Infinite_Kiumeni
JF-Expert Member
- Jan 23, 2023
- 382
- 661
Kila mtu na mapenzi yake apendayo.
Kila mtu na malengo yake kwenye mahusiano. Mwanaume kuwa na mwanamke zaidi ya mmoja ni jambo la kawaida, pia ni vyema afanye hivyo. Lakini inategemea maamuzi ya mtu binafsi. Hivyo, wakati unaamua angalia sababu hizi. Twende nyuma kwanza, zamani utajiri ulitegemea nguvu ya familia.
Kwahiyo kadri mnavyokua wengi thamani yenu na nguvu yenu inaongezeka na mnaweza kujilinda, kuzalisha mazao mengi vilevile mnaweza kuvamia wanyonge na mkashinda kirahisi. Kibaiolojia tunafahamu kuwa mwanamke ana ukomo wa uzao na mwanaume ana nafasi kubwa ya kuendelea kuzaa hata kama mke wake mmoja akiwa amefikia ukomo, hivyo basi ili kulinda nguvu na utajiri wa familia ilibidi mwanaume aongeze mwanamke amzalie watoto wengine.
Turudi sasa, kilichobadilika sasa ni kwamba hakuna haja ya kuwa na familia kubwa ili uweze kuilinda familia, polisi wapo. Lakini kibaiolojia hakuna kilichobadilika. Bado kama wanaume tunataka kuwa na urithi mkubwa, bado tunataka majina yetu yawe makubwa, bado tuna ile hamu ya kuwa na wanawake wengi. Haijafuka kwenye damu.
Mwanamke mmoja ana mudi tofauti kwenye mwezi.
Wengine husema ‘wanawake hawaeleweki’.
Wanaume wengi hawawezi kuyahimili mabadiliko hayo. Suluhisho ni kwenda kwa mwanamke mwingine hadi mwanamke wa kwanza awe mtulivu amrudie. Wapili nae akiwa na mudi tofauti, atarudi kwa wa kwanza, na mzunguko utaendelea hivyo.
Mwanamke ndiye anayechagua kuwa na mwanaume au la.
Wanawake wenyewe ndio wapo tayari kuwa na mwanaume mwenye wanawake wengi. Japo anaweza asilikubali hili wazi. Sababu, kwake huyo mwanaume ndo mshindi na jasiri kuliko wanaume wengine.
Wanawake wanapenda kuwa na wanaume jasiri na washindi.
Wanawake wana sehemu kubwa ya kuchagua kuliko wanaume.
Mwanamke mmoja wa kawaida tu anaweza kuwa anafukuziwa na wanaume hata watano.
Lakini mwanaume mmoja anaweza asifukuziwe na mwanamke hata mmoja.
Inapelekea hata ukiachana na mwanamke tayari ana mbadala wako, wakati we unabaki kuhangaika kurudiana naye. Ili kuweka mchezo sawa nawe ni muhimu uwe na mbadala pia. Usibaki ukaumia.
Mara nyingi mwanamke ana mtu wa kuchukua nafasi yako. Hata kama asipokuambia. Wewe pia kama mwanaume uwe na mtu wa kuchukua nafasi yake. Unakuta mwanamke wako anachombezana na wenzake sehemu anayoshughulika.
Ujue mbadala wako unaandaliwa.
Sababu kubwa kwamba mwanamke anamheshimu zaidi mwanaume ambaye anajua ana mwanamke zaidi ya mmoja. Anajua akizingua tu ameachika. Mwanamke anapenda kuacha kuliko kuachika, anaogopa kuumia. Hivyo, atajitahidi yeye awe namba moja. Katika kupambania huko, ni vigumu wewe kama mwanaume kuachwa. We kazi yako inakua kumridhisha kulingana na anavyojitolea kwenye mahusiano.
Kila mtu na malengo yake kwenye mahusiano. Mwanaume kuwa na mwanamke zaidi ya mmoja ni jambo la kawaida, pia ni vyema afanye hivyo. Lakini inategemea maamuzi ya mtu binafsi. Hivyo, wakati unaamua angalia sababu hizi. Twende nyuma kwanza, zamani utajiri ulitegemea nguvu ya familia.
Kwahiyo kadri mnavyokua wengi thamani yenu na nguvu yenu inaongezeka na mnaweza kujilinda, kuzalisha mazao mengi vilevile mnaweza kuvamia wanyonge na mkashinda kirahisi. Kibaiolojia tunafahamu kuwa mwanamke ana ukomo wa uzao na mwanaume ana nafasi kubwa ya kuendelea kuzaa hata kama mke wake mmoja akiwa amefikia ukomo, hivyo basi ili kulinda nguvu na utajiri wa familia ilibidi mwanaume aongeze mwanamke amzalie watoto wengine.
Turudi sasa, kilichobadilika sasa ni kwamba hakuna haja ya kuwa na familia kubwa ili uweze kuilinda familia, polisi wapo. Lakini kibaiolojia hakuna kilichobadilika. Bado kama wanaume tunataka kuwa na urithi mkubwa, bado tunataka majina yetu yawe makubwa, bado tuna ile hamu ya kuwa na wanawake wengi. Haijafuka kwenye damu.
Mwanamke mmoja ana mudi tofauti kwenye mwezi.
Wengine husema ‘wanawake hawaeleweki’.
Wanaume wengi hawawezi kuyahimili mabadiliko hayo. Suluhisho ni kwenda kwa mwanamke mwingine hadi mwanamke wa kwanza awe mtulivu amrudie. Wapili nae akiwa na mudi tofauti, atarudi kwa wa kwanza, na mzunguko utaendelea hivyo.
Mwanamke ndiye anayechagua kuwa na mwanaume au la.
Wanawake wenyewe ndio wapo tayari kuwa na mwanaume mwenye wanawake wengi. Japo anaweza asilikubali hili wazi. Sababu, kwake huyo mwanaume ndo mshindi na jasiri kuliko wanaume wengine.
Wanawake wanapenda kuwa na wanaume jasiri na washindi.
Wanawake wana sehemu kubwa ya kuchagua kuliko wanaume.
Mwanamke mmoja wa kawaida tu anaweza kuwa anafukuziwa na wanaume hata watano.
Lakini mwanaume mmoja anaweza asifukuziwe na mwanamke hata mmoja.
Inapelekea hata ukiachana na mwanamke tayari ana mbadala wako, wakati we unabaki kuhangaika kurudiana naye. Ili kuweka mchezo sawa nawe ni muhimu uwe na mbadala pia. Usibaki ukaumia.
Mara nyingi mwanamke ana mtu wa kuchukua nafasi yako. Hata kama asipokuambia. Wewe pia kama mwanaume uwe na mtu wa kuchukua nafasi yake. Unakuta mwanamke wako anachombezana na wenzake sehemu anayoshughulika.
Ujue mbadala wako unaandaliwa.
Sababu kubwa kwamba mwanamke anamheshimu zaidi mwanaume ambaye anajua ana mwanamke zaidi ya mmoja. Anajua akizingua tu ameachika. Mwanamke anapenda kuacha kuliko kuachika, anaogopa kuumia. Hivyo, atajitahidi yeye awe namba moja. Katika kupambania huko, ni vigumu wewe kama mwanaume kuachwa. We kazi yako inakua kumridhisha kulingana na anavyojitolea kwenye mahusiano.