Sakata la Lissu "Handle with care"

Sakata la Lissu "Handle with care"

Tumeshuhudia siku za hivi karibuni polisi imekuwa ikihangaika na matamshi ya Mbunge wa Singida Mashariki Mh. Tundu Lissu kuwa rais Magufuli ni "dikteta uchwara".

Hebu tujiulize nini hasa lengo la hili sakata kwa pande zote zinazovutana.

Haiwezekani mtu unakamatwa/shitakiwa kwa kosa fulani halafu unarudi kutenda kosa lilelile tena nje tu ya jengo la mahakama.

Binafsi naona ni kama kuna mtego fulani kwa chama tawala utakaohitimishwa September 1, chini ya Operation UKUTA.

Nafikiri nia hasa ya Chadema ni ama Lissu afungwe au awekwe ndani ipatikane sababu ya kufanikisha operation hiyo.

Lengo lingine nafikiri ni kukiweka chama kwenye headline kwa muda mrefu na kufifisha ziara za mtukufu rais zinazoendelea. Kumbuka kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Mh. Mbowe alisema wanauwezo wa kufanya siasa ndani na nje ya bunge.

Lengo lingine "nafikiri" ni mkakati wa kumuandaa mtu atakayeaminiwa na kuonewa huruma na jamii (Mandela style) ili labda baadaye aje kugombea cheo kikubwa ndani au nje ya chama.

Lengo lingine nafikiri ni kuionyesha dunia na watanzania kwa ujumla kuwa serikali ya Magufuli ni ya kidikteta inayovunja katiba yake ili kuthibitisha maneno ambayo yamekuwa yakisemwa na chama hicho.

Serikali ijue Chadema ni chama kikubwa kina uzoefu mkubwa kina wanasiasa wazoefu na wakongwe, hivyo kina mikakati yake na mbinu mbalimbali za kujiimarisha. Hivyo, serikali isilichukulie sakata la Lissu kama jambo dogo, should handle this issue with care.

Kumbuka moto huanza na cheche moja baadaye husambaa na kuunguza msitu mzima.

Haya ni mawazo yangu binafsi.
Ni andiko zuri tu kwa anaye tumia kichwa kufikiri...
 
Huwa wanamuita Mbowe kwa kebehi kuwa ni DJ, lakini ukweli ni kuwa kama ni DJ basi ni wa ukweli kwani kila muziki anaouweka Ccm wanaucheza na serikali wananengua mpaka basi.

Kamusi iko wazi kuhusu neno Dikteta jee wanashindwa kulisoma na kujua tafsiri yake kuwa sio matusi?

DJ Mbowe shusha CD za kutosha kwa mtindo wa bandika bandua wacheze mpaka nyonga zifyatuke.

Leo ni Lissu, kesho CD nyingine, hivyo hivyo hadi sept1 hapo ndio unashusha remix
Kama utani vile, lakini kuna cha kujifunza pia.
 
Hapo umeeleweka ila kama unauamusha upande wa kijani iv
 
Tumeshuhudia siku za hivi karibuni polisi imekuwa ikihangaika na matamshi ya Mbunge wa Singida Mashariki Mh. Tundu Lissu kuwa rais Magufuli ni "dikteta uchwara".

Hebu tujiulize nini hasa lengo la hili sakata kwa pande zote zinazovutana.

Haiwezekani mtu unakamatwa/shitakiwa kwa kosa fulani halafu unarudi kutenda kosa lilelile tena nje tu ya jengo la mahakama.

Binafsi naona ni kama kuna mtego fulani kwa chama tawala utakaohitimishwa September 1, chini ya Operation UKUTA.

Nafikiri nia hasa ya Chadema ni ama Lissu afungwe au awekwe ndani ipatikane sababu ya kufanikisha operation hiyo.

Lengo lingine nafikiri ni kukiweka chama kwenye headline kwa muda mrefu na kufifisha ziara za mtukufu rais zinazoendelea. Kumbuka kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Mh. Mbowe alisema wanauwezo wa kufanya siasa ndani na nje ya bunge.

Lengo lingine "nafikiri" ni mkakati wa kumuandaa mtu atakayeaminiwa na kuonewa huruma na jamii (Mandela style) ili labda baadaye aje kugombea cheo kikubwa ndani au nje ya chama.

Lengo lingine nafikiri ni kuionyesha dunia na watanzania kwa ujumla kuwa serikali ya Magufuli ni ya kidikteta inayovunja katiba yake ili kuthibitisha maneno ambayo yamekuwa yakisemwa na chama hicho.

Serikali ijue Chadema ni chama kikubwa kina uzoefu mkubwa kina wanasiasa wazoefu na wakongwe, hivyo kina mikakati yake na mbinu mbalimbali za kujiimarisha. Hivyo, serikali isilichukulie sakata la Lissu kama jambo dogo, should handle this issue with care.

Kumbuka moto huanza na cheche moja baadaye husambaa na kuunguza msitu mzima.

Haya ni mawazo yangu binafsi.
Kwa kila hoja nakuunga mkono sana. Polisi na serikali wanahitaji umakini sana.
Ushauri wangu ni kubadili namna ya kufanya ukamataji. Huu ukamataji baridi hautasaidia kumfanya mkosaji aache kuendelea na huu mchezo. Polisi waanze kufanya ukamataji wa nguvu halisi au zakutengeneza kiasi akitoka hapo ni hospitali tu. Kwa aina hii ya ukamataji itamfanya aache kufanya kosa hili, au akifanya kosa tu atakuwa anakwenda kujisalimisha polisi.
 
Kwahiyo mnataka kutuaminisha kuwa CHADEMA wanajua mbinu za siasa kuliko CCM?
 
Nafikiri nia hasa ya Chadema ni ama Lissu afungwe au awekwe ndani ipatikane sababu ya kufanikisha operation hiyo.

Unamtetea atoke!! Hapo kafika hakuna cha nini wala nini.CHADEMA waogopwe na POLISI!!!! Unaota.Operation gani watafanikisha!!! Sitaki kumwaga mtama hapa lakini wao wenyewe wako so frustrated kama hujui.Umeona Lowasa tu anavyotolewa mkuku utafikiri kibaka akienda vituo vya polisi.Maskini alidhani bado aweza heshimiwa hata na Koplo anajikuta wala hana heshima tena!!
 
Mbona mimi sioni watu wenyewe wakuitingisha serikali kiasi cha jumuia za kimataifa kuingilia?
 
Hakuna mpango wowote hapo, lissu amekosa jukwaa sasa ameamua kutafuta kwa njia nyingine. Tatizo lake anafikiri serikali ya sasa ni ile iliyo pita, kama atakutwa na kosa basi atahukumiwa na hakuna wa kufanya lolote. Tatizo la watanzania wengi wamesahau kuwa sisi tuko Africa na africa mambo ni tofauti na kwa wazungu. Huku kwetu hakuna kufata sheria, sio serikali wala upinzani, wote wanafata wanayo taka wao. Chukua mfano wa hii movie ya Lissu, anacho pigania ni nini hasa?
 
Wacha wacheze. Hata gadafi alianza ivi ivi na mwisho wake ulikuwa mbaya. Damu zinazomwagwa kila mwaka zinamlilia Mungu mbele ya kiti chake cha enzi. Ipo siku ghadhabu ya Mungu itawaka na hakuna atakae zuia na waonevu wote watalia na kusaga meno
Wapuuzi wenzako walishashituka kuwa walifanya kosa kumuondoa Gadaf bado wewe tu. yaelekea kwako Libya ya sasa ni Bora kuliko ile ya gadaf! kweli kwenye dunia hii kuna mataahira mengi sana.
 
Kwa kila hoja nakuunga mkono sana. Polisi na serikali wanahitaji umakini sana.
Ushauri wangu ni kubadili namna ya kufanya ukamataji. Huu ukamataji baridi hautasaidia kumfanya mkosaji aache kuendelea na huu mchezo. Polisi waanze kufanya ukamataji wa nguvu halisi au zakutengeneza kiasi akitoka hapo ni hospitali tu. Kwa aina hii ya ukamataji itamfanya aache kufanya kosa hili, au akifanya kosa tu atakuwa anakwenda kujisalimisha polisi.
Mkuu huwezi kuendesha msako wa kukamata watu hovyo bila grounds zozote za sheria.
 
Unamtetea atoke!! Hapo kafika hakuna cha nini wala nini.CHADEMA waogopwe na POLISI!!!! Unaota.Operation gani watafanikisha!!! Sitaki kumwaga mtama hapa lakini wao wenyewe wako so frustrated kama hujui.Umeona Lowasa tu anavyotolewa mkuku utafikiri kibaka akienda vituo vya polisi.Maskini alidhani bado aweza heshimiwa hata na Koplo anajikuta wala hana heshima tena!!
Mkuu simtetei atoke bali atatolewa na udhaifu wa makosa wanayomkamata nayo.
 
Back
Top Bottom