Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Bashungwa ameyasema hayo Machi 13, 2024 mkoani Tabora katika ziara ya Kamati hiyo ya kukagua maendeleo ya mradi huo na kusisitiza Wizara kupitia Wakala ya Barabara (TANROADS), itahakikisha inamsimamia Mkandarasi wa kampuni ya Beijing Construction Engineering Group (BCEG), kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha kazi hiyo kwa ubora.
Aidha, Bashungwa ameeleza kuwa moja ya sababu ya miradi kuchelewa ni kutokana na Taasisi za Serikali kutoshirikiana kwa karibu katika maandalizi na utekelezaji wa mradi na amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi kushiriana na Makatibu wakuu wengine katika uratibu wa utekelezaji wa miradi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso (Mb) amemuagiza Waziri Bashungwa kuhakikisha anamsimamia Mkandarasi anayejenga na kukarabati Kiwanja cha Ndege cha Tabora kufanya kazi kwa ufanisi na ndani ya muda uliopangwa.
Kadhalika, Kakoso amemtaka Bashungwa kufuatilia upatikanaji wa fedha za utekelezaji wa miradi kwa wakati ili kuwawezesha Wakandarasi wanaotekeleza miradi nchini kupokea malipo yao kwa wakati yatakayofanikisha ukamilishaji wa miradi kulingana na mikataba.