S400 missile systems mbioni kutua Uturuki

S400 missile systems mbioni kutua Uturuki

Ni kweli uturuki ni mwanachama wa nato but km utakuwa makini kwa siku za hivi karibuni relationship ya uturuki na EU imeshuka kwa kasi kubwa mno, siku ya Jana km nitakuwa sijakosea rais wao kawasemea mbovu EU

Sent from my GT-I9152P using JamiiForums mobile app

EU sio NATO na NATO si EU
Hakuna ulazima wa kuwa EU au NATO
Turkey anataka akubaliwe aingie EU
Turkey hawezi ondoka NATO
 
Hapa nawaza vitu 3

1.Turkey ni mwanachama wa NATO so anaweza kuleta mgogoro na NATO kama hakuna mpango mwingine nyuma ya pazia kwaio NATO wanaweza pata wasiwasi na Turkey na kuhisi hafai sababu sio mwanachama mtiifu


2.Pia nahisi Urusi hawezi kua mjinga kiasi hicho kumpa siraha nzito zaidi kwenye mfumo wa ulinzi wa taifa lake mwanachama wa NATO,nahisi kuna vitu Urusi atavibadirisha kidogo ili kuficha baadhi ya vitu

3.Yawezekana Turkey anatumia njia hii kuwaumiza EU sababu wanamsumbua sana kuhusu uanachama,pia kwa wanaofatilia Turkey ndie mwanachama wa NATO ambae mara nyingi ua ana amua mwenyewe mambo yake bila kupelekeshwa na NATO,kwa kifupi Turkey sio mtiifu sana kwa NATO

Maoni yangu binafsi:Urusi sio mjinga,kuna kitu anataka kuwachezea NATO na pia labda ana Tech nyingine
 
For
That's peanut money compared to that of Trump to Saudia's worth USD 350 bn/= the largest ever in mankind history.

Alaska yenye ukubwa wa 1.718 sq. km (almost twice the size of TZ) US aliinunua kutoka kwa warusi for just 7m/-
just 7m..!!uezi jua thamani ya hio pesa kwa miaka hio ilikuaje
 
EU sio NATO na NATO si EU
Hakuna ulazima wa kuwa EU au NATO
Turkey anataka akubaliwe aingie EU
Turkey hawezi ondoka NATO
turkey anaweza asiondoke NATO,hupo sahihi kabisa lakini Turkey anaweza asiwe mwanachama mtiifu kwa NATO kama ilivo Poland
 
Lakini hii deal ya S400 haijaanza leo,ni tangu Nov 2016,saivi wanakamilisha deal,na pia nadhani inasababishwa na mahusiano mabaya ya miaka ya karibuni kati ya Uturuki na ndugu zake NATO

Lakini pia Urusi anadeal la kuuza hizi kitu kwa China na India
 
That's peanut money compared to that of Trump to Saudia's worth USD 350 bn/= the largest ever in mankind history.

Alaska yenye ukubwa wa 1.718 sq. km (almost twice the size of TZ) US aliinunua kutoka kwa warusi for just 7m/-

Alaska iliuzwa mwaka 1867 mbona hilo ulisemi au unafikiri thamani ya Dola ya karne ya 18 ni sawa na karne ya 21?
 
Halafu sijui kwa nini Urusi hajifunzi yani... Maana ile S300 ya Ugiriki Israel na NATO kila siku wanaifanyia mazoezi kutafuta countermeasures zake.
Leo wanawapa Turkey S400 sitashangaa baada ya miaka 5-10 nikaona S400 ikiwa mazoezini na Marekani na NATO kiujumla ikiwemo Israel

Mambo mengine fanyeni utafiti kwanza, je, unajua kuna version ngapi za S-300? Nani kawambieni kwamba export version ya S-300 ni sawa sawa na inayo tumiwa na jeshi la Urusi!! FYI Warusi si wajinga kama unavyo wafikiria wewe, walijua wakiwauzia Wagiriki Air Defence System type S-300 bila shaka Israel na Amerika watakuwa na shahuku kubwa ya kujua inavyo fanya kazi ili wabuni mbinu za kui-defeat.

Soma taarifa za Israel na marafiki zake wanasema nini kuhusu uwezo wa S-300 iliyo nunuliwa na Wagiriki kutoka Urusi, Israel imejaribu mara lukuki kui-jam lakini walishindwa - wanakiri kwa kauli yao kwamba walikuwa wanawazuga Wagiriki kwa kujidai wafanye mazoezi ya kijeshi kwa pamoja kumbe lengo lao ni kutafuta mbinu za kutumia ECM zao ku-blind S-300, Waisrael wanasema mbinu zote walizotumia bado radar za S-300 zilikuwa zinatrack ndege zao hivyo zingekuwa rahisi kutunguliwa na missile za S-300.

Kumbuka S-300 waliyo wauzia Wagiriki ni export version i.e a watered down Defence System, kama Wayahudi na Uncle SAM hawajapata jibu la ku-defeat export version ya S-300, je, version inayotumiwa na jeshi la Urusi ndiyo wataiweza? labda watumie mbinu za kupora system nzima nzima kutoka kwa Wagiriki kama walivyo fanya wakati wa vita 1973 kwa kupora SAM-6 iliyo kuwa inatumiwa na Waarabu, licha ya kufanikisha uporaji huo yet it took Israel and US six years kuelewa SAM-6 inavyo fanya kazi - je,wakifanikiwa kupora S-300 itawachukua miaka mingapi kupata dawa yake - jibu unalo. Hata Turkey ikinunua S-400 mambo yatakuwa yale yale - watauziwa a watered down version ambazo hazitumiwi na jeshi la Urusi, hata Uturuki ikirubuniwa na Uncle SAM na Israel kwamba wastrip S-400 to bare bones ili waichunguze inavyo fanya kazi, Russians won't mind watabaki wanawacheka tu kwa kutapa tapa kwao.

Ukweli wa mambo Warusi wanajiamini ndiyo maana uwezi kusikia hata siku moja wanangahika kuiba au kununua ndege za kivita za Uncle SAM au silaha zao zingine na kwenda kufanya reverse engineering - tafuteni historia inayo eleza mbinu zilizo tumiwa na Amerika kuiba ndege za Warusi na kuzisafirisha kwa meli mpaka USA na ushahidi hupo - mfano: MiG-15, MiG-17, MiG-19, MiG-21 mwaka 1976 MiG-25 - Miaka ya hivi karibuni walinunua MiG-29 karibu 26 walinunua tena ndege za vita 19 aina ya Sukhoi-27 - ndege zote tajwa hapo juu zilinunuliwa kutoka katika nchi za Ulaya ya mashariki zilizo kuwa zinahunda SOVIET ya zamani - Taifa linalo jiamini aliwezi kuangahika kupora pora ndege na silaha nyingine za washindani wake kwenda kuzichunguza zinavo fanya kazi na kuishia ku-copy copy tu na mbwembwe chungu mzima.
 
Ni kweli uturuki ni mwanachama wa nato but km utakuwa makini kwa siku za hivi karibuni relationship ya uturuki na EU imeshuka kwa kasi kubwa mno, siku ya Jana km nitakuwa sijakosea rais wao kawasemea mbovu EU

Sent from my GT-I9152P using JamiiForums mobile app
Wazungu wanafiki Leo wanaweza kuwa adui kesho rafiki.Ref,Mohd Gadaffi walivyomgeuka kama hawamjui!
 
For

just 7m..!!uezi jua thamani ya hio pesa kwa miaka hio ilikuaje
Regardless ilikuwa mwaka gani bado wataalamu wengi hadi leo wana-challenge offer husika; was too little money. Hii ni kuonesha mrusi ni wa vidili vidogo dogo sana.
 
Halafu sijui kwa nini Urusi hajifunzi yani... Maana ile S300 ya Ugiriki Israel na NATO kila siku wanaifanyia mazoezi kutafuta countermeasures zake.
Leo wanawapa Turkey S400 sitashangaa baada ya miaka 5-10 nikaona S400 ikiwa mazoezini na Marekani na NATO kiujumla ikiwemo Israel
Njaa kaka! Hata hiyo miaka mitano mingi; soon watalifanyia reverse engineering kila kitu kitakuwa hadharani. Kama waajemi ndio wanaringishia hilo waandike maumivu; limewafikia US, Israel, na NATO indirectly.
 
Ili dunia iwe salama ni lazima marekani na urusi ziondoke kwenye dunia maana wao ndo wauzaji wakuu wa siraha
Zikiondoka USA na urusi kuna Yale maninja au majahedeen yatatutesa sana kutaka dunia nzima tuwe majahedeen
 
Moja ya majukumu ya iliyokuwa KGB ilikuwa ni kuiba technology mbali mbali hasa kutoka nchi za magharibi.

Low Observable (Stealth) technology, ni moja ya teknolojia iliyoibwa na warusi toka Marekani. Wizi huu wa teknolojia ni jambo la kawaida mno kwa haya mataifa yaliyoendelea.
 
Mambo mengine fanyeni utafiti kwanza, je, unajua kuna version ngapi za S-300? Nani kawambieni kwamba export version ya S-300 ni sawa sawa na inayo tumiwa na jeshi la Urusi!! FYI Warusi si wajinga kama unavyo wafikiria wewe, walijua wakiwauzia Wagiriki Air Defence System type S-300 bila shaka Israel na Amerika watakuwa na shahuku kubwa ya kujua inavyo fanya kazi ili wabuni mbinu za kui-defeat.

Soma taarifa za Israel na marafiki zake wanasema nini kuhusu uwezo wa S-300 iliyo nunuliwa na Wagiriki kutoka Urusi, Israel imejaribu mara lukuki kui-jam lakini walishindwa - wanakiri kwa kauli yao kwamba walikuwa wanawazuga Wagiriki kwa kujidai wafanye mazoezi ya kijeshi kwa pamoja kumbe lengo lao ni kutafuta mbinu za kutumia ECM zao ku-blind S-300, Waisrael wanasema mbinu zote walizotumia bado radar za S-300 zilikuwa zinatrack ndege zao hivyo zingekuwa rahisi kutunguliwa na missile za S-300.

Kumbuka S-300 waliyo wauzia Wagiriki ni export version i.e a watered down Defence System, kama Wayahudi na Uncle SAM hawajapata jibu la ku-defeat export version ya S-300, je, version inayotumiwa na jeshi la Urusi ndiyo wataiweza? labda watumie mbinu za kupora system nzima nzima kutoka kwa Wagiriki kama walivyo fanya wakati wa vita 1973 kwa kupora SAM-6 iliyo kuwa inatumiwa na Waarabu, licha ya kufanikisha uporaji huo yet it took Israel and US six years kuelewa SAM-6 inavyo fanya kazi - je,wakifanikiwa kupora S-300 itawachukua miaka mingapi kupata dawa yake - jibu unalo. Hata Turkey ikinunua S-400 mambo yatakuwa yale yale - watauziwa a watered down version ambazo hazitumiwi na jeshi la Urusi, hata Uturuki ikirubuniwa na Uncle SAM na Israel kwamba wastrip S-400 to bare bones ili waichunguze inavyo fanya kazi, Russians won't mind watabaki wanawacheka tu kwa kutapa tapa kwao.

Ukweli wa mambo Warusi wanajiamini ndiyo maana uwezi kusikia hata siku moja wanangahika kuiba au kununua ndege za kivita za Uncle SAM au silaha zao zingine na kwenda kufanya reverse engineering - tafuteni historia inayo eleza mbinu zilizo tumiwa na Amerika kuiba ndege za Warusi na kuzisafirisha kwa meli mpaka USA na ushahidi hupo - mfano: MiG-15, MiG-17, MiG-19, MiG-21 mwaka 1976 MiG-25 - Miaka ya hivi karibuni walinunua MiG-29 karibu 26 walinunua tena ndege za vita 19 aina ya Sukhoi-27 - ndege zote tajwa hapo juu zilinunuliwa kutoka katika nchi za Ulaya ya mashariki zilizo kuwa zinahunda SOVIET za zamani - Taifa linalo jiamini aliwezi kuangahika kupora pora ndege na silaha nyingine za washindani wako kwenda kuzichunguza zinavo fanya kazi na kuishia ku-copy copy tu na mbwembwe chungu mzima.
Mkuu kwani nani kasema kwamba export version inakua sawa og version inayotumiwa na nchi husika?!.Hata THAAD iliyopo Korea sio sawa na anayotumia Marekani na hata Barak 8 aliyouziwa India na Israel sio sawa na anayotumia mwenyewe Israel. Kila mtu anajua kwamba export versions zinakua downgraded ili zisifanane na ya nchi husika.

Taarifa za Israel na S300 nimezisoma nyingi sana na sijawahi ona mahali eti panasema Israel walishindwa kuijam S300 maana kama kawaida Israel hawanaga huo mtindo wa kutoa taarifa kamili ya nini kinachojiri maaana hata kwenye hayo mazoezi walikataa uwepo wa S300.Ila me nilichooona ni maelezo ya kamanda mmoja wa Urusi akieleza kuhusu hayo mazoezi ya Israel Vs S300,alikua akisema kwamba ukishajua jinsi hyo system (S300) inavyofanya kazi bhasi ushamaliza kila kitu maana una uwezo wa kuichezea itakavyo,mfano signal za radar zikija una uwezo wa kuzireplicate baada ya rada kuona ndege moja inaweza kuona mamia ya ndege hivyo kushindwa kuamua waitungue ipi au waache ipi. Au unaweza kuifanya rada ikuone kama ni friendly jet hivyo isioneshe uwepo wa ndege yoyote ile ngeni/adui na ndo hichi Israel amekua akifanya Syria kila siku maana hata baada ya Iran kubadili codes za S200 sijui lakini bado ndege za Israel zimekua zikiingia na kutoka Syria kila siku bila response yoyote ile toka Syria.Refer operation mbalimbali za Israel ndani ya Syria kuanzia Operation Mole Cricket, Operation Orchard, nk.

Kama nilivyoeleza huko juu export version haiwez fanana na og(domestic version) version. Hata hyo S400 ya Turkey haiwez fanana na anayotumia Russia.

Hakuna cha kujiamini wala nini, wote Russia na Marekani wanaibiana technology sema tu US ana pesa hivyo kwake inakua rahisi kurubuni maofisa wa Urusi na kupata anachokitaka. Rejea WWII ,warusi walikua wanataka Bombers ambazo zitakua na uwezo wa kupiga mabomu mengi na kusafiri umbali mrefu kama vile ilivyokua kwa Marekani (kipindi hicho US walikua wakitamba na B-29 iliyoangusha nuclear Japan). Marekani ilikataa kuwauzia USSR ndege yao hyo ya B-29 chini ya Lend-Lease policy(unaweza kuisoma hata Google) lakini mwaka 1944 B-29 ilitua kwa dharula ndani ya Soviet hapo kwa warusi ikawa mbuzi kafia kwa muuza supu. Marekani waliiomba USSR ilirudishe ndege yao lakini Soviet ilikataa wakaifanyia reverse engineering wakatoa yao TU-4.
2b48fea27b9c16e6fbfd3bd105f5fe0b.jpg
US B-29 bomber
38c8baa0b265ae3e5d3d3a1fcab662dc.jpg
Soviet Tu-4 bomber

Pia rejea kwenye vita ya Kosovo ambapo F-117 iliangushwa kule Serbia ambapo mainjinia wa kichina walikua wakizunguka Serbia kwa wanakijiji wakinunua mabaki ya F117 na kuyapeleka Uchina kusoma technology ya stealth ya mmarekani.
Hivyo kwenye hili la kuibiana technology sio geni baina ya US na Russia.
 
Moja ya majukumu ya iliyokuwa KGB ilikuwa ni kuiba technology mbali mbali hasa kutoka nchi za magharibi.

Low Observable (Stealth) technology, ni moja ya teknolojia iliyoibwa na warusi toka Marekani. Wizi huu wa teknolojia ni jambo la kawaida mno kwa haya mataifa yaliyoendelea.
Na mpaka leo China na Russia hawajaweza kuimaster vizuri hii technology na kuiapply kwenye ndege zao kama Marekani.
Fuatilia mgogoro wa India na Russia kuhusu ndege yao ya ushirikiano T-50 ,wahindi wanaiponda hiyo ndege wanasema sio 5th generation fighter bali ni 4.5 generation fighter.
 
Na mpaka leo China na Russia hawajaweza kuimaster vizuri hii technology na kuiapply kwenye ndege zao kama Marekani.
Fuatilia mgogoro wa India na Russia kuhusu ndege yao ya ushirikiano T-50 ,wahindi wanaiponda hiyo ndege wanasema sio 5th generation fighter bali ni 4.5 generation fighter.
mkuu mbona unatuongopea izo data umezitoa wapi,PAK TA(T-50) ni ndege ya mrusi peke yake ilo ya ushilikiano na India inaitwa Sukhoi/HAL FGFA.na mpaka leo hii india bado awajatoa pesa ya kuendeleza iyo project kwa iyo kuna uwezekano project yenyew ikawa imekufa.
 
Njaa kaka! Hata hiyo miaka mitano mingi; soon watalifanyia reverse engineering kila kitu kitakuwa hadharani. Kama waajemi ndio wanaringishia hilo waandike maumivu; limewafikia US, Israel, na NATO indirectly.
nani kakwambia warusi wana njaa?
 
Back
Top Bottom