Sakata la Lissu "Handle with care"

Sakata la Lissu "Handle with care"

Hakuna mpango wowote hapo, lissu amekosa jukwaa sasa ameamua kutafuta kwa njia nyingine. Tatizo lake anafikiri serikali ya sasa ni ile iliyo pita, kama atakutwa na kosa basi atahukumiwa na hakuna wa kufanya lolote. Tatizo la watanzania wengi wamesahau kuwa sisi tuko Africa na africa mambo ni tofauti na kwa wazungu. Huku kwetu hakuna kufata sheria, sio serikali wala upinzani, wote wanafata wanayo taka wao. Chukua mfano wa hii movie ya Lissu, anacho pigania ni nini hasa?
Mwenyewe umesema huku kwetu hakuna kufuata sheria ni kuoneana tu, likely na Lissu anatafutiwa sababu ya kufungwa.
 
Mwenyewe umesema huku kwetu hakuna kufuata sheria ni kuoneana tu, likely na Lissu anatafutiwa sababu ya kufungwa.
Na akiendelea hivi basi ujue anako elekea ni magereza. Hovi weee unafikiri Lissu akifungwa nini kitatokea? Nchi itachafuka au wazungu watakata misaada? Ukweli ni kuwa maisha yataendelea huku uraiani kama kawaida na atasahulika haraka sana.
 
Kuna kitu kinaitwa Presidential Decree.
Hakuna kitu kama hicho kunapokuwapo na katiba na uchaguzi wa kidemokrasia. Hicho huwapo pale nchi inapopinduiwa ikiwa katika kipindi cha mpito. Hicho iliwahi kuwepo hapa baada ya muungano wakati katiba ikiandaliwa. Baada ya hapo raisi akiapa kufuata katiba na akienda kinyume cha hapo hafai kuwa rais hata baba wa taifa alishawahi kusema sifa ya kwanza ya rais ni kufuata katiba aliyoapa kuongoza nchi. Alisema kinyume cha hapo ni uhuni. Rejea wakati ule wa Mwingi kwenye sakata la IOC na vugu vugu la kurudishwa kwa Tanganyika. Katiba ndio sheria mama mkuu na hakuna presidential decree Tanzania kwa sasa labda uniambie mabavu au hicho wanachomshtakia Lissu kinachohusiana na mambo ya uchwara! Ndio maana wapinzani wanatumia katiba na sheria zinazotambua shughuli zao lakini rais anasema tu mimi sijaribiwi mara oh mimi ndiye rais kana kwamba kuna mtu kasema yeye sio rais. Sasa kwa maelekezo ya rais vyama visivyokuwa na wabunge na madiwani lakini vina usajili wa kudumu visifanye mkutano? Na chama nini? Si watu? Sasa utaendeshaje chama bila kukutana na wanachama na kutafuta wanachama wapya? Si hata madhehebu ya dini yanafanya hivyo hivyo ndio maana unaona mihadhara na mikutano ya kidini ya hadhara na kupitia vyombo vya habari. Yote hiyo ni kuhubiri imani yao na kupata waumini au wafuasi wapya ili kukua na kujiimarisha vinginevyo basi baada ya watu kuokoka kungekuwa hakuna haja ya kuendelea na mahubiri au basi watu wangesali mara moja au mbili kwa mwaka. Ukweli ni kuwa katika mahali ambapo JPM anaiharibu CV yake yeye mwenyewe ni hapa kwenye kupiga marufuku mkutano na maandamano ya vyama vya siasa wakati yeye na CCM yake wakifanya na vile kuwapangia pa kufanya hii inabomoa umoja wa kitaifa. Vyama vimesajiliwa kitaifa na vinapaswa kufanya kazi hivyo yeye anasema wafanye tu kule walikochaguliwa. Analeta utengano badala ya utangamano! Mr. President, please rethink!
 
Serikali inacheza mziki wa Lissu
Kwa jinsi ilivyo badala ya kucheza itachezewa sana kwakuwa yenyewe haina sheria za kuhalalisha hayo inayoyafanya wakati mwenzao ana sheria na kanuni zinazoruhusu mikutano na maandamano kikatiba na sheria ya vyama vya siasa
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Wapuuzi wenzako walishashituka kuwa walifanya kosa kumuondoa Gadaf bado wewe tu. yaelekea kwako Libya ya sasa ni Bora kuliko ile ya gadaf! kweli kwenye dunia hii kuna mataahira mengi sana.
Libya ya Iraq au kuwait mkuu.
 
Tumeshuhudia siku za hivi karibuni polisi imekuwa ikihangaika na matamshi ya Mbunge wa Singida Mashariki Mh. Tundu Lissu kuwa rais Magufuli ni "dikteta uchwara".

Hebu tujiulize nini hasa lengo la hili sakata kwa pande zote zinazovutana.

Haiwezekani mtu unakamatwa/shitakiwa kwa kosa fulani halafu unarudi kutenda kosa lilelile tena nje tu ya jengo la mahakama.

Binafsi naona ni kama kuna mtego fulani kwa chama tawala utakaohitimishwa September 1, chini ya Operation UKUTA.

Nafikiri nia hasa ya Chadema ni ama Lissu afungwe au awekwe ndani ipatikane sababu ya kufanikisha operation hiyo.

Lengo lingine nafikiri ni kukiweka chama kwenye headline kwa muda mrefu na kufifisha ziara za mtukufu rais zinazoendelea. Kumbuka kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Mh. Mbowe alisema wanauwezo wa kufanya siasa ndani na nje ya bunge.

Lengo lingine "nafikiri" ni mkakati wa kumuandaa mtu atakayeaminiwa na kuonewa huruma na jamii (Mandela style) ili labda baadaye aje kugombea cheo kikubwa ndani au nje ya chama.

Lengo lingine nafikiri ni kuionyesha dunia na watanzania kwa ujumla kuwa serikali ya Magufuli ni ya kidikteta inayovunja katiba yake ili kuthibitisha maneno ambayo yamekuwa yakisemwa na chama hicho.

Serikali ijue Chadema ni chama kikubwa kina uzoefu mkubwa kina wanasiasa wazoefu na wakongwe, hivyo kina mikakati yake na mbinu mbalimbali za kujiimarisha. Hivyo, serikali isilichukulie sakata la Lissu kama jambo dogo, should handle this issue with care.

Kumbuka moto huanza na cheche moja baadaye husambaa na kuunguza msitu mzima.

Haya ni mawazo yangu binafsi.
Alifungwa Shekhe Ponda Issa Ponda waliojifanya want mihemko naye wakafyata mikia hapo hamna kitu anaweza kufungwa na wasifanye lolote
 
Dikteta anajiamini kupita kawaida, anadhani watanzania tunamuona malaika kumbe tunamuona kichekesho
Yaani nimeahidi mbele ya Mungu sitaki tens kusikiliza hotuba zake wala kuangalia TV kwa kipindi chote atalacho kaa madarakani kwani nafsi yangu imekereka kupita Maelezo.Hivi anadhani Nchi hii Ni take kama familia yake?
 
Back
Top Bottom