Sababu 5 CCM Kushinda Uchaguzi 2015

Sababu 5 CCM Kushinda Uchaguzi 2015

CHERISTIAN CHURCH MOVEMENT (CCM) Ni chama safi kabisa kwa sababu na KIKWETE hajawahi kutokea mfano wake kwa mamba makubwa alioyafanya na anayondelea kuyafanya, mfano;
1. 2005 sembe 250. 2012 sembe 1000.
2. 2005 nauli DAR-MLANDIZI 600. 2012 Nauli 1900.

Ilmu ya uchumi ni muhimu sana kwa jamii ili kuondoa masuala ya kitoto kama haya.

Pole sana

 
Ilmu ya uchumi ni muhimu sana kwa jamii ili kuondoa masuala ya kitoto kama haya.
Pole sana

Raisi wako mwenyewe mchumi lakini hali halisi ndio hiyo. Hatuhitajiki watu wote kuwa wachumi ili kujua kwamba hali ya ugumu wa maisha imepanda au imeshuka. Lakini kadri tunavyokwenda madukani na masokoni tunajua kwamba wachumi na watawala wameshindwa kuiongoza nchi kwa manufaa ya wananchi wenyewe, ikiwa ni pamoja na kushindwa kudhibiti mfumko wa bei za bidhaa.
 
Hahaha Elizabeth Dominic , nawachemsha tu wana Jf, I hate politics, sina chama, na sikuwahi kupiga kura
toka nizaliwe, BTW how was Diwali?? Juzi nilidhani nchi imevamiwa, baruti zilipopigwa usiku,jirani zangu wengi ni Baniani
Bro umesema hukuwahi kupiga kura toka uzaliwe. Kura haina uhusiano na kuipenda au kutoipenda siasa, Kura yako ni haki yako uwe mwanasiasa au raia wa kawaida. Kwanini hutaki kujiuliza swali dogo tu kuwa mbona wakati wa kupiga kura hatuendi kujitambulisha kwa kadi za vyama vyetu instead tunakuwa na kitambulisho cha kupigia kura anachopewa kila raia mwenye sifa ya kupiga kura???Kumbe wewe ndo unatucost. Ni aibu kuongea hadharani kuwa wewe hupigagi kura, hii nsawa kabisa na mtoto wa kiume kutamka hadharani kuwa hujatairiwa. Huo ni umaamuma!!
 
ccm hata kama ijijenge vp haitrudi kuwa chama chenye amani tanzania, wanaodanganyika ss hivi ni wale wlarushwa tu but watanzania wengi sasa hivi hawadanganyiki
 
Matola
Acha matumizi mabaya ya lugha wewe ni mchuuzi tu bado hujawa mfanyibiashara kulipa vibarua ndio unataka kujigeuza mfanyibiashara?


Chama
Gongo la mboto DSM
Whatever you want to call me, ila kuna watu wanaoniita Boss. Nina nambari ya Mlipa kodi na nina leseni ya Biashara na siyo leseni ya uchuuzi.
 
Ilmu ya uchumi ni muhimu sana kwa jamii ili kuondoa masuala ya kitoto kama haya.

Pole sana

Ni kweli nakuunga mkono, maana hata yule Mchumi namba moja Duniani Profesa Alhaj Pumba alituambia pale Jangwani CUF ikiingia madarakani atatugawia pesa bure Watanzania kutokana na raslimali zetu kama inavyofanyika kwenye moja ya jimbo pale Marekani.
 
Ni kweli nakuunga mkono, maana hata yule Mchumi namba moja Duniani Profesa Alhaj Pumba alituambia pale Jangwani CUF ikiingia madarakani atatugawia pesa bure Watanzania kutokana na raslimali zetu kama inavyofanyika kwenye moja ya jimbo pale Marekani.

Kwani hilo unafikiri haliwezekani?

Hata Padre Dr Slaa alisema akichaguliwa kuwa Rais atashusha bei ya vifaa vya ujenzi.

Hayo yote yanawezekana kabisaaa cha msingi ni watu kuwa wazalendo na kuwa na sera thabit za kudhibiti mapato ya nchi na kuyatumia kwa manufaa ya wote.

hakuna kinachoshindikana kwani Tanzania mumejaaliwa kila kitu kuanzia Ardhwi safi yenye rutba, madini, gas na mafuta, hali ya hewa nzuri pamoja na utulivu wa kisiasa na amani ya woga.



 
Raisi wako mwenyewe mchumi lakini hali halisi ndio hiyo. Hatuhitajiki watu wote kuwa wachumi ili kujua kwamba hali ya ugumu wa maisha imepanda au imeshuka. Lakini kadri tunavyokwenda madukani na masokoni tunajua kwamba wachumi na watawala wameshindwa kuiongoza nchi kwa manufaa ya wananchi wenyewe, ikiwa ni pamoja na kushindwa kudhibiti mfumko wa bei za bidhaa.


Hapo unachozungumzia ni SERA na sio mtu. Kumbuka kama utasoma Uganda, Rwanda na kenya somo la uchumi unaanza kufundishwa toka ukiwa skuli za msingi na kuendelea nalo mpaka chuo Kikuu.

Somo hili linawekwa ili kuwapa watu ujasiri na dhana ya KUJIAJIRI na SIO kusubiri kuajiriwa baada ya masomo yao. Kama mtu angelisoma somo hilo sifikirii kama angeuliza au kuandika vile alivyoandika.

Kumbuka kuwa BOttom line ya kitu chochote ni UCHUMI BORA (pesa) na SIO siasa bora kama mlivyo wa Tz.

NB: Nyerere aliwadanganya ili muendelee mlikuwa mnahitaji vitu vinne yaani watu, ardhwi, siasa safi na uongozi bora. sasa jiulizeni mumekosa kitu gani mpaka kila siku mnazidi kuwa nchi masikini duniyani?
 
kumbuka kwa mara ya kwanza udini umeasisiwa na JK wakati wa kampeni 2010 matunda yake yameonekana mwaka huu watu wanachoma makanisa na kukujolea msaafu huu ni uongozi wa ccm ndugu ccm imepoteza maadili ya kulinda amani ya tanzania.
 
Wajinga ndo waliwao.Mtu mwenye akili hawezi kwenda CCM,labda kama umekwapua mali za umma.
 
Hayo ni maneno ya wimbo wa komba...

Bila chama cha mapinduzi nchi ingekuwa wapi?
Bila Chama cha mapinduzi upinzani ungetoka wapi?
Bila chama cha......


Hebu tusaidiane kutafakari huu ujumbe wa kimyopic....unaodhihirisha upeo finyu wa CCM hawajui kama kuna nchi zinasonga mbele na hakuna kitu inaitwa CCM.
Wamenikera mbaya kwa kulemaza waTZ waendelee kufikiri within the box of CCM
 
Waheshimiwa huu ni wimbo wa Kapteni J.Komba aliouimba hivi punde baada kutangazwa matokeo ya uchaguzi ya wajumbe wa NEC toka bara na visiwani na ngazi ya Mwenyekiti na makamu wake wawili ambapo kwa kifupi kwa ngazi ya makamu M/kiti visiwani Dr. Shein kapata kura 100% na bara Mh. P.Mangula kapata kura 100% wakati M/kiti Taifa akishinda kwa kishindo kwa 99.92%. Mwisho Mh.Komba baada kuweka vikolezo mbalimbali katika wimbo huo anasema Chama kiheshimiwe! Kazi kwenu wadau CCM imetutoa mbali jamani!
 
Ndugu zangu ni vizuri kuambiana mambo ya msingi haswa linapokuja swala la hatma ya Taifa letu.
Tanzania ni nchi ya kipekee duniani na watu wake ni wa kipekee pia, utu wetu , utanzania wetu huwezi pata sehemu nyingine. Watanzania ni watu wenye upendo, amani na mshikamano huwezi linganisha na nchi yoyote ile. Tumekuwa tukiishi siku zote kwa amani, kupendana na kushirikiana kabla na hata baada ya kuasisiwa taifa letu. Lakini baada ya kuingia siasa za upinzani nchini mwetu , kumekuwa na fikra zenye kuhatarisha amani yetu. Hatukatai upinzani, ndio maana kumekuwa na vyama vingi vya siasa nchini Tanzania. lakini kamwe hatutaruhusu amani yetu kupotea na siasa za kutubagua. Hadi hapa, Amani na maendeleo yaliyopoTanzania yametokana na uongozi wa chama cha mapinduzi. Kuanzia kwa wazee wetu waasisi, na viongozi wetu wakiongozwa na Mwenyekiti wetu, Rais wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. Kwa siasa safi na uongozi makini, Sina budi kuzitaja sababu 5 kwa nini chama cha mapinduzi kitashinda uchaguzi wa 2015.

Moja; CCM imeweza kulinda na kudumisha Uhuru wa Nchi yetu na raia wake.
Muhimu kwa watanzania wote kukumbuka kwamba chama cha mapinduzi hakina udini wala ukabila kwa misingi hiyo kimeweza kudumisha amani na umoja wa nchi yetu.

Mbili; CCM imekuwa ya kwanza katika ushirikishwaji wa watanzania wote walio nje ya nchi katika kutoa mchango wao ili kuleta tija na maendeleo ya taifa letu.

Tatu; CCM imehakikisha kwamba Nchi yetu inatawaliwa kwa misingi ya kidemokrasia. Nchini Tanzania kuna demokrasia ya kutosha na hata kupitiliza. Mwananchi yoyote anao uhuru wa kuishi, kuabudu na kufanya maamuzi apendayo ili mradi sheria za nchi zinazingatiwa.

Nne; CCM haina ubaguzi, kila mtu anayo nafasi. Chama cha mapinduzi siku zote kimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba Serikali na vyombo vyote vya umma vinatoa nafasi zilizo sawa kwa raia wote, wanawake na wanaume bila kujali rangi, kabila, Dini, au hali ya mtu.

Tano; CCM iko mstari wa mbele katika kuimarisha uhusiano mwema na Vyama vyote vya Siasa vya Nchi nyingine vyenye itikadi kama ya CCM ambavyo kweli vinapinga Ukoloni, Ukoloni Mamboleo, Ubeberu na Ubaguzi wa aina yoyote.

View attachment 70958
Source: Vijimambo

Bila hawa Manyang'au nchi hii ingekuwa inatiririka Mana na Asali. Hebu angalia wanavyo tuibia kila kona.
 
Whatever you want to call me, ila kuna watu wanaoniita Boss. Nina nambari ya Mlipa kodi na nina leseni ya Biashara na siyo leseni ya uchuuzi.

Matola
Kuwa na leseni ya biashara ni hoja? Hata machinga wanazo; wewe ni mchuuzi tu matola usitafute kujikweza; kuuza fulana za Chadema tangu lini ikawa biashara?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
. .....kwanza kabisa Boflo.nakupongeza kwa kuanzisha thread kwenye jukwaa la siasa........ .

Pili unaiongelea ccm ya mwaka gani? Ya nyerere au ccm hii ya ufisadi na kulindana.....??

Of course 2015 ccm itashinda uchaguzi, lakini haitoshinda kwa kura za wananchi..................ila itashinda....lazima ilinde maslahi yake (hapa nazungumzia wanachama wake wakubwa hususan viongozi) kwa hali na mali.......
 
Last edited by a moderator:
CCM Haishindi ila inaiba kura kwa sababu hizi:
1.Tume ya Uchaguzi ni Wakristo na CCM watupu.
2. Police wote in CCM
3. Jeshi wote ni CCM
4. Mahkama zote ni CCM
5.Media zote Ni CCM
 
Back
Top Bottom