Chapakazi
JF-Expert Member
- Apr 19, 2009
- 2,874
- 310
Nadhani inatakiwa iwe ugomvi kwa wananchi wote wa tanzania. Kwa nini serikali itoe hela kugharimia vyama vya siasa ambavyo ni vyama vya hiari. Je watu ambao hawana vyama serikali inawatreat vipi. Watanzania tupo millioni 43 wanachama wa vyama vya siasa hawazidi millioni kumi hii ina maana kuwa kuna karibia watu 33 milioni ambao hawapati hiyo advantage ya kuchangiwa na serikali kila mwezi kwenye mambo ya siasa.
Wanasheria tusaidieni katika hili naona kama sheria inaruhusu ruzuku ni ya kibaguzi sana.
Yani mkuu....embu chukua tano. Nadhani wati kibao wame-miss hii point yako. Inabidi ufungue thread specieal ya ku-address hii kitu. Yani katika kodi ya Mtanzania...Billion moja inaenda kwenye vyama vya siasi kwa mwezi?????
huu ni utani. Kujenga hospitali moja ni kiasi gani wakuu?
kusomesha madkatari pale muhimbili ni kiasi gani?
hii billion moja kwa mwezi ingewawezesha walimu wangapi tanzania?
alafu leo mnaambiwa ni nchi maskini mnaitikia kama makondoo....
AM TIRED OF THIS BULL***
Lazima tuamke...
Uwe CHADEMA, CCM, CUF, nk....sema no to RUZUKU!!