Chilisosi
JF-Expert Member
- Oct 19, 2008
- 3,051
- 747
Ndugu zanguni.
Kama mjuavyo mheshimiwa Lema alikuwa hapa UK na alifanikisha zoezi la kufungua tawi la chadema UK.
Pamoja na hayo faida kubwa ya safari ya LEMA ambayo haikugharimu zaidi ya pounds £2,000 aliahidiwa ambulance mbili ambazo jumapili iliyopita zilikabidhiwa kwa mwenyekiti wa Chadema UK Chris Lukosi. ambulance hizi zitaenda kusaidia wajawazito na wagonjwa wengine jimboni kwake.
Wakati huo huo Mkulu alikuja hapa UK kuhudhuria semina ya uzazi wa mpango.
Msafra wa mkulu ulikuwa na watu kama 70 hivi na walifikia kwenye hoteli moja kubwa sana hapa UK inaitwa CHURCHILL HOTEL . Gharama za chumba cha kawaida kwa mtu mmoja kwenye hii hotel ni £500. (vyumba vywa walinzi, mawaziri na familia nzima ya mkuli ni more expensive kuliko vya kawaida)
Kwa hiyo watu sabini kwa siku ina cost £35,000 msafara ulikaa hapa wiki moja kwa hiyo iligharimu jumla £245,000 . hizi ni bila kuweka masuala ya chakula , usafiri, shopping nk.
Ambulance alizopewa Lema zinauzwa £4,000 kila moja hivyo basi katika £245,000 tungepata ambulance 61 ambazo zingesambazwa nchi nzima. Mkumbuke tuliambiwa vibajaji vitumike kubeba mama zetu wanapokwenda kujifungua wakati watu wanakuja kuhudhuria semina ya uzazi wa mpango na kutumia mihela yote hii!.
Maswali yangu kwa jamii.
Kuna umuhimu gani kuhudhuria semina inayohusu wazazi wakati wazazi wenyewe unawaambia wapande bajaji?
Kuna umuhimu ganin wa msafara mkubwa kama huo wakati kuna ubalozi hapa UK
Kazi ya waziri wa afya ni nini?
Kwangu mimi naona safari ya LEMA ina mafanikio makubwa zaidi kwa sababu walau amerudi na ambulance mbili na hakutumia hela nyingi £2,000.
Hii wenzangu mnaionaje?? hata kama wewe ni CCM una mawazo gani hapa?
Kama mjuavyo mheshimiwa Lema alikuwa hapa UK na alifanikisha zoezi la kufungua tawi la chadema UK.
Pamoja na hayo faida kubwa ya safari ya LEMA ambayo haikugharimu zaidi ya pounds £2,000 aliahidiwa ambulance mbili ambazo jumapili iliyopita zilikabidhiwa kwa mwenyekiti wa Chadema UK Chris Lukosi. ambulance hizi zitaenda kusaidia wajawazito na wagonjwa wengine jimboni kwake.
Wakati huo huo Mkulu alikuja hapa UK kuhudhuria semina ya uzazi wa mpango.
Msafra wa mkulu ulikuwa na watu kama 70 hivi na walifikia kwenye hoteli moja kubwa sana hapa UK inaitwa CHURCHILL HOTEL . Gharama za chumba cha kawaida kwa mtu mmoja kwenye hii hotel ni £500. (vyumba vywa walinzi, mawaziri na familia nzima ya mkuli ni more expensive kuliko vya kawaida)
Kwa hiyo watu sabini kwa siku ina cost £35,000 msafara ulikaa hapa wiki moja kwa hiyo iligharimu jumla £245,000 . hizi ni bila kuweka masuala ya chakula , usafiri, shopping nk.
Ambulance alizopewa Lema zinauzwa £4,000 kila moja hivyo basi katika £245,000 tungepata ambulance 61 ambazo zingesambazwa nchi nzima. Mkumbuke tuliambiwa vibajaji vitumike kubeba mama zetu wanapokwenda kujifungua wakati watu wanakuja kuhudhuria semina ya uzazi wa mpango na kutumia mihela yote hii!.
Maswali yangu kwa jamii.
Kuna umuhimu gani kuhudhuria semina inayohusu wazazi wakati wazazi wenyewe unawaambia wapande bajaji?
Kuna umuhimu ganin wa msafara mkubwa kama huo wakati kuna ubalozi hapa UK
Kazi ya waziri wa afya ni nini?
Kwangu mimi naona safari ya LEMA ina mafanikio makubwa zaidi kwa sababu walau amerudi na ambulance mbili na hakutumia hela nyingi £2,000.
Hii wenzangu mnaionaje?? hata kama wewe ni CCM una mawazo gani hapa?