kwa hiyo hii Gesi ikishafika Dar Viwanda vyote viko kwenye yadi moja tu??? Acha kutumika bwana!! Kwanza Watanzania wanataka Mkataba uwekwe wazi wa huu Mradi, pili uzalishaji waweza fanyika Mtwara na Dar kukawa na Center ya distribution. Mbona maji ya Ruvu kiwanda chake kiko pale Ruvu na yakifika Dar ndo yanasambazwa kwa matumizi.
Wananchi wa mtwara wanataka vitendo, wameshachoka kupewa ahadi kedekede zisizotekelezeka.
Tangu kikwete aingie madarakani amewaahidi mambo mengi sana moijawapo ni ujenzi wa barabara lakini kwa muda wa miaka yake saba ameweza kujenga barabara yenye urefu wa kilometa 60 tu!!
Wananchi wa Lindi waliahidiwa kiwanda cha mbolea sasa ni miaka nenda rudi lakini hakuna dalili ya kiwanda hicho kujengwa. Kama hiyo haitoshi, ilani ya uchaguzi ya ccm 2010 ibara ya 63 kifungu h na k vinataja ujenzi wa mitambo ya kuzalisha umeme mtwara (300MW) kwa gesi ya mtwara bay na Kinyerezi (240MW) kwa gesi ya songosongo. Sasa imekuwaje tena ccm na serikali yake wanahamisha magoli? au kwakuwa wamezoea kuhamisha na wananchi hukaa kimya? Mwaka jana mwishoni raisi kikwete alipokea ripoti ya wachina na siemens juu ya ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Mtwara/Lindi hadi singida yenye urefu wa kilometa 1,100 je mradi huo umeshatekelezwa?
Kama hali yenyewe ndio hii, unadhani wananchi hawana haki ya kumdharau profesa Muhongo ambaye ameshindwa kabisa kujibainisha usomi wake na kuishia kuongea na kutoa mifano dhaifu ambayo huwezi kumtofautisha na lakairo ama profesa maji marefu walioishia darasa la pili!!??
Safari hii hata ccm ifanyeje wananchi wa mtwara hawatakubali kurudi nyuma. Serikali lazima ijenge mtambo wa kuzalisha umeme kwa gesi asilia mkoani mtwara na ndipo iuingize kwenye gridi ya taifa. No more no less!!
Muhongo ana tatizo la mahusiano....hana lugha ya kiungwana (civilian) wala siyo mtu wa majadiliano. Atapata shida kama ataamua kubaki ktk siasa. Kwa utendaji na taalum kama mhandisi nafikiri hakuna tatizo
cement atazalisha kwa mabaki ya gesi. Sasa nyie mnatakaje[/COLOR]?
Kaka tafadhali weka kwanza kusudi la kunielewa, vinginevyo hata nikiongea mwaka mzima kama umedhamiria tu kubishana hakuna tunachoweza kuongea.
Kiwanda cha Mbolea kilichoahidiwa, malighafi ni ya kutengenezea mbolea ni mabaki ya uchafu unaotokana na shughuli ya gesi. Kama gesi haijachimbwa bado, kiwanda kitazalisha mbolea kutumia hewa? Hapa utaona kwamba, ni mpaka gesi izalishwe ndio mbolea itapatikana, AU?
Twende kwenye hili la umeme. Tata Mwita Maranya, naomba ujiulize mwenyewe, ikiwa wewe ndio kiongozi wa nchi hii, utafanya nini kwanza kati ya haya:
1. Kujenga mtambo wa umeme kwa ajili ya Dar es Salaam ambayo ina uhaba wa umeme na mahitaji ni makubwa, au kujenga mtambo Lindi na Mtwara ambapo hata uliopo hautumiki wote? (Hata hivi sasa, Mtwara kuna uzalishaji wa 11MW ambapo ni 5MW tu ndio zinatumika) sasa mnataka ufahari wa kwamba kuna zingine 306MW hazitumiki au ni nini?
2. Unaweza kuniambia Mtwara kama Mtwara inanufaika nini na ujenzi wa njia ya umeme unaoenda Singida ikizingatiwa hakuna mkoa unaolipwa fedha kwa kuwa mkoa huo kuna power station au power lines zimepita?
Mwita Maranya, gesi matumizi yake si umeme tu. Gesi lazima ifike Dar es Salaam liliko soko kubwa. Hebu jenga picha ni akili gani itakuwa imetumika, kuleta bomba Dar kwa ajili ya kusupply gesi viwandani, majumbani na kwenye magari, halafu wewe huyo huyo ujenge tena njia ya umeme toka Mtwara hadi Dar kuuingiza kwenye Grid ya Taifa!!!
Maneno yako ya kumalizia ya No more, no less hayaambatani na logistic reasoning ni ushabiki na si zaidi.
Tusipende kuwa washabiki ndugu zangu. Acha nikwambie kitu. Amin Dangote (yule Mnigeria tajiri mkubwa kuliko wote Africa) anaplan kujenga kiwanda cha Cement Mtwara. Mawazo ya kujenga kiwanda yanakuja kwa kuwa tu anajua atapata malighafi ya kutengenezea cement kutokana na machimbo na uchakataji wa gesi. Hapa utasikia wengine wanasema tumeahidiwa kiwanda mbona hakijengwi, jibu linakuja pale pale, cement atazalisha kwa mabaki ya gesi. Sasa nyie mnatakaje?
Mwita Maranya, yoote niliyoyaweka hapo hukuyaona bali uliona kipande hiki tu cha kukupatia ushindi wa UBISHI. Sikumaanisha kuwa ni gesi ndio hugeuzwa kuwa cement, mimi si mtaalamu wa cement na wala sijatumwa na mtu kama unavyosema lkn sipendi unafiki kama uliotumia kuruka mada zoote na kuja hapa na kipengele kimoja tu ili uendeleze ubishi.Sina sababu ya kujibu hayo mengine uliyoandika kwakuwa hakuna hata hoja ya kujadili zaidi ya kuwakilisha tabaka tawala na hujipi nafasi ya kutazama hoja ya wanamtwara bali unaimbishwa wimbo na watawala bila kujua nani kautunga na kwa madhumuni gani.
Kwa akili yako unataka niamini kwamba Tanga Cement (Tanga), Mbeya Cement (Mbeya), Twiga Cement (Dsm), Rhino Cement (Tanga na Mkuranga), Lake Cement (Dsm) na Dar es salaam (Cement) viwanda vyote hivyo vinafanya kazi kwakuwa huko viliko kwakuwa malighafi ambayo ni mabaki ya uchakataji wa gesi inapatikana kwa wingi? Ndugu shizukan ni aibu sana kuongelea vitu ambavyo hujui hata abc zake. Malighafi kubwa na ya msingi inayotakiwa kwa ajili ya kiwanda cha cement ni gypsum ambayo ndiyo sababu ya hivyo viwanda nilivyovitaja vimeendelea kuwepo kabla ya kuwepo kwa uvumbuzi na matumizi ya gesi asilia.
Siku nyingine usikurupuke kuandika vitu usivyovifahamu kwakuwa tu umetumwa kuitetea serikali yako. Haya ndiyo maswali ya msingi ambayo seri8kali ya ccm imeshindwa kuyajibu na kubaki kupiga propaganda za hovyo. Sasa kwakuwa wananchi wanauelewa wa kutosha wanawachora tu jinsi mnavyoweweseka. Wewe na profesa Muhongo wote ni manzi ga nyanja....
Labda ungesoma kwanza nyaraka za wana Mtwara kuhusu hili suala, hawajasema gesi isiondoke, wanataka waone matunda yake kwanza hapo walipo, kwa sababu wameachwa nyuma kwa miaka mingi, na hata sasa ambapo mlangoni kwao kuna opportunity ya kufaidika walau kidogo wanapitwa tu kama vile hawapo...
wamegundua kwamba "plans za mnaijeria tajiri, mikakati ya libandari likubwaaaa, na mipango kabambe" ni danganya toto, vinginevyo ingetekelezwa kabla au hata sambamba na ujenzi wa bomba la gesi. wanataka viwanda vijengwe, bandari ijengwe, barabara zijengwe etc ili nao waweze kupata ajira waweze kumudu kusomesha watoto wao kwenye shule za kawaida na sio unyagoni, na waweze kumudu hata huo umeme waliopunguziwa bei ambao sasa hivi hawana ubavu wa kuugusa kwa sababu ya umaskini.
Kaka tafadhali weka kwanza kusudi la kunielewa, vinginevyo hata nikiongea mwaka mzima kama umedhamiria tu kubishana hakuna tunachoweza kuongea.
Kiwanda cha Mbolea kilichoahidiwa, malighafi ni ya kutengenezea mbolea ni mabaki ya uchafu unaotokana na shughuli ya gesi. Kama gesi haijachimbwa bado, kiwanda kitazalisha mbolea kutumia hewa? Hapa utaona kwamba, ni mpaka gesi izalishwe ndio mbolea itapatikana, AU?
Twende kwenye hili la umeme. Tata Mwita Maranya, naomba ujiulize mwenyewe, ikiwa wewe ndio kiongozi wa nchi hii, utafanya nini kwanza kati ya haya:
1. Kujenga mtambo wa umeme kwa ajili ya Dar es Salaam ambayo ina uhaba wa umeme na mahitaji ni makubwa, au kujenga mtambo Lindi na Mtwara ambapo hata uliopo hautumiki wote? (Hata hivi sasa, Mtwara kuna uzalishaji wa 11MW ambapo ni 5MW tu ndio zinatumika) sasa mnataka ufahari wa kwamba kuna zingine 306MW hazitumiki au ni nini?
2. Unaweza kuniambia Mtwara kama Mtwara inanufaika nini na ujenzi wa njia ya umeme unaoenda Singida ikizingatiwa hakuna mkoa unaolipwa fedha kwa kuwa mkoa huo kuna power station au power lines zimepita?
Mwita Maranya, gesi matumizi yake si umeme tu. Gesi lazima ifike Dar es Salaam liliko soko kubwa. Hebu jenga picha ni akili gani itakuwa imetumika, kuleta bomba Dar kwa ajili ya kusupply gesi viwandani, majumbani na kwenye magari, halafu wewe huyo huyo ujenge tena njia ya umeme toka Mtwara hadi Dar kuuingiza kwenye Grid ya Taifa!!!
Maneno yako ya kumalizia ya No more, no less hayaambatani na logistic reasoning ni ushabiki na si zaidi.
Tusipende kuwa washabiki ndugu zangu. Acha nikwambie kitu. Amin Dangote (yule Mnigeria tajiri mkubwa kuliko wote Africa) anaplan kujenga kiwanda cha Cement Mtwara. Mawazo ya kujenga kiwanda yanakuja kwa kuwa tu anajua atapata malighafi ya kutengenezea cement kutokana na machimbo na uchakataji wa gesi. Hapa utasikia wengine wanasema tumeahidiwa kiwanda mbona hakijengwi, jibu linakuja pale pale, cement atazalisha kwa mabaki ya gesi. Sasa nyie mnatakaje?
Tusipende kuwa Wakomunisti wa maneno wakuu, alichosema Waziri ni sahihi. Nchi hii haina utaratibu wa ukanda au majindo, kwa hiyo kauli ya Waziri ni kuwakumbusha wakaazi wa Mtwara kuwa, kuna tofauti ya Korosho uliyolima na Gesi ambayo ni MALI YA ASILI.
Kuwa darasa la 7 haimaanishi kuwa huna akili, tazama wewe na madarasa yako umeshindwa kuelewa suala dogo sana. Waziri hafananishi usafirishaji, Waziri anahoji 'Korosho za Mtwara zinaenda sokoni, gesi ya Mtwara itashindwaje kwenda sokoni?' Shida ni kwamba unajaribu kutumia hisia kuelewa.
Haya anayoyasema Waziri Muhongo hata Zitto Kabwe aliyasema BBC (simaanishi hizo mnazoziita kejeli) kwamba kuna viongozi wa ngazi ya Mkoa, Wilaya, Halmashauri na Wabunge wa mikoa ya Kusini walipelekwa nje kujifunza mambo kadhaa juu ya gesi. Kama nia ni kuweka maazimio wazi kwa Wanamtwara, mbunge wa Mtwara mjini ambaye nasikia naye ni kinara wa maandamano, anataka kuieleza nini Tanzania juu ya ushiriki wake katika ziara na vikao hivyo?