Rushwa wazi wazi migodi ya Barrick

Inaonesha najibu hoja za wahuni maana unaposema "thieves" what do you really mean? Usitake kujaza server ya JF kwa post usizokuwa na uhakika nazo.
You have nothing to speak about this,so far you are employed for this purpose then i dont have to lament on you...this is what makes you feed,but for your imformation this is just a first step of my campaign against corruption in barrick,few days you will hear about in mass medias,am serious and i have reliable and admissible evidences
 
Nimefanya kazi bulyanhulu mwaka 2004 nikiwa kama security pale C.C.T.V nikaacha pia mwaka 2008 nikarudi nikafanya na Sandvik mining hapohapo barrick,nikaacha pia 2009 nikaingia underground mining hapo barrick,kwa hiyo naijua vizuri barrick,hakukuna rushwa ili kupata kazi ya barrick kwanza uwe mvumilivu kuna neno wanatumia USOTEAJI unaweza kukaa hata miaka 5 bila kupata kazi,pia kuomba kwa njia ya email ni ngumu maana wanapata email nyingi muno sasa hata shortlist inakuwa ngumu,mara zote wanachukua watu walioko sehem ya tukio hasa kakola,bugarama,na ilogi ambao wanaomba jamaa zao kuwapelekea barua na CV moja kwa moja HR Pia wanaogopa kuajiri mtu umetoka Dar au mtwara ukiacha kazi au kufukuzwa inabidi wakulipi nauli yako na familia mpk huko ni hasara kwao,pia mara zote mgodin kuna kazi kwa watu wenye uzoefu ndio maana utakuta wafanyakazi wa mgodini ni walewale migodi yote sijui buzwagi tulawaka,maana tiyari wako training wana cv za kutosha hata mimi nikiomba kesho kurudi maadamu sikufukuzwa napata kazi haraka maana tiyari ninauzoefu,HAKUNA RUSHWA labda kwa makampuni ya macotractor sio barrick,USHAURI KWA MLETA UZI WAHI MGODI WA KABANGA NIKKEI kasotee kazi,kazi za mgodi ni nzuri kuwahi kabla hawajaanza production wahi haraka kasotee acha kulalamika rushwa.pia kuwa mvumilivu sisi tulikuwa tunalala shuleni hapo shule ya msingi kakola tunasotea kazi hata hiyo bugarama na ilogi ni vichaka tu sasa wewe unafikia kwa jamaa unalala kitandani na unakula milo mitatu unalalamika KAZA BUTI KAMANDA UTAWINI TU ,PIA UKIIPATA ZICHANGE USEPE ZINA MADHARA SANA HIZO KAZI
 
kaka unachoongea ni ukweli kabisa yan pindi wakitangaza kazi za miner trainee yan hapo watu wanafurahia, pia kuna kazi za udereva zilitoka na kuna mtu aliapply na akaambiwa atoe laki 2 na atapata chaka na alifanyiwa hivo coz anafahamiana na wahusika.Hata maexpert wanaokuja wengi ni vilaza au Kamlete yan kaletwa na mtu
 
kaka unachoongea ni ukweli kabisa yan pindi wakitangaza kazi za miner trainee yan hapo watu wanafurahia, pia kuna kazi za udereva zilitoka na kuna mtu aliapply na akaambiwa atoe laki 2 na atapata chaka na alifanyiwa hivo coz anafahamiana na wahusika.Hata maexpert wanaokuja wengi ni vilaza au Kamlete yan kaletwa na mtu
Yes,ushahidi upo wazi kabisa,hasa pale bulyanhulu
 
Kaka hata email za matangazo yao ya kazi huwa haziendi. Nilishtuma saa nzima cafe mpka jamaa akaniambia hizo email wameziblock hata yeye amempa barua mtu kwa mkono anayefanya kazi humo.this is stupid nadhani vyombo huska vinapaswa kuangalia hili. Wacha watu wapambane gpa plus skilss
jamani jamani watanzania tuache kuzungumza mambo ambayo hhujayafanyia utafiti wa kutosha...nijuavyo mimi ABGM wao kazi ni lazima watangaze na ikitangazwa waombaji wa online wanatakiwa watumie barrick.taleo.net kutuma maombi yao na si vinginevyo
 
Watanzania tunatia huruma kwelikweli...yaani mikataba badala ya kutumia rate za kwao katika kulipa mishahara tunatumia rate zetu ambazo si sahihi! Hivi tumelogwa? dhahabu inathamani kiasi gani mpaka mtumishi alipwe laki nane za kitanzania kabla ya makato mengine? kwanini kwenye hii mikataba isiwe wazi kuwa mwekezaji atalazimika kulipa kulingana na mishahara ya nchi zilizotoka hizo kampuni? Umbumbu umetujaa mmmnooooo....
 
Watanzania tunatia huruma kwelikweli...yaani mikataba badala ya kutumia rate za kwao katika kulipa mishahara tunatumia rate zetu ambazo si sahihi! Hivi tumelogwa? dhahabu inathamani kiasi gani mpaka mtumishi alipwe laki nane za kitanzania kabla ya makato mengine? kwanini kwenye hii mikataba isiwe wazi kuwa mwekezaji atalazimika kulipa kulingana na mishahara ya nchi zilizotoka hizo kampuni? Umbumbu umetujaa mmmnooooo....
Halafu mtu mweusi nywele ngumu kama zangu anakuja humu kuwatetea,laana tu
 
Watanzania tunatia huruma kwelikweli...yaani mikataba badala ya kutumia rate za kwao katika kulipa mishahara tunatumia rate zetu ambazo si sahihi! Hivi tumelogwa? dhahabu inathamani kiasi gani mpaka mtumishi alipwe laki nane za kitanzania kabla ya makato mengine? kwanini kwenye hii mikataba isiwe wazi kuwa mwekezaji atalazimika kulipa kulingana na mishahara ya nchi zilizotoka hizo kampuni? Umbumbu umetujaa mmmnooooo....
naamini panakuwa na maafikiano kabla hujapewa kusaini mkataba wa ajira...na hiyo laki nane ni kwa watu ya level ya chini sana na wasio na ujuzi wowote
sijui kwenye kampuni yako watumishi wasio na ujuzi mnawalipaje
 
Inaonekana wewe umekosa kazi ndio maana umekuja na accusations. Kama una ushahidi sema uliomba nafasi gani na ukakosa kwa sababu hukutoa rushwa, sio kutuaminisha kuwa kuna rushwa bila ushahidi. Unasema tukaulize watu wa Kakola, Ilogi na Bugarama, unafikiri hao wanakijiji wote wanajua mambo ya barrick bila hata wao kuomba kazi?

Kazi kutangazwa gazetini sio lazima wewe upate, hata walio ndani ya shirika nao wanatakiwa kuomba hiyo kazi kama itakuwa ni ya juu kulingana na current position aliyonayo huyo mtu, ikija kwenye interview kuna uwezekano akapewa internal candidate kwanza.

Toa ushahidi ulifanyiwa interview na nani, kazi gani, mlikuwa wangapi na akachaguliwa nani?
Mwisho hiyo mikataba unayosema miezi sitasita, unanifanya niamini kuwa hiyo ni casual labour ambayo ni miezi mitatu mitatu na wanaopewa priority ni wananchi wanaotoka maeneo ya jirani na migodi kupitia chama chao ambacho Barrick huwa haiwachunguzi maana walishakuwa mature enough kujiendesha, ndio maana umesema tuulize vijiji vya jirani na migodi.

Majibu haya hapa....

Nenda kwa human resource manager pale,ana vijana wake hata hujaongea naye lazima uache mzigo kwa vijana hawa,halafu watapeleka jina lako moja kwa moja,wewe ukisikia tangazo la kazi barrick nenda moja kwa moja na milioni waone hao vijana mmoja yupo ilogi halafu ndani ya siku tatu ulishatoka,pale training napo acha pesa mambo yanakwenda...halafu mtu anakuja kubisha hapa...wakazi wanaozunguka mgodi wana ofisi yao ya ibuka cooperative society,pale napo barrick wameshikilia bila laki tano hujapata kazi,msipende kubisha sisi tuna data na kila siku tunawaona tu
 
naamini panakuwa na maafikiano kabla hujapewa kusaini mkataba wa ajira...na hiyo laki nane ni kwa watu ya level ya chini sana na wasio na ujuzi wowote
sijui kwenye kampuni yako watumishi wasio na ujuzi mnawalipaje
Kohen, Tunazungumzia Dhahabu hapa, MNC's huwa wanatumia model kama nne hivi; Polycentric, Ethnocentric, RegioCentric and Geocentric approaches kwenye issues za staffing... kutokana na hizo model malipo yanaweza kufuata balance sheet ama going rate approach. hapa kwetu kapuya aliamua tufuate going rate approach baada ya kulipwa ndururu! Makaburu walisherehekea usiku kucha baada kuchukua TBL na kukuta mishahara ya kijinga! Anyway...kama nchi ilitakiwa hivi vipengele vinawekwa bayana kwenye mikataba! Faida kubwa ni kuwa wananchi wa nchi husika wakilipwa mishahara mikubwa serikali nayo inafaidi kwakuwa kodi nazo zinakuwa kubwa...RIP mwalimu kweli UJINGA ni adui hatari sana maana umasikini unashamiri, maradhi yanaongezeka kutokana na adui huyu hatari...
 
Ni wawekezaji,ambao waliahidi kutoa fursa sawa za ajira kulingana na fani ya muombaji,lakini hali si shwari migodi ya barrick hasa buzwagi na bulyanhulu... Rushwa iko wazi bila pesa kazi hazipo,wanatangaza magazetini kila kukicha lakini kwa uhalisia barrick wameendekeza rushwa sana.

Tumefika hapo, tumekaa hapo muda mrefu imefikia hatua mtu anakuambia ni kiasi gani cha pesa utatoa ili kupata nafasi fulani,mfano kama kazi ina mshahara wa laki 8 kwa mwezi utatakiwa kutoa rushwa ya million moja,na watakupa mkataba wa miezi sita,ukihitaji kuendelea utatakiwa kulipa millioni tena'

Kwa ujumla migodi ya barrick hasa buzwagi na bulyanhulu imetapakaa rushwa,kazi inayohitaji mtu wa digrii utamkuta form four kigezo ni kwamba alitoa rushwa:Wanao husika hususani TAKUKURU tembeleeni maeneo hayo nendeni kijiji cha kakola,bugarama,ilogi na mwingiro halafu waulizeni wananchi suala hili watawaambia sababu ni jambo ambalo sasa limekuwa ni kama utamaduni..

Kama wapo humu wanaohusika waje wakanushe.

Binafsi nitakuwa wa mwisho kuamini hiki ulichokiweka hapa jamvini kwa sababu ninafahamu ajira zinapatikana vipi ndani ya Barrick. Naomba uniamini kwamba mtu wa HR pekee hana uwezo wa kumpatia mtu ajira ndani ya Barrick. Hata akichukua pesa, kama idara inayotaka kuajiri haikutaki hutapata nafasi hiyo. Amini hilo mkuu.
 
Binafsi nitakuwa wa mwisho kuamini hiki ulichokiweka hapa jamvini kwa sababu ninafahamu ajira zinapatikana vipi ndani ya Barrick. Naomba uniamini kwamba mtu wa HR pekee hana uwezo wa kumpatia mtu ajira ndani ya Barrick. Hata akichukua pesa, kama idara inayotaka kuajiri haikutaki hutapata nafasi hiyo. Amini hilo mkuu.
Si lazima uwe wa kwanza kuamini,na si lazima uamini but in fact ukweli uko wazi na kama tutaendelea hivi nitataja majina ya watu watano wanaofanya biashara hii ya rushwa mgodini,na wameingiza watu wengi kwa njia hizi wanajulikana sana...hao watano ni pamoja na maajenti wao.
 
Binafsi nitakuwa wa mwisho kuamini hiki ulichokiweka hapa jamvini kwa sababu ninafahamu ajira zinapatikana vipi ndani ya Barrick. Naomba uniamini kwamba mtu wa HR pekee hana uwezo wa kumpatia mtu ajira ndani ya Barrick. Hata akichukua pesa, kama idara inayotaka kuajiri haikutaki hutapata nafasi hiyo. Amini hilo mkuu.

hata mimi nilipata kazi buzwagi bila rushwa,wale chinja chinja hawapo?
 
Si lazima uwe wa kwanza kuamini,na si lazima uamini but in fact ukweli uko wazi na kama tutaendelea hivi nitataja majina ya watu watano wanaofanya biashara hii ya rushwa mgodini,na wameingiza watu wengi kwa njia hizi wanajulikana sana...hao watano ni pamoja na maajenti wao.

Bandiko langu halikuwa na lengo la kukubishia mkuu ila nilikuwa najaribu kueleza kile ninachokifahamu kama jinsi ambavyo wewe umetueleza kile unachokijua. Labda kama utakuwa unaongelea kazi za vibarua ambazo mara nyingi huwa ni za muda mfupi na hazihitaji ujuzi isipokuwa nguvu na mafunzo kidogo ukiwa hapo hapo kazini. Kwa kazi ambazo zinahitaji ujuzi na ni za muda mrefu, hicho ulichokisema sijawahi kukiona wala kukisikia. Ni mawazo yangu tu mkuu.
 
Kweli kabisa, hawa jamaa hua nashangaa sana wanatoa post za kazi daily, ila omba na ku omba hakuna kitu duh!
 
Haya msemayo wandugu yanaweza kuwa kweli.

IBUKA ni Ilogi, Bugarama na Kakola....lakini nasikia imetengenezwa na mtu mmoja au wachache ili wachote ela Barrick kwani wakazi wa Kakola na Bugarama wanasema iko onwned na mtu mmoja toka Moshi. in the name of hivyo vijiji....mimi niko kwenye research fulani na hayo yalikuwa ni majibu ya wadau...ingawa ilikuwa nje ya scope ya research yangu...wadhungu unajua wakimuamini mmbongo hata akiwa mwizi hawaoni...mbaya zaidi kuna watu walinambia kabisa wana ajira kwa kutoa kitu kidogo.
 
I totally disagree with you that HR Manager has his guys, who works for him for malpractices purposes. Ninachoweza kusema ni kuwa kuna vijana wengi pale mitaani Kakola, Bugarama na Ilogi wanao tapeli watu kuwa watawapa kazi kupitia kwao. Hao watu kwa sababu ya kutaka kazi wanaingia mkenge, sasa aliyeliwa pesa yake anajua hiyo ni Barrick, which is not true.

Kuhusu chama cha IBUKA, kama nilivyosema awali ni chama kilichoanzishwa na wanakijiji wanaozunguka maeneo ya mgodi wa Bulyanhulu ili vijana wanao toka eneo hilo wapate ajira. Barrick ilichokifanya ni kuhakikisha kuwa chama kinapata viongozi wanakijiji watakao kiongoza, tokea muda mrefu chama kinajiendesha chenyewe na Barrick wakitaka kuajili kutoka kijijini wanawasiliana na viongozi wa IBUKA na viongozi wa IBUKA ndo wanaoleta watu kulingana na idadi waliyo ambiwa na Barrick. If there is any malpractices katika hicho chama that is not Barrick it is IBUKA, wanakijiji wanaopatwa na matatizo ya kuombwa rushwa watoe taarifa katika uongozi wa mgodi, ili uongozi ujue, maana unakuta mtu ametoa rushwa halafu anakaa kimya na badala yake anakuja kulalamika huku JF.

Lakini pia hiyo IBUKA ni kwa ajili ya wanakijiji wanaozunguka mgodi ila unakuta watu kutoka Kahama, Shinyanga, Mwanza, Kagera, Dar es salaam etc. ambao sio wakazi wa pale wanaenda kuomba kazi na hao ndo wanashawishi viongozi wa IBUKA kupokea rushwa.

kaka kumbe wewe ndo mwajiriwa wa barrick jitmbulishe na kujibu allegation hizo kwa kina!
 
Halafu mtu mweusi nywele ngumu kama zangu anakuja humu kuwatetea,laana tu


Mie nipo karibu sana na watu wanaosotea kazi Buzwagi au Bully, na mara nyingi kwenye maongezi yao utasikia wameambiwa wakatoe kiasi fulani cha pesa ili wapate ajila, na kweli wengi wamepata kazi kwa njia hiyo na hivi sasa wanatinga,

Ndugu yangu HR wa Barrick unayewatetea ma HR wenzako hapa JF jaribu kuliangalia jambo hili wewe kama wewe na si kutetea watu wengine kwani hawa majamaa "Watingaji" mara nyingi ni watundu ktk nyanja nyingi na kama unang'ang'ania ushahidi wao basi very soon mtaadhirika au mtu ataadhirika kutokana na tabia mbaya mlizozizoea, utakuta kijana hana kazi, uzoefu anao kutoka migodi mingine then mkijua huyu lazima atapata kazi ndipo nyie mnaweka cha juu ...very sad and silly professionalism,

ACHENI KUFANYA KAZI KAMA VILE MPO SERIKALINI, BANK KUU, IKULU etc, WASWAHILI WENZETU MNATIA AIBU
 
I totally disagree with you that HR Manager has his guys, who works for him for malpractices purposes. Ninachoweza kusema ni kuwa kuna vijana wengi pale mitaani Kakola, Bugarama na Ilogi wanao tapeli watu kuwa watawapa kazi kupitia kwao. Hao watu kwa sababu ya kutaka kazi wanaingia mkenge, sasa aliyeliwa pesa yake anajua hiyo ni Barrick, which is not true.

Kuhusu chama cha IBUKA, kama nilivyosema awali ni chama kilichoanzishwa na wanakijiji wanaozunguka maeneo ya mgodi wa Bulyanhulu ili vijana wanao toka eneo hilo wapate ajira. Barrick ilichokifanya ni kuhakikisha kuwa chama kinapata viongozi wanakijiji watakao kiongoza, tokea muda mrefu chama kinajiendesha chenyewe na Barrick wakitaka kuajili kutoka kijijini wanawasiliana na viongozi wa IBUKA na viongozi wa IBUKA ndo wanaoleta watu kulingana na idadi waliyo ambiwa na Barrick. If there is any malpractices katika hicho chama that is not Barrick it is IBUKA, wanakijiji wanaopatwa na matatizo ya kuombwa rushwa watoe taarifa katika uongozi wa mgodi, ili uongozi ujue, maana unakuta mtu ametoa rushwa halafu anakaa kimya na badala yake anakuja kulalamika huku JF.

Lakini pia hiyo IBUKA ni kwa ajili ya wanakijiji wanaozunguka mgodi ila unakuta watu kutoka Kahama, Shinyanga, Mwanza, Kagera, Dar es salaam etc. ambao sio wakazi wa pale wanaenda kuomba kazi na hao ndo wanashawishi viongozi wa IBUKA kupokea rushwa.

Mkuu hueleweki! Ww ni mtu wa Takukuru wa mfanyakazi wa Buly (HR Dept)? Kama ni mfanyakazi wa Buly kubali kuchunguza hili kuliko kuzua ubishi unaotia shaka. ningekushauri weka jina lako kamili na capacity yako hapa JF na Andrew naye afanye hivo ili mshirikiane ktk uchunguzi! Otherwise PM each other ili ku-effect uchunguzi. Lisemwalo lipo kama halipo laja! Ni uchunguzi shirikishi tu ndo utaweka mambo wazi!
 
Back
Top Bottom