CoW ni biashara, hatuna cha undugu wala udada, kila nchi lazima siku zote ijihami na ikae mkao wa kuzicheza mambo yakienda kivingine. Jiwe la Migingo haliwezi fanya tupigane ovyo, kuna jinsi nyingine za kusuluhisha tunazozifuata. Vita ni gharama kubwa na ndio unaona Watanzania hawajakimbilia kupigana na Malawi baada ya kuzuka ugomvi kuhusu ziwa.
Tanzania ilijifunza walipoingia Uganda, nchi inarudi nyuma kiuchumi halafu vizazi vya kesho vinabaki kuumia. Yaani nimesema siku nyingi, ni bahati sana Waganda walikua wamemchoka Id Amin kiasi kwamba walikubali nchi yao ikojolewe, bure wangejitokeza kwa mamilioni kutetea bendera yao na hapo ndio umwagikaji wa damu ungekua kama bahari. Muulize Mmarekani kilichomkuta Vietnam, wanavijiji waliamua wafe wote.
Hata sisi bahati yetu Wasomali wamewachoka Alshabaab, bure pale Somalia ingekua kichinjio cha jeshi letu la KDF.
Kwanza wewe
jMali unafaa kuwa umejua hili wakati wa vita vyenu huko Rwanda baina yenu na Kagame, wengi wenu mmeishia kujificha Tanzania.