Ruzuku itatuathiri kichama - CHADEMA

Ruzuku itatuathiri kichama - CHADEMA

PENDEKEZO.Kama ruzuku itazuiliwa
1.Wabunge wote na wengine wenye kipato kikubwa ndani ya chadema wakubali kuchangia % fulani kwenye chama
2.Kuanzishwe harambee ya kitaifa na kimataifa kukichangia chama
3.Waliosababisha dhahma hii kwa kujua ama kutokujua wachukuliwe hatua mf.ndani ya chama,CAG ama waziri au katibu wa wizara
4.Kamati PAC ichunguzwe kama nayo imetekeleza majukumu yake pasi na shinikizo mf.je,ni kazi ya bunge kusimamia vyama vya siasa ama serikali? kwa nn wasingemwajibisha CAG au msajili ?
 
Ccm kudhoofika ni ndoto ndugu zangu nyie jipangeni vizuri na zile harambee zenu za mia mia la sivyo mjichimbie kaburi mapema.
 
Hili ndilo ilibidi liwanyime usingizi ila wao wakaitisha vyombo vya habari na kutoa tamko na vielelezo,anyways ngoja tuone umakini wa vyama katika kutatua changamoto!!!!!!

Hongera sana kamati kwa kutingisha mibuyu

CCM uu mwaka wake wa kutikisika, kila jambo limaitikisa , mbona kazi ipo.
 
Katibu wa Baraza la Wadhamini la CHADEMA Anthony Komu amesema usitishwaji wa Ruzuku kwa vyama vya siasa utakiathiri chama hicho kwa kiwango kikubwa.

Kiongozi huyo mwenye mamlaka ya kifedha ndani ya CHADEMA amesema chama hicho kinategemea asilimia 45% ya Ruzuku ya kila mwezi kulipa mishahara ya wafanyakazi na watendaji wa chama kote nchini.

Komu amesema ingawa wana vyanzo vingine vya mapato lakini havitoshi bila kutegemea Ruzuku.

Komu amesema pia usitishwaji huo wa Ruzuku utaathiri kwa kiwango kikubwa mipango ya chama hasa uimarishwaji wake katika operesheni zinazoendekea kote nchini.

Kiongozi huyo amelaani uamuzi wa Kibabe wa Kamati ya bunge kuzuia Ruzuku kwa vyama vyote huku CHADEMA wakiwa hawana kosa lolote na wakiwa wameshakabidhi mahesabu yao ofisi ya msajili wa vyama siku nyingi.

Source:Mwananchi.

Kamanda Anthony Komu usiogope, waache wazuie, TANU wakati inapigania uhuru, haikuwa ikipata ruzuku toka kwa mzungu

Hii ni hali ya kawaida, hiyo ruzuku ni sisi wananchi ndiyo tunaitoa kupitia kodi na sisi wanachama na wapenzi wa chadema kama tukihamasishwa tunaweza tukatoa mchango mzuri na wafanyakazi wa chama kote nchini wakalipwa na elimu ya ukombozi ikafika kila pembe ya nchi

Tusiogope, tunapaswa kuangalia juu ya uchaguzi 2014 and 2015

Chadema for Nation

Member
 
Amani kwenu wana JF,

Kwa takribani siku tatu mfululizo kumekuwa na mjadala mzito juu ya swala la ruzuku kwa vyama vya siasa. Mjadala huu ulianza pale Mh. Zitto kama mwenyekiti wa POAC kuhoji uhalali wa kuendelea kupewa ruzuku kwa vyama vya CCM, CDM, NCCR, TLP na CUF among others. Binafsi nilishawishika na kukubaliana na maelezo ya Zitto kwani alijinasibu kuwa anasimamia sheria na taratibu.

Well, nami sikutaka afanye vinginevyo bali kuvibana vyama vya siasa, kikiwemo CHADEMA hasa akiwa kiongozi wa ngazi ya juu kiutawala na kimamlaka, kuweza kutupeleka taarifa za mapato na matumizi kwa CAG! Hata hivyo nilikuwa nikipata tabu sana kuamini kuwa chama changu CDM hakikuandaa taarifa za mapato na matumizi, hasa nikiamini ndicho chama pekee makini kilichobaki Tanzania kinachoenda kupewa dola 2015.

Punde kidogo akaja Anthony Komu (msimamizi wa maswala ya fedha ndani ya chama) nakutoa nyaraka zenye ushahidi juu ya mwenendo na taarifa za ruzuku.

Hili aliliweka sawa na amani ikanirudi nakujua chama changu kipo macho kwani kinajua adui yake (ma-ccm) yatatafuta kila sababu yakumbana ili kuondoa ule uamnifu kwa jamii. Uaminifu unaokua kwa kasi kila uchao. Heko kwa umakini CDM

Leo nimepata nyepesi eti ile kodi ya watanzania (inayoitwa ruzuku) imesitishwa! Nataka nikiondoe hofu CHADEMA. Binafsi nitatoa SEHEMU YA MSHAHARA WANGU KILA MWEZI kuweza kufidia pengo la ruzuku.

Ndugu zangu wapenda maendeleo na mabadiliko kaeni mkitambua na iwaangie akilini kuwa hizi ni mbinu chafu za kukikwamisha CDM.

Mbinu hizi ni mwendelezo wa zile nyingi kukwama. Natambua wengi vimshahara vyetu ni vidogo mno lakini nina hakika endapo tutaamua kwa moyo mmoja basi chama kinauwezo wakupata pesa nyingi zaidi ya hizo za ruzuku.

Waswahili husema 'kamba hukatikia pembamba' na 'kondoo ni mkia'. Viongozi wetu wameshapambana na wanazidi kupambana. Kamba imefikia ukingoni/kwembamba.

Yaani ukombozi ndo unawaidia halafu wanarudishwa nyuma! Nasema hapana hapana hapana nimekataa. Naomba chama kitoe utaratibu maalumu kiweze kupata pesa yangu na wengine wengi walioguswa kila mwisho wa mwezi.

Tuamke na tuwashangaze mafisadi kuwa tumeamua kwa dhati kumkomboa mtanzania kutoka kwa wakoloni weusi ma-ccm.

Naomba kuwasilisha.
 
Kamanda Anthony Komu usiogope, waache wazuie, TANU wakati inapigania uhuru, haikuwa ikipata ruzuku toka kwa mzungu

Hii ni hali ya kawaida, hiyo ruzuku ni sisi wananchi ndiyo tunaitoa kupitia kodi na sisi wanachama na wapenzi wa chadema kama tukihamasishwa tunaweza tukatoa mchango mzuri na wafanyakazi wa chama kote nchini wakalipwa na elimu ya ukombozi ikafika kila pembe ya nchi

Tusiogope, tunapaswa kuangalia juu ya uchaguzi 2014 and 2015

Chadema for Nation

Member


Good spirit na hili likwezekana ndio ukombozi utakuwa wa kweli kabisa!!!!!

Tuone kama watu watakubali matumizi ya chopa na safari za kwenda kuzindua matawi ulaya na marekani!!!!
 
Kweli kamanda lazima tuoneshe kuwa ni uzalendo wa kweli kwa ajili ya nchi yetu.
 
Katibu wa Baraza la Wadhamini la CHADEMA Anthony Komu amesema usitishwaji wa Ruzuku kwa vyama vya siasa utakiathiri chama hicho kwa kiwango kikubwa.

Nashauri Uongozi CDM uache mara moja kulalama na kuanza kuchukua hatua za kuziba pengo litakalosababiswa na zuio la ruzuku. Kulalama hakutasaidia. Wape wananchi wenye chama jukumu la kuziba pengo hata kama ni kwa muda mfupi. Inabidi muwe na ankara kwamba zinahitajika kiasi gani kuziba pengo. Then, zungumza na makampuni ya simu kuwe na mpango wa kuokoa chama na watu watumie hiyo account kuchangia.

Msisubiri chama kiathirike ndipo mje na mipango hafifu kama ya CCM. We know you can do better than this.

Hilo ni wazo tu
 
Kama umekosa kitu cha maana cha kufanyia na hizo hela zako, ni bora hizo hela zako ukatoe sadaka kanisani au msikitini.
 
CDM lazima wanajua wanalofanya this country will ultimately be polarized btn CDM and CCM ndio vyama pekee vinaweza cheza na rules mpya kama hizi.
'when the going gets tough the toughs get going'
 
Ruzuku inasagwa na viongozi wachache ndani ya chama halafu na wewe unataka kuendeleza kuchangia wanaume wenzako waweze kulea wake zao na vimada wao? Hii ni aibu.
 
Ushauri: CDM incase ruzuku imesitishwa sisi wanachama wenye mapenzi mema tutachanga pesa kwa sehemu yetu. Hivyo andaeni namna ili tuchangie kwa kidogo kitakachopatikana. Najua gatuwezi fikia hiyo bilioni 9 lakini pesa za kuwalipa wavuja jasho zitapatikana.
 
Hivi kupeleka hesabu kwa ukaguzi ni jambo gumu kiasi suluhu iwe kuchangishana????!!!

Hivi ku comply na request/order ya kamati ni jambo gumu kiasi hiki???!!!!
 
Kama wakifanya hivyo watakuwa wamekata tawi nalo walilokalia kwa hiyo muda si mrefu nao watapiga makelele.
 
Back
Top Bottom