Heaven Sent
Platinum Member
- Sep 27, 2013
- 32,719
- 98,386
Swadaqta Khaswa..!! hiyo umeiweka faswaha na kuvunja ukimya mwanaume "SEMA UKITAKACHO na uigharamie walau 50%" utapata zaidi ya nje !! (unazopeleka kwa michepuko siulete nyumbani kwako?)
Mwanaume kaa ujue una watoto wa damu na nyama yako, wanahitaji MALEZI,MATUNZO,HOME-WORK na majukumu hayo yapo mgongoni mwa MKEO (mama watoto wako) !!
mengine malizieni.........
FarePlay Geniustin
Umeona sasa, yani kuna familia zinaishi kwa tabu kuliko maelezo kwa sababu tu baba kakolezwa na michepuko so hajali tena familia yake. Watoto wanaishi kama hawana baba, wanakosa Upendo wa baba na matunzo pia.
Ukiacha tu hilo, kuchepuka kuna gharama zake. Mnawaletea wake zenu magonjwa ndani. Msipowaletea basi mtaanza kuumwa wee, na michepuko mingi hainaga muda wa kumuuguza mtu. Nepi kavalishwe kwa mkeooo
Michepuko mingine ni washirikina kupitiliza, wataroga hadi watake kumuua mkeo maskini afu watoto ndo wataoteseka zaidi
Mnahonga huko Nje hadi mnabaki na suruali tu, michepuko itawafukuza afu mnarudi kwa wake zenu bila cent na aibu juuu
Yani Hamna ndoa isiyo na matatizo. Na kuna Vitu vichache kwenye ndoa vinabadilika kadri mnavyozidi kuishi. Cha muhimu ni kuwa tu muwazi kwa mwenzako. "VUNJA UKIMYA". Utachepuka hadi lini?
Last edited by a moderator: