Your browser is not able to display this video.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, amesisitiza kuwa dhana ya haki na amani haziwezi kutenganishwa katika ujenzi wa taifa imara, akizitaja kuwa ni pande mbili za sarafu moja.
Akizungumza jana, Machi 4, 2026, katika Maadhimisho ya Siku ya Maridhiano (Maridhiano Day) nchini Tanzania, Mtanda ambaye alimwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mtanda amebainisha kuwa bila amani, hakuna mazingira yanayoruhusu taasisi na mifumo ya kisheria kufanya kazi ya kutoa haki na amekiri kuwa bila haki, amani inayokuwepo inakuwa haina msingi imara wa kudumu.
Pia soma: Mzee Butiku: Tukubali tunaye Rais
“Kwa hiyo hatuwezi kuzungumza kuhusu amani kama hakutakuwa na haki. Lakini pia ili haki iweze kupatikana ni lazima amani iwepo ndani ya taifa. Kwa hiyo amani ni jamvi la kuelekea upatikanaji wa haki na haki nayo ni jamvi kuelekea upatikanaji wa amani”, ameeleza.