Safari ya JK Davos Pata Picha

kwa hiyo unataka kusema Jk aache kusafiri kwa sababu tu madaktari wamegoma.....are you kidding? tupate hasara mara mbili kwani amekwenda kutembea au kwa faida ya nchi? wabunge nao wakigoma abaki Ikulu, waalimu na wengineo vivyo hivyo...hapana haikubaliki Rais ni taasisi ndio maana chini ya Rais kuwa viongozi rukuki wa kumsaidia. kwani wakikutana na Pinda kuna tatizo gani?

Unajua mgomo wa madaktari na madai yao nini? Hilo fungu la safari kwa nini wasiwape madaktari wanachodai? Safari zake huwa zinaisha? Akimaliza hiyo ataanzisha nyingine..
 
Mkapa amehudhuria vikao vyote vya Davos alipokuwa madarakani. Kelele hizi hazikuwepo! Hadi akatibiwa huko kile/ule kiuno/mguu chake/wake kilichokuwa/uliokuwa kimetenguliwa/umetenguliwa na Mama nanihii.
 
Jamaa mkali
Masoud namkubali sana yuko wazi na wala hafichi fichi wala kuogopa impact ya kile atakachokiandika

Na hili litamtengezea maadui wa kutosha. Hii ni nchi ambayo watawala wake wanapenda sana kuzungukwa na watu wanafiki na wapamba maneno mazuri kwao.
 
Mama Porojo!!!!!!!!!!! Hapo kwenye Katuni kuna Tusi lolote??????????? UNless mimi ndo sijui maana ya tusi!!!!!!!!!!!!!!! Hii inanikumbusha maelzi watu wengi wamekuwa wanaambiwa kuwa mkubwa hakosolewi? Sasa mtu kama ni mkubwa jiulize kaupataje? Huu ukubwa wa raisi, waziri, ktibu mkuu,mkuuu wa mkoa,Mbunge diwani ni kutokana na ridhaa yetu. Kwa hiyo kama mkubwa hajui kuwa sisi ndo tumempa ukubwa na hataki kukosolewa, theni yeye ndo amepotea. Ni lazima mkubwa afahamu waajiri wake(sisi wananchi) na kusikiliza mawazo, lawama, ushauri na haa akubali kukosolewa. Mama Porojo umeniacha hoi!
Ili uwe mzalendo mtukane kikwete...... hiki ni kipimo kipya kabisa cha uzalendo kilichotolewa na maabara ya Froida. kwa mwendo huu uzalendo kwa nchi yetu utazidi kufa
 
Wilcard! Kwa hiyo tuufanye huu kuwa utamaduni (tuhalarishe) wa watanzania kuendelea kuona viongozi wakiwa busy na mambo mengine nyakati za migogoro kama sasa? Kimsingi kila kiongozi ni bora apimwe kwa mizania tofauti,maana wanakuwa ktk nyakati tofauti! Suala la kuhalarisha uovu kwa kisingizio 'this has been the previous practice' halina mantiki hapa. Kwa hiyo Mkapa, Mwinyi na hata Nyerere kama walifanya hivyo hatuwezi kukubali kuwa huo ndo utamaduni unaofaa kwa viongozi.Upingwe kwa nguvu zote. BUT, kwa kuwa Mh Kikwete ndo yupo madarakani, sasa bora kujiuliza is this the right thing and right moment kwake kuwa Davos wakati tuna crisis kama hii?
Mkapa amehudhuria vikao vyote vya Davos alipokuwa madarakani. Kelele hizi hazikuwepo! Hadi akatibiwa huko kile/ule kiuno/mguu chake/wake kilichokuwa/uliokuwa kimetenguliwa/umetenguliwa na Mama nanihii.
 
Hivi ninyi kwani mnamatatizo gani,kwani si anaenda tu maramoja atarudi kuyatatua matatizo yao,hawawezi kusubiri,ninajua kabisa kura walisha mpa ila kwani kiongozi wetu ni msikivu ,asiye na husuda,mkiendelea kumkasirisha najua ataweza toa kauli kama hii.SIZITAKI KURA ZENU.ila tuvute subira tu atarudi,pia kuna timu ya wabunge pia wanaweza wakavaa jezi za madaktari wakaanza kazi wafanya kama madaktari haina shida,kwani kama wao wanaweza pewa kipaumbele kuliko watu ambao ni proffesionals inasikitisha.Juzi kuna Mbunge anajiita eti ni mtoto wa mkulima andiriki kabisa kutetea mishahara na posho za wabunge eti ni kidogo sana sasa fanyeni na hao wabunge:A S embarassed:
 
Mkapa amehudhuria vikao vyote vya Davos alipokuwa madarakani. Kelele hizi hazikuwepo! Hadi akatibiwa huko kile/ule kiuno/mguu chake/wake kilichokuwa/uliokuwa kimetenguliwa/umetenguliwa na Mama nanihii.
Uchumi wa nchi ulikuwa mzuri wakati ule!
 
Back
Top Bottom