Gan star
JF-Expert Member
- Jul 7, 2016
- 380
- 980
Mwanadada na mfanya biashara Anerlisa , ametishia kumchukulia hatua za kisheria aliyekuwa mume wake, Ben Pol kutokana na madai kuwa amekuwa akimchafua kwenye mitandao ya kijamii. Anerlisa amepanga kumfikisha mahakamani mwimbaji huyo iwapo ataendelea kumtaja au kumhusisha kwenye mazungumzo yake au kwenye mitandao. Pia amemtaka amuombe radhi kwa kumchafua na kumpa siku 14 za za kutekeleza hilo. Taarifa hizo zimekuja baada ya kuvuja kwa barua ya mwanasheria iliyoandikwa kwa niaba ya Arnelisa kwenda kwa Ben Pol ambae hivi karibuni alifungua jalada mahakamani hapa nchini akiomba mahakama kuidhinisha kuachana kwao.
Kwa upande mwingine Ben Pol ametumia ukurasa wake wa Instagram kuelezea duku duku lake kutokana na sakata Hilo...
Anaandika Ben Pol
TAARIFA,SHAURI LA TALAKA.
Ben Pol angependa kuthibitisha uwepo wa shauri la talaka dhidi ya mke wake linaloendelea katika Mahakama ya mwanzo hapa Dar es salaam. Mahakama bado HAIJATOA talaka/ maamuzi yoyote mpaka pale litakaposikilizwa na kukamilishwa. Masuala haya ni ya BINAFSI sana na kwa kuwa shauri linaendelea Mahakamani Ben Pol asingependa lizungumzwe zaidi kwa heshima ya pande zote na kwa kuheshimu kazi ya Mahakama. Pia anaomba nafasi na faragha kwake na kwa familia katika kipindi hiki kigumu. Anawashukuru wote kwa uelewa na pia kwa familia, marafiki na mashabiki wote kwa support mnayoendelea kuionesha. Uongozi wa Ben Pol.
KIMOMBO
By date: 29 April 2021 Headline: Ben Pol's divorce proceedings are ongoing. At this time, Ben Pol would like to confirm that his divorce proceedings are in progress at the primary court but have not yet been finalised. These proceedings are a very private matter and he will not discuss any details out of respect for all parties involved. He kindly asks that space and privacy be given to him and his family during these challenging times. He appreciate everyone's understanding and takes this opportunity to thank his family, his friends and his fans for their ongoing support. Ben Pol’s management
Soma pia
1. Ben Pol aomba Talaka Mahakamani dhidi ya Mke wake Anerlisa
2. Hatimaye Anerlisa asaini Hati ya Talaka iliyowasilishwa na Ben Pol Mahakamani
Kwa upande mwingine Ben Pol ametumia ukurasa wake wa Instagram kuelezea duku duku lake kutokana na sakata Hilo...
Anaandika Ben Pol
TAARIFA,SHAURI LA TALAKA.
Ben Pol angependa kuthibitisha uwepo wa shauri la talaka dhidi ya mke wake linaloendelea katika Mahakama ya mwanzo hapa Dar es salaam. Mahakama bado HAIJATOA talaka/ maamuzi yoyote mpaka pale litakaposikilizwa na kukamilishwa. Masuala haya ni ya BINAFSI sana na kwa kuwa shauri linaendelea Mahakamani Ben Pol asingependa lizungumzwe zaidi kwa heshima ya pande zote na kwa kuheshimu kazi ya Mahakama. Pia anaomba nafasi na faragha kwake na kwa familia katika kipindi hiki kigumu. Anawashukuru wote kwa uelewa na pia kwa familia, marafiki na mashabiki wote kwa support mnayoendelea kuionesha. Uongozi wa Ben Pol.
KIMOMBO
By date: 29 April 2021 Headline: Ben Pol's divorce proceedings are ongoing. At this time, Ben Pol would like to confirm that his divorce proceedings are in progress at the primary court but have not yet been finalised. These proceedings are a very private matter and he will not discuss any details out of respect for all parties involved. He kindly asks that space and privacy be given to him and his family during these challenging times. He appreciate everyone's understanding and takes this opportunity to thank his family, his friends and his fans for their ongoing support. Ben Pol’s management
Soma pia
1. Ben Pol aomba Talaka Mahakamani dhidi ya Mke wake Anerlisa
2. Hatimaye Anerlisa asaini Hati ya Talaka iliyowasilishwa na Ben Pol Mahakamani