Sababu zinazofanya wanatajirisha wengine wao wanabakia masikini

Da'Vinci

JF-Expert Member
Dec 1, 2016
35,688
106,809
Mates
Inawezekana hua unajiuliza kwanini labda wachawi/waganga hua wanaweza kumpa utajiri mtu lakini wao wanabaki kwenye umaskini wa hali ya juu huku wateja wao wakineemeka na mali zao. Hawa watu hua ni smart sana kichwani na kiroho ,wanajua jinsi gani ulimwengu wa roho na huu tuishio usiwachukulie poa kabisa.

Kwanza ni wazuri wa kucheza na saikolojia za wagonjwa wao ndio maana anaweza kukupatia dawa ya kutatua shida Fulani ukaitumia ukapona ukadhani labda ile dawa ndio imekupunya kumbe sivyo. Mfano unaweza kuumwa tatizo Fulani labda figo akakupa dawa ukatumia kisha ukapona ila kinacho behind the curtain ni kwamba wao wanafahamu kwamba kila kitu kinachofanyika kwenye ulimwengu tunaoishi kinaanzia katika ulimwengu wa roho na wanajua kwamba roho kama power house ya mwili ina uwezo (Psychic power) wa kutenda(manifest) lolote katika ulimwengu wa mwili/mazingira.

Wanachofanya ni Reorientation of the spirit to better heal the body kwamba unaweza kua na tatizo Fulani mwilini ukaukonvisi mwili wako kwamba hauna tatizo hilo unapofanya hivyo unakua unaifanya roho yako iweze kumanifest cellular regeneration kisha cell zitazalishwa za kutosha na kutibu ugonjwa ambao mtu alikua anaumwa. So hapo kinachokua kimeponya si dawa bali ni roho yako mwenyewe. Jifikirie unaenda kupewa dawa ya kuongeza wateja dukani kwako halafu location ya duka lako ni city centre yenye mkusanyiko wa watu hapo watu lazima waje kununua tu…sio kwamba ajili ya dawa bali kwakua umeweka sehemu ambapo watu wanakuja kutafuta mahitaji yao. Ukitaka ujaribu hizo dawa nenda nje ya mji au porini uone kama hiyo dawa itafanya wateja wakufate huko.

Turudi kwenye mada, kunasababu kadhaa zinazowafanya wachawi/waganga watajirishe wengine huku wao wakibaki na umaskin, zifuatazo zinaweza kua sababu kuu.​
  • Respecting Laws of Natures
Kwanza kabisa kwa kutumia ithibati ya pili katika uthibitisho wa uwepo wa Mungu ulivyoelezwa na mwanafalsafa Thomas wa Akwino ambayo ni The First Causation wachawi/waganga nao wanaamini kwamba Mungu yupo na kila kitu kimetokea kwa sababu yake pia kwa kulitambua hilo wanaamini katika Scale of balance kwamba kila kitu kina kinyume chake kama Kuna nuru basi kuna giza, kama kuna kushoto basi kuna kulia,kama kuna mwanamke basi kuna uhai, kama kuna uhai basi kuna kifo nk nk.

Kiufupi ni kwamba wachawi/waganga wanatambua Mungu yupo kaumba kila kitu na kaweka Kanuni Fulani za kimazingira zinazoongoza ulimwengu huu (Laws of nature) na wanajitahidi kuzifuata ili kutimiliza jambo lao. Basi moja kati ya kanuni wanayoishika sana ni Earning what you have. Kwa lugha rahisi ni kwamba wanajua kwamba kila mwanadamu anatakiwa atoke jasho/afanye kazi ndio apate kile anachotaka. Kwa mantiki hii ndio maana wao hawahangaiki kujitajirisha kwa kutumia dawa zao lakini akija mteja anataka dawa ya utajiri wanampatia halafu wenyewe wanabaki kwenye umaskini wao.

Baada ya kukupa dawa ulizohitaji anakutoza tu kiwango cha ghalama ya huduma au anakuambia nenda “ukifanikiwa utaniletea shukrani yoyote”. Unaona sasa hapa wewe unakua umepata pesa za mteremko kama ni kuoza mguu, kutoa umri wako,mtoto, nk baadae ukimlipa pesa aliyokuambia Techinically yeye anakua kaivujia jasho (earning) pesa hiyo maana kakuuzia huduma huku wewe umepata pesa za mteremko. Hence yeye kapata hela halali huku wewe umepata zisizo ndio maana hiyo pesa anaweza hata kuitolea fungu la kumi bila kinyongo maana ameihangaikia…Kazi inabaki kwako uliyehudumiwa sasa. Kwa sababu hii wachawi/waganga hawawezi kujitajirishi kwa kuumia dawa zake.

Hint 1: Sometimes mtoto wa mganga anaweza akaumwa ila mganga huyo akashindwa kumponya mpaka ampeleke kwa mganga mwingine. Na huko pia akitibiwa bure inawezekana asipone mpaka pesa itoke.
  • Attachment to the material is detachment to the spiritual
Sababu nyingine inayofanya wachawi/waganga wanabaki kwenye umaskini mkubwa huku wakitajirisha wengine ni kua unapojishikiza sana kwenye vitu/pesa unakua unajitenga na mambo ya kiroho.Mungu alivyomuumba mwanadamu akamtaka ajipatie riziki yake kwa kufanya kazi pia Mungu alimtaka mwanadamu akijipatia ridhiki atumie na kutafuta nyingine na sio kujilimbikizia mali, Watu wa zamani waliishi kwa upendo na amani kwakua walikua wanaishi kwa kutafuta na kutumia kwa pamoja na sio kijilimbikizia peke yako.

Dunia ilichuka sura mpya baada ya mwanadamu kuanza kujilimbikizia mali hapo ndipo kukatoka Uasi wa kila namna…mtu yupo radhi kuua ilia pate mali, ubinafsi,uchoyo, roho mbaya nk. Mpaka sasa tunaoana effect za Capitalism model of production duniani. Kuna nchi watu hawana amani ajili ya watu wachache wenyekujali maisha yao binafsi.

Kama nilivyosema huko juu kwamba hawa watu wanaheshimu kanuni ya kujitafutia kwa jasho lakini pia wanaelewa kwamba Mtu ni roho, kuna ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili. Hivyo basi wanajua ulimwengu wa roho unajengwa kwa kutena yale ya rohoni na pindi unapoanza kujishikiza katika ulimwengu wa mwili ambao ni kutafuta mali na kujilimbikizia materials kwa ajili ya kufurahisha mwili huu basi anakua anajipunguzia nguvu zake za kiroho.

Same applied kwa sisi tuifatayo Nuru kama una upako wako/roho mtakatifu rohoni mwako ukianza tu kujikita kutafuta mali basi ule uwezo wako unaanza kuupoteza maana unakua umewekeza nguvu zaidi katika kutafuta mali za mwili na sio mali za roho yako. Kwa kulizingatia hilo ndio maana watawa wa kikatoliki hua hawajishikizi katika materials kama vile pesa,majumba,watoto,mke nk maana wanajua wakiruhusu hiyo itokee basi hakutakua kuna Integrity ya utume wao maana huwezi tumikia mabwana wawili.

Wewe wakati unayapima mafanikio kwa kuangalia materials uliyonayo ila hawa watu utajiri wao unapimwa kwa nguvu zake alizonazo, ndio maana utamuona mtu huyu ana maisha duni ila huko kwingine anaheshimika sana kwa uwezo na nguvu alizonazo. Kuwanga ni moja ya ibada za hawa watu na moja ya mwiko wao wakiwa katika ibada zao ni kuchukua material yoyote (hasa pesa) yatakayokutwa kwenye nyumba za mtu anayewangiwa kwa tama zake binafsi…ndio maana hata ulale na begi la hela ndani mchawi akija atakuawangia ataondoka bila kuchukua hata mia na akijichanganya akachukua hata mia basi hawezi kutoka ndani mwako maana anakua kakiuka sharti la ibada yao. Ukiona mchawi kaja kwako akachukua kitu basi sio kwa personal desire zake bali kitu hicho (sio pesa) kinahitajika katika kufanikisha shughuli zao Fulani.

Basi kwasababu hizo zinafanya hawa ndugu zetu wazidi kubaki kwenye hali duni ya maisha ila kwenye ufalme wao huko ni watu matajiri sana. Furaha yao ni kuongeza nguvu zao za uchawi/kuroga kama alikua ana uchawi wa kuua kwa saa apate uchawi wa kuua kwa sekunde. Halafu jambo moja ambalo hawa watu wanaliheshimu sana katika mambo yao ni Kutoa sadaka…

Hint 2: Wakati mimi na wewe tukiambiwa tutoe michango ya pesa tunalaumu sana ila wao michango yao si ya pesa bali ni michango ya Damu. Tunaomuabudu Mungu hatutoi sadaka za damu maana kuna damu iliyokwisha tolewa (Mwaka 33AD) hivyo basi sisi tunatoa kile tunachojipatia kwa kufanya kazi wao wanatoa sadaka ya Damu tena ya mtu. Ndio maana wanaua.

Hint 3: Matajiri ndio kundi lingine la watu ambalo wanaheshimu sana sadaka ya fungu la kumi. Kwanza wanaelewa kwamba biashara yako ilinikue zaidi itatokana na kile unachokitoa. Ndio maana jinsi ya mtu Bill Gates anavyotoa mapesa kusaidia Shittholes landers anazidi kupata. Note that sio kwamba hua wanatoa ili waweze kusaidia bali wanajua wanavyotoa ndio wanapata maradufu...Katika zile Golden numbers ambazo business giants wanazifuata zinaeleza katika kutoa ndio maana ni mara chache kusikia tajiri kafirisika ajili ya kutoa msaada.

Bilionea wa kwanza kufirisika kwa kutoa sana misaada kwa wasio jiweza ni J.K. Rowling mwandishi wa vitabu vya Harry Potter. Technically hakufirisika kabisa ila alitoka ubilionea hadi umilionea kwa kutoa sana misaada.

~Da'Vinjiii
 
Further Explanation about Reorientation

Kweye kuuconvice mwili kua unaweza kutembea wakati mtu huyo ameparalaizi inakua hivi.

Kama mtu kapalalaizi akiwa anatibiwa daktari nazipangilia upya neva zilizoharibika kwa madawa na upasuaji..hapo Cell zitauponyesa mwili huo uliopalalaizi mwili huo, hapo Cell zinakua zimeprogramiwa/Programmed na Daktar kujirudisha kama ilivyokua mwanzo ili mtu apone..kitendo hicho kinaitwa Cellular regeneration.

Sasa kila kitu kinaanza rohoni as a power house ya mwili...Mara nyingi tunavyotibiwa hospital tunatibiwa kutokea nje (mwilini) sio kutokea ndani ya Roho. So hivyo basi ukitaka kujitibu kupitia rohoni kama hivyo mtu aliyeparalaizi kujiconvice kwamba anaweza kutembea. Anapojikonvisi hivo anaruhusu roho yake kuachilia nguvu zake za kioho (Psychic Power) kuja kwenye mwili wake.

Zinapoingia mwilini mwake in Extraordinary way mtu anajikuta ameweza kutembea. So technically mtu anakua hajatibiwa kwa cellular regeneration bali zile nguvu zake kiroho alizoziachia kuingia kwenye mwili wake.

Magufuli anafanya hiki kitu either kwa kujua au bila kujua..Maana anajua watu wanamchina ila yeye anataka awatoe hofu. It's good but kinachotendeka ndani its beyond kuwatoa hofu. Technically anawafanya watu kuconvice miili yao kwamba hawana mchina Hence mind inakua postive. You know Power of postive thought. Thought shape Reality

Be careful with what you think because Thought shape Reality. You're what you think and you will get what you think. What you seek is what you will get. Be postive no matter how physical world treat you. You're only weak outside/physically. But inside you're so powerful spiritually. Draw out your spiritual strength to face the physical world.

You're inner strength start with postive thought.

Trust your Inner you!!

👉This is biologically Correct
 
Wow, well written, where did you learn all of this. Unaandika vitu vikubwa sana nimejifunza kitu.
Thanks for sharing.
Sometimes I think knowledge is my Curse🤔
Nilikua mahali nawaza Kuhusu hiyo phrase ya Convincing the body. Then all this stuff/information popped up on my head.. Ndivyo navyopataga ideas.

Nafarijika kusikia umejifunza vitu toka kwangu
 
J.K. Rowling hawajawahi kufulisikia,utajiri wake mpaka sasa unakadiriwa na Forbes kuwa dola bilioni 1 za kimarekani, Hatakaa afilisike hata akiamua kugawa utajiri wake wote na kuendelea kuishi kwa royalties tu za kazi yake.
 
"Wanachofanya ni Reorientation of the spirit to better heal the body kwamba unaweza kua na tatizo Fulani mwilini ukaukonvisi mwili wako kwamba hauna tatizo hilo unapofanya hivyo unakua unaifanya roho yako iweze kumanifest cellular regeneration kisha cell zitazalishwa za kutosha na kutibu ugonjwa ambao mtu alikua anaumwa. So hapo kinachokua kimeponya si dawa bali ni roho yako mwenyewe"

Hii nadharia Inaweza kuthibitishwa kisayansi au ni suala la imani tu?
 
"Watu wa zamani waliishi kwa upendo na amani kwakua walikua wanaishi kwa kutafuta na kutumia kwa pamoja na sio kijilimbikizia peke yako"

Sio kweli kwamba watu wa zamani waliishi kwa upendo na amani kuliko wakati huu. Watu wa zamani ukichukulia karne ya 20 kurudi nyuma walikuwa na migogoro na vita kuliko karne ya 21. Watu wa zamani ilikuwa hata kuoana kati ya makabila ni vigumu, facts zinaonyesha kadri muda unavyosonga mbele ndivyo dunia imekuwa ya amani na kuelewana zaidi.

Watu wa zamani pia walikuwa wanajilimbikizia mali sana tena zaidi kwa nguvu na unyang'anyi sio hata kwa regulated businesses kama wakati huu.
 
"Furaha yao ni kuongeza nguvu zao za uchawi/kuroga kama alikua ana uchawi wa kuua kwa saa apate uchawi wa kuua kwa sekunde"

Kama hii ndio furaha sidhani kama hawa ni watu smart sana kichwani au rohoni, labda hawa wachungaji matapeli wanaojitajirisha kupitia waumini wao unaweza kuwapa hiyo sifa.
 
"Furaha yao ni kuongeza nguvu zao za uchawi/kuroga kama alikua ana uchawi wa kuua kwa saa apate uchawi wa kuua kwa sekunde"

Kama hii ndio furaha sidhani kama hawa ni watu smart sana kichwani au rohoni, labda hawa wachungaji matapeli wanaojitajirisha kupitia waumini wao unaweza kuwapa hiyo sifa.
Kuna tofauti kubwa kati ya mganga na mchawi, usichanganye mambo, kuna wachawi kazi yao ni uchawi tu, na hata huwezi kujua au kukisia kuwa huyu ni mchawi, lkn kuna wengine ni waganga tu, kazi yao ni kutibu na kuponyesha, haruhusiwi kuuwa wala kushika dawa mbaya inayoambatana na kuua, lkn kuna wengine kazi yao ni kutabili tu, unakwenda kwake anakutabilia, anakuambia na vitu utakavyoviona, kama utakutana na simba au mwehu au itakuja mvua au kuna tukio litatatukia mda furani wewe ukiona hivyo fanya hivi na itakuwa hivi

Kwa hiyo hawa watu wanatofauti sana, na si kweli kuwa ni watu waovu, Hapana, ni watu wazuri sana na sana hofu sana ya mungu, shida kuna watu wanaamini mungu yupo kanisani au msikitini, ndio maana wanawahukumu kuwa ni watu waovu,
 
J.K. Rowling hawajawahi kufulisikia,utajiri wake mpaka sasa unakadiriwa na Forbes kuwa dola bilioni 1 za kimarekani, Hatakaa afilisike hata akiamua kugawa utajiri wake wote na kuendelea kuishi kwa royalties tu za kazi yake.
Ameandika "Technically hakufirisika kabisa ila alitoka ubilionea hadi umilionea kwa kutoa sana misaada."

Alikuwa ni billionaire na akapoteza her billionaire status because she donated so much money to charity. So she's no longer a billionaire. Hii ina maana gani?
 
Ina maana kama mtu bado ni milionea hajafilisika kwa tafsiri yoyote ile. Zaidi sana mtu aliyetoa asilimia kama 10 tu ya utajiri wake haitakiwi kuehesabiwa kama amefilisika.
Ameandika "Technically hakufirisika kabisa ila alitoka ubilionea hadi umilionea kwa kutoa sana misaada."

Alikuwa ni billionaire na akapoteza her billionaire status because she donated so much money to charity. So she's no longer a billionaire. Hii ina maana gani?
 
"Same applied kwa sisi tuifatayo Nuru kama una upako wako/roho mtakatifu rohoni mwako ukianza tu kujikita kutafuta mali basi ule uwezo wako unaanza kuupoteza maana unakua umewekeza nguvu zaidi katika kutafuta mali za mwili na sio mali za roho yako. Kwa kulizingatia hilo ndio maana watawa wa kikatoliki hua hawajishikizi katika materials kama vile pesa,majumba,watoto,mke nk maana wanajua wakiruhusu hiyo itokee basi hakutakua kuna Integrity ya utume wao maana huwezi tumikia mabwana wawili"

1.Wewe uifatayo Nuru upako wako huwa unautuma kwa kazi zipi? Huwa unakusaidiaje?
Huwa unajuaje upako wako umepoteza maana?

2.Watawa wa kikatoliki huwa wanahudumiwa kila kitu na kanisa, ni mmojawapo ya kundi la watu wenye maisha mazuri sana yasiyo na shurba nyingi katika dunia hii.
Pia watoto, mke na mume sio mali, hao ni watu.Hawawezi kuwa daraja moja na mali.
Mates
Inawezekana hua unajiuliza kwanini labda wachawi/waganga hua wanaweza kumpa utajiri mtu lakini wao wanabaki kwenye umaskini wa hali ya juu huku wateja wao wakineemeka na mali zao. Hawa watu hua ni smart sana kichwani na kiroho ,wanajua jinsi gani ulimwengu wa roho na huu tuishio usiwachukulie poa kabisa.

Kwanza ni wazuri wa kucheza na saikolojia za wagonjwa wao ndio maana anaweza kukupatia dawa ya kutatua shida Fulani ukaitumia ukapona ukadhani labda ile dawa ndio imekupunya kumbe sivyo. Mfano unaweza kuumwa tatizo Fulani labda figo akakupa dawa ukatumia kisha ukapona ila kinacho behind the curtain ni kwamba wao wanafahamu kwamba kila kitu kinachofanyika kwenye ulimwengu tunaoishi kinaanzia katika ulimwengu wa roho na wanajua kwamba roho kama power house ya mwili ina uwezo (Psychic power) wa kutenda(manifest) lolote katika ulimwengu wa mwili/mazingira.

Wanachofanya ni Reorientation of the spirit to better heal the body kwamba unaweza kua na tatizo Fulani mwilini ukaukonvisi mwili wako kwamba hauna tatizo hilo unapofanya hivyo unakua unaifanya roho yako iweze kumanifest cellular regeneration kisha cell zitazalishwa za kutosha na kutibu ugonjwa ambao mtu alikua anaumwa. So hapo kinachokua kimeponya si dawa bali ni roho yako mwenyewe. Jifikirie unaenda kupewa dawa ya kuongeza wateja dukani kwako halafu location ya duka lako ni city centre yenye mkusanyiko wa watu hapo watu lazima waje kununua tu…sio kwamba ajili ya dawa bali kwakua umeweka sehemu ambapo watu wanakuja kutafuta mahitaji yao. Ukitaka ujaribu hizo dawa nenda nje ya mji au porini uone kama hiyo dawa itafanya wateja wakufate huko.

Turudi kwenye mada, kunasababu kadhaa zinazowafanya wachawi/waganga watajirishe wengine huku wao wakibaki na umaskin, zifuatazo zinaweza kua sababu kuu.
  • Respecting Laws of Natures
Kwanza kabisa kwa kutumia ithibati ya pili katika uthibitisho wa uwepo wa Mungu ulivyoelezwa na mwanafalsafa Thomas wa Akwino ambayo ni The First Causation wachawi/waganga nao wanaamini kwamba Mungu yupo na kila kitu kimetokea kwa sababu yake pia kwa kulitambua hilo wanaamini katika Scale of balance kwamba kila kitu kina kinyume chake kama Kuna nuru basi kuna giza, kama kuna kushoto basi kuna kulia,kama kuna mwanamke basi kuna uhai, kama kuna uhai basi kuna kifo nk nk.

Kiufupi ni kwamba wachawi/waganga wanatambua Mungu yupo kaumba kila kitu na kaweka Kanuni Fulani za kimazingira zinazoongoza ulimwengu huu (Laws of nature) na wanajitahidi kuzifuata ili kutimiliza jambo lao. Basi moja kati ya kanuni wanayoishika sana ni Earning what you have. Kwa lugha rahisi ni kwamba wanajua kwamba kila mwanadamu anatakiwa atoke jasho/afanye kazi ndio apate kile anachotaka. Kwa mantiki hii ndio maana wao hawahangaiki kujitajirisha kwa kutumia dawa zao lakini akija mteja anataka dawa ya utajiri wanampatia halafu wenyewe wanabaki kwenye umaskini wao.

Baada ya kukupa dawa ulizohitaji anakutoza tu kiwango cha ghalama ya huduma au anakuambia nenda “ukifanikiwa utaniletea shukrani yoyote”. Unaona sasa hapa wewe unakua umepata pesa za mteremko kama ni kuoza mguu, kutoa umri wako,mtoto, nk baadae ukimlipa pesa aliyokuambia Techinically yeye anakua kaivujia jasho (earning) pesa hiyo maana kakuuzia huduma huku wewe umepata pesa za mteremko. Hence yeye kapata hela halali huku wewe umepata zisizo ndio maana hiyo pesa anaweza hata kuitolea fungu la kumi bila kinyongo maana ameihangaikia…Kazi inabaki kwako uliyehudumiwa sasa. Kwa sababu hii wachawi/waganga hawawezi kujitajirishi kwa kuumia dawa zake.

Hint 1: Sometimes mtoto wa mganga anaweza akaumwa ila mganga huyo akashindwa kumponya mpaka ampeleke kwa mganga mwingine. Na huko pia akitibiwa bure inawezekana asipone mpaka pesa itoke.

  • Attachment to the material is detachment to the spiritual
Sababu nyingine inayofanya wachawi/waganga wanabaki kwenye umaskini mkubwa huku wakitajirisha wengine ni kua unapojishikiza sana kwenye vitu/pesa unakua unajitenga na mambo ya kiroho.Mungu alivyomuumba mwanadamu akamtaka ajipatie riziki yake kwa kufanya kazi pia Mungu alimtaka mwanadamu akijipatia ridhiki atumie na kutafuta nyingine na sio kujilimbikizia mali, Watu wa zamani waliishi kwa upendo na amani kwakua walikua wanaishi kwa kutafuta na kutumia kwa pamoja na sio kijilimbikizia peke yako.

Dunia ilichuka sura mpya baada ya mwanadamu kuanza kujilimbikizia mali hapo ndipo kukatoka Uasi wa kila namna…mtu yupo radhi kuua ilia pate mali, ubinafsi,uchoyo, roho mbaya nk. Mpaka sasa tunaoana effect za Capitalism model of production duniani. Kuna nchi watu hawana amani ajili ya watu wachache wenyekujali maisha yao binafsi.

Kama nilivyosema huko juu kwamba hawa watu wanaheshimu kanuni ya kujitafutia kwa jasho lakini pia wanaelewa kwamba Mtu ni roho, kuna ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili. Hivyo basi wanajua ulimwengu wa roho unajengwa kwa kutena yale ya rohoni na pindi unapoanza kujishikiza katika ulimwengu wa mwili ambao ni kutafuta mali na kujilimbikizia materials kwa ajili ya kufurahisha mwili huu basi anakua anajipunguzia nguvu zake za kiroho.

Same applied kwa sisi tuifatayo Nuru kama una upako wako/roho mtakatifu rohoni mwako ukianza tu kujikita kutafuta mali basi ule uwezo wako unaanza kuupoteza maana unakua umewekeza nguvu zaidi katika kutafuta mali za mwili na sio mali za roho yako. Kwa kulizingatia hilo ndio maana watawa wa kikatoliki hua hawajishikizi katika materials kama vile pesa,majumba,watoto,mke nk maana wanajua wakiruhusu hiyo itokee basi hakutakua kuna Integrity ya utume wao maana huwezi tumikia mabwana wawili.

Wewe wakati unayapima mafanikio kwa kuangalia materials uliyonayo ila hawa watu utajiri wao unapimwa kwa nguvu zake alizonazo, ndio maana utamuona mtu huyu ana maisha duni ila huko kwingine anaheshimika sana kwa uwezo na nguvu alizonazo. Kuwanga ni moja ya ibada za hawa watu na moja ya mwiko wao wakiwa katika ibada zao ni kuchukua material yoyote (hasa pesa) yatakayokutwa kwenye nyumba za mtu anayewangiwa kwa tama zake binafsi…ndio maana hata ulale na begi la hela ndani mchawi akija atakuawangia ataondoka bila kuchukua hata mia na akijichanganya akachukua hata mia basi hawezi kutoka ndani mwako maana anakua kakiuka sharti la ibada yao. Ukiona mchawi kaja kwako akachukua kitu basi sio kwa personal desire zake bali kitu hicho (sio pesa) kinahitajika katika kufanikisha shughuli zao Fulani.

Basi kwasababu hizo zinafanya hawa ndugu zetu wazidi kubaki kwenye hali duni ya maisha ila kwenye ufalme wao huko ni watu matajiri sana. Furaha yao ni kuongeza nguvu zao za uchawi/kuroga kama alikua ana uchawi wa kuua kwa saa apate uchawi wa kuua kwa sekunde. Halafu jambo moja ambalo hawa watu wanaliheshimu sana katika mambo yao ni Kutoa sadaka…

Hint 2: Wakati mimi na wewe tukiambiwa tutoe michango ya pesa tunalaumu sana ila wao michango yao si ya pesa bali ni michango ya Damu. Tunaomuabudu Mungu hatutoi sadaka za damu maana kuna damu iliyokwisha tolewa (Mwaka 33AD) hivyo basi sisi tunatoa kile tunachojipatia kwa kufanya kazi wao wanatoa sadaka ya Damu tena ya mtu. Ndio maana wanaua.

Hint 3: Matajiri ndio kundi lingine la watu ambalo wanaheshimu sana sadaka ya fungu la kumi. Kwanza wanaelewa kwamba biashara yako ilinikue zaidi itatokana na kile unachokitoa. Ndio maana jinsi ya mtu billgert anavyotoa mapesa kusaidia Shittholes landers anazidi kupata. Note that sio kwamba hua wanatoa ili waweze kusaidia bali wanajua wanavyotoa ndio wanapata maradufu...Katika zile Golden numbers ambazo business giants wanazifuata zinaeleza katika kutoa ndio maana ni mara chache kusikia tajiri kafirisika ajili ya kutoa msaada.

Bilionea wa kwanza kufirisika kwa kutoa sana misaada kwa wasio jiweza ni J.K. Rowling mwandishi wa vitabu vya Harry Potter. Technically hakufirisika kabisa ila alitoka ubilionea hadi umilionea kwa kutoa sana misaada.

~Da'Vinjiii
 
Ameandika "Technically hakufirisika kabisa ila alitoka ubilionea hadi umilionea kwa kutoa sana misaada."

Alikuwa ni billionaire na akapoteza her billionaire status because she donated so much money to charity. So she's no longer a billionaire. Hii ina maana gani?
Exactly pesa zilipungua lakini kwakua ni mfanyabiashara hopefully alirudia alipokua.
 
"Wanachofanya ni Reorientation of the spirit to better heal the body kwamba unaweza kua na tatizo Fulani mwilini ukaukonvisi mwili wako kwamba hauna tatizo hilo unapofanya hivyo unakua unaifanya roho yako iweze kumanifest cellular regeneration kisha cell zitazalishwa za kutosha na kutibu ugonjwa ambao mtu alikua anaumwa. So hapo kinachokua kimeponya si dawa bali ni roho yako mwenyewe"

Hii nadharia Inaweza kuthibitishwa kisayansi au ni suala la imani tu?
hii ina act kama counselling kwenye psychotherapy
 
Ulichoolezea hapa sio cellular regeneration. Katika matibabu ya cellular regeneration hakuna matumizi ya madawa na upasuaji. Msingi wa utabibu wa cellular regeneration ni kuepuka maumivu makubwa yatokanayo na njia ngumu zilizozoeleka kama za upasuaji na madawa ambayo mara zote huwa na side effects.

Ukiitizama vizuri Imani ya kuuconvince mwili kupitia roho inataka kufanana kama ile ya Kinijikitile
Further Explanation about Reorientation

Kweye kuuconvice mwili kua unaweza kutembea wakati mtu huyo ameparalaizi inakua hivi.

Kama mtu kapalalaizi akiwa anatibiwa daktari nazipangilia upya neva zilizoharibika kwa madawa na upasuaji..hapo Cell zitauponyesa mwili huo uliopalalaizi mwili huo, hapo Cell zinakua zimeprogramiwa/Programmed na Daktar kujirudisha kama ilivyokua mwanzo ili mtu apone..kitendo hicho kinaitwa Cellular regeneration.

Sasa kila kitu kinaanza rohoni as a power house ya mwili...Mara nyingi tunavyotibiwa hospital tunatibiwa kutokea nje (mwilini) sio kutokea ndani ya Roho. So hivyo basi ukitaka kujitibu kupitia rohoni kama hivyo mtu aliyeparalaizi kujiconvice kwamba anaweza kutembea. Anapojikonvisi hivo anaruhusu roho yake kuachilia nguvu zake za kioho (Psychic Power) kuja kwenye mwili wake.

Zinapoingia mwilini mwake in Extraordinary way mtu anajikuta ameweza kutembea. So technically mtu anakua hajatibiwa kwa cellular regeneration bali zile nguvu zake kiroho alizoziachia kuingia kwenye mwili wake.

Magufuli anafanya hiki kitu either kwa kujua au bila kujua..Maana anajua watu wanamchina ila yeye anataka awatoe hofu. It's good but kinachotendeka ndani its beyond kuwatoa hofu. Technically anawafanya watu kuconvice miili yao kwamba hawana mchina Hence mind inakua postive. You know Power of postive thought. Thought shape Reality

Be careful with what you think because Thought shape Reality. You're what you think and you will get what you think. What you seek is what you will get. Be postive no matter how physical world treat you. You're only weak outside/physically. But inside you're so powerful spiritually. Draw out your spiritual strength to face the physical world.

You're inner strength start with postive thought.

Trust your Inner you!!

This is biologically Correct
 
Nafikiri unamaanisha kitendo cha pesa kupungua tutakiitaje na sio mtu.
Kama ni hivyo, Inategemea zimepunguaje. Kama pesa zimepungua katika michakato ya biashara inawezekana tukaita kupata hasara na kuna kiwango kikifika inaitwa kufilisika(sio kila pesa kupungua ni kufilisika).
Hebu nieleweshe mtu ambae pesa zake zimepungua tutamuitaje??
 
Back
Top Bottom