo ndivyo. Hata ukiwa kaburini haizuii watu kufukua uozo wa kiongozi tunahitaji taifa la waadilifu na majibu kama "viongozi wote wanafanya" ni hoja legevu na lemavu. Wachina wana msemo "a journey of thousands miles starts with single step" nasi tuanze na huyo na wengine mpaka tutafika.
 
Maadili ni muhimu uzinifu na kutoheshimu ndoa ni sehemu ya ufisadi. Kiongozi anaeisaliti ndoa yake na familia yake ( watu ambao yupo karibu nao sana kila siku ) hatoshindwa kuwasaliti watanzania kwa uwingi wao.

Nawapongeza Global publishers kwa uthubutu wao huu mkubwa. Vita ya ufisadi lazima ianzie huko majumbani mwao (charity begins at home) Hizi hoja za asie na dhambi aanze kurusha jiwe ( Bwana Yesu hakumaanisha kuhalalisha uzinzi) tunazitafsiri sivyo ndivyo. Hata ukiwa kaburini haizuii watu kufukua uozo wa kiongozi tunahitaji taifa la waadilifu na majibu kama "viongozi wote wanafanya" ni hoja legevu na lemavu. Wachina wana msemo "a journey of thousands miles starts with single step" nasi tuanze na huyo na wengine mpaka tutafika.


hahahaha mkuu wajifanya kipofu? hakika na kujifanya kipofu ni ufisadi pia.
jiulize kwa nini global publishers waje na habari hii leo wakati habari hii ilikwishatoka siku nyingi huko nyuma, na kama kumbukumbu zangu ziko sawa hata humu jf limeshawahi kutajwa.

sasa hapa unataka kusema nini? kwamba nape naye ni visadi au baba yake?
 
Awe mtoto wake asiwe wake, awe wa nje, asiwe wa nje....sisi yote hayo hatujali...tunachojali nikile kitu anachokitoa kwa jamii katika kuwatetea kwa kuukemea ufisadi......msitake kutuchanganyia habari hapa.!
 
hahahaha mkuu wajifanya kipofu? hakika na kujifanya kipofu ni ufisadi pia.
jiulize kwa nini global publishers waje na habari hii leo wakati habari hii ilikwishatoka siku nyingi huko nyuma, na kama kumbukumbu zangu ziko sawa hata humu jf limeshawahi kutajwa.

sasa hapa unataka kusema nini? kwamba nape naye ni visadi au baba yake?

Swadakta!! upofu wa kufumbia ufisadi ni ufisadi. Ndio maana hiyo habari hata kama ilikuwa ni ya miaka 100 iliyopita ni valid kuja sasa haijalishi kama itamvurugia mtu mambo yake au laa. Suala kuwa limeshajadiliwa humu haiwi immunity ya kufanya lisijadiliwe tena as long as wachangiaji wapo ndio uhuru wa kujieleza wenyewe huo.

Nani fisadi kati ya Nape na baba yake its up 2 u 2 figure out, do ur home work mate...
 
Weka vitu hadharani hayo ndio tunayoyataka...

Unataka zile picha za jamaa zirudishwe tena hapa? Tusiwe na double standard ... ziliwekwa picha hapa watu wakapiga kelele kama nini na kulazimisha mtu aombe radhi. Leo kwa kuwa ni mambo ya Marehemu Mzee Nnauye ndiyo tunajifanya kwamba usaliti wa ndoa nao ni ufisadi.

Ukiuliza lile swali la ambaye hajawahi kuzini ama kutoka nje ya ndoa yake na arushe jiwe, vigogo wote wa CCM na serikali hakuna hata mmoja ambaye ataweza kurusha jiwe. Na siyo kwa vigogo tu bali ni sehemu kubwa ya wanajamii watashindwa kurusha mawe. Cheating ni sehemu ya maisha wa waafrika, japo sisi huwa ni wepesi wa kuwanyooshea kidole wengine wakati ya kwetu tumeyaficha ama hayajulikani kwa kuwa hakuna mtu ambaye ana interest ya kuyafuatilia.

Naona wewe unataka Manumba aishike JF kwa muda, maana vitu vikianza kuwekwa hapa sijui hata kama JF itamaliza siku ikiwa hewani!
 
Back
Top Bottom