Saga la Makonda: My Take

NN

Mh Rais asingeliongelea leo ingesaidia zaidi, kwasasa limepapalia curiosity

1. Kitwanga alitmbuliwa hadharani
2. Wilson Kabwe (RIP) hadharani hadi mauti
3. Wakurugenzi kama akina Rashed Badi Hadharani
4. Anne Kilango , hadharani
5. Kila siku Gery analeta barua za waliotumbuliwa

Orodha ni ndefu sana. Watu wanajiuliza hata kama si kutumbuliwa ni upi ukweli kuhusu Makonda? Kwanini anakingiwa kifua tofauti na wengine?

Sula litapoa, lakini makovu yake yatabaki yakivuja damu kila siku
Leo nani mwenye uthubutu wa kuongelea uhakiki wa vyeti?
Credibility ya Rais kuinyosha nchi ipo wapi?
Kwanini cheti cha Luhende kilikuwa hadharani, vya Makonda iwe siri?
Waliotumbuliwa kwa vyeti feki wanalitazamaje hili jambo? fair au kuna double std

Hili si la Makonda tena, linaigusa serikali na credibility yake. Mbaya sana
Leo zigo la Makonda anabebeshwa Rais!

Kuna tatizo gani wakitoka na kueleza wanachojua?
 


"walitegemea Raisi amfukuze kazi Mkuu wa Mkoa kwa kuwa wametaka wao iwe hivyo?"

Tunategemea amuwajibishe kwa kuwa katiba,sheria, kanuni na maadili ya uongozi wa nchi yetu Tanzania vimesha ainisha hivyo.
 
Tumeitikia wito wa kusafisha na kuwafichua wenye vyeti feki...ametuacha Msamvu.
Tumeambatana nae kufuatilia shilawadu na umbra wa mitandaoni... Ametukana kwani tumezidisha ubuyu.hakuna jipya kwani Hata yesu alitolewa akasurubiwe badala ya mnyanganyi na mhalifu baraba miaka 2000 iliyopita.
Wengi wa watu wanaofuga majini huwa yanawageuka.
 

Umejenga hoja nzuri sana kuhusu suala la imani [credibility].

Hapa nilipo najiandaa kuleta mada kuhusu suala zima la uchunguzi-usuli [background checks] unaofanywa kwa viongozi wa umma na watumishi wa umma kwa ujumla kabla hawajapewa kazi.

Nitaliunganisha na suala zima la mfumo na jinsi suala hili [la mfumo] ulivyolizungumzia kipindi kile ambapo wachache kati yetu ndiyo tulikuelewa vyema.

Nadhani sasa somo la mfumo linaweza kueleweka zaidi kupitia hili sakata la Makonda.
 
Neno upinzani unalitumia vibaya...sio kila anaejadili hili jambo ni upinzan. Fanyia kazi tafiti yako.
 
We si ulikuwa unasema makonda anaonewa leo ume surrender

Unafiki uache nyani ngabu
Huyu jamaa mnafiki kweli utafikiri hapo mwanzo alikuwa haoni makosa ya huy Mr. Zero brain, na usiishangae kesho akimtetea tena maana watu wenye mtindio wa ubongo wana kawaida ya kufanya mambo bila kumbukumbu
 

Magufuli anatakiwa "amtumbue" Makonda sio kwasababu wapinzani wake na watu wa "mitandaoni" wanataka hivyo. Ni kwasababu, maadili (udanganyifu wa vyeti vya elimu), sheria (udanganyifu wa vyeti na kupora kwa kutumia silaha), na ukosefu wa busara wa Makonda katika kutekeleza kazi zake, unamtaka rais amtumbue. Akifanya hivyo, atakuwa ameonyesha kwamba yeye ni rais makini, mtenda haki, na hapendelei mtu yoyote. Huo utakuwa ni ushindi wa rais na serikali yake, na sio wapinzani na mitandao inayomsaidia tu kutekeleza wajibu wake huo.
 
That's Very True Mkuu.
Kuhusu Ego..
 
Mtu mwenye akili anajua Makonda atatumbuliwa tu. It's a matter of time.
 
Rais anatuonyesha tabia yake,hajui maana ya kuwa rais na urais ni taasis
 
Kumbe wanaotaka RC wa DSM achukuliwe hatua ni wapinzani? Kumbe wapinzani wa nchi hii ndio wamesoma kwa shida na kihalali hivyo kuwa na uchungu na elimu kuliko wale wa chama tawala?
 
Kwanini Makonda aliandaa ile video na akalazimisha irushwe??
 
Mkuu hizo kelele ni za watu wa upande wa pili hasa wanaohusika na madawa ya kulevya,mbona hapo nyuma Makonda alifanya maamuzi mengi yenye kutia shaka na hatusikia hizi kelele .Kuna watu wanataka Makonda asurubiwe kwa kuwagusa wauza unga na hiyo inaonyesha kweli kwamba Makonda amefanya kazi nzuri na amewashika pabaya wauza unga hasa hao wauza unga madhahabuni na kwenye siasa na wengine waowatetea dada zao kwa sababu wanazozijua wao wenyewe hadi wanjitoa ufahamu eti kwa kuwa wengine ni brand zilizojengwa kwa muda mrefu.
 
Kikubwa hapo akimuondoa kwa cheti feki, wapinzani watarudi na PHD yake inaweza kuwa tatizo
 
Kwa hiyo vyeti katafutiwa na aliyemuwea?LB7 mmekosa cha kuandika
 
Hatomtumbua bcz serikali ina inteligency system. Rais anajua yote kuhusu makonda kupitia information system .
Kinachonishangaza ni tabia ya nyumbu kuamin na kushadadia haya mambo huku wakikiamin kinywa cha Gwajima na video clip ya sekunde 3.
Hv nyinyi NYUMBU kwann amreason.
 
Rais anawaongoza wananchi,na waliopo mitandaoni ni wananchi sasa unakataa maoni ya watanzania kwasababu wanasemea mitandaoni.
Mitandaoni ndiyo njia nyepesi ya kutoa maoni kwa wananchi wengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…