Rwanda inatuwashia double indicator & full Light, CCM ondokeni hatuwataki

Rwanda inatuwashia double indicator & full Light, CCM ondokeni hatuwataki

East African Eagle, na wote mnaojarb kupinga maendeleo ya mji msafi wa kigali, et kigal co rwanda, hv na cc mbna serikal inatumia maguv kuijenga dar lakn bado dar n jij chafu, lisilo na plan nzur mafuriko kila leo? kwann mnakua na wivu wa kike kwa waafrika wenzenu wanaopiga hatua za maendeleo, katk uwepo wa ccm tusahau maendeleo ya miji, Delete Maccm
 
Hii ni neema ya mungu,, Ni wapi hapo tumetumia akili zetu,, hiyo ni fukwe ambayo tumepewa na mungu Sasa sijui unataka kusema nini!!!
Ujue dada toka tumepata uhuru, maendeleo yetu hayalingani na muda ambao CCM imekaa madarakani,,, toka 1961 bado tunajenga barabara, shule, maabara, nk... Yaani namaanisha toka 1961 mpaka leo bado miundombinu mibovu,elimu duni, huduma za afya shida,,,
kimsingi hata barabara zinazojengwa ni 10yrs life span,,,, tunapolalamika nikwamba tunauchungu na wachache wanaoitafuna hii nchi kwa manufaa yao na familia zao...
dada umeshawahi kupita kwenye hizi barabara zinazojengwa na wachina ukajionea Mwenyewe maisha ya hizi barabara???

Hebu tazama vizuri picha iliyowekwaa halafu unieleze viko wapi? hizo ni ndoto za alinacha. Tunajivunia tulichonacho sasa hivi ndiyo majaaliwa yetu tuliyojaaliwa na Mwenyeezi Mungu.

Sikutaka kukuonesha majumba na mabarabara tuliyonayo sasa hivi, ambayo pia ni kwa neema za Mwenyeezi Mungu, na mengine tuliyonayo hakuna katika Afrika ya Mashariki na kati. Nakumbuka kauli ya Magufuli, barabara za mali zilizopo sasa hivi Tanzania zikihamishiwa Rwanda, basi Rwanda yote itakuwa hakuna pa kujenga wala kulima, tutaifunika, unayajuwa hayo?

Ikiwa projections za miji tu, Jee, hujapitia vizuri hii nyuzi na kuziona projection zetu?

Tujivunie tulivyonavyo sasa hivi, iwe majumba, mabarabara, watu, fukwe, mbuga za wanyama na mengineyo yawayo, yote ni shani yake Mwenyeezi Mungu.

Tusianze kuota ndoto za alinacha kushindana na picha za kubuni za vitu visvyokuwepo. Tutakuwa majuha na mapunguani kama mleta mada.
 
Tujivunie umaskini kama huu? Kweli???? We ndiye msukule namba moja
untitled+of+tz.jpg

Copy-2-of-Mr.-Simango-holding-baobab-shell-600x402.jpg

Hizo picha zisikustuwe, utakuta mwanawe huyo mmoja wa wakurugenzi wa chadema, yeye anakula bata mzee wake kamsahau.
 
Nilicho nacho kipi ,UFISADI ? au MAFISADI ? Tz haijawahi kukumbwa na vita ndani ya nchi vya kuwawa kwa maelfu ,kilichotokea Rwanda kinajulikana ,leo hii katika muda mfupi sana wamefanikiwa kuona wanakokwenda na matarajio ,Hapa Tz ni kiza huko tuendako matumaini yanakatishwa kila siku skendo jipya,wala hulijui mwisho wake,linafifia kiajabu ajabu ,walewale wanaotuhumiwa na kuondolewa wadhifa ndio wale wale wanaobandikwa vyeo na wengine kuthubutu hata kugombea Uraisi ,sijui wanataka kuja kulipiza kisasi ?(SMS)

Hizo ni porojo na kuhororoja, hakuna wakati Tanzania ina muelekeo wa inakokwenda kama leo hii, na ndiyo maana unaona viongozi wa mataifa makubwa makubwa wakimiminika hapa kwani wanajua kuna muelekeo.
 
sioni sababu ya kutoa povu jingi unless unaishobokea rwanda ovyo. hiyo ni plan tu. dar ipo plan ya kigamboni na isitoshe tuna miji mingi kuliko rwanda na sio kwamba miji haina masterplan

Cjui unaelewa inaposemwa Masterplan ? In a short time wameweza kutoa muelekeo ,leo hii RwandaAir inasafirisha abiria wa Tz kutoka nchi za nje ,ipo wapi AirTanzania ? Au plan yake hamnayo ? mshaipiga tagi ,moyo ulinigonga sana kuona RwandaAir ikituletea abiria ,alitokea kibweka mmoja wa CCM akajisifu kuwa wanajenga viwanja vya ndege vya kisasa katika mikoa ,nilitegemea atasema na AirTanzania imezidisha safari za nchi za nje ,lakini wapi naambiwa hawana ndege hata moja ,wameila mpaka imekufa limebaki jina tu skeleton ,jiulize nini kimepelekea kudhoofika kwa shirika hili ,kilichosababisha ndischo hicho kinachozielekea hospitali za serikali ,chini ya utawala huu wa miccm hakutafufuka kitu ni kufa tu. ,

Tuna miji mingi kuliko Rwanda ,haijulikani hata unataka kusema nini ! Sema Mkoa wa Tanga ni mkubwa kuliko Rwanda ningekufahamu ni rahisi kuendeleza mji mdogo kuliko mkubwa ,yaani hata kujibu mnahitaji akili za kuchangiwa.

Kimbembe watu hatushobokei nchi ingine ,tunapima maendeleo ya tulitotokea,tulichokipokea kwa hao waliotukoloni ,umeona ,sasa maendeleo yetu ukilinganisha na nchi iliyokubwa na vita mfano wa Angola ,sisi ilikuwa tuwepo mbele sana tu, Angola hiyo hapo tumesaidia sana kuipatia uhuru hata watu wetu walikuwepo huko katika kuikomboa nchi ya Angola,tuliowakomboa leo hii wapo wapi ? Sisi ndio kwanza tunapigania ardhi miongoni mwetu ,tumejenga Taifa au tumebomoka ?

Mtz ulikuwa ukienda SouthAfrika unathaminiwa,ukienda Uganda na nchi zote wakituthamini tena wakituthamini mmmoja mmoja, utawasikia Mtz mkombozi wetu ,leo hii tunafukuzwa wala hawatupi tena ile heshima ,tunaonekana wezi tu !

Hata Bagamoyo kuna plan ,Tanga ipo na sehemu nyingi tu,ila plan hizo zina wenyewe sio za kuelekezwa kwa mwananchi wa kawaida ,mwananchi anafukuzwa ili kupisha wenyewe,upanuzi wa uwanja wa ndege KIA,unasikia mizengwe ,wananchi wanalalamika ,nani anawasikiliza kilio chao ,miccm imeshagawana vitalu katika nchi hii ndio ukaona kila mmoja anamwogopa mwenzake,ukimwaga mboga anatia mchanga ugali !
 
Hebu tazama vizuri picha iliyowekwaa halafu unieleze viko wapi? hizo ni ndoto za alinacha. Tunajivunia tulichonacho sasa hivi ndiyo majaaliwa yetu tuliyojaaliwa na Mwenyeezi Mungu.

Sikutaka kukuonesha majumba na mabarabara tuliyonayo sasa hivi, ambayo pia ni kwa neema za Mwenyeezi Mungu, na mengine tuliyonayo hakuna katika Afrika ya Mashariki na kati. Nakumbuka kauli ya Magufuli, barabara za mali zilizopo sasa hivi Tanzania zikihamishiwa Rwanda, basi Rwanda yote itakuwa hakuna pa kujenga wala kulima, tutaifunika, unayajuwa hayo?

Ikiwa projections za miji tu, Jee, hujapitia vizuri hii nyuzi na kuziona projection zetu?

Tujivunie tulivyonavyo sasa hivi, iwe majumba, mabarabara, watu, fukwe, mbuga za wanyama na mengineyo yawayo, yote ni shani yake Mwenyeezi Mungu.

Tusianze kuota ndoto za alinacha kushindana na picha za kubuni za vitu visvyokuwepo. Tutakuwa majuha na mapunguani kama mleta mada.

Dada yangu faizafox nashukuru nimetembea tanzania nzima kwa njia ya barabara,, sehemu nyingi nikipita nakuta watu wakichimba hizo barabara na kuziba viraka na nyingi ya hizo barabara hazina hata miaka kumi,,, nyingine mkandarasi hajafika mwisho tayari alikoanzia barabara imeshaanza kutitia,,, umeona ile barabara iliyorudiwa na kajima pale mbagala ilivyoanza dalili mbaya??? Kule mtwara umeona ile barabara inamiaka mingapi inajengwa??? Pale sekenke kuelekea mwanza umepaona palivyo,, shinyanga to mwanza mitaa fulani umepaona palivyo,, moshi to arusha kuna jamaa wameshaanza kuchimba na sululu kuweka viraka!!!! Umeona quality ya barabara kutokea dom to iringa kupitia mtera ilivyo??? Kama tunajali miundombinu vipi pale daraja la wami hatulioni??? Usiku ukitembea barabara zetu zote sio safe hazina taa kiasi kwamba inahitaji uzoefu..
dada makambako to songea ile lami ni ya mkoloni lakini mpaka leo ipo poa tunaitembelea vipi kuhusu life span ya hizi lami za mchina maana inaonyesha raisi ajaye atarudia kazi ya kujenga tena barabara,, umeona maisha ya ile barabara ya tandale uzuri to sinza??? ..
halafu dada kujenga maghorofa sio ndio nchi imeendelea maana tusingekuwa na deni la taifa lililopitiliza na wala dola isingekuwa sh 1700,, unaweza ukanifafanulia impact ya daraja la kigamboni kwa uchumi wa nchi,,, unaweza ukaniwekea sawa impact ya uwanja wa ndege wa songwe mbeya kwa uchumi wa nchi???? Unajua kuwa kuna barabara nyingine tunazojisifia nazo ni kwa msaada wa watu wa marekani na mabango makubwa yamewekwa,,, je kodi zetu zinafanya nini kama hata barabara za dar taa haziwaki???
 
... Unajivunia Mji Wa Marekani Ndan Ya Nchi Yako?

Hapana. Najivunia hatua za awali za utekelezaji wa mji mpya wa kisasa kigamboni na united african university... at least utekelezaji si haba
 
Kigali ni wapi? haya Tanzania mji upi wa kujivunia? Maana hilo jiji la Dar ndio linaloongoza kwa kulipuka chemba za maji taka, au ndio maisha bora hayo kuonyesha kwamba watanzania wanashiba?

hivi unajua kigali haina centralized sewage system? Bora hata sisi ambao chemba zinazibuka lakini angalau mfumo tunao. Waulize wakishatoa sewage wanapeleka wapi?
 
Cjui unaelewa inaposemwa Masterplan ? In a short time wameweza kutoa muelekeo ,leo hii RwandaAir inasafirisha abiria wa Tz kutoka nchi za nje ,ipo wapi AirTanzania ? Au plan yake hamnayo ? mshaipiga tagi ,moyo ulinigonga sana kuona RwandaAir ikituletea abiria ,alitokea kibweka mmoja wa CCM akajisifu kuwa wanajenga viwanja vya ndege vya kisasa katika mikoa ,nilitegemea atasema na AirTanzania imezidisha safari za nchi za nje ,lakini wapi naambiwa hawana ndege hata moja ,wameila mpaka imekufa limebaki jina tu skeleton ,jiulize nini kimepelekea kudhoofika kwa shirika hili ,kilichosababisha ndischo hicho kinachozielekea hospitali za serikali ,chini ya utawala huu wa miccm hakutafufuka kitu ni kufa tu. ,

Tuna miji mingi kuliko Rwanda ,haijulikani hata unataka kusema nini ! Sema Mkoa wa Tanga ni mkubwa kuliko Rwanda ningekufahamu ni rahisi kuendeleza mji mdogo kuliko mkubwa ,yaani hata kujibu mnahitaji akili za kuchangiwa.

Kimbembe watu hatushobokei nchi ingine ,tunapima maendeleo ya tulitotokea,tulichokipokea kwa hao waliotukoloni ,umeona ,sasa maendeleo yetu ukilinganisha na nchi iliyokubwa na vita mfano wa Angola ,sisi ilikuwa tuwepo mbele sana tu, Angola hiyo hapo tumesaidia sana kuipatia uhuru hata watu wetu walikuwepo huko katika kuikomboa nchi ya Angola,tuliowakomboa leo hii wapo wapi ? Sisi ndio kwanza tunapigania ardhi miongoni mwetu ,tumejenga Taifa au tumebomoka ?

Mtz ulikuwa ukienda SouthAfrika unathaminiwa,ukienda Uganda na nchi zote wakituthamini tena wakituthamini mmmoja mmoja, utawasikia Mtz mkombozi wetu ,leo hii tunafukuzwa wala hawatupi tena ile heshima ,tunaonekana wezi tu !

Hata Bagamoyo kuna plan ,Tanga ipo na sehemu nyingi tu,ila plan hizo zina wenyewe sio za kuelekezwa kwa mwananchi wa kawaida ,mwananchi anafukuzwa ili kupisha wenyewe,upanuzi wa uwanja wa ndege KIA,unasikia mizengwe ,wananchi wanalalamika ,nani anawasikiliza kilio chao ,miccm imeshagawana vitalu katika nchi hii ndio ukaona kila mmoja anamwogopa mwenzake,ukimwaga mboga anatia mchanga ugali !

Jifunze kuchambua mambo. Tanzania tuna airlines ngapi na rwanda ziko ngapi? Tanzania tuna viwanja vya ndege 101 kudadeki, Rwanda hata 10 hawana. So what if we don't have a national carrier? kwanza ni asilimia ngapi ya wanyarwanda ambao wanapanda hiyo rwandair au asilimia ngapi ya watanzania ambao wangepanda Air tanzania mpaka national carriers ziwe na umuhimu kihivyo katika kulinganisha maendeleo kati ya nchi na nchi?
Unachotakiwa kufanya ni kuangalia kubwa hili: wanyarwanda ndio huja Tanzania kama wahamiaji haramu na kila siku unasikia madada wa kitutsi wanakamatwa wakifanya uchangudoa Tanzania. Je unaweza kusema hivyo kwa watanzania huko Kigali? Maisha ya mtanzania ni mazuri kuliko maisha ya mnyarwanda hilo liko wazi.
 
Kama alivyosema mbunge mmoja bungeni, baada ya Nyerere (RIP) kututoka, ccm waliondoa magoli uwanjani. Sasa hivi kila kiongozi anajipigia mpira bila ya kujua goli liko wapi. Matokeo yake ni ufisadi na wizi uliopindukia. Center half wetu ndio huyo kende zinamsumbua. Ndio maana toka mwanzo ameshindwa kutuliza mpira kifuani na kupanga timu yake.
Umenikuna mkuu! Mungu akubariki.
 
Jifunze kuchambua mambo. Tanzania tuna airlines ngapi na rwanda ziko ngapi? Tanzania tuna viwanja vya ndege 101 kudadeki, Rwanda hata 10 hawana. So what if we don't have a national carrier? kwanza ni asilimia ngapi ya wanyarwanda ambao wanapanda hiyo rwandair au asilimia ngapi ya watanzania ambao wangepanda Air tanzania mpaka national carriers ziwe na umuhimu kihivyo katika kulinganisha maendeleo kati ya nchi na nchi?
Unachotakiwa kufanya ni kuangalia kubwa hili: wanyarwanda ndio huja Tanzania kama wahamiaji haramu na kila siku unasikia madada wa kitutsi wanakamatwa wakifanya uchangudoa Tanzania. Je unaweza kusema hivyo kwa watanzania huko Kigali? Maisha ya mtanzania ni mazuri kuliko maisha ya mnyarwanda hilo liko wazi.

Hivyo viwanja vya ndege 102 vina impact gani kwenye uchumi??? Pale songwe mbeya mmewajengea fastjet,,, eti songwe international airport,,, kudadeki flight ni fastjet dar mbeya dar, kuna ndege ngapi zinatua pale kwa siku hakuna hata ndege moja inayolala pale,,, kuna na viwanja vya ndege 101 sio dili, ni dili tu kama vinatumika 70%,, ni bora ukawa na airline iliyo stable italeta faida kuliko kuwa na viwanja vya ndege 101 kwa ajili ya kupokea majeneza yetu.... Toka 1961 tumekuwa na mipango mingi mno lakini ni zero,,, kama ukahaba ndio unadetermine umasikini wa nchi basi sisi tunaongoza,,,, nenda pale China ukaone dada zako,, 70% ya makahaba tanzania ni watanzania wenyewe, nenda pale dubai uone siku hizi wanauza mpaka india... Vuka pale Nakonde zambia uone dada zako!!!
 
Hebu tazama vizuri picha iliyowekwaa halafu unieleze viko wapi? hizo ni ndoto za alinacha. Tunajivunia tulichonacho sasa hivi ndiyo majaaliwa yetu tuliyojaaliwa na Mwenyeezi Mungu.

Sikutaka kukuonesha majumba na mabarabara tuliyonayo sasa hivi, ambayo pia ni kwa neema za Mwenyeezi Mungu, na mengine tuliyonayo hakuna katika Afrika ya Mashariki na kati. Nakumbuka kauli ya Magufuli, barabara za mali zilizopo sasa hivi Tanzania zikihamishiwa Rwanda, basi Rwanda yote itakuwa hakuna pa kujenga wala kulima, tutaifunika, unayajuwa hayo?

Ikiwa projections za miji tu, Jee, hujapitia vizuri hii nyuzi na kuziona projection zetu?

Tujivunie tulivyonavyo sasa hivi, iwe majumba, mabarabara, watu, fukwe, mbuga za wanyama na mengineyo yawayo, yote ni shani yake Mwenyeezi Mungu.

Tusianze kuota ndoto za alinacha kushindana na picha za kubuni za vitu visvyokuwepo. Tutakuwa majuha na mapunguani kama mleta mada.

Wewe kama ni muislamu,kwanza unatakiwa uichukie CCM ndani ya moyo wako,hilo moja,hizo sio ndoto kama ulivyochomekea kwenye akili yako duni,hiyo inaitwa MasterPlan ya mji au nchi ,utakavyojengwa ,kwa wameweka iwe imekamilika kwenye 2040 ,

Halafu wacha mara moja kumsingizia Mwenyezi Mungu ,wala usitake kuwapeleka wengine huko, eti haya ndio majaaliwa yetu ,mwenyezi Mungu katujalia hivi ,huachi mtu mzima wewe ! Hizo barabara za Makufuli huna haja ya kuzipeleka Ruanda ,hapo Zanzibar tu itatosha.hayo unayoyasifu ,kwanza siyaoni,halafu siyajui na wala sitaki kuyajua ,maana itanifanya nipige mahesabu iligharimu kiasi gani .ugunduzi bila ya shaka yeyote utazidi bei ya kujenga barabara hizo kwa mabilioni ,wakati ukiuliza kwanini gharama hizo zimekuwa kubwa kiasi hicho,huwezi kupata jibu ,hivi unajua kile kiruka njia kilichojengwa Mwanza kiligharimu kiasi gani ? Porojo au uzandiki mlio kuwa nao hamna lingine.

Kama haitoshi Raisi ameagiza mahindi ya wananchi yanunuliwe ,jiulize leo ni muda gani umepita tokea Raisi atoe agizo hakuna hata gunzi lililonunuliwa ,nikikwambia kwamba kwa muda huu unaousema wewe hakuna anemsikiliza Raisi wala kumpatiliza ,au hilo nalo uongo ? Just akizungumza wanampigia makofi ya nguvu.

Na nyie mnaojifanya mnaitetea CCM na serikali yake hapa JF nionavyo hamuitetei ila mnazidi kuizamisha maana hamna hoja za msingi zaidi ya kubwabwaja ,chambilecho wapemba mmejaa reja.
 
Hivyo viwanja vya ndege 102 vina impact gani kwenye uchumi??? Pale songwe mbeya mmewajengea fastjet,,, eti songwe international airport,,, kudadeki flight ni fastjet dar mbeya dar, kuna ndege ngapi zinatua pale kwa siku hakuna hata ndege moja inayolala pale,,, kuna na viwanja vya ndege 101 sio dili, ni dili tu kama vinatumika 70%,, ni bora ukawa na airline iliyo stable italeta faida kuliko kuwa na viwanja vya ndege 101 kwa ajili ya kupokea majeneza yetu.... Toka 1961 tumekuwa na mipango mingi mno lakini ni zero,,, kama ukahaba ndio unadetermine umasikini wa nchi basi sisi tunaongoza,,,, nenda pale China ukaone dada zako,, 70% ya makahaba tanzania ni watanzania wenyewe, nenda pale dubai uone siku hizi wanauza mpaka india... Vuka pale Nakonde zambia uone dada zako!!!

1. TUNA VIWANJA 101 na vyote hivyo zinatua ndege hata kama sio za ATC. Rwanda wana viwanja vingapi na hiyo national carrier yao? Je hiyo national carrier yao inapiga safari ngapi NDANI YA RWANDA? ....MOJA TU! Na hata hiyo safari moja sasa hivi haipo! Right now hakuna safari ya ndege ndani ya Rwanda to Rwanda isipokuwa kwa ndege binafsi! tunarudi pale pale, mnyarwanda anafaidika nini kwa kuwa na ndege zinazoenda nje ya Rwanda ambacho sisi watanzania hatuna? sisi tuna ndege nyingi zaidi zinazoenda nje na ndani. tunafaidika sana na sekta ya aviation kuliko rwanda.

2. China wako makahaba toka dunia nzima, india wako makahaba toka dunia nzima. Pointi yangu ni hii, je umewahi kusikia makahaba wa kitanzania Rwanda/kigali? Mbona unakwepa kujibu how come watutsi wanajiuza dar na dodoma, kampala na nairobi ikiwa Rwanda mambo yake ni safi? Na mbona unakimbilia kutoa mifano ya ukahaba majiji ya kimataifa ambako wako makahaba mpaka wa kimarekani? na usisahau ishu ya wahamiaji haramu, je umewahi kusikia watanzania wamehamia kiharamu Rwanda? je hao wahamiaji haramu toka Rwanda huwa wanafuata nini bongo ikiwa kwao mambo safi wana ndege yao ya taifa ambayo Tanzania hatuna?
 
1. TUNA VIWANJA 101 na vyote hivyo zinatua ndege hata kama sio za ATC. Rwanda wana viwanja vingapi na hiyo national carrier yao? Je hiyo national carrier yao inapiga safari ngapi NDANI YA RWANDA? ....MOJA TU! Na hata hiyo safari moja sasa hivi haipo! Right now hakuna safari ya ndege ndani ya Rwanda to Rwanda isipokuwa kwa ndege binafsi! tunarudi pale pale, mnyarwanda anafaidika nini kwa kuwa na ndege zinazoenda nje ya Rwanda ambacho sisi watanzania hatuna? sisi tuna ndege nyingi zaidi zinazoenda nje na ndani. tunafaidika sana na sekta ya aviation kuliko rwanda.

2. China wako makahaba toka dunia nzima, india wako makahaba toka dunia nzima. Pointi yangu ni hii, je umewahi kusikia makahaba wa kitanzania Rwanda/kigali? Mbona unakwepa kujibu how come watutsi wanajiuza dar na dodoma, kampala na nairobi ikiwa Rwanda mambo yake ni safi? Na mbona unakimbilia kutoa mifano ya ukahaba majiji ya kimataifa ambako wako makahaba mpaka wa kimarekani? na usisahau ishu ya wahamiaji haramu, je umewahi kusikia watanzania wamehamia kiharamu Rwanda? je hao wahamiaji haramu toka Rwanda huwa wanafuata nini bongo ikiwa kwao mambo safi wana ndege yao ya taifa ambayo Tanzania hatuna?

Mkuu hivyo viwanja 101 vina impact gani kwenye uchumi wa nchi ukilinganisha na gharama za kuvijenga???

Hata tanzania kuna makahaba kutoka dunia nzima wapo mpaka wachina na wazungu,,, Uganda hakuna soko la ukahaba kwa kifupi hakulipi kwani hakuna wateja wa hiyo biashara,,, wahamiaji haramu rwanda hakuna kwani system sio za ovyo kwa watu kupenya kiholela,,, na kama unataka kajaribu kuingia kiholela!!!!

Anachojaribu kusema mtoa maada ni kwamba tanzania imepata uhuru 1961 na RWANDA wamepata uhuru juzi na walikuwa kwenye vita muda mrefu ila toka wamekuwa stable inaonekana tunakimbizana nao kiuchumi,,, wakati tulitegemea tungewaacha mbali sana na wangejifunza kupitia sisi, ila hawana chakujifunza sasa......
 
Hebu tazama vizuri picha iliyowekwaa halafu unieleze viko wapi? hizo ni ndoto za alinacha. Tunajivunia tulichonacho sasa hivi ndiyo majaaliwa yetu tuliyojaaliwa na Mwenyeezi Mungu.

Sikutaka kukuonesha majumba na mabarabara tuliyonayo sasa hivi, ambayo pia ni kwa neema za Mwenyeezi Mungu, na mengine tuliyonayo hakuna katika Afrika ya Mashariki na kati. Nakumbuka kauli ya Magufuli, barabara za mali zilizopo sasa hivi Tanzania zikihamishiwa Rwanda, basi Rwanda yote itakuwa hakuna pa kujenga wala kulima, tutaifunika, unayajuwa hayo?

Ikiwa projections za miji tu, Jee, hujapitia vizuri hii nyuzi na kuziona projection zetu?

Tujivunie tulivyonavyo sasa hivi, iwe majumba, mabarabara, watu, fukwe, mbuga za wanyama na mengineyo yawayo, yote ni shani yake Mwenyeezi Mungu.

Tusianze kuota ndoto za alinacha kushindana na picha za kubuni za vitu visvyokuwepo. Tutakuwa majuha na mapunguani kama mleta mada.

Ni upumbavu tena wa hali ya juu kwa mtu aliyefika kigali kisha akashindwa kubaini kuwa Rwanda inapiga hatua nzuri na inajua inachotaka. Si uzalendo kusifia ujinga, Tanzania ina mengi ya kujifunza kutoka Rwanda na hata tukiyataja hapa hatutoyamaliza. Acheni ujuha wenu ccm imeiweka nchi hii katika ramani mbaya sana, tusijilinganishe kabisa na Rwanda linapokuja suala la "kuendelea". Kuna dalili zote kwamba rwanda wanaweza kuruka baadhi ya hatua za maendeleo na kuwa ktk uchumi wa daraja zuri katika muda mfupi ujao. Ukubwa au udogo wa nchi si kigezo cha kuendelea au kutoendelea. Ni mfumo mzuri wa kitaasisi unaojikita katika kukemea rushwa, uzembe, ubabaishaji, na dhamira ya kutekeleza kile serikali inachopanga ikiwa pamoja kuwa na vipaumbele vinavyotekelezeka.

Rwanda ni mfano mzuri katika hayo ambapo nidhamu ya kazi na maadili ni jambo lililo na umuhimu pekee katika serikali yao. Kwa sasa, wamejiwekea lengo, ifikapo 2017, kila kaya iwe imefikiwa na umeme. Nimetembea maeneo mengi ya kigali, kwa taarifa tu ni kuwa ule usafi wa kigali ndio hali iko hivyo hadi vijijini kwao. Tena suala la msingi la kupaswa kujua ni kuwa, population density ya Rwanda ni kubwa mara nyingi ya Tanzania, lakini mji wa Kigali hauk populated kama ulivyo wa Dar. Why? Because of inclusive development plan katika maeneo yote ya miji na vijiji na hivyo kupunguza urbanizatio. Tujifunze tu kutoka kwao tuacheni blabla za ccm, cdm, cuf. Hazitusaidii kamwe.
 
Cjui unaelewa inaposemwa Masterplan ? In a short time wameweza kutoa muelekeo ,leo hii RwandaAir inasafirisha abiria wa Tz kutoka nchi za nje ,ipo wapi AirTanzania ? Au plan yake hamnayo ? mshaipiga tagi ,moyo ulinigonga sana kuona RwandaAir ikituletea abiria ,alitokea kibweka mmoja wa CCM akajisifu kuwa wanajenga viwanja vya ndege vya kisasa katika mikoa ,nilitegemea atasema na AirTanzania imezidisha safari za nchi za nje ,lakini wapi naambiwa hawana ndege hata moja ,wameila mpaka imekufa limebaki jina tu skeleton ,jiulize nini kimepelekea kudhoofika kwa shirika hili ,kilichosababisha ndischo hicho kinachozielekea hospitali za serikali ,chini ya utawala huu wa miccm hakutafufuka kitu ni kufa tu. ,

Tuna miji mingi kuliko Rwanda ,haijulikani hata unataka kusema nini ! Sema Mkoa wa Tanga ni mkubwa kuliko Rwanda ningekufahamu ni rahisi kuendeleza mji mdogo kuliko mkubwa ,yaani hata kujibu mnahitaji akili za kuchangiwa.

Kimbembe watu hatushobokei nchi ingine ,tunapima maendeleo ya tulitotokea,tulichokipokea kwa hao waliotukoloni ,umeona ,sasa maendeleo yetu ukilinganisha na nchi iliyokubwa na vita mfano wa Angola ,sisi ilikuwa tuwepo mbele sana tu, Angola hiyo hapo tumesaidia sana kuipatia uhuru hata watu wetu walikuwepo huko katika kuikomboa nchi ya Angola,tuliowakomboa leo hii wapo wapi ? Sisi ndio kwanza tunapigania ardhi miongoni mwetu ,tumejenga Taifa au tumebomoka ?

Mtz ulikuwa ukienda SouthAfrika unathaminiwa,ukienda Uganda na nchi zote wakituthamini tena wakituthamini mmmoja mmoja, utawasikia Mtz mkombozi wetu ,leo hii tunafukuzwa wala hawatupi tena ile heshima ,tunaonekana wezi tu !

Hata Bagamoyo kuna plan ,Tanga ipo na sehemu nyingi tu,ila plan hizo zina wenyewe sio za kuelekezwa kwa mwananchi wa kawaida ,mwananchi anafukuzwa ili kupisha wenyewe,upanuzi wa uwanja wa ndege KIA,unasikia mizengwe ,wananchi wanalalamika ,nani anawasikiliza kilio chao ,miccm imeshagawana vitalu katika nchi hii ndio ukaona kila mmoja anamwogopa mwenzake,ukimwaga mboga anatia mchanga ugali !
naona anticcmism imekuaffect hadi huoni maendeleo mengi nchini bali ubaya tu. mbona huoni udikteta rwanda na ufisadi angola? mbona huoni demokrasia tz? ungekua rwanda na kukejeli utawala ovyo ungeokotwa kwenye lile ziwa kusini ya kigali.
 
Ni upumbavu tena wa hali ya juu kwa mtu aliyefika kigali kisha akashindwa kubaini kuwa Rwanda inapiga hatua nzuri na inajua inachotaka. Si uzalendo kusifia ujinga, Tanzania ina mengi ya kujifunza kutoka Rwanda na hata tukiyataja hapa hatutoyamaliza. Acheni ujuha wenu ccm imeiweka nchi hii katika ramani mbaya sana, tusijilinganishe kabisa na Rwanda linapokuja suala la "kuendelea". Kuna dalili zote kwamba rwanda wanaweza kuruka baadhi ya hatua za maendeleo na kuwa ktk uchumi wa daraja zuri katika muda mfupi ujao. Ukubwa au udogo wa nchi si kigezo cha kuendelea au kutoendelea. Ni mfumo mzuri wa kitaasisi unaojikita katika kukemea rushwa, uzembe, ubabaishaji, na dhamira ya kutekeleza kile serikali inachopanga ikiwa pamoja kuwa na vipaumbele vinavyotekelezeka.

Rwanda ni mfano mzuri katika hayo ambapo nidhamu ya kazi na maadili ni jambo lililo na umuhimu pekee katika serikali yao. Kwa sasa, wamejiwekea lengo, ifikapo 2017, kila kaya iwe imefikiwa na umeme. Nimetembea maeneo mengi ya kigali, kwa taarifa tu ni kuwa ule usafi wa kigali ndio hali iko hivyo hadi vijijini kwao. Tena suala la msingi la kupaswa kujua ni kuwa, population density ya Rwanda ni kubwa mara nyingi ya Tanzania, lakini mji wa Kigali hauk populated kama ulivyo wa Dar. Why? Because of inclusive development plan katika maeneo yote ya miji na vijiji na hivyo kupunguza urbanizatio. Tujifunze tu kutoka kwao tuacheni blabla za ccm, cdm, cuf. Hazitusaidii kamwe.

Kigali yote ni kama Ilala tu.
 
Kigali sio Rwanda.Jiji la kigali linakula sehemu kubwa mno ya bajeti ya Serikali kuliko miji mingine ya Rwanda.Miji mingine iko hoi.Kila siku serikali inaongelea kupaka poda na hina jiji la kigali. Masterplan za miji mingine ya Rwanda ziko wapi?
Kigali inajifanya ndio Rwanda Washamba wengi hasa kutoka Tanzania wakitembelea Kigali wakirudi Utasikia Rwanda kuzuri hivi ajabu Tanzania bure kabisa! Niwaulize swali Kigali ndio Rwanda? Unaijua miji mingine ilivyo hovyo Rwanda?


Waulize hawa 'watumbafu' maana wanafikiri kila mtu ni mshamba kama wao.
Kwanza hata mengi yanayoonyeshwa kwenye hiyo video bado ni 'NDOTO ZA MCHANA' kwa maana kwamba hayapo bali yanapangwa kufanywa baadaye!
UPUUZI MTUPU!
 
Ni bora uuliwe kuliko kuteswa Serikali yako ya ccm na miccm inawatesa WaTanzania ,huduma za maji umeme kwa Tz nzima ni 0% ,hivi ni mji gani hapa Tz una taa za barabani zinazowaka usiku ? WALLAHI unapoingia kwa ndege jijini Dar usiku utafikiri unatua kwenye kambi ya kijeshi ,mji ni kiza tu zaidi ya taa za magari ,eti ndio kituo kikuu na mji mkubwa wenye kila kitu, mi ukiniita Mnyaruanda nafarijika sana kuliko kuniita kibaka.

CCM inachaguliwa na wananchi ni kweli wale mapolisi waliokimbia na masanduku ya kura Pemba ilikuwaje ? Matokeoa ya kura za siri BMK kucheleweshwa kwa masiku inakuwaje hapo ,watu wakizungumza bora mnyamaze kwani hamuwezi kabisa kuitetea CCM na serikali yake ,itakuwa kama mnamtetea mwizi aliyehukumiwa kunyongwa. eti inachaguliwa kihalali na wananchi safari hii itachaguliwa kiusingizi !

Hapo kwenye red jibu ni hakuna, ukipita na ndege usiku utaona kama vikoroboi vinawaka katikati ya msitu. Ningekuwa rais wa Tanzania ningekuwa mtu mnyonge sana, unawezaje kuwakaribisha viongozi wa nchi zingine ambao kwao kuko vizuri, barabara nzuri, miji imejipanga kwa ramani safi halafu kwako giza totoro, barabara mbovu, chafu, maplastic bags yanarushwa na upepo mpaka juu ya magari ya viongozi, mavi yananuka kutokana na vyoo na mitaro iliyofumuka, na wewe raisi uso mkavu hata aibu huna.

Sasa ukiulizwa vipi mbona umeme hauwaki unaanza ooh, mvua hakuna, mtera maji yameisha, absolute nonsense!
 
Back
Top Bottom