MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,564
- 847
SADC
1. Ilianzishwa kama Front Line States za ukombozi
2. Zinaheshimiana kihistoria
3. Zina mali asili nyingi sana kuliko EAC
4. Zina soko kubwa la uhakika
Zina matatizo ya uongozi kwa sasa
Wananchi hawajashirikishwa kikamilifu zaidi ya mipakani
Asante mkuu. Based on this umetoa uzuri na kasoro za SADC je kwa maoni yako ipi kati ya SADC na EAC ni bora zaidi kama ungeambiwa uchague moja?
Kwa wale wajuzi wa mambo ningependa kufahamu kati ya shirikisho hizi mbili za kikanda, Southern African Development Community (SADC) na East African Community (EAC), ni ipi yenye manufaa zaidi kwa Tanzania?
Asante mkuu. Based on this umetoa uzuri na kasoro za SADC je kwa maoni yako ipi kati ya SADC na EAC ni bora zaidi kama ungeambiwa uchague moja?
SADC ipo ki-strategic zaidi ya EAC ambayo ipo kisiasa zaidi ( Muungano unasukumwa na political Interest). Mambo mengi yanayojadiliwa na kufanyiwa maamuzi EAC ni contrary na ushauri wa wataalamu (mfano single currency - wachumi wameshauri tusikimbilie kutumia single currency kabla ya kurekebisha sheria na taratibu za ki-fedha kwa kila nchi in short harmonization ya sheria na sera za fedha,hali kadhalika swala la vitambulisho-sheria za uhamiaji zioanishwe kwanza) .Ila cha kushangaza hizi nchi za EAC hususani Kenya ,Uganda na Rwanda wanakimbiza mambo kama vipofu.Kwa wale wajuzi wa mambo ningependa kufahamu kati ya shirikisho hizi mbili za kikanda, Southern African Development Community (SADC) na East African Community (EAC), ni ipi yenye manufaa zaidi kwa Tanzania?
SADC ipo ki-strategic zaidi ya EAC ambayo ipo kisiasa zaidi ( Muungano unasukumwa na political Interest). Mambo mengi yanayojadiliwa na kufanyiwa maamuzi EAC ni contrary na ushauri wa wataalamu (mfano single currency - wachumi wameshauri tusikimbilie kutumia single currency kabla ya kurekebisha sheria na taratibu za ki-fedha kwa kila nchi in short harmonization ya sheria na sera za fedha,hali kadhalika swala la vitambulisho-sheria za uhamiaji zioanishwe kwanza) .Ila cha kushangaza hizi nchi za EAC hususani Kenya ,Uganda na Rwanda wanakimbiza mambo kama vipofu.
SADC ni muunganiko wa kihistoria zaidi hivyo kuvunjika kwake ni kama kuifuta historia ambapo haiwezekani. EAC kuvunjika ni rahisi ktokana na kwamba ni muunganiko wa kisiasa -Unategemeana na kiongozi wa nchi aliyeko madarakani na mtazamo wake.
Conclusion
SADC ni bora kuliko EAC.
Inawezekana kote kukawa na faida, kwa maoni yangu. EAC, COMESA na SADC zote ni njia kuu za kuifanya Afrika ije kuwa chini ya ya muungano mmoja siku za baadaye. Kwa hiyo kila walalofanya, wanafocus Africa intergration bid.
Lakini udhaifu wa Tanzania kuwa EAC ni kuwa kwenye nchi nyingi zilizoko COMESA, na ambazo hazitaki kuheshimu uhuru wa Tanzania kuwa SADC. Kwa sababu zenyewe ziko COMESA, basi zinai bully Tanzania nayo iwe COMESA.
Pia, in terms of trading, Tanzania imekuwa zaidi ni soko la Kenya ambayo private sector ilianza siku nyingi, hivyo kutufanya tuwe koloni la Kenya kiuchumi. Kenya ina tatizo la kuwa dishonest inapokuwa kwenye maslahi, na hili linatokana na ukweli kuwa ina nguvu za kuichumi kuliko jirani zake. Kama kungekuwa na nchi nyingi zaidi kwenye block hii ambazo ama zingekuwa na nguvu au dhaifu, zingesaidia kuneutralize msimamo huu wa Kenya.
Unapopima mafaniko ya EAC, kumbuka pia kuwa kuna focus ya federation. Politically, nchi zote hizi zinatofautiana sana namna ya kutatua political upsets. Of all, Tanzania pamoja na matatizo yake, ndo the most stable one, na wananchi wake wana muundo wa ajabu wa kutatua matatizo yao.
Hii ina maana kuwa Over ambitions za watu kama Museveni inapokuja suala la urais wa EAC, na namna tatizo la akina Kony, tribalism kwenye politics both Uganda na Kenya, vinawaput off wengi wetu katika EAC.
Nikipata wasaa mzuri zaidi nitatafuta takwimu zinazofaa. Bado nadhani sijajiubu swali lako sawa sawa, lakini SADC ilianza kwa political thrust wakati ule ikiwa SADCC, na baadaye ikashift. SADC, kwa kuwa ina member wengi, maamuzi yake yamekuwa thabiti, japo nayo huwa inachemsha sehemu fulani. South Africa huwa inatoa mchango mkubwa kwenye SADC kwa kuwa inataka iwe zaidi ya rival wake COMESA. Na hii ni healthy situation.
Binafsi naona EAC kama utapeli mwingi, huku kila mtu akitolea macho resources za Tanzania. Kumbuka hata namna wazo la kuanzisha EAC lilivyochemshwa: from Up to bottom, badala ya bottom up. Ndo maana kwenye survey ya watu wanaotaka ku fast track federation, imeshindikana.
SADC the club of giants.
DRC , Angola, South Africa, Zambia, Zimbabwe, Mozambique all wants TZ to join the club of giants.
EAC is hungry for everything, poor market, poor in land, poor in security, poor in money, poor in resources.
Nyinyi wa TZ muna fikiria nini?
Nilivyofanya utafiti wa siku hizi mbili, naona kama watz wanapenda zaidi SADAC kuliko huu ukoloni wa Kenya na matatizo ya vinchi vingine.
Hivi, kama Tz itakataa kuendelea na fast truck ya EAC, au federation, halafu uganda kenya rwanda na burundi wakajiunga wao tu, sisi tutapata hasara gani? Je, hizi nchi zote hizi zina resources sawasawa? i mean, resources zilizoko Kenya na namna ya umilikaji wa ardhi nk, vivyo hivyo resources zilizoko uganda rwanda na burundi, najua hazilingani, tz ndo tajiri kuliko zote na ndo yenye eneo kubwa kuliko zote...je watz wameshaweka mikakati ya kwamba pale tutakapojiunga hasa kuwa federation, watz wetu watafaidika kidhabiti na utajiri wao huu? manake hatuwezi kufaidi pamoja na watu wa nje wakati wao huko kwenye nchi zao walishazila kwa pupa na hawana....., vinalingana?
Mbona naona kama tz ndo tajiri kuliko wote hapa na hivi vinchi vingine vya east africa vimegutuka na kuona kumbe bongo kule ulaji na wanataka waje wafaidi? kwanini hii fast truck haikuwapo kipindi cha nyuma wakat Tz utalii, madini, mafuta na gesi vilikuwa havijagunduliwa? Mimi naona, ni bora na sisi tuwafanye wenzetu makoloni yetu kwa kuwauzia raslimali zetu...yaani tuchimbe mafuta haya ambayo yamekuwa confirmed kwamba yapo, madini na tushindane kiutalii.
Kama hawataki, basi sisi tutalala mbele na sadc, tutafungua milango nchi hizi za kusini kama tulivyoanza kwa mozambique, malawi zambia na DRC, hadi South Africa kabisa kwasababu uwezo tunao na resources tunazo. Why hawa jamaa wanataka harakaharaka peke yao lakini watz hatutaki? Do they feel that they need us more than we need them? or we need them more than they need us?