Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Hawa CCM kweli wanatisha .Nimeona wameamua kujenga jengo jina na wameanzia kitu kinaitwa Videco .CCM kweli ni mali ya wahindi maana hata pesa za usafiri kwa Vijana wa CCM kwenda Dodoma kwenye kuchambua majina ya wagombea pesa zimetolewa na wahindi na huku JK anasema CCM ni ya watanzania .Ama kweli baba ombaombana mtoto the same .Aibu kubwa hii .

kaka yani bado kidogo tu hata ikulu itakua ishauzwaa!!watanzania tutabaki kumiliki roho zetu tuuuu
 
jumuiya ya vijana muwe makini na utashi wa mtu, inaonekana sasa jumiya ya vijana ni mali ya mtu na si ya vijana wote, tendeni haki kwa kufuata kanuni na taratibu, msimuumize mtu kwa mapenzi ya mtu, kama nape amesema hilo na kama ni uongo basi mtoe vielelezo vya kuonyesha uongo wake, mana hata mkitumia nguvu bado hamaturidhisha kwamba nyinyi ni wasafi zaidi ya kuwaona waovyo, jengeni hoja msiumizane kwa kusema kweli, nape hadi sasa anaonekana mkweli mbele ya watu wengi hasa sisi tulio nje ya jumuiya mana tunaielewa na tunamuelewa mwenzetu kiongozi wa jmuiya na vipi anavyoongoza jumuiya hiyo. angalieni maslahi ya jumiya na chama chetu, mana sasa kila mtu anapata nafasi ya kutupa madongo na hakuna wa kukitetea. zaidi ni ukimya.
 
angalieni maslahi ya jumiya na chama chetu,

Mkuu Mohamed,

Heshima mbele bro, exactly hicho ndio kinacho-miss kwenye this whole mess ya Umoja Wa Vijana, hakuna record wala mifano ya uongozi, ungetegemea kuwa by now wananchi wa Tanzania, tutakuwa tumejifunza namna ya kuheshimu uwezo wa kiongozi, kwa kuuchambua wazi tena bila unafiki,

Nchimbi, sio siri ni a great campaigner lakini hana strong record ya uongozi, zaidi tu ya kuwatumia viongozi wengine tena mpaka wenye academic qualifications kuliko zake, kwa ajili ya manufaa yake, lakini record ya kazi ya uongozi wake kwa wananchi hakuna! record ya uongozi wake kwa taifa hakuna!

Sawa at one point alikuwa ni mmoja wa the architects, waliomsaidia Rais wa sasa na mtandao mzima kuingia kwenye power, lakini record nzima ya Mtandao na Rais wa sasa, ni mfano tosha wa kumuweka pembeni kabisa na mchakato mzima wa huu uchaguzi, na hata kumkatalia kabisa mgombea anayetaka kumpigia debe, kwa sababu amepiga sana debe kwa Kiwete, Lowassa, na Rostam kushika power, and they did, matokeo yako wazi kwa kila mwananchi wa taifa hili, sasa iweje tena huyu huyu Nchimbi bado tu aendelee kujaribu kutuchagulia viongozi wengine tena?

Hapa ndipo ninaposema kuwa hawa viongozi wetu wa taifa, wana-benki sana kwenye uwezo mdogo wa wananchi kuelewa kinachoendelea, mimi nilitegemea Nchimbi ajitokeze public na kusema wazi kuwa ameshindwa ku-prove wananchi wrong kuwa hana uwezo mkubwa wa uongozi kisiasa on the national level, kwa hiyo anajitoa kwenye any-process ya kutafuta viongozi wengine wa siasa wa taifa, lakini here he is bila aibu eti this time amempa Nape, alama ya E sasa swali hapa linapaswa kuwa nani hasa anastaili kupewa E, kati ya Nape, Lowassa, Kikwete, na Chimbi? Eti unahitaji kuwa professor kulijibu hili, ambalo realistically ni a none political question?

Kwa wale mnaomfagilia Nchimbi na huu udikteta wake kwenye hiki chama, can you just for once mkatupa his leadership record? Halafu ni lini mtakubali publicly kuwa amekuwa akiwa-back wrong political leaders? na wasiokuwa na record kama yeye? I mean ifike mahali ukweli uwekwe wazi, marafiki wa Nchimbi, siku zote wamekuwa ni kina Lowassa, Rita mlaki, na Rostam, halafu leo tena huyu huyu Nchimbi bado anakuwa na political power ya kujaribu kutuwekea another joker huko Vijana?

Hivi kweli anaweza kujibu swali la kwa nini siku ya kutajwa majina ya wabunge wa kuliwakilisha bunge kwenye mazishi ya Mheshimiwa Mbunge Amina Chifupa (RIP) huko Iringa, ilibidi Spika aliruke jina lake bila kulitaja ingawa na yeye alikuwemo kwenye lists hiyo? Hivi anakumbuka maneno ya Spika later on katika kujaribu kuwaelewesha waandishi wa habari kuwa ni kwa nini aliliruka jina lake? Ile tu peke yake haimtoshi kukubali kuwa it ia about time sasa akakaa pembeni na kuwaachia kina Nape nao wajaribu?

Ameshasahau jinsi alivyokuwa akililia mtandao kupewa nafasi kwenye vikao vya kamati kuu, na kwamba wasipopewa nchi haitawalika, hivi kweli anaweza kusimama na kusema wazi kuwa sasa yeye na wenzake wakiwa kwenye power kama walivyokuwa wakililia, nchi inatawalika kweli? Unajua ni ishu kama hizi ndio zinaeleza wazi, uwezo wetu wananchi wa kuelewa siasa yetu, wengine wanasema maneno ya Ridhiwani, hivi jamani kweli record ya baba yake kama rais wa nchi hii for the last two years, kweli inampa huyu kijana nafasi ya kutaka kuamua kiongozi wa vijana awe nani?

I mean to you rais Kikwete, huwezi tena kumlaumu mtu ulitaka nafasi, wananchi tutakupa, hivi kweli haya unayoyafanya sasa ndio hasa iliyokuwa your vision kwa taifa hili? What is the vision anyways? Hii debate nzima ya uongozi wa Vijana hivi kweli exactly what it is all about? Watu waliohusika na failed policies leo tena wanataka kutuamulia our future leaders? Wanataka kutuwekea viongozi wa mfano kama wao tena?

Halafu na sisi wananchi we are so much caught up na huu ujinga hata kurushiana maneno mazito as if kuna viongozi kweli, kumbe ni mfano tu wa viongozi ambao hili la uongozi wa vijana wa CCM ni clear example of how they think of us wananchi, kuwa ni wajinga, wakuu it is about time tukawaambia hawa viongozi kuwa enough is enough! Enough of the last two years, tuliyoyaona yametutosha hatutaki zaidi tena!
 
Simply PR gimmicks...

Ni vigumu watu wengine kujua lengo lao ni nini: kijana huyu kafanya makubwa ambayo Masatu anadiriki kuyafunika kwa kejeli ya "PR gimmicks"! Sitashangaa kujua kuwa Masatu pengine ni mjomba wa Nchimbi, hivyo anajiingiza kichwa kichwa kwenye ugomvi asiojua kiini chake. Nape ni shujaa, anastahili pongezi za kila raia mwema. Mafisadi wamkandie, wasimkandie, huyu kijana ni dume, kammaliza fisadi Lowassa!
 
Najua siku zote chuki za Field marshal dhidi ya nchimbi lakini hainizuii kuendelea kumwelimisha......record ya nchimbi kwenye uongozi wa nchi yetu....akiwa DC wa bunda alikuta bunda ikiwa na shule za sekondari zipatazo saba tu...lakini kwa kipindi cha mwaka mmoja wa u dc wake aliweza kusimamia ujenzi wa shuile mpya 17 za sekondari..hakuna mkuu wa wilaya alieweza fanya hivyo kwa kipindi chote cha awamu ya tatu ya Mkapa...

Bunda wanamuheshimu kwa hilo na ndio maana wakati jk akisema kila kata ijenge shule kwa kipindi kifupi cha mwaka mmoja alitoa mfano wa bunda na alisema wao mbona waliwezana alieweza alikuwa na mpiganaji Nchimbi...akiwa mwenyekiti wa vijana alikuta umoja huo ukiwa na graduates wapatao watatu tu..lakini aliweza kuwateua wafuatao mpaka nao wameingia katika siasa kama mnavyowaoona nacho ni kipaji cha kutambua uwezo wa wenzako..nao ni alimteua Dk cyril Chami kuwa mratibu wa maswala ya uchumi ya uvccm,alimteua dk kamala kuwa mwenezi, alimteua makala akitokea IFM kuwa muhasibu kabla ya hapo muhasibu wao alikuwa hana ata certificate,alimteua Mwita rais wa udsm kuwa katibu wa mkoa,sixmund na hadija faraji wote wa UDSM kuwa makatibu wa mikoa, dk Tizeba kuwa mjumbe wa baraza kuu, Masha kuwa mjumbe wa kamati ya utekelezaji, john mongela kuwa mjumbe wa kamati ya utekelezaji,na wengine wengi...sasa hizo chuki zako kaka umetoka nazo wapi wewe mjukuu wa mzee JM....unatuletea mpaka taarifa za msafara wa kuzikwa AC...jina lililukwa wewe ndiwe ulijaza hayo majina????falasi.

Vita hiyo Nape kamwe haiwezi atachapwa kama amesimama na kama Nchimbi kwela ameamua kula sahani moja na nape nakwambia Nape hana pa kutokea....hatoki maisha yakenasema.niko tayari kuweka dau la milioni 50...mziki wa nchimbi Nape hauwezi....tarehe sita baraza kuu.sikiliza kama Nape hatopewa alama F
 
Sometimes ni kuziachia facts zi-speak for itself, mkuu mimi sijikombi kwa viongozi mufilisi kama Nchimbi, hapa linalosemwa ni kumpa heshima Nape, na ni bunge la taifa, ambalo siku Amina alipofariki, huyo bosi wako unakumbuka alivyozomewa mle ndani, pamoja na kutokubaliana na mawazo yako ya kumsifia Chimbi kama Mungu, bado suwezi kukuita wewe bina-adam kama mnyama Falasi, that is very low and pathetic thinking naona umepania sana kuwa mtoto wa kiongozi mpaka kujiita haya majina, maana ndio ndoto yako siku zote kuonekana kuwa ni mtoto wa kiongozi mbele ya jamiii, exactly marafiki wa Nchimbi's characters, sasa kula facts hapa chini labda sasa utaelewa ni kwa nini siku zote ninasema kuwa viongozi wetu wa bongo wana-benki kwenye ujinga wetu wananchii:-

1.
Quote: Fisadi Mtoto

unatuletea mpaka taarifa za msafara wa kuzikwa AC...jina lililukwa wewe ndiwe ulijaza hayo majina????falasi.Vita hiyo Nape kamwe haiwezi atachapwa kama amesimama na kama Nchimbi kwela ameamua kula sahani moja na nape nakwambia Nape hana pa kutokea....hatoki maisha yakenasema.niko tayari kuweka dau la milioni 50...mziki wa nchimbi Nape hauwezi....tarehe sita baraza kuu.sikiliza kama Nape hatopewa alama F
Yesterday 09:13 PM
2.
Quote: Kutoka Bungeni

Mgombea wa kiti cha Uenyekiti, Vijana (UVCCM), Nape Nauye, ambaye anaelekea kutokuwa chaguo la uongozi uliopo madarakani aliyeshangiliwa kwa nderemo katika ukumbi wa Bunge, Dodoma Ijumaa.

Tausi Mbowe, Dodoma
Mwananchi

MGOMBEA wa kiti cha Uenyekiti katika Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Nape Nauye, jana alilitikisa Bunge pale alipotambulishwa na kushangiliwa na idadi kubwa ya wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kushangiliwa huko kulimfanya Nape, anyanyuke mara tatu kuwashukuru wabunge waliokuwa wakimshangilia kwa kugonga meza zao kama ishara ya kumkubali huku yeye akiwapungia mikono wabunge hao.

Shangwe hizo ziliwafanya wabunge hao kushindwa kuendelea kumsikiliza Spika Samuel Sitta, aliyekuwa akitoa matangazo mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu. Hali hiyo ilimlazimisha Spika Sitta, kusubiri Wabunge hao wamalize kumshangilia Nape, ambaye katika siku za hivi karibuni ameingia katika mzozo mkubwa na baadhi ya viongozi wa juu wa CCM mara tu baada ya kutangaza kuwania nafasi hiyo na kutoa tuhuma zito kwa baadhi ya viongozi wa umoja huo.

Baada ya kuona hali ya mambo imetulia Spika Sitta, alisema Nape, ni mmoja wa vijana machachari aliyeibuka siku za hivi karibuni katika UVCCM.
Sitta alisema anamtakia kila la heri mgombea huyo, katika mambo yake hasa katika kipindi hiki anachoelekea bila kufafanua ni kipindi gani lakini kwa hali ya mambo ilivyo alikuwa akimaanisha mchakato wa uchaguzi wa UVCCM.
"Huyu ni kijana machachari umoja wa vijana wa CCM na nimtakia kila la heri katika mambo yake yajao," alisema Spika na kushangiliwa na wabunge wengi.
 
Where were Nchimbi, Makamba and Lowassa when Nape received standing ovation?
 
Najua siku zote chuki za Field marshal dhidi ya nchimbi lakini hainizuii kuendelea kumwelimisha......record ya nchimbi kwenye uongozi wa nchi yetu....akiwa DC wa bunda alikuta bunda ikiwa na shule za sekondari zipatazo saba tu...lakini kwa kipindi cha mwaka mmoja wa u dc wake aliweza kusimamia ujenzi wa shuile mpya 17 za sekondari..hakuna mkuu wa wilaya alieweza fanya hivyo kwa kipindi chote cha awamu ya tatu ya Mkapa...

Hivi ni shule za Serikali au za jumuiya na wananchi? Unaweza kutupatia majina ya shule hizo na utendajiufanisi wao tangu zikamilike?
 
With all respect kwa wakuu wote, naomba kuigusa hii topic kidogo, maaan imenigusa sana:-

1. Wa-Tanzania tumefikia mahali ni lazima tukubali kuwa ufisadi ndio siasa ya sasa kwa taifa letu, kwamba pmaoja na matatizo yote tuliyonayo ukweli wa mbali ni kwamba tukiweza kulikabili tatizo la ufisadi, basi mengine yote yaani matatizo tuliyonayo, yatajinyoosha yenyewe, lakini the name of the game ni ufisadi.

2. Sasa kwenye hili la ufisadi, lets be honest with each other, yaani wananchi at large ni lazima tuamue sasa tunataka kuwa upande gani kwa sababu, hakuna neutrality, wala middle position na ufisadi, either you are for it au you are not, either uko with us tunaoupinga au uko na wanaoufanya na wanaoushangilia.

3. Kwenye hili ninaomba kusema wazi kuwa ninatoa heshima nzito na a strong support kwa kiongozi huyu kijana Nape, ninajua for a fact kwamba record yake ni safi haina mikwaruzo, na heshima yangu kwake ilianzia pale ambapo yeye kama mimi pia, tuliitwa na muungwana kwa wakati tofauti wakati wa uchaguzi wa urais uliopita, katika kutaka our support kwa kambi yake, yeye ninajua kuwa alimkatalia kata kata muungwana, kwa sababu nyingi sana lakini ya msingi ilikuwa ni marafiki wengi wa muungwana, hawakuwa safi kushirki nao kwenye coaliton ya kisiasa kwa maneno mengine ni corrupt, kama wote tunavyojua sasa kutokana na ushahidi mbali mbali uliokwisha jitokeza, wazi.

4. Inanisikitisha sana kwamba somehow tumewaachia viongozi wasiofaa kuushika Umoja Wa Vijana ambao one time ulikuwa umeshikiliwa na Mzee Joseph Nyerere ambaye hakuwa na mchezo kabisa katika kufuata haki, sasa huu umoja umekuwa almost wa mtu mmoja, ambaye kwa kuamini kuwa ana ukaribu na the powers wa sasa basi anaweza kufanya atakalo that is pathetic.

Hapa again ninamlaumu Rais wa sasa, kwa sababu haiwezekani kiongozi mmoja wa CCM apewe alama ya E kiuongozi na uongozi huu suspect wa Vijana halafu aende bungeni na kushangiliwa namna hii na viongozi wengine tena wa CCM, something is not right na uongozi wa sasa!

Kwa kumaliza ninasema kuwa kwa wale wapenda mabadiliko kwa taifa letu, huwezi ukasema serikali ya sasa haifai lakini ukampondea huyu kijana Nape, huwezi ukampenda Obama, anayesimamia change, halafu ukamponda Nape ambaye pia anasiamia hiyo hiyo change, ila kwa njia tofauti kuliko ya Obama, hasa kutokana na tofauti ya mazingara ya kisasa ya grounds wanazozisimamia.

Nape, aendelee ksuimama kidete akielewa kuwa mabadiliko ya kisiasa sio kitu rahisi kukubalika, Umoja Wa Vijana yes ni step kubwa sana katika kutafuta nafasi ya kiongozi kuonyesha uwezo wake wa kulilia na kuleta mabadiliko, kwa hiyo Nape apokee kwa heshima kubwa vietndo kama hivi vya kusimamiwa na wabunge karibu wote bungeni kutoa heshima zao kwa ushujaa wake wa kusimama kidete,

Hakuna tatizo la time kwenye kutafuta mabadiliko, kwa hiyo ni sawa kabisa kwa Nape ksuema maneno mazito now kwa sababu politically huu ndio hasa wakati wa kusema na usikike wakati wa kukaribia uchaguzi, kwa sababu huyu mama Pelin huko kwao Alsaka kula Moose ni sawa, lakini sio sasa wakati yeye na Makeni wakigombea urais, sasa ataulizwa kwamba kwa nini unakula yule mnyama, asingekwua mgombea isingekuwa tatizo, ndio siasa inavyochezwa, maswali serious kuhusu nonesense huulizwa wakati wa uchaguzi sio kabla, kwa hiyo Nape hakukosea kuuliza kuhusu majengo sasa, yaani wakati wa uchaguzi kukaribia.

Mkuu Nape, tunakutakia mafanikio katika hivi vita ambavyo wengine tumevulia nguo siku nyingi sana, na sasa tuko kwenye kuvioga, usimame imara bila kuogopa, you have our attention sasa wewe ni kungalia mbele tu, hata ukikosa huu Umoja wa vijana, bado kuna nafsi nyingi sana tena muhimu kuliko hiii, ninasema bravo Nape, na kuna mabao tuko nyuma yako. na heshima kwa wabunge wote waliotoa heshima kwako.

Mingu Aibariki Tanzania.


Mkuu,

Heshima yako mbele.Kwa kweli Taifa hili limekosa watu wenye msimammo na wanaoishi kwa bahati nasibu.

Naona Nape anawachanganya watu sana huko UVCCM kufikia hatu jamaa mmoja ananisumbua kwenye Inbox, anataka Dataz za Nape wakati akiwa ansoma huku India, mimi nikamwambia unataka kumjua Nape as aliekua Student wa Bangalore University,au Nape as UVCCM Candidate ama kama mtu aliyekua kiongozi wakati fulani wa serikali ya wanafunzi wa Kitanzania hapo chuoni?

Bado hajajibu la maana nikamwambia nita-block mail zake.
Nimemwambia atafute njia nyingine.

BTW. Sasa Nchimbi nae ni Failure wa karne.Ona jinsi alivyoaibika.Tatizo mtu ukishachonga vyeti lazima vikuumbue tu.

Mkuu,FMES bravo kwa makombora yako
 
Hivi ni shule za Serikali au za jumuiya na wananchi? Unaweza kutupatia majina ya shule hizo na utendajiufanisi wao tangu zikamilike?
Huzo shule zote zilikuwa chini ya serikali kuu na zilipata usajili mwaka wa 2005...wananchi wenyewe wa bunda wanajua hilo vizuri sana.shule utendaji wao ni ngumu kuujua kwa kuwa form four wa kwanza wanatoka mwakani...najua imewauma kuona jamaa kumbe ana record bora na ya mfano ambayo imekuja kutumika kwa nchi nzima.na hapo bado.
 
Mkuu vipi ukwieka majina ya hizo shule 17, alizozijenga in one year huku akiwa hayupo kwenye kituo chake cha kazi kwa karibu mwaka mzima akiwa Dar na Mwanza, kutengenza kampeni za urais wa mtandao!

Ilimchukua almost miezi sita ya u-DC kutayarisha yale maandamano yake bubu, yaliyozimwa na uwt akitaka kwenda Ikulu Chamwino kumtishia Mkapa kuwa lazima mtandao ushinde! Mkuu kuwa mkweli useme wazi hapa katika kipindi cha karibu mwaka na nusu ya u-DC wa Nchimbi, alikuwepo physically kule Bunda kwa muda gani?

Eti alijenga shule 17? ziko wapi mkuu hasa hizo shule? Madaraka wamepata matokeo tumeyaona tena wazi, sasa ungetegemea waanze kujiweka pembeni na uongozi baada ya hii aibu ya kujifanya tunataka viongozi vijana, kumbe ni bure ya ghali! Wakajifanya wana hela sana za kampeni kumbe ni kuchota BOT kwa ujanja ujanja, aibuu kubwa sana kwa taifa,

Bravo Nape, kwa kusimama kidete, Tanzania tunahitaji viongozi angalau wanne tu kama Nape, wanaoweza kusimama na ksuema msimamo wao bila kuogopa mtandao wala wanaojikomba kwa hao matandao!

Hapa ni taifa kwanza, na hizo affiliation na wapambe baadaye.
 
Hizi ni zama za mabadiliko.

Mtake msitake na CCM hivi sasa wanapaswa wawatumie wabunge wake machachari kama kina Mwakyembe, Anne Kilango, Zambi, Mpendazoe na wengineo na katika CCM wahakikishe wanakuwa na watu kama Nape na si waliochoka kama Makamba, Nchimbi, Kingunge ambao kwa madaraka ni kwa gharama zozote hata ikibidi kusema uongo.

Kama mnakumbuka hata Makamba ukimsikiliza utabaini kwamba anasema serikali ya sasa imeshindwa kutekeleza hata Ilani na ahadi zake kwa vitendo na alisema Bungeni kwamba viongozi wanahubiri wasichotenda na walichokiandika katika Ilani hawakitekelezi. Bila kuwatumia hawa wanaojitokeza wazi wazi kutaka mabadilikoCCM itazama.

Hawa wanasiasa ndio "life jackets" kwa CCM kuweza kujiokoa katika hili dhoruba na wakiwaacha tu wamekwisha watazama. Waige mfano wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, anayewatumia kina Zitto Kabwe na Dk. Slaa kuelea katika siasa za Tanzania hadi sasa wanamtafutia mizengwe na salam zao wamezipata huko Tarime alipokwenda Dk. Mvungi kuhutubia na kumponda Mbowe akiamini ata-win matokeo yake wakamshambulia.

Watanzania wa sasa wana uelewa mkubwa sana, HAWAZUGIKI tena na maandamano ya kupongeza HOTUBA wala habari za KUTUNGA za magazeti yaliyochoka.
 
Kama mimi ningekua Nchimbi, ningekuwa shujaa kwa kumpigia debe na hatimaye kuhakikisha Nape anashinda. Siasa ndio zinataka mtu anayeweza kubadilika. Naamini kwa hili Nchimbi atakua ameelea na kuvuka katika hili dhoruba
 
Kama mimi ningekua Nchimbi, ningekuwa shujaa kwa kumpigia debe na hatimaye kuhakikisha Nape anashinda. Siasa ndio zinataka mtu anayeweza kubadilika. Naamini kwa hili Nchimbi atakua ameelea na kuvuka katika hili dhoruba

Hivi kumpigia debe Nape ndio ushujaa? Ndio uzuri wa Bongo wewe ukitaka umaarufu wa ghafla very easy just make contraversial statament then media ina pick overnight ushakuwa mkombozi, shujaa, nk

It did work kwa Mrema, Kaburu, Zitto, Slaa nk
 
Huyu Nchimbi ndo anajichimbia kabuli labda asubili ubunge wa kuteuliwa na rais lakini sera hana kwa kweli ni bora tu apumnzike yaani ni mmoja wapo ya wabunge wasio uzika kabisa.
 
Tatizo hiyo kamati kuu ya CCM na NEC ya CCM imejaa mafisadi tu, si ajabu kijana akaambulia patupu
 
wakubwa tuking'ang'ania ubishi hakuna tunalojenga, wengine hapa wanajifanya vipofu, hawasikii ama hawataki kuelewa...habari ndo hiyo, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni jamani, hivi kuna ubishi gani katika hili?
..kwamba nape kasema ukweli juu ya ubadhirifu uvccm lina mashaka? Mbona hakuna hata mmoja aliyejaribu kujibu? Kajaribu makamba huyo kakimbia kaona maji marefu....
...hivi mapokezi ya nape bungeni yanahitaji degree ngapi kujua ni heshima kubwa kapewa kwa kusema ukweli na kuwa tayari kuutetea na kuusimamia?
...hivi hili la nchimbi kuongoza kikao kumpa nape alama 'e' linahitaji diploma ngapi kujua kwamba kilichotumika ni ubabe na nguvu kubwa kuliko busara?
...nitashangaa kama nec na cc watabariki haya maana yake ni matusi kwao kuwa nape hafai hata kuwa mjumbe wa nyumba kumi nao ndio walio mpitisha juzi kuwa anafaa kuwa mnec na mkutano mkuu ukampa heshima kubwa ya kumpa kura nyingi....
..pita mtaani leo uliza who is nape,,utasikia habari yake, na haya hayana chumvi, mnyonge lakini haki yake mpeni?
..inasikitisha kuona eti kuna mtanzania anatetea wizi wa wazi wazi wakina nchimbi wanao shirikiana na lowassa na muhindi subash patel kuibia uvccm bila hofu wanajigamba kuwa eti hao wezi ni mashujaa??!1!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Inashangaza mno
..angalia mwanahalisi kesho bodi nzima ya uvccm imekana kuujua mkataba ule maana yake nchimbi na lowassa wamesaini mkataba wao, leo kuna mtanzania anatoka na kuwaona hawa wezi mashujaaaa!!!!!!!!!!!!!!hakika ajabu kubwa....
..makamba anaficha wapi uso wake baada ya kubwata eti bodi ya wadhamini imetimiza wajibu wake kupita kiasi na kumkemea nape hadharani...hakika anapaswa kufukuzwa hata kazi hiyo maana yeye na hosea mtetezi wa richmond hawapishani.....
 
Hivi kweli haya niyasomayo juu ya anayosifiwa nchimbi yanaandikwa na mtu kwa ujasiri?siamini...come again nije na nondo za kukutoshaaaa
 
Mkuu vipi ukwieka majina ya hizo shule 17, alizozijenga in one year huku akiwa hayupo kwenye kituo chake cha kazi kwa karibu mwaka mzima akiwa Dar na Mwanza, kutengenza kampeni za urais wa mtandao!

Ilimchukua almost miezi sita ya u-DC kutayarisha yale maandamano yake bubu, yaliyozimwa na uwt akitaka kwenda Ikulu Chamwino kumtishia Mkapa kuwa lazima mtandao ushinde! Mkuu kuwa mkweli useme wazi hapa katika kipindi cha karibu mwaka na nusu ya u-DC wa Nchimbi, alikuwepo physically kule Bunda kwa muda gani?

Eti alijenga shule 17? ziko wapi mkuu hasa hizo shule? Madaraka wamepata matokeo tumeyaona tena wazi, sasa ungetegemea waanze kujiweka pembeni na uongozi baada ya hii aibu ya kujifanya tunataka viongozi vijana, kumbe ni bure ya ghali! Wakajifanya wana hela sana za kampeni kumbe ni kuchota BOT kwa ujanja ujanja, aibuu kubwa sana kwa taifa,

Bravo Nape, kwa kusimama kidete, Tanzania tunahitaji viongozi angalau wanne tu kama Nape, wanaoweza kusimama na ksuema msimamo wao bila kuogopa mtandao wala wanaojikomba kwa hao matandao!

Hapa ni taifa kwanza, na hizo affiliation na wapambe baadaye.
Kaka mwenye chuki dhidi ya Nchimbi....ulikuwa unampa ruhusa wewe kutokuwa eneo lake la kazi au unajitungia tu wewe..hujui siasa za tanzania ndio maana mambo menginine ya ndani inabidi tuwaaachie walioko nyumbani tz.ili nchimbi aweze kuooperate sio lazima atembee yeye,tayari ana watu kila sehemu ya tanzania....
umetaka pia kujua shule ambazo zilijengwa na uongozi wa Nchimbi mpaka zikawa ni mfano kwa kujenga shule za kata tanzania,kabla ya kuzitaja kwanza ningependa kukupa hali halisi ilikuwaje bunda pamoja na kupata kuwa na waziri mkuu warioba na watu kama kina wasira etc...kulikuwa na shule tano tu za umma wilaya nzima hivyo kupelekea asilimia 20 tu ya wanafunzi waliofauru darasa la saba kupata nafasi ya kujiunga sekondari...bajeti ya halmashauri ikawa haitoshi..ikabidi mh Nchimbi awaombe wananchi wajifunge mkanda kuhakikisha watoto wote wanapata shule..aksaanza operation ya mawka mmoja ilioleta shule zifuatazo:
1.Emanuel Nchimbi{walimpa jina kwa heshima yake}sec
2.Sazira Sec
3.Kunzungu Sec
4.Rubana Sec
5,Nyiendo Sec
6.Sizaki Sec
7.Sarama Sec
8.Wariku Sec
9.Gutta Sec
10.Nyeruma Sec
11.Muranda Sec
12.Chitengule Sec
13Kisorya Sec
14.Mwigundu Sec
15.Mihingo Sec
16.Mekomariro Sec
17.Hunyari Sec
Na pia baada ya thesis yake ya masters kuwa abt saccos alienda na kuanzisha kwa vitendo bank kata katika kata ya bunda ambapo zilijengewa ofisi na waratibu...kwa sasa unaposikia watu wanaenda bunda kujifunza bank kata bunda basi ujue ni kazi ya Nchimbi...bravooooo mpiganaji.
 
Last edited:
Back
Top Bottom