Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,025
Nenda katika msitu wenye nyani wengi.Msitu huo uwe na akina mama wanaokata kuni,kufunga mizigo ya kuni na kuibeba kichwani.Daima nyani huwaangalia kwa makini sana hawa akina mama wakidhani kwamba ile mizigo ya kuni inayoinuliwa na kuwekwa kichwani ni miti inang'olewa.Sasa jaribu kwenda chini ya mti wenye nyani juu,weka kata kichwani halafu jifanye kama unajitwisha ule mti.Kitakachotokea hapo,hata kama huo mti una urefu gani,nyani wote watajirusha mpaka chini wakihofu kupinduliwa pamoja na ule mti.