1000 digits
JF-Expert Member
- Oct 16, 2012
- 7,802
- 10,291
Hivi serikali nzima inashindwa akili na mtu mmoja?
Hapo ni man against man.
Mtu ndiye anayeongoza hoja za serikali na mtu ndiye anayeongoza hoja za wapinzani dhidi ya serikali.
Hakuna Aliyeshuka toka mbinguni. Wote ni wanadam na wote ni watanzania. Wote wanapata uongozi kupitia binadam wengine.
Jambo baya ni kuanzisha siasa zisizojali uhai na utu wa watu wengine.
Taifa halina raha ,watu wanaishi kwa huzuni na woga.
Hawa wanawawinda wengine kama swala na wengine nao wanaruka ruka huku na kule kutafuta pa kujificha nyuma ya wananchi.
Hawa wanatafuta huruma ya wananchi na hawa wanatafuta ulinzi na nguvu za silaha na majeshi.
Sheria na katiba zimewekwa pembeni.
Chadema kama Katiba inakiukwa nendeni Mahakamani. Kwa nini mnatumia nguvu zenu wenyewe wakati mahakama zipo.
Serikali inavunja katiba lakini Chadema nao wanavunja sheria na katiba kwa kuchukua sheria mikononi.
Tamko la polisi linaweza kupingwa mahakamani na sio maandamano na maneno ya kejeli au matamko.