Rwanda inatuwashia double indicator & full Light, CCM ondokeni hatuwataki

Rwanda inatuwashia double indicator & full Light, CCM ondokeni hatuwataki

Unajua umezungumza jambo zuri sana ila upofu ukio nao huwezi kuona kina cha ulichokiandika ,unaitetea serikali ya CCM kumbe unazidi kuiuwa, MiCCM imeua kila kitu na inaendelea kuuwa mambo au miradi yote ya kiserikali ili waingize na kuchomekea miradi yao,kama wamejenga viwanja vya ndege basi ujue si kwa ajili ya miradi ya serikali,wametumia mgongo wa serikali kujiwekea mazingira mazuri ,upo !

Wameua AirTz wamefungua ya kwao,wameua na wanaendelea kuuwa mahospitali ya serikali wanafungua ya kwao au wanakuwa wabia(Share) ,kwa mashule ndio usiseme ,mnavunja kila kitu,kulikuwa na viwanda hapa vya serikali vimeajiri watz kibao mmeviua vyote,hebu jiulize inakuwaje tajiri mmoja anaweza kuendesha kiwanda serikali haina uwezo ,inaingia akilini,mtasma harama za uendeshaji nyingi ,wakati sio kweli ,katika serikali kumejaa mafisadi ,hakuna hata kimoja mnachoweza kukiendeleza kwa moyo wa kizalendo zaidi ya kuwadanganya masikini kwa ahadi hewa ,haya mahindi yanaoza ,mliwapiga kampeni wakulima walime kwa bidii mtanunua mazao yao ,leo wakulima wanapiga makelele mazao yao yanawaozea ,wakisafirisha mnawakamata. Wakiyapeleka FAO kuuza hawayanunui,ila kigogo wa ccm anawaendea na kuyanunua kwa bei ya chini kisha anayapeleka kulekule FAO kwenda kuyauza tena anapewa bei nzuiri ,mara mbili ya bei aliyonunulia,kama si ukiritimba ni kitu gani ,hii serikali ndugu zangu imewashinda na itaendelea kuwashinda ,hata mkiiba uraisi ujao mambo yatazidi kuwa worse kuliko ilivyo sasa ,kwani ndani ya ccm system hakuna ,ni uwoza mtupu.

Wewe ndio kipofu. Ukisoma vizuri utagundua kuwa siitetei CCM, bali ninachotetea ni Tanzania. Wewe ulipobugi ni kuleta mada ya kuiponda CCM kwa kutumia Rwanda, hilo ndio tatizo. Tanzania versus Rwanda ni kama mbingu na nchi my friend. Lete mada ya kuiponda CCM bila kuingiza Rwanda hapo tutakubaliana. Sio kufananisha Tanzania nzima na kigali.
 
acha ujinga, safisha kwanza jiji la dar liwe safi ndiyo ulete mbwembwe zingine!siyo Prof Global Trotter anashindwa kuboresha hospital zake anaenda kupasuliwa BUSHA marekani eti nchini kwake hakuna usalama!

Kutibiwa ni mara moja moja sio mbaya. Lakini watoto wa kikwete wamesomea nchini tena baadhi yao shule za serikali. je huko rwanda mnakosifia mbona watoto wa rais wamesoma nje eti "kwa ajili ya usalama wao"? Nchi gani haina amani kiasi hicho?

Ivan is the eldest of President Paul Kagame’s sons. He was educated abroad due to security and privacy concerns.
....Is President Paul Kagame’s second child and only daughter. As President Kagame’s daughter, she completed her education abroad for security and privacy reasons.
source: President Paul Kagame & Jeannette Kagame – The First Couple of Rwanda News Of Rwanda – Rwanda News

Linganisha na hii:
Binti wa JK aitwaye Salama Kikwete amehitimu digrii ya Doctor of Dental Surgery Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili.

Hii inafurahisha kwa baadhi ya viongozi wetu kusomesha watoto wao hapa hapa bongo. source:https://www.jamiiforums.com/celebrities-forum/21731-mtoto-wa-jk-ahitimu-muhimbili.html

JK%2BDAUGHTER%2B2.JPG
 
Tukizungumza kijinga ni afadhali ya Rwanda wanaoiba raslimali za Kongo na kujenga kwao Rwanda kuliko sisi tunaojiibia na kujidhoofisha wenyewe.

aliokwambia Rwanda nzima imeiba congo ni nani? walioiba ni kagame na mafisadi wenzie wachache, wanyarwanda wa kawaida wako maporini kagera huko wanatafuta vibarua.
 
Cjui unaelewa inaposemwa Masterplan ? In a short time wameweza kutoa muelekeo ,leo hii RwandaAir inasafirisha abiria wa Tz kutoka nchi za nje ,ipo wapi AirTanzania ? Au plan yake hamnayo ? mshaipiga tagi ,moyo ulinigonga sana kuona RwandaAir ikituletea abiria ,alitokea kibweka mmoja wa CCM akajisifu kuwa wanajenga viwanja vya ndege vya kisasa katika mikoa ,nilitegemea atasema na AirTanzania imezidisha safari za nchi za nje ,lakini wapi naambiwa hawana ndege hata moja ,wameila mpaka imekufa limebaki jina tu skeleton ,jiulize nini kimepelekea kudhoofika kwa shirika hili ,kilichosababisha ndischo hicho kinachozielekea hospitali za serikali ,chini ya utawala huu wa miccm hakutafufuka kitu ni kufa tu. ,

Tuna miji mingi kuliko Rwanda ,haijulikani hata unataka kusema nini ! Sema Mkoa wa Tanga ni mkubwa kuliko Rwanda ningekufahamu ni rahisi kuendeleza mji mdogo kuliko mkubwa ,yaani hata kujibu mnahitaji akili za kuchangiwa.

Kimbembe watu hatushobokei nchi ingine ,tunapima maendeleo ya tulitotokea,tulichokipokea kwa hao waliotukoloni ,umeona ,sasa maendeleo yetu ukilinganisha na nchi iliyokubwa na vita mfano wa Angola ,sisi ilikuwa tuwepo mbele sana tu, Angola hiyo hapo tumesaidia sana kuipatia uhuru hata watu wetu walikuwepo huko katika kuikomboa nchi ya Angola,tuliowakomboa leo hii wapo wapi ? Sisi ndio kwanza tunapigania ardhi miongoni mwetu ,tumejenga Taifa au tumebomoka ?

Mtz ulikuwa ukienda SouthAfrika unathaminiwa,ukienda Uganda na nchi zote wakituthamini tena wakituthamini mmmoja mmoja, utawasikia Mtz mkombozi wetu ,leo hii tunafukuzwa wala hawatupi tena ile heshima ,tunaonekana wezi tu !

Hata Bagamoyo kuna plan ,Tanga ipo na sehemu nyingi tu,ila plan hizo zina wenyewe sio za kuelekezwa kwa mwananchi wa kawaida ,mwananchi anafukuzwa ili kupisha wenyewe,upanuzi wa uwanja wa ndege KIA,unasikia mizengwe ,wananchi wanalalamika ,nani anawasikiliza kilio chao ,miccm imeshagawana vitalu katika nchi hii ndio ukaona kila mmoja anamwogopa mwenzake,ukimwaga mboga anatia mchanga ugali !

Umeongea vizuri ila ulipofika hapo kwenye Red ukaharibu kila kitu. Hivi unajua Angola kilichowapiga tafu ni nini?? Unajua wao walianza kuchimba mafuta lini?? Unaujua Ukubwa wa uchumi wa Angola kulinganisha na nchi zingine za Afrika?? Tunaingia kwenye Uchumi wa mafuta na gesi, after ten years from now tukiwa bado hapahapa hapo tunapaswa kujilaumu kwa kujifananisha na Angola.

Back to the Topic, hiyo ni masterplan tu, inaweza ikawa kweli ama wala wasifikie nusu ya hapo mpaka hiyo 2040. Ni kama ulivyosema tu tulidanganywa tutaanza kuchimba uranium mwaka 2011 ila mpaka sasa hamna lolote. Masterplan kama hizo NHC washazitoa kwa sehemu kadhaa hapa Nchini na tayari pesa za utekelezaji zipo tayari. Vipi hiyo masterplan ya Kigali itacost pesa ngapi?? Vipi hizo pesa vipo tayari?? Au watajenga ni Phases, kama ndivyo, zimetengwa pesa ngapi mpaka sasa kwa Phase one?? Hapa naona unajadili Tanzania pekee, vipi miji mingine ya Afrika Mashariki umeshaitembelea, ikoje?? Ni wazi tu kwamba Masterplan kubwa za mji wote kama Kigali ni vigumu kutekelezeka either in Dar, Nairobi ama Kampala unless zitacost twice as expected fund to accomplish such Project. Jambo la kukazania ni katika miji inayoendelea kwa kasi kama Mtwara, Dodoma hizi project zikawe implemented huko, lakini ma ccm wao wamekazana na Dar tu.
 
Miji mingine ya nini wakati hapo hapo kigali hali ndio hii:
slum.jpg
Street-children.jpg
slums-in-kigali.jpg
source: https://www.jamiiforums.com/interna...i-jiji-la-mfano-afrika-mashariki-na-kati.html

hahahahaha Mkuu sana tatizo watu tunakuwa so obsessed na mambo ya kando then tunakuja kuikandia serikali yetu kwasababu tu wanaoiongoza hutuwapendi. Mi si ccm lakini unapokuja na masterplan ambayo haijawa implemented hata kwa 0.2% then unakuja kuitupia lawama serikali yako sidhani kama ni jambo la busara.. Tanzania tuna GDP kubwa sana ukilinganisha na nchi zingine za Africa, na inasemekana tukifanya rebaising tunaweza next year tunaweza ingia Top 10. Hilo watu hawaliona wala. Waarabu wana miji mizuri duniani hata hao wazungu wakitaka kupumzika wanaenda huko lakini interms of maendeleo wameachwa mbali sana.. Maendeleo hayapimwi kwa masterplan wala uzuri wa mji
 
Tatizo mnachanganyikiwa na main point ,kwa muda mfupi Rwanda wameweza kutoa masterplan nchi ambayo imekumbwa na vita ,sisi hapa tuna miaka mingi na hakuna tatizo la kuitikisa nchi zaidi ya vita ya Uganda,leo tena ccm inapotaka kuuliwa ndio mnakurupuka na mipango ,wachilia mafuta na gesi ,mbuga hizi za wanyama na alimasi tokea sijazaliwa nasikia mwadui ,na bado inachimbwa hadi leo.

Nchi hii Tz ina maskendo kibao,yanaibuka na kutiwa kwenye madroo ,ndio imetoka,hayo mafuta na gesi ,tunachokiona ni mafisadi kibao kutaka kugombea Uraisi, hizo picha za Kigali ni bora zaidi kwa nchi iliyokumbwa na vita vya kukimbiza roho kwa kila raia ,ukilinganisha na nchi inayosifiwa kuwa kisiwa cha amani ,amani gani watu wanaishi kama wakimbizi ndani ya Dar ,kama huamini angalia kipindi cha USWAZI ,utaona maajabu ,utasikia mipango miji ujue hapo kuna masikini anataka au wanataka kumvunjia nyumba yake ni udhalimu wa hali ya juu.

MiCCM hamna cha kumuleza mwananchi wa leo akawaelewa maana masuali aliyonayo ni mengi kuliko majibu mliyonayo zaidi ni ubabaishaji na ujuwaji wa kupitiliza ,mnajifanya kila kitu mnajua nini kumbe hamna isipokuwa ulaghai tu. MiCCM ni waongo wa kupigiwa mfano ,ila mfa maji hawachi kutapatapa ,ni bora mkakaa kimya kuliko kujifanya ni watetezi ,ipo wapi AirTanzania ,reli ya kati hiyo hapo ,mara kapewa mhindi mara kuna mabehewa mapya yanakuja,mara tutakarabati na kutengeneza engene hapa hapa,siku mbili tatu kimya na ndio imetoka.

Tatizo ni pale mnapoonekana ni watu wa ajabu kabisa ,mnawaeleza wananchi mambo ambayo hamuwezi kuyatekeleza na kuwadanganya ,miaka tisa imepita eti mnafungua miradi mwaka wa kumalizia uraisi ,mnatesa miaka tisa mnafurahisha mwaka wa uchaguzi ,kama ilivyokufa AirTanzania,reli ndivyo zitakavyokufa hospitali ,eti bungeni leo mnapotosha umma kuwa mmeagiza dawa ,na kupelekwa Muhimbili ,hivi tatizo lipo Muhimbili tu ? Mnajaribu kujikaza kisabuni,ila kusema ukweli mmenasa na serikali ndio hiyo waziri mkuu anakimbia bungeni.

Miccm na ccm yao itadhirika tu ,hili halina ubishi ,endeleeni kujikaza hivyohivyo na kuupotosha umma lakini njia ya muongo ni fupi,,hapa JF hamuwezi kabisa kuitetea CCM na serikali yake zaidi ya kuzidi kuiangusha.
 
Kigali sio Rwanda.Jiji la kigali linakula sehemu kubwa mno ya bajeti ya Serikali kuliko miji mingine ya Rwanda.Miji mingine iko hoi.Kila siku serikali inaongelea kupaka poda na hina jiji la kigali. Masterplan za miji mingine ya Rwanda ziko wapi?
Kigali inajifanya ndio Rwanda Washamba wengi hasa kutoka Tanzania wakitembelea Kigali wakirudi Utasikia Rwanda kuzuri hivi ajabu Tanzania bure kabisa! Niwaulize swali Kigali ndio Rwanda? Unaijua miji mingine ilivyo hovyo Rwanda?

Funga mdomo kama hujui kitu kaa kimya, nchi ya Rwanda miji yote inakuwa kwa pamoja pamoja na Kigali japo hawana rasilimali tulizo nazo watanganyika. Mikataba serekali yao inayoingia ipo wazi siyo ya siri kama ya mccm wa tz. Azam walikuwa wanapeleka unga Rwanda lakini wakaambiwa wajenge Kiwanda Rwanda wakajenga ajira zikaongezeka huko. Rwanda air walikuwa na ndege kubwa 12 mwaka 2010 ambazo siyo za mkopo wa tz mna ndege ngapi shirika la uma?
 
hivi unajua kigali haina centralized sewage system? Bora hata sisi ambao chemba zinazibuka lakini angalau mfumo tunao. Waulize wakishatoa sewage wanapeleka wapi?

.... Hayo Ndo Mawazo Mgando Ya Maccm, Kwan Sewage Lazma Ipelekwe Baharini? Kubwa Pumba
 
.... Naipenda Sana Rwanda, Natamani Nitafute Uraia Wa Huko, Maana Hii Tanzania Yetu Inanuka
 
hahahahaha Mkuu sana tatizo watu tunakuwa so obsessed na mambo ya kando then tunakuja kuikandia serikali yetu kwasababu tu wanaoiongoza hutuwapendi. Mi si ccm lakini unapokuja na masterplan ambayo haijawa implemented hata kwa 0.2% then unakuja kuitupia lawama serikali yako sidhani kama ni jambo la busara.. Tanzania tuna GDP kubwa sana ukilinganisha na nchi zingine za Africa, na inasemekana tukifanya rebaising tunaweza next year tunaweza ingia Top 10. Hilo watu hawaliona wala. Waarabu wana miji mizuri duniani hata hao wazungu wakitaka kupumzika wanaenda huko lakini interms of maendeleo wameachwa mbali sana.. Maendeleo hayapimwi kwa masterplan wala uzuri wa mji

ndio maana hawa jamaa huwa nawauliza swali hili lakini sijibiwi: kwa nini wanyarwanda ni wahamiaji haramu tanzania lakini watanzania sio wahamiaji haramu Rwanda?
 
Funga mdomo kama hujui kitu kaa kimya, nchi ya Rwanda miji yote inakuwa kwa pamoja pamoja na Kigali japo hawana rasilimali tulizo nazo watanganyika. Mikataba serekali yao inayoingia ipo wazi siyo ya siri kama ya mccm wa tz. Azam walikuwa wanapeleka unga Rwanda lakini wakaambiwa wajenge Kiwanda Rwanda wakajenga ajira zikaongezeka huko. Rwanda air walikuwa na ndege kubwa 12 mwaka 2010 ambazo siyo za mkopo wa tz mna ndege ngapi shirika la uma?
Usimtishie mwenzio eti afunge mdomo wewe jibu haya mambo kwa hoja:

1. Asilimia zaidi ya 90% ya private sector ni makampuni ya chama tawala cha RPF ambacho mwenyekiti wake Paul Kagame ndie pekee anayejua mahesabu yake (kama chama fulani hivi cha upinzani bongo), katika hali hiyo unawezaje kufurahia kuwa "mikataba iko wazi", wakati mikataba hiyo LAZIMA wapewe crystal ventures?

2. Toka rwandair ianzishwe umewahi kuona statement zake za kifedha? kwa taarifa yako ndege hii haijawahi kutoa mahesabu yake bunge la rwanda hata siku moja. mahesabu yote yanapelekwa kwa kagame, na kagame himself ndio anachagua viongozi wa hilo shirika. Wapi umewahi kuona duniani kokote ambako mashirika ya umma hayatoi mahesabu kwa CAG wala bunge ila yanachukua fedha za umma? Rwandair has been operating at a loss toka inanzishwe. Sisi ATC yetu iko hoi kwa sababu mahesabu yake yako WAZI! Tungeweza na sisi kuchukua hela za maskini walipa kodi na kununua ndege JUST SO WE CAN SAY LOOK AT US WE HAVE AN AIRLINE kama ambavyo kagame anafanya. Rwandair haina faida yoyote kwa Rwanda isipokuwa show-off.
Halafu unadanganya wazi wazi eti ndege zao sio za mkopo, are you serious? hebu pitia hapa, hii ni habari ya MWAKA HUU HUU halafu njoo uthibitishe madai yako:Rwanda's national carrier RwandAir, has received a loan facility worth $40 million (Rwf22.8 billion) to support the carrier's development plans. The loan is to be secured from the Eastern and Southern African Trade and Development Bank (PTA). source: Rwandair gets $40 Million and dumps aircraft provider | News | alternativeairlines.com
 
Tatizo mnachanganyikiwa na main point ,kwa muda mfupi Rwanda wameweza kutoa masterplan nchi ambayo imekumbwa na vita ,sisi hapa tuna miaka mingi na hakuna tatizo la kuitikisa nchi zaidi ya vita ya Uganda,leo tena ccm inapotaka kuuliwa ndio mnakurupuka na mipango ,wachilia mafuta na gesi ,mbuga hizi za wanyama na alimasi tokea sijazaliwa nasikia mwadui ,na bado inachimbwa hadi leo.

Nchi hii Tz ina maskendo kibao,yanaibuka na kutiwa kwenye madroo ,ndio imetoka,hayo mafuta na gesi ,tunachokiona ni mafisadi kibao kutaka kugombea Uraisi, hizo picha za Kigali ni bora zaidi kwa nchi iliyokumbwa na vita vya kukimbiza roho kwa kila raia ,ukilinganisha na nchi inayosifiwa kuwa kisiwa cha amani ,amani gani watu wanaishi kama wakimbizi ndani ya Dar ,kama huamini angalia kipindi cha USWAZI ,utaona maajabu ,utasikia mipango miji ujue hapo kuna masikini anataka au wanataka kumvunjia nyumba yake ni udhalimu wa hali ya juu.

MiCCM hamna cha kumuleza mwananchi wa leo akawaelewa maana masuali aliyonayo ni mengi kuliko majibu mliyonayo zaidi ni ubabaishaji na ujuwaji wa kupitiliza ,mnajifanya kila kitu mnajua nini kumbe hamna isipokuwa ulaghai tu. MiCCM ni waongo wa kupigiwa mfano ,ila mfa maji hawachi kutapatapa ,ni bora mkakaa kimya kuliko kujifanya ni watetezi ,ipo wapi AirTanzania ,reli ya kati hiyo hapo ,mara kapewa mhindi mara kuna mabehewa mapya yanakuja,mara tutakarabati na kutengeneza engene hapa hapa,siku mbili tatu kimya na ndio imetoka.

Tatizo ni pale mnapoonekana ni watu wa ajabu kabisa ,mnawaeleza wananchi mambo ambayo hamuwezi kuyatekeleza na kuwadanganya ,miaka tisa imepita eti mnafungua miradi mwaka wa kumalizia uraisi ,mnatesa miaka tisa mnafurahisha mwaka wa uchaguzi ,kama ilivyokufa AirTanzania,reli ndivyo zitakavyokufa hospitali ,eti bungeni leo mnapotosha umma kuwa mmeagiza dawa ,na kupelekwa Muhimbili ,hivi tatizo lipo Muhimbili tu ? Mnajaribu kujikaza kisabuni,ila kusema ukweli mmenasa na serikali ndio hiyo waziri mkuu anakimbia bungeni.

Miccm na ccm yao itadhirika tu ,hili halina ubishi ,endeleeni kujikaza hivyohivyo na kuupotosha umma lakini njia ya muongo ni fupi,,hapa JF hamuwezi kabisa kuitetea CCM na serikali yake zaidi ya kuzidi kuiangusha.

tatizo wewe hueleweki nia yako ni nini, kuikosoa CCM au kulinganisha Rwanda na Tanzania chagua moja.

1. Rwanda wameweza kutoa masterplan nchi ambayo imekumbwa na vita : Nashindwa kuelewa unaisifiaje Rwanda kwa kutoa masterplan ya kigali tena ya miaka 26 ijayo? Dar es salaam ndio jiji letu kuu sisi watanzania, na LIMESHAJAA. Ndio maana serikali yetu ikaandaa masterplan ya CBD mpya kigamboni. Hivyo unachotakiwa kufanya ni kulinganisha utekelezaji wa hiyo master plan ya kigali na utekelezaji wa masterplan ya kigamboni. ya kwetu ya kigamboni kwa mwenye macho anaona, na hata kwenye taarifa za habari kila siku unaona kikwete anazindua phases mpya za daraja kwa kuanzia, je hiyo ya Rwanda imefikia hatua gani ya utekelezaji zaidi ya kuonyeshana video kwenye youtube?

2. kweli tanzania ina maskendo kibao. Lakini the only reason unayajua ni kwa kuwa tuna uhuru wa vyombo vya habari kwa kiasi hicho na uhuru wa kujieleza. Huko Rwanda unakokusifia maskendo hakuna kwa sababu vyombo vyote vya habari tecnically ni vya serikali, kukosoa serikali maana yake ni usaliti na utaishia jela, waandishi wamewahi kuuawa kwa kuandika habari za rushwa serikalini. Rushwa iko tena kubwa sana, isipokuwa imekuwa ni kati ya vigogo tu.

3. Kipindi cha USWAZI kama kinavyojieleza kinaelezea maisha ya watu maskini wanaoishi kwenye slums, na sio maisha ya wana dar es salaam, nikianzisha kipindi kinaitwa USHUANI nikaonyesha watu wanavyoishi oysterbay, masaki na mbezi beach utasema kuwa Dar es salaam nzima watu wanaishi peponi? Hiyo kigali unayoisifia kwa taarifa yako watu wanakamatwa kwa kuvaa nguo kuukuu, watu maskini waliovaa kandambili wanakamatwa wakionekana wamekaa sehemu ambazo wageni ("wazungu") wanapita ili kuleta picha kuwa kigali ni mji mzuri, kama huamini google this! Ndio maana hata new york, london, tokyo japan na kwingineko kwenye maendeleo kuna homeless people barabarani, BUT NOT RWANDA ambayo zaidi ya 50% ni maskini wa kutupwa, hebu shangaa hili! Hiko kipindi cha USWAZI kingerushwa episode moja tu ya Kigali hiyo TV ingefungiwa!

4. CCM imechemsha mambo mengi sikatai, ila leta thread ya kivyakevyake tuijadili kama CCM.
 
Tukizungumza kijinga ni afadhali ya Rwanda wanaoiba raslimali za Kongo na kujenga kwao Rwanda kuliko sisi tunaojiibia na kujidhoofisha wenyewe.

Haujajibu hilo la pili, nilikuuliza Kagame anaua wapinzani wake. Unashauri na Kikwete afanye hivyo hivyo?
 
Kigali sio Rwanda.Jiji la kigali linakula sehemu kubwa mno ya bajeti ya Serikali kuliko miji mingine ya Rwanda.Miji mingine iko hoi.Kila siku serikali inaongelea kupaka poda na hina jiji la kigali. Masterplan za miji mingine ya Rwanda ziko wapi?
Kigali inajifanya ndio Rwanda Washamba wengi hasa kutoka Tanzania wakitembelea Kigali wakirudi Utasikia Rwanda kuzuri hivi ajabu Tanzania bure kabisa! Niwaulize swali Kigali ndio Rwanda? Unaijua miji mingine ilivyo hovyo Rwanda?

Kwani Tanzania ni mji gani unaweza sema ni wa mfano? Mimi binafsi nawapongeza kwa kuwa wameamua angalau kuanza na mji mkuu. Kila kitu ni lazima kiwe na mwanzo! Miji mingi SSA including Dar 90% ni slums.
 
Hii kitu ni kweli rwanda wako speed sana mfano rwanda walikuwa hawalimi pareto lakin walikuja tanzania wakachukua mbegu ya pareto na saizi rwanda kwa east aftica ndo wanazalisha pareto yenye standard soko la dunia si bado pareto yetu iko chini bodi ya pareto wamekuwa madali wa kuua wakulima
 
sioni sababu ya kutoa povu jingi unless unaishobokea rwanda ovyo. hiyo ni plan tu. dar ipo plan ya kigamboni na isitoshe tuna miji mingi kuliko rwanda na sio kwamba miji haina masterplan

Kigamboni is another white elephant! Na hizo masterplans za miji mbona hazifuatwi?? Sina hata mji mmoja TZ wa kujivunia. Nimetembea nchi nyingi Africa SSA, kuna miji ukienda leo na ukarudi baada ya miaka mitatu unakuta imeboreka ikiwa ni pamoja na Kigali na Nairobi. Mingine inazidi kukomaa kwa kuwa na slums kubwa ikiwa ni pamoja n Dar. Naipenda sana nchi yangu ila wenye mamlaka wanatuangusha. Hata sehemu ndogondogo zenye masterplans zinageuka slums kwa sasa, mfano Sinza.
 
Mleta mada,

Ni dhahiri wewe sio Mtanzania. Kama ungekuwa Mtanzania, basi usingeandika huu upuuzi wako.

Njia pekee ya kuitoa CCM ni kupitia uchaguzi. Kwa sasa tunaelekea kwenye uchaguzi, sasa kwanini usisubiri huo uchaguzi ili uikatae hiyo CCM!?
Lukuvi sema, nyie wote kwenye ccm vichwa vyenu ni weupe pee
 
Back
Top Bottom