Safari ya Spika Sitta Urambo baada ya NEC August 2009

Zyansiku

Member
Jul 27, 2009
49
10
Katika kile kinachoonekana kutofautiana na maamuzi ya NEC, baadhi ya wapambe wa Mh SS wanaoshi katika jimbo la Urambo wanafanya maandalizi makubwa ya kumpokea Mh SS kwa maandamano makubwa ikiwa ni pamoja na kukodi piki piki zote za kibiashara katika mji wa urambo, aidha mapokezi hayo ya aina yake yatafanyika katika kijiji cha Ndorobo nje kidogo ya mji wa Urambo na kwa kiasi kikubwa maandalizi yote yamekamilika chini ya uongozi wa Bwana Welly aliyekuwa katibu uchumi na fedha wilaya ya urambo na Katibu mhamasishaji wa vijana mkoa wa Tabora kwa mwaka 2003-2004.

Wakati huo huo taarifa nilizopata muda si mrefu kutoka kwa wadau wa siasa wa mji wa Tabora

Ni kwamba maandalizi kama hayo pioa yanafanyika Tabora mjini chini ya katibu wa siasa na uenezi wa CCM wa Tabora mjini bwana Rashid Ramadhani Tall. kila la kheri Spika tunakusubiri kwa hamu Tabora na mapokezi ya nguvu!
 
Last edited by a moderator:
tehe tehe tehe mitanzania bana.......sijui niipe jina gani.....
 
Jamani,

Mzee huyu wa Urambo anapokelewa kwa shangwe, kwa kitu gani hasa? Huyu si ametuhumiwa waziwazi ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya chama chake cha CCM kuwa, kwa vitendo vyake, anakisaliti chama hicho na akanusurika kung'olewa baada ya kuomba radhi? Sasa ndiyo anazidi kujichimbia kaburi la kisiasa. Si aliwahi kushindwa huyu Urambo mwaka 1995? Sasa, tangu 2005, amekuwa akijaribu kujijenga upya kisiasa, kuchukua ajenda ya "Ufisadi" imsaidie (kwa kushirikiana na timu yake ya Wabunge, wenye gele na usongo na UWAZIRI, inayoitwa "First Eleven": akina Dk. Mwakyembe, Ole Sendeka, Lucas Selelii, Anne Kilango,Stella Manyanya, Betrice Shelukindo n.k. anaowapangilia Bungeni). Lakini kumbe, kwa vile zote hizo ni hila, sasa ameshitukiwa na Chama chake. Hii kwamba anapokewa kwa shangwe ni propaganda tu za kujaribu kumvika nguo!

LAKINI, kama nilivyowahi kueleza hapo awali, mahali pengine humu katika JF, tatizo la mzee huyu la fitina na usaliti wa kisiasa, halikuanza leo! Katika miaka ya mwanzoni ya 1990, akiwa Waziri wa Sheria (na baadaye akaondolewa, baada ya kushindwa Ubunge wa Urambo), alishiriki "kiujanjaujanja" katika hoja ya kutaka kuleta Serikali ya Tanganyika katika mfumo wa Muungano, ili uwe wa Serikali Tatu badala ya Mbili.
Katika kitabu chake, UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA. Uk. wa 20 hadi Uk. 27, Mwalimu Nyerere alimsema vibaya sana Sitta, kwa kupeleka mbele ya Halmashauri Kuu ya CCM, Dodoma, "TAARIFA YA SERIKALI JUU YA AZIMIO LA BUNGE KUHUSU HAJA YA KUUNDA SERIKALI YA TANGANYIKA NDANI YA MUUNDO WA MUUNGANO". Mwalimu Nyerere alisema, kuhusu taarifa hiyo, katika kijitabu hicho: "Taarifa yenyewe ni ndefu, maana ina maelezo mengi ya mapambo tu, au ya kiinimacho(Uk. 20)...Baadaye, baada ya kikao, nilimtafuta Ndugu Sitta, nikampa pole kwa kupewa jukumu la kueleza jambo ambalo halielezeki (Uk. 27)...". Huyo ndiyo Spika Sitta, mbele ya macho na fikra za Mwalimu Nyerere! Hivi ni mpiganaji kweli wa vita dhidi ya "Ufisadi", au ni msaliti tu wa Chama chake? Wana-CCM na msio wana-CCM na ni Watanzania tu wenye nia njema, pimeni!

Bwassa
 
6 hana lolote ni zezeta wa kisiasa tuuu,wacha aandamane aone kilichomtoa kanga manyoya!Injii hii bwana,achana nayo.
 
karibuni wabaya wa Sitta, hapa linapendwa Taifa siyo chama na kuchukiwa mafisadi. wote.
 
Jamaa yangu mmoja ananikumbusha kuwa aliyekubali kufa kwa ajili ya watu alikuwa yesu peke sijui kama sita ataweza kuvaa viatu vya yesu, any way lets wait and see!
 
Katika kile kinachoonekana kutofautiana na maamuzi ya NEC, baadhi ya wapambe wa Mh SS wanaoshi katika jimbo la Urambo wanafanya maandalizi makubwa ya kumpokea Mh SS kwa maandamano makubwa ikiwa ni pamoja na kukodi piki piki zote za kibiashara katika mji wa urambo, aidha mapokezi hayo ya aina yake yatafanyika katika kijiji cha Ndorobo nje kidogo ya mji wa Urambo na kwa kiasi kikubwa maandalizi yote yamekamilika chini ya uongozi wa Bwana Welly aliyekuwa katibu uchumi na fedha wilaya ya urambo na Katibu mhamasishaji wa vijana mkoa wa Tabora kwa mwaka 2003-2004. wakati huo huo taarifa nilizopata muda si mrefu kutoka kwa wadau wa siasa wa mji wa Tabora
ni kwamba maandalizi kama hayo pioa yanafanyika Tabora mjini chini ya katibu wa siasa na uenezi wa CCM wa Tabora mjini bwana Rashid Ramadhani Tall. kila la kheri Spika tunakusubiri kwa hamu Tabora na mapokezi ya nguvu!

Nazidi kushangaaa.......hapa cha kufurahia ni nini sasa? Huyo six, maandamano au ufujaji wa pesa kwa kukodi mapikipiki ambapo zingeweza kutumika kwa masuala mengine ya maendeleo ya wananchi? Embu tuamke wa TZ siyo kushabikia kila jambo.........
 
Jamani acheni wivu, c wananchi wake wa Urambo wanamwamini bado? Mbona bwana Chenge nae alipokelewa kwa mbwembwe kipindi kileeee.......
 
Sitaa badoo anatapatapaa..amue mojaa..uspikaa sio mama yake, ccm sio mama yakee..
 
Katika kile kinachoonekana kutofautiana na maamuzi ya NEC, baadhi ya wapambe wa Mh SS wanaoshi katika jimbo la Urambo wanafanya maandalizi makubwa ya kumpokea Mh SS kwa maandamano makubwa ikiwa ni pamoja na kukodi piki piki zote za kibiashara katika mji wa urambo, aidha mapokezi hayo ya aina yake yatafanyika katika kijiji cha Ndorobo nje kidogo ya mji wa Urambo na kwa kiasi kikubwa maandalizi yote yamekamilika chini ya uongozi wa Bwana Welly aliyekuwa katibu uchumi na fedha wilaya ya urambo na Katibu mhamasishaji wa vijana mkoa wa Tabora kwa mwaka 2003-2004. wakati huo huo taarifa nilizopata muda si mrefu kutoka kwa wadau wa siasa wa mji wa Tabora

Huyu Bwana Welly naona anataka kujipalia mkaa. Kuna wakati yeye na Brother wake waliwahi kutishwa kuwa sio raia baada ya kutoonyesha mapenzi mema kwa sisiemu. Kwa vile ameamua kusigana na NECK ambayo inabeba HEAD(Fisadis) ya sisiemu basi awe tayari kwa Mapambano from RA et al.
 
Jamani,

Mzee huyu wa Urambo anapokelewa kwa shangwe, kwa kitu gani hasa? Huyu si ametuhumiwa waziwazi ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya chama chake cha CCM kuwa, kwa vitendo vyake, anakisaliti chama hicho na akanusurika kung'olewa baada ya kuomba radhi? Sasa ndiyo anazidi kujichimbia kaburi la kisiasa. Si aliwahi kushindwa huyu Urambo mwaka 1995? Sasa, tangu 2005, amekuwa akijaribu kujijenga upya kisiasa, kuchukua ajenda ya "Ufisadi" imsaidie (kwa kushirikiana na timu yake ya Wabunge, wenye gele na usongo na UWAZIRI, inayoitwa "First Eleven": akina Dk. Mwakyembe, Ole Sendeka, Lucas Selelii, Anne Kilango,Stella Manyanya, Betrice Shelukindo n.k. anaowapangilia Bungeni). Lakini kumbe, kwa vile zote hizo ni hila, sasa ameshitukiwa na Chama chake. Hii kwamba anapokewa kwa shangwe ni propaganda tu za kujaribu kumvika nguo!

LAKINI, kama nilivyowahi kueleza hapo awali, mahali pengine humu katika JF, tatizo la mzee huyu la fitina na usaliti wa kisiasa, halikuanza leo! Katika miaka ya mwanzoni ya 1990, akiwa Waziri wa Sheria (na baadaye akaondolewa, baada ya kushindwa Ubunge wa Urambo), alishiriki "kiujanjaujanja" katika hoja ya kutaka kuleta Serikali ya Tanganyika katika mfumo wa Muungano, ili uwe wa Serikali Tatu badala ya Mbili.
Katika kitabu chake, UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA. Uk. wa 20 hadi Uk. 27, Mwalimu Nyerere alimsema vibaya sana Sitta, kwa kupeleka mbele ya Halmashauri Kuu ya CCM, Dodoma, "TAARIFA YA SERIKALI JUU YA AZIMIO LA BUNGE KUHUSU HAJA YA KUUNDA SERIKALI YA TANGANYIKA NDANI YA MUUNDO WA MUUNGANO". Mwalimu Nyerere alisema, kuhusu taarifa hiyo, katika kijitabu hicho: "Taarifa yenyewe ni ndefu, maana ina maelezo mengi ya mapambo tu, au ya kiinimacho(Uk. 20)...Baadaye, baada ya kikao, nilimtafuta Ndugu Sitta, nikampa pole kwa kupewa jukumu la kueleza jambo ambalo halielezeki (Uk. 27)...". Huyo ndiyo Spika Sitta, mbele ya macho na fikra za Mwalimu Nyerere! Hivi ni mpiganaji kweli wa vita dhidi ya "Ufisadi", au ni msaliti tu wa Chama chake? Wana-CCM na msio wana-CCM na ni Watanzania tu wenye nia njema, pimeni!

Bwassa


Mkuu nakitafuta hicho kitabu kwa udi na uvumba!!! Unaweza kunipatia mkuu???
 
Katika kile kinachoonekana kutofautiana na maamuzi ya NEC, baadhi ya wapambe wa Mh SS wanaoshi katika jimbo la Urambo wanafanya maandalizi makubwa ya kumpokea Mh SS kwa maandamano makubwa ikiwa ni pamoja na kukodi piki piki zote za kibiashara katika mji wa urambo, aidha mapokezi hayo ya aina yake yatafanyika katika kijiji cha Ndorobo nje kidogo ya mji wa Urambo na kwa kiasi kikubwa maandalizi yote yamekamilika chini ya uongozi wa Bwana Welly aliyekuwa katibu uchumi na fedha wilaya ya urambo na Katibu mhamasishaji wa vijana mkoa wa Tabora kwa mwaka 2003-2004. wakati huo huo taarifa nilizopata muda si mrefu kutoka kwa wadau wa siasa wa mji wa Tabora
ni kwamba maandalizi kama hayo pioa yanafanyika Tabora mjini chini ya katibu wa siasa na uenezi wa CCM wa Tabora mjini bwana Rashid Ramadhani Tall. kila la kheri Spika tunakusubiri kwa hamu Tabora na mapokezi ya nguvu!

Oh My Gosh!!!

Mzee sitta, kama unasoma humu jamvini... achana kabisa na huo upuzi wa maandamano!!!! fanya kazi yako na usiendeleze huu ujinga wa kupokelewa kwa vifijo wakati kazi bado ngumu.

Tumeshaona ya CHENGE, LOWASA sasa naona na wewe unaingia chunguni

WAKATI UMEFIKA TU-ADDRESS DEVELOPMENT ISSUES NA KUACHA WAFU WAZIKE WAFU WAO
 
Jamani acheni wivu, c wananchi wake wa Urambo wanamwamini bado? Mbona bwana Chenge nae alipokelewa kwa mbwembwe kipindi kileeee.......

Sio wananchi wote wana mwamini. Nenda pale Kalemela na Ussoke sehemu ambazo zilikuwa moja ya ngome zake utapata habari kamili. Magazeti yamefanikiwa kwa kiasi fulani kumchafua. Hasa issue ya Kodi ya nyumba na kupenda vimwana(japo hili ni personal).
 
Katika kile kinachoonekana kutofautiana na maamuzi ya NEC, baadhi ya wapambe wa Mh SS wanaoshi katika jimbo la Urambo wanafanya maandalizi makubwa ya kumpokea Mh SS kwa maandamano makubwa ikiwa ni pamoja na kukodi piki piki zote za kibiashara katika mji wa urambo, aidha mapokezi hayo ya aina yake yatafanyika katika kijiji cha Ndorobo nje kidogo ya mji wa Urambo na kwa kiasi kikubwa maandalizi yote yamekamilika chini ya uongozi wa Bwana Welly aliyekuwa katibu uchumi na fedha wilaya ya urambo na Katibu mhamasishaji wa vijana mkoa wa Tabora kwa mwaka 2003-2004. wakati huo huo taarifa nilizopata muda si mrefu kutoka kwa wadau wa siasa wa mji wa Tabora
ni kwamba maandalizi kama hayo pioa yanafanyika Tabora mjini chini ya katibu wa siasa na uenezi wa CCM wa Tabora mjini bwana Rashid Ramadhani Tall. kila la kheri Spika tunakusubiri kwa hamu Tabora na mapokezi ya nguvu!


Saaaaafi sana! Na wale vibaraka wa mafisadi mliotumwa kmpiga vita Mh. Sitta karibuni uwanjani mmwage sumu zenu, hazisaidii. Wanananchi wameamua. Si afadhali kumpokea Sitta kwa vifijo kuliko yale ya Fisadi Chenge??? Nitacheka pale atajitokeza kibaraka wa mafisadi hapa na kusema hastahili mapokezi!!!! Kwani yale ya Chenge alistahili??? Sitta amefanya kazi, je Chenge alifanya nini?? Ningeweza ningeshiriki kabisan ili kumuunga mkono shujaa pekee katika historia ya maspika wa bunge letu ambao aliruhusu demokrasia ya mawazo Bungeni. Bunge ni chombo cha Wananchi!! Si mali ya NEC!!!
 
Bila shaka atapata muda wa kuyahutubia maandamano hayo. Atasema alichoambiwa kwenye vikao hivi "vizito" vya chama chake na huenda akaenda mbali zaidi ya hapo.....
 
Saaaaafi sana! Na wale vibaraka wa mafisadi mliotumwa kmpiga vita Mh. Sitta karibuni uwanjani mmwage sumu zenu, hazisaidii. Wanananchi wameamua. Si afadhali kumpokea Sitta kwa vifijo kuliko yale ya Fisadi Chenge??? Nitacheka pale atajitokeza kibaraka wa mafisadi hapa na kusema hastahili mapokezi!!!! Kwani yale ya Chenge alistahili??? Sitta amefanya kazi, je Chenge alifanya nini?? Ningeweza ningeshiriki kabisan ili kumuunga mkono shujaa pekee katika historia ya maspika wa bunge letu ambao aliruhusu demokrasia ya mawazo Bungeni. Bunge ni chombo cha Wananchi!! Si mali ya NEC!!!

Ni kweli ni vizuri CREDIT iende pale inapostahili. Lakini wasiwasi wangu ni juu ya organizer wa mapokezi bwana Welly, sidhani kama ana ujasiri wa kusimama akitishwa kidogo tu. Manake historia ya huko nyuma inamhukumu. Yalifaa yaandaliwe na mtu mwenye wasifu uliojengeka ndani ya jamii lakini sio huyu ambaye wasifu wake unamfanya kuwa mwepesi kwenye jamii.
 
morland_557777a.jpg
 
Mugo"The Great";557959 said:
Ni kweli ni vizuri CREDIT iende pale inapostahili. Lakini wasiwasi wangu ni juu ya organizer wa mapokezi bwana Welly, sidhani kama ana ujasiri wa kusimama akitishwa kidogo tu. Manake historia ya huko nyuma inamhukumu. Yalifaa yaandaliwe na mtu mwenye wasifu uliojengeka ndani ya jamii lakini sio huyu ambaye wasifu wake unamfanya kuwa mwepesi kwenye jamii.

Mugo sina habari za huyu Welly, ila kama si nzuri katika jamii, naomba mtu wa karibu na spika au kamati ya maandalizi wafanye mabadiliko haraka sana. Anatakiwa mtu credible kwa jamii ajitose kuyaandaa. Asante mkuu kwa hint na kama nilivyosema walioko humu wawasiliane haraka na waandaaji warekebishe. Pia dondosha kidogo ya Welly hapa ili isije ikawa atatuchafulia hali ya hewa hasa ukizingangatia kampeni za 2010 zimeshaanza.
 
Ama kweli mafisadi wako kila mahali. Hata kwenye JF kibao.Tanzania kazi tunayo. sasa nyinyi mnaomshambulia spika mnatofauti na waliokuwa ndani ya NEC? Kuna msemo wengi wape lakini kwa hili mmegonga mwamba. Hata zito alimshambulia karamagi ,akasimamishwa lakini baadaye mnajua kilichomkuta mwana Kara..kwenye Richmond .hakuna tofauti.
 
Back
Top Bottom