Rwanda inatuwashia double indicator & full Light, CCM ondokeni hatuwataki

Rwanda inatuwashia double indicator & full Light, CCM ondokeni hatuwataki

Kigali yote ni kama Ilala tu.

Then what? Hiyo ilala inayonuka? Uchafu umepandana utadhani indi ya zamani au dampo ya tabata enzi hizo. Ramadhan iliyopita nilipanga kufungia dar, lkn hali ilivyo hapo Ilala, sikuweza kukaa Dar hata wiki moja. Kwa kifupi dar ni jiji letu, tanzania ni nchi yetu, lakini kamwe sitakuwa kipofu wa kutoona mazuri ya wenzetu na mabaya yetu. Yatubidi tujipange sana tuache porojo huku duniani tunakashfika sana huku nje kutokana na kuwa na lundo la utajiri lkn jiji linanuka uchafu. Very sorry for that!
 
Jifunze kuchambua mambo. Tanzania tuna airlines ngapi na rwanda ziko ngapi? Tanzania tuna viwanja vya ndege 101 kudadeki, Rwanda hata 10 hawana. So what if we don't have a national carrier? kwanza ni asilimia ngapi ya wanyarwanda ambao wanapanda hiyo rwandair au asilimia ngapi ya watanzania ambao wangepanda Air tanzania mpaka national carriers ziwe na umuhimu kihivyo katika kulinganisha maendeleo kati ya nchi na nchi?
Unachotakiwa kufanya ni kuangalia kubwa hili: wanyarwanda ndio huja Tanzania kama wahamiaji haramu na kila siku unasikia madada wa kitutsi wanakamatwa wakifanya uchangudoa Tanzania. Je unaweza kusema hivyo kwa watanzania huko Kigali? Maisha ya mtanzania ni mazuri kuliko maisha ya mnyarwanda hilo liko wazi.


Unajua umezungumza jambo zuri sana ila upofu ukio nao huwezi kuona kina cha ulichokiandika ,unaitetea serikali ya CCM kumbe unazidi kuiuwa, MiCCM imeua kila kitu na inaendelea kuuwa mambo au miradi yote ya kiserikali ili waingize na kuchomekea miradi yao,kama wamejenga viwanja vya ndege basi ujue si kwa ajili ya miradi ya serikali,wametumia mgongo wa serikali kujiwekea mazingira mazuri ,upo !

Wameua AirTz wamefungua ya kwao,wameua na wanaendelea kuuwa mahospitali ya serikali wanafungua ya kwao au wanakuwa wabia(Share) ,kwa mashule ndio usiseme ,mnavunja kila kitu,kulikuwa na viwanda hapa vya serikali vimeajiri watz kibao mmeviua vyote,hebu jiulize inakuwaje tajiri mmoja anaweza kuendesha kiwanda serikali haina uwezo ,inaingia akilini,mtasma harama za uendeshaji nyingi ,wakati sio kweli ,katika serikali kumejaa mafisadi ,hakuna hata kimoja mnachoweza kukiendeleza kwa moyo wa kizalendo zaidi ya kuwadanganya masikini kwa ahadi hewa ,haya mahindi yanaoza ,mliwapiga kampeni wakulima walime kwa bidii mtanunua mazao yao ,leo wakulima wanapiga makelele mazao yao yanawaozea ,wakisafirisha mnawakamata. Wakiyapeleka FAO kuuza hawayanunui,ila kigogo wa ccm anawaendea na kuyanunua kwa bei ya chini kisha anayapeleka kulekule FAO kwenda kuyauza tena anapewa bei nzuiri ,mara mbili ya bei aliyonunulia,kama si ukiritimba ni kitu gani ,hii serikali ndugu zangu imewashinda na itaendelea kuwashinda ,hata mkiiba uraisi ujao mambo yatazidi kuwa worse kuliko ilivyo sasa ,kwani ndani ya ccm system hakuna ,ni uwoza mtupu.
 
Rwanda nchi yote ni ndogo kupita mkoa wa Iringa. Kuifananisha Tanzania na Rwanda ni sawa na kufananisha kichuguu na mlima Kilimanjaro. Bahresa pekee anao uwezo wa kuilisha nchi ya Rwanda mwaka mzima
 
Hata sisi tumeshaanza.Angalia miaka ya mbele kigamboni Tanzania itakavyokuwa

https://www.youtube.com/watch?v=Oy1Usi8DrC8

Wenye mji tuneshagoma, tumeona usanii umepitiliza. Tumesubiri miaka kibao, tathmini walifanya, sasa notisi ime expire!

Mimi nimeshaanza kuendeleleza kaeneo kangu na sitaki kusikia huo upuuzi wao kuhusu Kigamboni, walivyotupigisha marktime yatosha. Nasikia sasa wameshabuni mji mwingine Kawe, sasa kipi ni kipi?

Maigizo yametuchosha, uvumilivu umetuishia. Kigamboni itawagharimu sana kuliko ilivuokuwa awali, njoo Kigamboni ujionee tunavyopiga hatua za haraka.
 
Rwanda kaiba rasilimali za kongo, Rwanda kaua wapinzani wake kwa risasi. Unashauri na Tanzania yafanyike hayo?

Tukizungumza kijinga ni afadhali ya Rwanda wanaoiba raslimali za Kongo na kujenga kwao Rwanda kuliko sisi tunaojiibia na kujidhoofisha wenyewe.
 
Kigali sio Rwanda.Jiji la kigali linakula sehemu kubwa mno ya bajeti ya Serikali kuliko miji mingine ya Rwanda.Miji mingine iko hoi.Kila siku serikali inaongelea kupaka poda na hina jiji la kigali. Masterplan za miji mingine ya Rwanda ziko wapi?
Kigali inajifanya ndio Rwanda Washamba wengi hasa kutoka Tanzania wakitembelea Kigali wakirudi Utasikia Rwanda kuzuri hivi ajabu Tanzania bure kabisa! Niwaulize swali Kigali ndio Rwanda? Unaijua miji mingine ilivyo hovyo Rwanda?

wewe unayeijua miji mingine ya rwanda tuonyeshe siyo unabwabwaja tu!
 
Rwanda nchi yote ni ndogo kupita mkoa wa Iringa. Kuifananisha Tanzania na Rwanda ni sawa na kufananisha kichuguu na mlima Kilimanjaro. Bahresa pekee anao uwezo wa kuilisha nchi ya Rwanda mwaka mzima

mawazo yako yamekaa kimakali.o, huna lolote la maana unalojua!
 
Mkuu, FF hatajibu hoja yako hapa, ataanza tu kuhorojoka na kukuita punguani.

Hata hivyo nampongeza FF kwa uhodari wake wa kutetea hata yasitowezekana. Kuitetea Serikali ya CCM lazima uwe na akili kama ya FF.
I
Dada yangu faizafox nashukuru nimetembea tanzania nzima kwa njia ya barabara,, sehemu nyingi nikipita nakuta watu wakichimba hizo barabara na kuziba viraka na nyingi ya hizo barabara hazina hata miaka kumi,,, nyingine mkandarasi hajafika mwisho tayari alikoanzia barabara imeshaanza kutitia,,, umeona ile barabara iliyorudiwa na kajima pale mbagala ilivyoanza dalili mbaya??? Kule mtwara umeona ile barabara inamiaka mingapi inajengwa??? Pale sekenke kuelekea mwanza umepaona palivyo,, shinyanga to mwanza mitaa fulani umepaona palivyo,, moshi to arusha kuna jamaa wameshaanza kuchimba na sululu kuweka viraka!!!! Umeona quality ya barabara kutokea dom to iringa kupitia mtera ilivyo??? Kama tunajali miundombinu vipi pale daraja la wami hatulioni??? Usiku ukitembea barabara zetu zote sio safe hazina taa kiasi kwamba inahitaji uzoefu..
dada makambako to songea ile lami ni ya mkoloni lakini mpaka leo ipo poa tunaitembelea vipi kuhusu life span ya hizi lami za mchina maana inaonyesha raisi ajaye atarudia kazi ya kujenga tena barabara,, umeona maisha ya ile barabara ya tandale uzuri to sinza??? ..
halafu dada kujenga maghorofa sio ndio nchi imeendelea maana tusingekuwa na deni la taifa lililopitiliza na wala dola isingekuwa sh 1700,, unaweza ukanifafanulia impact ya daraja la kigamboni kwa uchumi wa nchi,,, unaweza ukaniwekea sawa impact ya uwanja wa ndege wa songwe mbeya kwa uchumi wa nchi???? Unajua kuwa kuna barabara nyingine tunazojisifia nazo ni kwa msaada wa watu wa marekani na mabango makubwa yamewekwa,,, je kodi zetu zinafanya nini kama hata barabara za dar taa haziwaki???
 
Rwanda nchi yote ni ndogo kupita mkoa wa Iringa. Kuifananisha Tanzania na Rwanda ni sawa na kufananisha kichuguu na mlima Kilimanjaro. Bahresa pekee anao uwezo wa kuilisha nchi ya Rwanda mwaka mzima

Hata huko Bakareza yupo ,yupo,msumbiji amepewa bandari pale ,yupo Uganda ,ila hapa tz yupoyupo tu ,anaendesha kwa hasara ni lazima awahonge miccm,

Ila kati ya kichuguu na mlima inategemea anaeishi katika vitu viwili hivyo ,ila hapo kwenye mlima kama pamevamiwa na mafisadi hakuna wala hakutapatikana faida mpaka mafisadi hao wameondolewa.Vinginevyo watateketeza miti yote na kuwamaliza wanyama waishio humo na kuuangamiza mlima huo. Kwa huo Mlima uliooukusudia kuwa ni Tz basi miccm inauangamiza kila kukicha.
 
Anatuletea habari za kufikirika mwaka 2014!

Jivunie ulichonacho sasa hivi, usijivunie ndoto za mwenzako.

Amma kweli kuna misukule si mchezo.
ha ha ha ha! unajivunia rais kikwete kwenda kutibiwa BUSHA marekani?

 
hebu tazama vizuri picha iliyowekwaa halafu unieleze viko wapi? Hizo ni ndoto za alinacha. Tunajivunia tulichonacho sasa hivi ndiyo majaaliwa yetu tuliyojaaliwa na mwenyeezi mungu.

Sikutaka kukuonesha majumba na mabarabara tuliyonayo sasa hivi, ambayo pia ni kwa neema za mwenyeezi mungu, na mengine tuliyonayo hakuna katika afrika ya mashariki na kati. Nakumbuka kauli ya magufuli, barabara za mali zilizopo sasa hivi tanzania zikihamishiwa rwanda, basi rwanda yote itakuwa hakuna pa kujenga wala kulima, tutaifunika, unayajuwa hayo?

Ikiwa projections za miji tu, jee, hujapitia vizuri hii nyuzi na kuziona projection zetu?

Tujivunie tulivyonavyo sasa hivi, iwe majumba, mabarabara, watu, fukwe, mbuga za wanyama na mengineyo yawayo, yote ni shani yake mwenyeezi mungu.

Tusianze kuota ndoto za alinacha kushindana na picha za kubuni za vitu visvyokuwepo. Tutakuwa majuha na mapunguani kama mleta mada.

kama uongo ungekuwa hela basi we mama ungekuwa tajiri .
 
Mkuu hivyo viwanja 101 vina impact gani kwenye uchumi wa nchi ukilinganisha na gharama za kuvijenga???

Hata tanzania kuna makahaba kutoka dunia nzima wapo mpaka wachina na wazungu,,, Uganda hakuna soko la ukahaba kwa kifupi hakulipi kwani hakuna wateja wa hiyo biashara,,, wahamiaji haramu rwanda hakuna kwani system sio za ovyo kwa watu kupenya kiholela,,, na kama unataka kajaribu kuingia kiholela!!!!

Anachojaribu kusema mtoa maada ni kwamba tanzania imepata uhuru 1961 na RWANDA wamepata uhuru juzi na walikuwa kwenye vita muda mrefu ila toka wamekuwa stable inaonekana tunakimbizana nao kiuchumi,,, wakati tulitegemea tungewaacha mbali sana na wangejifunza kupitia sisi, ila hawana chakujifunza sasa......

1. viwanja havijajengwa jana wala juzi, vimejengwa kutokana na haja ya kuwapo na uchumi wetu kuruhusu. Viwanja vya ndege mfano vya mwadui vilijengwa kwa sababu ya biashara ya almasi tangu hujazaliwa. Unataka kusemaje? kwamba tumejijengea tu viwanja bila kuwa na matumizi navyo au?

2. hahahaa. eti wahamiaji haramu hakuna kwani system zao sio za ovyo. Okay, so kwa maoni yako kule marekani ambapo suala la illegal immigrants toka mexico ni suala zito la kila uchaguzi na hadi sasa obama anahangaika nalo unataka kusemaje? kuwa marekani nao wana system za ovyo kama Tanzania au? What about Saudi na illegal immigrants toka ethiopia? What about SA? Kote huko wana system mbovu kuliko Rwanda? Sijui kama hata unaamini ulichoandika, but for any serious person anajua kuwa HAKUNA ILLEGAL IMMIGRANTS IN RWANDA KWA SABABU HAKULIPI! Hakuna mtu mwenye matatizo kiasi hicho mpaka Rwanda iwe afadhali kuliko huko anakotoka, labda kwa mbali awe anatoka burundi!
Vile vile usisahau kuwa wahamiaji haramu toka Rwanda kwenda mataifa mengine ni wengi mno, wako DRC, Uganda, Tanzania, wakati hakuna wahamiaji haramu kuingia Rwanda, this means what to you?

3. Tanzania haijawahi kupata uhuru, Tanzania imeanza mwaka 1964, nadhani ulitaka kusema Tanganyika...anyway, kwa kukusahihisha Rwanda haikupata uhuru "juzi", imepata uhuru mwaka 1959 baada ya wanyarwanda kupindua utawala wa kifalme wa watutsi chini ya mkoloni mbelgiji. Hivyo kihistoria ya kupata uhuru ni kama tuko sawa tu.
Pili, ni kweli kuwa vita iliharibu mambo mengi na wamepiga hatua kubwa kwa muda mfupi. Lakini Rwanda ni ndogo sana kulinganisha na Tanzania, hivyo kwa vyovyote wangepiga hatua kubwa tu, unaongelea mkoa mmoja tu wa kilimanjaro! Hivi sisi toka 1961 au 1964 mpaka leo Tanzania ingekuwa ni mkoa mmoja tu wa kilimanjaro tungefanana na Rwanda?
Tatu, ingawa nakubali kuwa Rwanda imepiga hatua toka vita vya 1990-1994 katika kujenga upya nchi yao, most of these news coming from Rwanda ni propaganda za serikali ambazo zina-exagerate mafanikio. Ndio maana kila wakati narudia kwenye mifano yangu ya kuangalia wanyarwanda wakimbizi haramu na machangudoa toka Rwanda, surely huwezi kunionyesha the same kwa watanzania walioko Rwanda.
 
Tujivunie umaskini kama huu? Kweli???? We ndiye msukule namba moja
untitled+of+tz.jpg

Copy-2-of-Mr.-Simango-holding-baobab-shell-600x402.jpg

naona BI MKUBWA WAMEMMALIZA NA VIJISALE VYA CHAMA ! ASANTE SANA MKUU KWA PICHA INAYOONYESHA MAISHA HALISI YA MTANZANIA .
 
Hivi viongozi hawa wa kiCCM wanajua wanachokifanya au ni wao na kukumbatia ufisadi na kuikausha nchi kwa kujazana ikulu wakijaza matumbo yao ,hebu angalia hawa waKigali na matumaini yao ambayo utayapenda na kuwaonea wivu pengine ikazidi kukufanya uichukie miccm na ccm yao. Miccm ni kujisifu tu tuna mbuga,tuna bahari,tuna maziwa,tuna gesi ,tuna mafuta kama haitoshi tuna Uranium ,yule waziri aliesema Uranium itakuwa tayari 2011 yupo wapi leo tunaelekea 2015 ,Warwanda hao wanaitangazia dunia kule wanakoelekea, Miccm mnatuchelewesha ,ondokeni tushawachoka.



CC: Money Stunna
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom