Safari za E. Lowassa Mikoani: Anamwakilisha nani!?

Safari za E. Lowassa Mikoani: Anamwakilisha nani!?

Wana-JF,

Nimekuwa najaribu kufikiria jinsi Mbunge wa Monduli na Waziri aliyejihuzuru kwa kashfa ya Mradi tata wa Richmond, Bw. E. Lowassa anavyotemebelea mikoa na wilaya mbalimbali hapa Tanzania. Amekuwa akijihusisha na harambee na kuchangia miradi mbalimbali ya maendeleo hasa inayoendeshwa na makundi ya kidini.
Katika siku za hivi karibuni, EL amejikita hata katika kukutana na wazee wa jadi. Kwa hali ilivyo safari hizi zinatumia hela nyingi sana.

Lakini unaweza kunisaidia kutafakari kidogo!
1. Hizi kazi anazofanya anafanya kama nani, mfano ni mkutano wake wa Shinyanga ambao amesikika akitoa siri za Baraza la Mawairi katika Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria pia na mkutano na Chama cha Waendesha Boda Boda, Tabora. EL akiwa ameweka Jiwe La Msingi katika Kaburi la Mnyugumba; EL katika Tambiko
2. Nani anagharimia safari zake??? Ni chama tawala au serikali kuenzi utumishi wake wa Uwaziri Mkuu!
3. Nini hasa lengo lake kwa nchi yetu, kama hela anazotumia hazina chanzo kilichowazi?
4. Ni nani anayeanda mikutano hii ya kumkutanisha na wananchi? CCM! Serikali!

Naomba ufikiri kwa kina kabla hujajibu.



Anatafuta kupigwa risasi coz Tsh 152,000, 000/= per day bado tunazikumbuka.
 

Mkuu kwa masilahi ya wengi, unafikiri leo EL akipata Urais huo atatelekeza sera za nani? Kwanza siamini ati bado Watanzania wanamhitaji Mh Lowasa kuongoza hii nchi kwa sababu amepata fursa zaidi ya moja kuongoza idara na taasisi mbali mbali za umma ambazo hakutuachia kumbukumbu nzuri za ku-miss huduma yake. Ninachofikiri ni kuwa Mh Lowasa anakusudia kuingia madarakani kwa inda na hila ili atekeleze matakwa binafsi. Kwa muktadha huu sidhani ati atazingatia sera za chama ama kundi lolote atakapokuwa raisi wa nchi hii.

Mpaka sasa anafanya mambo yote haya pekee yake?
Swali zuri sana hili, hata hivyo binafsi sijui kama anafanya harakati zote hizi peke yake. Endapo anafanya harakati zote hizi peke yake basi yatupasa tujiulize ni nini msukumo wa harakati hizi. Ama endapo anafanya harakati hizi chini ya uratibu wa kikundi binafsi ama kikundi fulani ndani ya CCM pia tunalazimika kujiuliza ni nini dhamira inayosukuma mipango na utekelezaji wa harakati hizi. Watanzania tunalo angalizo zuri tuliloachiwa na Mwl Nyerere kuwa 'mtu anayeng'ang'ania kuingia ikulu hatuna budi kumwogopa kama ukoma'. Ingawa kauli hii ya mwalimu inastigmatize wenye ukoma, lakini maudhui ya kauli hii ni kuwa Watanzania tupambane kwa kila mbinu kuepukana na tatizo baya kama la ugonjwa wa ukoma. Hivyo yeyote anayelazimisha kwenda ikulu hatuna budi kumkatalia maana hatujui dhamira yake ya kung'ang'ania kufikia nafasi ya maamuzi ya mwisho katika nchi yetu hii tunayoiita nchi changa.
Achilia wapinzani wake wa ndani ya chama chake na vyama pinzani. Anachofanya Mh Lowasa kinawatia ukakasi baadhi ya wanaCCM ambao hawaridhishwi na harakati zake hizi, hivyo kwanza atalazimika kupata ridhaa ya wanaCCM kabla hajapeperusha bendera ya CCM. Hii sio kazi nyepesi kama wengi wetu tunavyofikiria na kujiaminisha kuwa Lowasa atawabwaga wana CCM wenzake kirahisi kwa vile eti anakubalika sana kwa wajumbe wa NEC na CCM

Mkuu uchaguzi mkuu ujao ni mgumu sana kwa CCM kuliko ilivyo kwa vyama vya upinzani. Swali ni je, CCM wanajua kuwa watalazimika kufanya kazi ya ziada ili kushinda uchaguzi ujao?
 
peleka unafiki wako huko na hao wanaokutuma,umeena ww ndo unamjua yesu tu peke yako mchawi mkubwa ww,na ulaaniwe na ww na kizazi chenu chote asibakie hata panya,unajidai mlokole kumbe umekali ushirikina tu,

usimuamshe aliyelala maana akiamka utalala wewe ! Umepanic mkuu , hapa jf ukizidiwa kwa hoja unaruhusiwa kuomba msaada .
 
josephine,

ni kweli wewe hujawahi kugombea uongozi. Sababu ya kutokugombea ilikuwa ni kukosa kwako kujiamini na ulikuwa unaamini mpaka upate mtu wa kukukingia kifua ndio ugombee. Sasa hivi umeshapata mtu wa kukukingia kifua na tutakuona unagombea uongozi very soon. Post hii naitunza kama ushahidi.

Ni kweli kuwa kamati kuu ya chadema ilikudhibiti ulipanza kufuja pesa za chama kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulipwa sh. Milioni 10 kwa kazi unayoiita ya kujitolea. Bila kamati kuu kuwa macho ungesababisha hasara kubwa zaidi.

Siku hizi umekuja na gear nyingine ya igehete na imeshafaamika jinsi unavyotumia jina la chadema katika kujipatia pesa kwenye ngo yako ya magumashi ya igehete.

Dr. Slaa zamani alikuwa mtu focused, ila sasa hivi umeshamdiverge towards uroho wa pesa na madaraka.

mjomba umeambiwa lete ushahidi , sasa porojo za nini tena ? Kuwa gt bhana ! Huu ndiyo wakati wako wa kumuumbua josephine , kinyume chake utadhalilika sana !
 
Jina la EL sasa ni koras humu jf, endeleeni kumpaisha hadi jumba jeupe tutamuingiza!, na kwa vile anakuwa amepaishwa juu sana, mule ndani ataingilia kutoka juu kwa kufanya kutua!.
Pasco

haya baba/kaka endelea hivyo ukuu wa wilaya unakusubiri.
 
mimi mwenyewe huyu jamaa namshanga sana dini na matambiko wapi na wapi kwamaana kanisani yeye misikitini yeye na kutambikwa yeye na ufisadi yeye lengo ni nini anaye fahamu lengo la huyu jamaa aniambie.

  • :heh:
 
Anatafuta kupigwa risasi coz Tsh 152,000, 000/= per day bado tunazikumbuka.
Kumbe Richmond ambayo ilikuwa kampuni feki, ilifua umeme feki na kutuibia TZS, 152,000,000/= kwa siku as capacity charge!. Tukaikataa na kukataa kuinunue ile mitambo!.

Ila kampuni ya Simbion ambayo ndio kampuni ya ukweli, inafua umeme wa ukweli, na inacharge TZS 152,000,000 za ukweli, as a capacity charge!.
Pasco
 
mimi mwenyewe huyu jamaa namshanga sana dini na matambiko wapi na wapi kwamaana kanisani yeye misikitini yeye na kutambikwa yeye na ufisadi yeye lengo ni nini anaye fahamu lengo la huyu jamaa aniambie.

  • :heh:

Rais wa Tanzania ni RAIS WA WAUMINI WA DINI ZOTE, IKIWA NI PAMOJA NA WALE WASIOABUDU POPOTE!
 
Wana-JF,

Nimekuwa najaribu kufikiria jinsi Mbunge wa Monduli na Waziri aliyejihuzuru kwa kashfa ya Mradi tata wa Richmond, Bw. E. Lowassa anavyotemebelea mikoa na wilaya mbalimbali hapa Tanzania. Amekuwa akijihusisha na harambee na kuchangia miradi mbalimbali ya maendeleo hasa inayoendeshwa na makundi ya kidini.
Katika siku za hivi karibuni, EL amejikita hata katika kukutana na wazee wa jadi. Kwa hali ilivyo safari hizi zinatumia hela nyingi sana.

Lakini unaweza kunisaidia kutafakari kidogo!
1. Hizi kazi anazofanya anafanya kama nani, mfano ni mkutano wake wa Shinyanga ambao amesikika akitoa siri za Baraza la Mawairi katika Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria pia na mkutano na Chama cha Waendesha Boda Boda, Tabora. EL akiwa ameweka Jiwe La Msingi katika Kaburi la Mnyugumba; EL katika Tambiko
2. Nani anagharimia safari zake??? Ni chama tawala au serikali kuenzi utumishi wake wa Uwaziri Mkuu!
3. Nini hasa lengo lake kwa nchi yetu, kama hela anazotumia hazina chanzo kilichowazi?
4. Ni nani anayeanda mikutano hii ya kumkutanisha na wananchi? CCM! Serikali!

Naomba ufikiri kwa kina kabla hujajibu.



Tunaishi kwenye wakati tofauti. Ukitaka urais lazima useme na uwe na mkakati mradi usivunje sheria. Enzi zile za kupata urais Mwinyi bila kusema anataka zimepitwa na wakati. Sio kosa kutaka urais ili mradi una nia njema na uadilifu kuwaletea wananchi maendeleo. Laigwenan EL anautaka urais na historia yake inaonyesha ni mtu wa matendo kuliko maneno. Tusubiri muda ukifika wananchi wataamua.
 
Tunaishi kwenye wakati tofauti. Ukitaka urais lazima useme na uwe na mkakati mradi usivunje sheria. Enzi zile za kupata urais Mwinyi bila kusema anataka zimepitwa na wakati. Sio kosa kutaka urais ili mradi una nia njema na uadilifu kuwaletea wananchi maendeleo. Laigwenan EL anautaka urais na historia yake inaonyesha ni mtu wa matendo kuliko maneno. Tusubiri muda ukifika wananchi wataamua.
Kutaka Urais hata mimi naweza. Kikubwa ni kuangalia mipango yangu inaendeshwaje. Chukulia, EL anafuata utaratibu wa nani kufanya hayo. Kama chama chake hakitampitisha, unafikiri nini kitatokea?

Pia, akipata unafikiri ataendesha serikali ya mrengo gani?
 
Kutaka Urais hata mimi naweza. Kikubwa ni kuangalia mipango yangu inaendeshwaje. Chukulia, EL anafuata utaratibu wa nani kufanya hayo. Kama chama chake hakitampitisha, unafikiri nini kitatokea?

Pia, akipata unafikiri ataendesha serikali ya mrengo gani?
Laigwenan EL anakaribishwa na wanajamii mbalimbali wanaotambua uwezo wake wa kuvuta wafadhili kuchangia miradi ya kijamii, iwe ya jumuia mbalimbali au ya kidini. Kwa hilo naona anastahili pongezi na sio shutuma. Kama chama chake hakitampitisha bila shaka itakua mwisho wa safari yake kutaka urais kupitia ccm japo anaweza kufunguliwa mlango na katiba kama mgombea binafsia. Kwamba ataendesha serikali ya mrengo gani; sina hakika sana ila jambo moja la uhakika ana uwezo wa kufanya maamuzi magumu. Kama maamuzi yake ni sahihi na manufaa ni jambo la mjadala.
 
Back
Top Bottom