Safari yangu ya dhahabu Botswana

Safari yangu ya dhahabu Botswana

Kama ilivyo kwa wengine wapenda kusafiri kama mimi, daima tunapenda ku- share some stories na watu wengine ili nao angalau wapate kidogo mwanga wa maisha ya sehemu nyingine za mbali kidogo na nyumbani Tanzania.

Miaka kadhaa iliyopita kulikuwa na wimbi kubwa sana la vijana wa kitanzania kutamani kuondoka nchini na kukimbilia nchini Afrika ya kusini almaarufu bondeni kwa wakati huo. Nakumbuka sikuwa muhanga wa matamanio hayo yaliyokuwa sehemu kubwa ya vijana vijiweni kote huko, kuanzia temeke hadi kinondoni.

Nakumbuka rafiki zangu wengi tuliokuwa tukikaa pamoja pale maeneo ya Abbas club kama sikosei wakati huo miaka ya 2000 mwanzoni kabisa. Enzi za uwanja wa ugimbi na vita vya marefa na mashabiki...acha kabisa yaani, ukitoa matumizi ya bange kulikuwa na kubeli zilizotumiwa bila idadi maeneo hayo ya pembezoni mwa viwanja hivyo vyenye mchanga kibao. Kwa wakaazi wa kurasini, maeneo yote ya keko, zamkago kule na beach yetu pendwa ya Sava mtakuwa mnanipata vyema hapa.

Basi kipindi ndio safari za magendo zikiwa zimepamba moto huku waliokuwa washkaji kipindi hicho, maana kama kuna waliopo hai wakati huu wa sasa sio vijana tena. Mipango mingi ya kutafuta pesa za nauli za safari ilikuwa ikifanyikia nyuma ya kuta za bandari...aisee wizi wa mafuta ulipamba moto kweli kweli, kuna jamaa mmoja maarufu miaka hiyo aliita Jongo.

Kwa sasa ni marehemu kama walivyolala washkaji wengine wengi tu waliojihusisha na maswala ya wizi wa mafuta na vitu mbali mbali, kama unamfahamu Jongo na habari zake saluti kwako mkuu.

Huyu jamaa na genge lake walikuwa ni watu wakukaa nao mbali kabisa. Wakati mwingine unaweza kusema ni bora kushirikiana na wachuna ngozi wa mbeya huko kuliko hao jamaa.

Acha. Tusonge mbele sasa, baada ya vijana wengi kunogewa na habari za south na baadhi ya nchi nyingine za ulaya, ndipo safari za kuzamia meli zikaanza kwa Fuji sana na bila mpangilio na plan nzuri.
Nakumbuka kuna jamaa kadhaa waliobahatika kuzamia meli na hatukupata tena habari zao tena, hatujui kama walifanikiwa kufika walipo kusudia au la.

Kuna waliopitia njia za barabara kuelekea south Afrika ambapo ndio nchi pekee pendwa zaidi wakati ule.

Baadhi walizamia omani na kutokomea huko huko hadi hii leo tukiwa tunakisubili kwa hamu kimbunga chetu Jobo sijui nani.
Sasa wakati huo nchi kama Msumbiji, Kenya, sijui Uganda na huu upuuzi mwingine wote wa Afrika mashariki na kati sijui kama vijana walikuwa wanazifahamu kama zipo duniani hapa. Issue kubwa ilikuwa bondeni, Ulaya au angalau Arabuni kidogo kujipanga na kisha kuingia nchi za ulaya, na hata South Afrika ilikuwa ni kama njia tu au kituo cha kuelekea Italian, Finland, na kwingineko huko mbele kwa mbele.

Kwa upande wangu nilikuwa mwoga sana na ikizingatiwa makuzi na mazingira ya nyumbani yalivyokuwa. Maana kulikuwa na matabaka ya vijana kati ya watoto wa kota, watoto wa changanyikeni huko keko machungwa, keko mwanga, Tandika na viunga vyote vya wilaya ya Temeke (TMK) wilaya yetu ngumu na ya wagumu haswaaa.
Mwanzoni sikuwa na mawazo ya kusafiri nje kabisaaa, kwangu ilikuwa ngumu sana kushiriki katika mipango na plan za kutoroka nyumbani huku ukiwa umewaachia hasara kubwa ya wizi wa fedha, deki VHS kwa wale mnaozijua, TV Hitachi ya chogo, na vikorokolo kibao ilimradi tu upate kianzio cha safari.

Mwishoni mwa miaka ya 1999 kuelekea 2000 hivi kipindi kama sikosei ndio watu wengi wanaanza kumiliki simu za mkononi na zile vocha zetu pendwa zilizoitwa Dollar. Zilikuwa mtindo wa karatasi hivi, unalichana katikati na tarakimu unazikuta ndani kisha mkononi una Nokia yako kubwa 30410 jeneza full vibration, au Philips kidole juu.

Basi baada ya stori nyingi za marafiki waliofanikiwa kuescape manyumbani kwao kutufikia kuwa wanakula bata mbele huko, ndipo na mimi nilipo amua kujilipua na kuondoka na jamaa zangu wawili.


(Tukutane leo jioni hapa hapa)
Utunzi mzuri mwanangu
 
Muda huu saa tisa kamili usiku 3:00 huwa kuna maelfu ya watanzania walio macho kwa kukosa usingizi kutokana na mambo mbalimbali. Nimeanza KUANDIKA



Napenda niwashukuru kwanza wale mliochangia comment zenu hapa. Wale mliowafahamu wazi wazi baadhi ya watu niliowataja hapa, kama vile marehemu mkongwe Jongo. Wale ambao najua kama nikiendelea kuweka wazi mambo watanifahamu kabisa, na jamaa wote mnaoshiriki pamoja nami hapa ahsanteni sana.

Sipendi niache baadhi ya issue zenye kunifanya niwe na huzuni wakati nikikumbuka yaliyopita huko. Jina X kama upo hapa unaweza kunifahamu, bado nakumbuka msisimko nilioupata baada ya miaka tisa ya panda shuka za ajabu na taarifa yako ya kifo cha binti mrembo sana moyoni mwangu. Sasa ni zaidi ya miaka 22 na bado ahadi yangu ya kuliona kabuli na kwenda kulia kwa sauti kubwa na machozi mengi sijaitimiza, lakini kwa hapa nilipo sasa naahidi sitalala kimya milele kabla ya kutimiza ahadi ya moyo wangu.
( NAKUWA NA WAKATI MGUMU SANA KUANDIKA, MUDA MWINGI MACHOZI NASHINDWA KUYAZUIA)

Basi baada ya siku ya nne ya kuusikilizia upepo, hao tukaondoka na gari ya mzigo, tuliyokuwa tunaisubili na ilitufanya tuongeze siku moja mbele mbadala wa siku tatu tulizopanga. Sisi hatukuacha alama kabisa ya wapi tulipotokomea, hii ilikuwa tofauti kabisa na vijana wengine ambao japo waliacha taarifa kwa rafiki zao na vijiweni huko. Kilichotufanya tuwe hivi nadhani ni hadaa za vipindi vya televisheni hasa zile movie za Lino lensi yule jamaa aliyekuwa pikpik kuubwa na minywele kibao, Isidingo pia ilichangia pakubwa kutupa moja na mbili katika maswala ya ujanja ujanja tofauti na vijana wengine ambao nadhani kwa wakati huo wazee kumiliki Panasoniki au Hitachi haikuwa jambo la mchezo.
Mdogo mdogo tumebanana kwenye kichwa cha gari, nakumbuka ustaarabu wa ndugu utingo wa lile gari. Kipindi hicho kiukweli nilikuwa sijui kabisa na sijawahi kufika hata hapo kimara. Kwa watu walioishi ukanda wa bandali kule watanielewa. Hivi mtoto wa kurasini kimala unafuata nini hasa kipya wakati huo???
Labda kwa wale waliokuwa wanapita huko kwenda mikoani kwao na wazee wao nyakati za likizo.
Sasa hofu, furaha ya safari, mashaka na wasi wasi vyote vilikuwa vinapita pita tu hovyo ovyo kichwani. Safari ya usiku na magari ya mizigo sio mchezo, tena unapoenda haupajui. Tuliimaliza dsm bila kujua, safari sasa pwani hiyo gari mdogo mdogo, kwa maelezo ya utingo tukaingia mkoani morogolo na kidogo kuanzia hapo tukaanza kuenjoy mazingira mazuri ya njiani huko.. .. Huku baadhi ya vipande vya barabara vikipitika kwa shida shida yaani.

Wenzangu hawakupata bahati sana ya kushangaa nje maana walikaa ndani kidogo mafichoni nyuma ya kibin huko, safari ikaendelea taratibu sana kutokana na ubovu wa gari na vipande korofi vya barabara. Kufika mbele mbele huko mara gari inaanza kuchemsha, lile gali lilikuwa kimeo sana muda wote spana mkononi.
Kwa kipindi kile yale maeneo gari lilipo pata hitilafu sikuwa nayajua kabisa. Ila kwa sasa ni pale kwenye mitelemko ya iyovi kama nipo sahihi..huku kibariidi tukikisikia kwa mbali, utingo anatuambia tutafurahia shoo tukifika juu huko Iringa na Mbeya. Sasa hatukubeba nguo yoyote zaidi ya tulizo vaa ni kwa sababu kama mbili tatu hivi. Moja ni kutogundulika kila hisi nyumbani wakati tunatoka, pili tuliamini huko tunakoelekea kuna mavazi bora zaidi na tatu hatukuwa tayali kuona tunaibiwa chochote au kupoteza kitu, na kwa urahisi wa safari tulipendelea kuwa free bila mzigo wowote hadi tufikapo.
Hatukuwa na passport wala nyaraka yoyote ile. Hata dereva na utingo hawakuwa wakijua kama tunampango wa kwenda nje.
Asubuhi kabisa majira ya saa nne hivi safari ikaendelea baada ya chombo kupoa poa pale, tukapita ruaha mbuyuni kwa mara ya kwanza, aisee maeneo ni mazuri sana yanavutia sana, hapo baridi linaongezeka taratibu taratibu, safari hadi mlima kitonga chini kabisa gari ikabuma kimoja...


Aisee uzuri wa kuadithiwa nenda ukajionee. Japo barabara haikuwa bora sana kama hii leo lakini mazingira yalikuwa na mvuto zaidi ya hii leo.. Sisi kazi ilikuwa kufikicha mikono kwa kibaridi na kushangaa shangaa milima na vingedere watu maeneo yale... Muda kidogo ulivyoenda ndipo kwa msaada wa dereva tuliombewa lifti kwenye gari ya mastista lililokuwa linaishia sehemu moja hivi inaitwa mafinga.
Basi ndani ya gari ilikuwa tumsifu yesu kristu kibaooo.. Navile udogoni tuluwahi kutumikia kanisani ndo ikawa kama gari yetu na sisi ni wanafamilia pamoja nao. Kuna sehemu gari ilisimama tukapata chai pale kwa hisani ya ndugu zetu wa kiroho na safari ndefu ikaendelea. Tatizo ilikuwa wale masister walikuwa na maswali mengi mno, hadi unatamani gari ifike ushuke na wala haifiki. Rafiki yangu alipewa sweta baada ya kuzibuliwa miswali kibao na kuwa anaijibu papo kwa hapo.
Tulifika hapo mwisho wa lifti mafinga na baridi ilitulegeza kweli kweli, wale jamaa wanaishi ndani ya friji aisee, tulivutiwa sana na ka- harufu fulani hivi sijui kanatokana na nini hasa, maana DSM hatukuwai kabisa kukaskia, yaana harufu flani nzuri ya hali ya hewa.
Hatukua na mapepe na haraka sana hapo, pia hatukuitaji kupoteza pesa nyingi hapo. Basi kuna sehemu majamaa yamewasha moto karibu kabisa na stend tukajumuika nao kuota moto. Yaani walipotuona tu wakajua hawa jamaa wageni huku, maana mgeni hajifichi ugenini. Watu wa kule sio wabaya kabisa wana roho nzuri na wakalimu sana,
Baada ya muda kidogo tuliulizia ulizia namna ya kupata usafiri hapo wa kutufikisha jijini mbeya. Na kutokana na mionekano yetu ya kitown town kila mtu alikuwa anataka kuwa mwenyeji wetu..
Haikuwa rahisi kupata gari ya mizigo pale japokuwa zilikuwa nyingi zinapita hapo.

Basi kutokana na maelezo ya mwenyeji wetu ilibidi tulale hapo siku hiyo na tungeondoka kesho yake asubuhi na magari ya kiwanda cha karatasi yatakayopita mapema hapo kuelekea mikoa ya juu huko.
Kwa msaada wa mwenyeji wetu tukapata guest moja ya bei nafuu hapo na tukarundikana humo humo kwa hisani ya mwenyeji wetu.
Aisee lile baridi sio mchezo tulipitiwa na usingizi hadi saa tatu hivi au nne kabisa
Nje ukungu, maji hayashikiki, ukiyanawa usoni mikono inakufa ganzi, mafua si mafua yaana tabu tupu ni mwendo wa kutetemeka tu.
Tukaona hapa hapatufai kabisa na sio sehemu salama kwetu. Shida sasa tumeshachelewa kuvizia yale magari tuliyo elekezwa.

(Saa 5:34 nimefikia hapa, tunaendelea baadae kidogo baada ya kutoka kanisani)
 
Aisee ubaharia ni kutoka na nguo uliyovaa pekee afu nani jamaa sasa mkuu?
Hiyo nafikiri ilikuwa staili yao ya nitoke vipi( kumbuka kasema hata stori za vijiwe zilikuwa na ushawishi katika maamuzi yao).

Mkuu kisa neno "jamaa" unataka kunipasua, sijamaanisha asee ulikuwa utani. Hope mzima first born.
 
Muda huu saa tisa kamili usiku 3:00 huwa kuna maelfu ya watanzania walio macho kwa kukosa usingizi kutokana na mambo mbalimbali. Nimeanza KUANDIKA



Napenda niwashukuru kwanza wale mliochangia comment zenu hapa. Wale mliowafahamu wazi wazi baadhi ya watu niliowataja hapa, kama vile marehemu mkongwe Jongo. Wale ambao najua kama nikiendelea kuweka wazi mambo watanifahamu kabisa, na jamaa wote mnaoshiriki pamoja nami hapa ahsanteni sana.

Sipendi niache baadhi ya issue zenye kunifanya niwe na huzuni wakati nikikumbuka yaliyopita huko. Jina X kama upo hapa unaweza kunifahamu, bado nakumbuka msisimko nilioupata baada ya miaka tisa ya panda shuka za ajabu na taarifa yako ya kifo cha binti mrembo sana moyoni mwangu. Sasa ni zaidi ya miaka 22 na bado ahadi yangu ya kuliona kabuli na kwenda kulia kwa sauti kubwa na machozi mengi sijaitimiza, lakini kwa hapa nilipo sasa naahidi sitalala kimya milele kabla ya kutimiza ahadi ya moyo wangu.
( NAKUWA NA WAKATI MGUMU SANA KUANDIKA, MUDA MWINGI MACHOZI NASHINDWA KUYAZUIA)

Basi baada ya siku ya nne ya kuusikilizia upepo, hao tukaondoka na gari ya mzigo, tuliyokuwa tunaisubili na ilitufanya tuongeze siku moja mbele mbadala wa siku tatu tulizopanga. Sisi hatukuacha alama kabisa ya wapi tulipotokomea, hii ilikuwa tofauti kabisa na vijana wengine ambao japo waliacha taarifa kwa rafiki zao na vijiweni huko. Kilichotufanya tuwe hivi nadhani ni hadaa za vipindi vya televisheni hasa zile movie za Lino lensi yule jamaa aliyekuwa pikpik kuubwa na minywele kibao, Isidingo pia ilichangia pakubwa kutupa moja na mbili katika maswala ya ujanja ujanja tofauti na vijana wengine ambao nadhani kwa wakati huo wazee kumiliki Panasoniki au Hitachi haikuwa jambo la mchezo.
Mdogo mdogo tumebanana kwenye kichwa cha gari, nakumbuka ustaarabu wa ndugu utingo wa lile gari. Kipindi hicho kiukweli nilikuwa sijui kabisa na sijawahi kufika hata hapo kimara. Kwa watu walioishi ukanda wa bandali kule watanielewa. Hivi mtoto wa kurasini kimala unafuata nini hasa kipya wakati huo???
Labda kwa wale waliokuwa wanapita huko kwenda mikoani kwao na wazee wao nyakati za likizo.
Sasa hofu, furaha ya safari, mashaka na wasi wasi vyote vilikuwa vinapita pita tu hovyo ovyo kichwani. Safari ya usiku na magari ya mizigo sio mchezo, tena unapoenda haupajui. Tuliimaliza dsm bila kujua, safari sasa pwani hiyo gari mdogo mdogo, kwa maelezo ya utingo tukaingia mkoani morogolo na kidogo kuanzia hapo tukaanza kuenjoy mazingira mazuri ya njiani huko.. .. Huku baadhi ya vipande vya barabara vikipitika kwa shida shida yaani.

Wenzangu hawakupata bahati sana ya kushangaa nje maana walikaa ndani kidogo mafichoni nyuma ya kibin huko, safari ikaendelea taratibu sana kutokana na ubovu wa gari na vipande korofi vya barabara. Kufika mbele mbele huko mara gari inaanza kuchemsha, lile gali lilikuwa kimeo sana muda wote spana mkononi.
Kwa kipindi kile yale maeneo gari lilipo pata hitilafu sikuwa nayajua kabisa. Ila kwa sasa ni pale kwenye mitelemko ya iyovi kama nipo sahihi..huku kibariidi tukikisikia kwa mbali, utingo anatuambia tutafurahia shoo tukifika juu huko Iringa na Mbeya. Sasa hatukubeba nguo yoyote zaidi ya tulizo vaa ni kwa sababu kama mbili tatu hivi. Moja ni kutogundulika kila hisi nyumbani wakati tunatoka, pili tuliamini huko tunakoelekea kuna mavazi bora zaidi na tatu hatukuwa tayali kuona tunaibiwa chochote au kupoteza kitu, na kwa urahisi wa safari tulipendelea kuwa free bila mzigo wowote hadi tufikapo.
Hatukuwa na passport wala nyaraka yoyote ile. Hata dereva na utingo hawakuwa wakijua kama tunampango wa kwenda nje.
Asubuhi kabisa majira ya saa nne hivi safari ikaendelea baada ya chombo kupoa poa pale, tukapita ruaha mbuyuni kwa mara ya kwanza, aisee maeneo ni mazuri sana yanavutia sana, hapo baridi linaongezeka taratibu taratibu, safari hadi mlima kitonga chini kabisa gari ikabuma kimoja...


Aisee uzuri wa kuadithiwa nenda ukajionee. Japo barabara haikuwa bora sana kama hii leo lakini mazingira yalikuwa na mvuto zaidi ya hii leo.. Sisi kazi ilikuwa kufikicha mikono kwa kibaridi na kushangaa shangaa milima na vingedere watu maeneo yale... Muda kidogo ulivyoenda ndipo kwa msaada wa dereva tuliombewa lifti kwenye gari ya mastista lililokuwa linaishia sehemu moja hivi inaitwa mafinga.
Basi ndani ya gari ilikuwa tumsifu yesu kristu kibaooo.. Navile udogoni tuluwahi kutumikia kanisani ndo ikawa kama gari yetu na sisi ni wanafamilia pamoja nao. Kuna sehemu gari ilisimama tukapata chai pale kwa hisani ya ndugu zetu wa kiroho na safari ndefu ikaendelea. Tatizo ilikuwa wale masister walikuwa na maswali mengi mno, hadi unatamani gari ifike ushuke na wala haifiki. Rafiki yangu alipewa sweta baada ya kuzibuliwa miswali kibao na kuwa anaijibu papo kwa hapo.
Tulifika hapo mwisho wa lifti mafinga na baridi ilitulegeza kweli kweli, wale jamaa wanaishi ndani ya friji aisee, tulivutiwa sana na ka- harufu fulani hivi sijui kanatokana na nini hasa, maana DSM hatukuwai kabisa kukaskia, yaana harufu flani nzuri ya hali ya hewa.
Hatukua na mapepe na haraka sana hapo, pia hatukuitaji kupoteza pesa nyingi hapo. Basi kuna sehemu majamaa yamewasha moto karibu kabisa na stend tukajumuika nao kuota moto. Yaani walipotuona tu wakajua hawa jamaa wageni huku, maana mgeni hajifichi ugenini. Watu wa kule sio wabaya kabisa wana roho nzuri na wakalimu sana,
Baada ya muda kidogo tuliulizia ulizia namna ya kupata usafiri hapo wa kutufikisha jijini mbeya. Na kutokana na mionekano yetu ya kitown town kila mtu alikuwa anataka kuwa mwenyeji wetu..
Haikuwa rahisi kupata gari ya mizigo pale japokuwa zilikuwa nyingi zinapita hapo.

Basi kutokana na maelezo ya mwenyeji wetu ilibidi tulale hapo siku hiyo na tungeondoka kesho yake asubuhi na magari ya kiwanda cha karatasi yatakayopita mapema hapo kuelekea mikoa ya juu huko.
Kwa msaada wa mwenyeji wetu tukapata guest moja ya bei nafuu hapo na tukarundikana humo humo kwa hisani ya mwenyeji wetu.
Aisee lile baridi sio mchezo tulipitiwa na usingizi hadi saa tatu hivi au nne kabisa
Nje ukungu, maji hayashikiki, ukiyanawa usoni mikono inakufa ganzi, mafua si mafua yaana tabu tupu ni mwendo wa kutetemeka tu.
Tukaona hapa hapatufai kabisa na sio sehemu salama kwetu. Shida sasa tumeshachelewa kuvizia yale magari tuliyo elekezwa.

(Saa 5:34 nimefikia hapa, tunaendelea baadae kidogo baada ya kutoka kanisani)
Mafinga miaka ya nyuma ilikuwa ni changamoto kwa baridi
 
Kabla ya kusoma uzi nikashuka moaka chini nione yaliyomo ndani na speed yako ya uandishi..

Kisha ulipotaja kurasini nikaikumbuka kurasini primary school niliposoma, nikakumbuka shimo la udongo, wiston(r.i.p), braza wangu juma mpogo (r.i.p).

Nina kumbukumbu nyingi kule kurasini, miaka ya hapa kati nilienda nikafika mpaka ugimbi kifupi kurasini ishajifia.
 
Back
Top Bottom