Sabodo aichangia CHADEMA milioni mia moja

Sabodo aichangia CHADEMA milioni mia moja

hivi Gaddafi hajawahi kuimwagia CCM pesa through bernard membe mpaka membe akaamuliwa na Ghaddafi ajenge misikiti jimboni kwake?

Hapana aliyechangisha fedha hizo ni Nyerere. In fact hichi kitendo cha Nyerere kuchangisha fedha kutoka kwa Dikteta Gaddafi ili kujenga msikiti huko Butiama kinachukuliwa kama "muujizi" ambao utampelekea Nyerere kupata UTAKATIFU!
 
barabara afu tunaomba tupewe mapato na matumizi ya pesa za sabodo maana baadhi ya wanachama wa CDM niliongea nao wanalia njaa sana wakati viongozi wakuu wanakula peke yao
Mhe. Kashaga ,Hivi ilitolewa kwa ajili ya kupunguza njaa za wanachama ?
 
HIzi za sabodo zilikuwa zinapitia mgongoni mwa mtu toka nje
Ili hoja yako iwe na nguvu na ikubalike, itabidi uthibitishe, bila hoja hiyo kutia wasiwasi wowote kabisa, kuwa hizo pesa za Sabodo zinapitia mgongoni mwa mtu kutoka nje. Usipofanya hivyo utaonekana kuwa wewe ni mmojawapo wa vibaraka, wapinga maendeleo ambao wametumwa hapa jamvini kupotosha na kuchanganya mawazo ya watu. Hata hivyo uelewe kuwa wana JF wengi ni waelewa wazuri wa mambo, wa kutoa na kupima hoja. Hivyo basi unapoandika, andika ukijua kuwa hoja zako zitachambuliwa kwa umakini, ama sivyo, zitadharauliwa na kutosomwa kabisa.
 
barabara afu tunaomba tupewe mapato na matumizi ya pesa za sabodo maana baadhi ya wanachama wa CDM niliongea nao wanalia njaa sana wakati viongozi wakuu wanakula peke yao
Unatia aibu sana wewe... Chama hakina uwezo wa kuondoa njaa kwa wanachama wake kwa kuwa wanachama tunafanya kazi zetu na tunalipwa mishahara mwisho wa mwezi. Viongozi wanaotumia hela za chama wanafuata taratibu zote za kifedha. Mawazo yako haya ya Kifisadi yanatokana na ukweli kwamba umelelewa ktk mfumo wa kiccm ambao mnadhani chama ndio kitawaondolea njaa na sio kazi mnazofanya. Pole sana.
 
Sabodo alitoa mchango katika uchaguzi na siyo kuchangia kupinga malipo kwa dowans. Hakuna chama cha siasa hapa nchini ambacho kwa namna moja ama nyingine haipati misaada kutoka vyama rafiki au mashirika au watu binafsi. Hivyo sioni sababu ya watu kujadili sijui nani anapata hela wapi au kiasi gani, cha msingi kama nilivyomwelewa Mh. Mnyika ni kwamba kuna tuhuma kuwa chadema wanapewa pesa kutoka ubalozi fulani kufadhili uvurugaji wa nchi au nchi ionekane haitawaliki. Mimi nimefurahi sana kusikia kuwa chadema wanataka kwenda mahakamani na siyo kila siku lawama tu na kutaka serikali iende mahakamani nashauri wasichelewe waende mahakamani haraka sana ili tujue kile anachosema Rais ni kweli ama la kama ni kweli nini kifanyike? chadema kifutwe, kama la basi serikali ya ccm iondoke madarakani haraka sana. Tukumbuke kauli hiyo haijaanza kwa Membe na Simba tu bali Rais Kikwete alishawahi sema hivyo kuwa kuna balozi anachotaka yeye ni kuona ccm inaondoka madarakani.

Upande wangu sasa. Ni kweli kabisa kuna balozi hapa nchini ambaye anataka kuona ccm inaondoka madarakani na kinaingia chama anachokitaka yeye kwa maslahi ya nchi yake. Balozi huyo alifanya kazi ya ziada Zanzibar kuhakikisha kuwa cuf inaingia madarakani na aliweza kupanga hata safu ya mawaziri lakini alishindwa kucheza na system iliyopo mwisho karume akampasha maalimu kuwa nchi ni yao na si ya balozi huyo wanachotaka wenzetu ni mafuta. maalimu akakubali wakaleta serikali ya umoja wa kitaifa kitu ambacho kilimchukiza sana balozi huyo akiamini jk pamoja na taasisi fulanifulani walihusika kupanga huo mkakati. Nafurahi sana kwa kuwa waliyemtaka awe waziri wa uchumi hakupata uwaziri ila ni mwakilishi tu. Sasa wanahamia bara na gia ni ileile ya uchonganishi ili ifike mahali mtu wa ccm, cuf, tlp, nccr, nk asimwombe chumvi mtu wa chadema na hata kura zipigwe za chuki kama alisema karume.

mimi sitaki longolongo naweka mambo wazi kuwa balozi huyo ni balozi wa Denmark akisaidiwa na global platform na action aid. Hili hata management blog hii ya JF inalifahamu vyema. Ni kweli kuna matatizo mengi ya kiuongozi hapa nchini lakini isifike mahali tukagombanishwa na mataifa mengine kwa kutumia udhaifu wetu.

Nawasilisha.
Tu-assume kuwa haya uliyoandika hapa ni kweli 100%. Swali: Nchi hii haina serikali??? Mataifa mengine ungesikia tu balozi wetu kaitwa nyumbani, au balozi wao hapa kaitwa ikulu na kupewa onyo/malalamiko. Sasa serikali hii ya wizi inataka kutudanganya nini? balozi anayefadhili fujo kwa nini asitimuliwe??? Sisi siyo misukule banaa, hizi pumba hatuli kuleni wenyewe na mkwere wenu.
 
Mhe. Kashaga ,Hivi ilitolewa kwa ajili ya kupunguza njaa za wanachama ?

kwa ajili ya uchaguzi kwamaana wagombea wa nafasi mbalimbali wangefaidika nazo,wgombea wengine waliuza mali zao binafsi ili kuhakikisha cdm inashinda na wao binafsi wanashinda,matokeo yake pesa zikaenda moshi kwa ndesa na baadhi ya maeneo na zingine viongozi wa juu kuneemeka,kwanini wengine hawakupewa salio? mfano yule kijana alyieshinda kule mbeya hakuona hata senti ni juhudi za wazazi wake na wankijiji wenzake kumchangia,leo ameshinda CDM inajifanya kujivunia nae! NARUDIA TENA TUNAOMBA MATUMIZI YA PESA ZA SABODO YATOLEWE WAZI MAANA YAMEJAA UBADHIRIFU
 
itakuitaji muda mrefu kufikiria na kuconnect dots membe na sofia wanachosema kina ukweli ndani yake. Inawezekana wahisani wa nje wanapitia migongo ya wengine kusponsar vyama, na inawezekani hii imeanza muda mrefu.

Mzee sabodo amekuwa akimwaga hela kwa cdm kwa muda mrefu na mara nyingi. Je wahisani wamepitia kwa sabodo kuipa nguvu cdm?

Naweza kusema hii ni moja wapo ya ushahidi wa cdm kupokea mkwanja toka nje


dsc09389.jpg


:msela::msela:

kama kweli nyie chadema mnasema mnachukia ufisadi tunaomba mtuwekee wazi matumizi ya pesa za sabodo maana kuna tetesi zilitumika ndivyo sivyo
 
Nadhani Watanzania tumefikia ukomo wa kufikiri. Sabodo amekuwa akiwapa pesa nyingi sana CCM tangu miaka ya nyuma, je wakati huo pia mataifa ya nje walikuwa wanapitishia kwa Sabodo? Kwani kuandamana kunahitaji pesa gani ya kupata msaada wa wahisani? Think positive siyo kinjaa njaa hivi.
 
Kashaga nakushauri uende Loliondo kwanza unywe dawa kwa babu kisha urejee jamvini maana hoja zako eti wanachama CDM wanalia njaa hazina nguvu wala mvuto hata kidogo. Washauri CCM wenzako wajibu hoja na siyo kuwaachia viongozi wa serikali kuwatetea. Yusuf Makamba yuko wapi hadi akina Membe na Sophia wawe wasemaji wa chama? Una habari Sabodo anatoa msaada mkubwa kwa CCM kuliko CDM? Au unataka Sabodo aitishe press conference? Foleni imepungua sana Loliondo wahi mapema kabla tiba haijasitishwa au dawa kuisha.
 
mbona sebodo huyu huyu anaisaidia hadi serikali?na hiyo misaada kama zile ambulance alikopewa ndio basi na hizo fedha anazowapa chadema ndio anapozipata....
"Mfa maji haishi kutapatapa"
 
KAMA NISINGETUMIA BUSARA NINGESEMA HUJATUMIA BUSARA na ni mchochezi KUTAKA FEDHA ZA MSAADA WA KUIMARISHA CHAMA ZIFAIDIWE NA WANACHAMA.
Chochote kitakachofanywa basi kiwe kwa manufaa ya wanachama au unafikiri hizo pesa bora zitumike kuleta machafuko? Hapo kweli zitakuwa haziwanufaishi wanachama kwani CDM ilikwishakataa kuwa ina lengo la kuleta machafuko!
 
Heeeee nguvu ya umma imewauma sasa mwatafutwa wapi wanapata pesa,Kwa ufupi pesa inatafutwa,wametafuta wamepata.Ni pesa ya kuimalisha chama.Nabado watu waijiita maDr,sasa wanaogopa kujiita tena,mtaumia sana........... ndo maaana mmekimbilia kwa babu kunywa dawa.
 
Heeeee nguvu ya umma imewauma sasa mwatafutwa wapi wanapata pesa,Kwa ufupi pesa inatafutwa,wametafuta wamepata.Ni pesa ya kuimalisha chama.Nabado watu waijiita maDr,sasa wanaogopa kujiita tena,mtaumia sana........... ndo maaana mmekimbilia kwa babu kunywa dawa.

hivi nguvu ya umma mzee ni kuwa na wabunge 23 tuu katika bunge lenye wabunge 293?? umati unawasanifu tuu
 
Itakuitaji muda mrefu kufikiria na kuconnect dots membe na sofia wanachosema kina ukweli ndani yake. inawezekana wahisani wa nje wanapitia migongo ya wengine kusponsar vyama, na inawezekani hii imeanza muda mrefu.

Mzee Sabodo amekuwa akimwaga hela kwa CDM kwa muda mrefu na mara nyingi. Je wahisani wamepitia kwa sabodo kuipa nguvu cdm?

Naweza kusema hii ni moja wapo ya ushahidi wa cdm kupokea mkwanja toka nje. END QOUTE]

Eti niulize hivi NJE ni wapi?
Kuna sheria yoyote inayozungumzia INCOME GENERATION ya chama cha siasa??
kwani pesa za CCMzinatoka NDANI?
kwa maana hiyo NDANI ni wapi?
 

Mkurugenzi wa Kampuni ya ALTAF AND COMPANY Bw, Zulfqal Ali (kushoto) akimvisha mgeni wake saa ya mkononi kama zawadi kwa Katibu Mkuu wa CCM Bw. Yusufu Makamba alipotembelea Tabata Dar es salaam jana kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya kiwanda hicho kilichotoa msada mkubwa wakati wa kampeni za CCM?????????????
 
Back
Top Bottom