Sababu za kitaalamu na za kisayansi kwanini wanaume waoe wake wengi na waruhusiwe kuchepuka

py thon

JF-Expert Member
Sep 11, 2016
2,471
4,424
1. Takwimu za kidunia zinaonyesha kuna idadi kubwa ya wanawake kuliko wanaume ,wanawake wamewazidi wanaume kwa 20%.Tukichukua ratio kila mwanaume asimame na mwanamke basi 20% ya wanawake watabaki pekee yao,

Je kila mwanaume aoe mwanamke mmoja hawa 20% wataolewa na kusitiriwa na nani? unakuta mwanamke ana miaka 36 yupo single siyo kwamba kapenda ila Takwimu za kidunia zimemfanya awe single.

2. Takwimu zinaonyesha wanaume ndio wanafungwa jela sana tofauti na wanawake, ukienda magereza mbali mbali na kutafuta idadi ya wafungwa basi utaona wafungwa wa kiume wapo wengi kuliko wa kike ,asilimia 90 ya wafungwa ni wanaume na 10% ni wanawake

3. Sababu nyingine ni matukio ya vifo ni wazi kwamba wanaume wanakufa mapema na kwa wingi kuliko wanawake,idadi ya vifo ya wanaume kwenye vita ni kubwa ,

Mara nyingi kwenye vita wanaume ndio hupelekwa mstari wa mbele kupigana na machafuko yote wanaume ndio hupigana na idadi kubwa ya wapiganaji hupoteza maisha pia wanaume hufa sana kwenye ajali kama za pikipiki. Leo hii ukienda hospitali za Muhimbili na Mwananyamala na kutafuta idadi ya waliokufa kutokana na bodaboda basi asilimia kubwa ni wanaume,

Ukienda migodini idadi ya watu wanaofukiwa na vifusi ni wengi, Mapigano baina ya wakulima na wafugaji wanaopoteza maisha wengi ni wanaume bado hatujazungumzia wanaokufa maji kutokana na shughuli za uvuvi . Wanaume pia huongoza kuuliwa kutokana na wizi na ujambazi , Mifano tunayo mingi mamia ya watu huchomwa moto, hupigwa mpaka kufa kutokana na uporaji, ukwapuaji nk na 99% ni wanaume

4. Sababu nyingine ni ongezeko la mashoga ni wazi kwamba kwenye ulimwengu wa sasa wa utandawazi kumekuwepo na matatizo ya wanaume kugeuzwa kuwa wanawake na tumeona mataifa makubwa duniani yakipigania haki za mashoga na kumekuwa na NGOs nyingi zinazopigania haki za mashoga

Kama umebahatika kuona maandamano ya LGTB huko USA hakika utaona msururu wa maelfu ya wanaume mapusti yakipigania haki zao na hata huku Tanzania kuna idadi kubwa ya mashoga ukienda mitandaoni utawakuta wengi tena wengine wanajitangaza wazi, ukienda kwenye njenje, taarabu, klabu nk utakutana na wanaume wasioridhki wengi..

5. Kuna idadi kubwa ya wanaume wasiokuwa na uwezo wa kuzalisha na wana upungufu mkubwa wa nguvu za kiume, Leo hii ukipita barabarani utakutana na matangazo mengi ya kutibu nguvu za kiume, wauzaji wa mihogo mibichi wameongezeka nk, uwepo wa vyakula feki zenye sumu na mafuta mengi yamewafanya baadhi ya watu kupoteza nguvu za kiume na uwezo wa kuzalisha.

6. Ongezeko ya watumiaji wa dawa ya kulevya "mateja". Hakika dunia ya leo imekumbwa na idadi kubwa ya watu wasiokuwa na mbele wala nyuma "mateja" tuchukulie mfano hapa kwetu Tanzania tumeona vijana wengi walioathiriwa na dawa za kulevya walivyopotea, watizame mateja waliopo stendi za mabasi, mitaani walivyochoka na kudhoofika na teja siku zote hawazi mwanamke yeye mwanamke wake ni heroin na teja haoi,

Kuna mateja wa aina nyingi hawa mateja matajiri tuwaache tuwazungumzie mateja wasiokuwa na pesa ambao wanashinda stendi, vibarazani, vichochoroni n.k na wapo wengi sana

*******************************

Takwimu zinasema wanawake wapo wengi kuliko wanaume duniani na shirika la utafiti duniani wamesema wanawake wamewapita wanaume kwa wingi wa 20% ,Leo hii kila mwanaume apewe msichana 1 hakika 20% ya wanawake watabaki single ..

Sasa kama wanawake wapo wengi kwa 20% kuliko wanaume ukijumlisha na ongezeko kubwa la mashoga, idadi kubwa ya vifo kwa wanaume, idadi kubwa ya wafungwa wanaume kuliko wanawake, idadi kubwa ya mateja wasiokuwa na future, idadi kubwa ya watu wasiokuwa na uwezo wa kuzalisha na wenye upungufu mkubwa wa nguvu za kiume. Hakika wanawake wengi zaidi watakosa wanaume..

Kama kiidadi tu wanawake wengi wapo single kutokana na upungufu wa idadi ya wanaume, je vipi factors 5 hizo zingine si itakuwa hatari zaidi ,ongezeko ya wanawake wengi kuwa single itakuwa kubwa zaidi

NB: Ewe mwanamke ukimuona mwanaume wako anachepuka usikasirike sababu wanawake wenzako pia wanahitaji kusitiriwa sababu nature wanaume wapo wachache sana je wewe ukiwa mchoyo wenzako watapata huduma wapi na pia watakuwa single milele

Pia nashauri wanaume tuoe wanawake wengi au tuchepuke sababu demand ya wanaume ni kubwa ,supply ni chache kutokana na scarcity ya wanaume iliyopo ..hivyo tusipo oa wengi na kuchepuka tutakuwa hatuwatendei haki wanawake
 
Hiyo sababu ya kwanza ni uongo mkavu! hakuna gender deffernce ya 20%.

Sababu ya pili ni kweli na ni kwa sababu wanaume wana homoni ya Testosterone inayowafanya kuwa wakatili na waovu kuliko wanawake.

Hauhitaji kuwa na sababu ili kufanya kitu unachokipenda.........kama unapenda kuchepuka ni sawa tu.
 
Pumba tupu !! Lazima wanawake wawe wengi, hebu piga picha endapo wanaume ndio tungekuwa wengi kuliko wanawake ingekuwaje?? Nadhani wababe tuu ndio wangeoa
 
Siku ngumu sana kwa wazinzi: Pale mwenza halali na jambazi (mchepuko) wanapodai haki sawa leo # *ValentinesDay*
 
Kuna Wanawake Wasagaj Pia,wanawake Mastista ni wengi kuliko mapadri,wanawake wanakufa wengi kwa uzazi na kansa ya uzaz na matiti!
Kwanin Kuna Mwanamke Mmoja Anakua na wanaume zaid ya mmoja!?
The world is nt fair, hata useme wawe na wanawake kumi bado wapo watakaobaki!
tukirud kwenye uhalisia wa sasa mitandao ya kimapenz ni hatari sana kueneza magonjwa yatokanayo na zinaa!Na ndicho chanzo cha vifo ving vya wanaume na sababu ya kuongezeka wajane mitaan life style ya michepuko inawamaliza sana wanaume
Pia wanaume wa siku hz kumridhisha na kumhudumia mwanamke mmoja tu mtihan akiwa nao wawil watatu si ataishia kuadhirika tu!twende na uhalisia "You Cant Solve Everyone's Problem On Earth"
 
Hao wanawake Wemgi wako wapi? Mbona kila mtu ansema na mtu wake? Kadem unakasotea weee utafkiri enzi hizo
 
Back
Top Bottom