Ruzuku itatuathiri kichama - CHADEMA

Ruzuku itatuathiri kichama - CHADEMA

Ruzuku inasagwa na viongozi wachache ndani ya chama halafu na wewe unataka kuendeleza kuchangia wanaume wenzako waweze kulea wake zao na vimada wao? Hii ni aibu.

zile mlizoficha uswisi mmeshazirudisha?
 
Wangeifuta kabisa ili hawa wachumia tumbo, CHADEMA wajifunze adabu!

View attachment 117425 View attachment 117428

Ikifutwa unafikiri hawa misukule mnayoitumikisha mtaiona tena, maana yote haya wanayafanya kwa sababu ya Ruzuku mnayopewa
BOMU.jpg

Na Ruzuku ikifutwa hii kitu hapo juu hamtaweza tena kununua na itakuwa nafuu kwa CHADEMA mikutano itakuwa salama.
 
EPA,DEEP GREEN na MEREMETA

RADA, NDEGE YA RAIS, RICHMOND, DOWANS, IPTL, NBC, KIWIRA, KUSAFITISHA WANYAMA HAI KIA, PESA ZA USWISI, BUZWAGI N.K.
 
Mkuu mamseri binafsi napendekeza viongozi wa Chadema waitishe harambee ya dharura kwa wanachama kote nchini ili operesheni za chama zisisimame.

hata mimi nasapoti cdm waitishe harambee haraka iwezekanavyo tukichangie chama chetu cha ukombozi wa kweli.ila tu naskitika ile timu y lb7 itakufa kifo cha panya.
 
Last edited by a moderator:
Kama kweli kuna ufujaji basi anayetoa hizo fedha bila udhibiti wa matumizi yake yu -------- zaidi
 
Kamati ya PAC inatekeleza majukumu yake kisheria. Hii ni taarifa njema kwa wapenda nchi yao.
 
Hivi kwani kufuata utaratibu kuna shida gani? Nilivyosikia vyama vinatakiwa kwanza kupitisha report zao kwa mkaguzi mkuu wa serikali ambae atapitia akiridhika ata sign na kuweka muhuri wake,kabla ya kupeleka kwa msajiri. Vyama havikupitosha kwa CAG kwa kuogopa kubanwa kimahesabu wenyewe wakakimbilia kupeleka kwa msajiri.VYAMA VYOTE VYA SIASA Acheni ubabaishaji fuateni utaratibu kwani hizo ni KODI ZETU
 
Chama chetu cha CDM hakina deni. Sakata la kuwang'oa hawa wababe linaendelea kama kawaida nchini kote.
 
Nahisi zile safari za USA na Uk zitapungua hata uratibu wa maandamano utadhoofika, kelele nyingi kumbe unategemea nyumba ya kupanga kama ni kweli ruzuku imezuiwa tusubiri ofisi za CDM zikifungwa kwa kushindwa kulipa kodi.
 
katibu wa baraza la wadhamini la chadema anthony komu amesema usitishwaji wa ruzuku kwa vyama vya siasa utakiathiri chama hicho kwa kiwango kikubwa.

Kiongozi huyo mwenye mamlaka ya kifedha ndani ya chadema amesema chama hicho kinategemea asilimia 45% ya ruzuku ya kila mwezi kulipa mishahara ya wafanyakazi na watendaji wa chama kote nchini.

Komu amesema ingawa wana vyanzo vingine vya mapato lakini havitoshi bila kutegemea ruzuku.

Komu amesema pia usitishwaji huo wa ruzuku utaathiri kwa kiwango kikubwa mipango ya chama hasa uimarishwaji wake katika operesheni zinazoendekea kote nchini.

Kiongozi huyo amelaani uamuzi wa kibabe wa kamati ya bunge kuzuia ruzuku kwa vyama vyote huku chadema wakiwa hawana kosa lolote na wakiwa wameshakabidhi mahesabu yao ofisi ya msajili wa vyama siku nyingi.

Source:mwananchi.

kama ni kweli basi huu ukali wote utakuwa umeratibiwa na ccm kwa ajili ya kuvihujumu vyama vya upinzani vinavyotegemea ruzuku katika kutekeleza shughuli zao za kichama na kimaendeleo ila kwa ccm wao wako imara kwa kuwa na vyanzo vingi vya upatikanaji wa hela..mfano leo karibia viwanja vyote vitaingizia ccm hela kibao
 
Kama ni kweli ruzuku ingesitishwa, na kama ni kweli Chadema ingeathirika, basi CCM ndio ingekufa kabisa!.
Ndio maana ruzuku haitasimamamishwa. CCM nao wamo katika mkumbo huo!
 
Nimekwama ada ya shule jamani, kwa yule mwenye mapenzi naomba msaada wake ili niweze kutimiza ndoto yangu! na amini watanzania mara zote si watu wa kutupana bali ushikamana pale kunapokuwa na uhitaji. natanguliza shukurani zangu za dhati kabisa kwa yoyote atakaeguswa, kwa maelezo zaidi tafadhari ni PM
 
Kamanda Anthony Komu usiogope, waache wazuie, TANU wakati inapigania uhuru, haikuwa ikipata ruzuku toka kwa mzungu

Hii ni hali ya kawaida, hiyo ruzuku ni sisi wananchi ndiyo tunaitoa kupitia kodi na sisi wanachama na wapenzi wa chadema kama tukihamasishwa tunaweza tukatoa mchango mzuri na wafanyakazi wa chama kote nchini wakalipwa na elimu ya ukombozi ikafika kila pembe ya nchi

Tusiogope, tunapaswa kuangalia juu ya uchaguzi 2014 and 2015

Chadema for Nation

Member

Mungu akubariki kwa mawazo mazuri sana ya kujenga.

Naamini viongozi wamekupata sawasawa.

Tumaini Makene Ben Saanane
 
Last edited by a moderator:
Amani kwenu wana JF,

Kwa takribani siku tatu mfululizo kumekuwa na mjadala mzito juu ya swala la ruzuku kwa vyama vya siasa. Mjadala huu ulianza pale Mh. Zitto kama mwenyekiti wa POAC kuhoji uhalali wa kuendelea kupewa ruzuku kwa vyama vya CCM, CDM, NCCR, TLP na CUF among others. Binafsi nilishawishika na kukubaliana na maelezo ya Zitto kwani alijinasibu kuwa anasimamia sheria na taratibu.

Well, nami sikutaka afanye vinginevyo bali kuvibana vyama vya siasa, kikiwemo CHADEMA hasa akiwa kiongozi wa ngazi ya juu kiutawala na kimamlaka, kuweza kutupeleka taarifa za mapato na matumizi kwa CAG! Hata hivyo nilikuwa nikipata tabu sana kuamini kuwa chama changu CDM hakikuandaa taarifa za mapato na matumizi, hasa nikiamini ndicho chama pekee makini kilichobaki Tanzania kinachoenda kupewa dola 2015.

Punde kidogo akaja Anthony Komu (msimamizi wa maswala ya fedha ndani ya chama) nakutoa nyaraka zenye ushahidi juu ya mwenendo na taarifa za ruzuku.

Hili aliliweka sawa na amani ikanirudi nakujua chama changu kipo macho kwani kinajua adui yake (ma-ccm) yatatafuta kila sababu yakumbana ili kuondoa ule uamnifu kwa jamii. Uaminifu unaokua kwa kasi kila uchao. Heko kwa umakini CDM

Leo nimepata nyepesi eti ile kodi ya watanzania (inayoitwa ruzuku) imesitishwa! Nataka nikiondoe hofu CHADEMA. Binafsi nitatoa SEHEMU YA MSHAHARA WANGU KILA MWEZI kuweza kufidia pengo la ruzuku.

Ndugu zangu wapenda maendeleo na mabadiliko kaeni mkitambua na iwaangie akilini kuwa hizi ni mbinu chafu za kukikwamisha CDM.

Mbinu hizi ni mwendelezo wa zile nyingi kukwama. Natambua wengi vimshahara vyetu ni vidogo mno lakini nina hakika endapo tutaamua kwa moyo mmoja basi chama kinauwezo wakupata pesa nyingi zaidi ya hizo za ruzuku.

Waswahili husema 'kamba hukatikia pembamba' na 'kondoo ni mkia'. Viongozi wetu wameshapambana na wanazidi kupambana. Kamba imefikia ukingoni/kwembamba.

Yaani ukombozi ndo unawaidia halafu wanarudishwa nyuma! Nasema hapana hapana hapana nimekataa. Naomba chama kitoe utaratibu maalumu kiweze kupata pesa yangu na wengine wengi walioguswa kila mwisho wa mwezi.

Tuamke na tuwashangaze mafisadi kuwa tumeamua kwa dhati kumkomboa mtanzania kutoka kwa wakoloni weusi ma-ccm.

Naomba kuwasilisha.

You are a star! Great Idea.
 
Ushauri: CDM incase ruzuku imesitishwa sisi wanachama wenye mapenzi mema tutachanga pesa kwa sehemu yetu. Hivyo andaeni namna ili tuchangie kwa kidogo kitakachopatikana. Najua gatuwezi fikia hiyo bilioni 9 lakini pesa za kuwalipa wavuja jasho zitapatikana.

Hongera kwa ujasiri na kuwatia moyo viongozi.
 
Ccm kudhoofika ni ndoto ndugu zangu nyie jipangeni vizuri na zile harambee zenu za mia mia la sivyo mjichimbie kaburi mapema.

bora kidogo kuliko kikubwa cha masimango!sisi maskin wa mia mia tutakichangia inshallah
 
Nahisi zile safari za USA na Uk zitapungua hata uratibu wa maandamano utadhoofika, kelele nyingi kumbe unategemea nyumba ya kupanga kama ni kweli ruzuku imezuiwa tusubiri ofisi za CDM zikifungwa kwa kushindwa kulipa kodi.

pole kwa mawazo mgando.
 
Back
Top Bottom